Watanzania 90 wakamatwa Afrika Kusini

Watanzania 90 wakamatwa Afrika Kusini

Mkalukungone Mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
2,913
Reaction score
6,508
Ubalozi wa Tanzania Nchini Afrika Kusini umethibitisha kukamatwa kwa zaidi ya raia 90 wa Tanzania na kuwekwa katika Kituo cha Lindela kufuatia msako wa Wahamiaji Haramu unaoendelea Nchini humo.

Akizungumza kwa njia ya simu na AyoTv_ Balozi wa Tanzania Nchini humo James Bwana amethibitisha kuwapo kwa Watanzania waliokamatwa kutokana na vuguvugu linaloendelea dhidi ya Raia wa Kigeni.

Soma Pia: Balozi Bwana: Video inayosambaa mitandaoni haihusiani na matukio ya vurugu dhidi ya Waafrika Kusini na raia wa kigeni, Watanzania wapo salama

"Hawa 60 wanatoka maeneo ya kwetu huko Nchini Tanzania ikiwemo Mbagala, Ilala, Tandika,Kilwa, Magomeni, Temeke, Kariakoo, Mbezi Juu, Manzese, Mwananyamala, Kiwalani, Keko, Mbezi, Kimara, Tabata, Zingiziwa na mmoja ni Tanga kwahiyo ukiangalia hapo kwa tathmini ya haraka asilimia 99 ya hawa Watu wanatoka mkoa wa Dar es salaam”—— Bwana.

 
Kwa usalama zaidi, ni vizuri wakarejea nyumbani haraka,

Hakuna haja ya kung'ang'ania au kulazimisha kuishi mahali ambapo wenyewe hawakutaki 🐒
 
Police wa South Africa huwapora passport na kuzichana kisha kuwabambikia kesi za uongo kuwa ni wahamiaji Haramu, Ubalozi huwa wanawahukumu juu kwa juu hawaka kusogea walipo wawasikilize wajue ukweli, Nchi zingine huwa hawataki huo ujinga wa police wa South Africa balozi zao hufanya uchunguzi na kujiridhisha kwanza ikiwemo kuangalia viza immigration kujua uingiaji wao, lakini kwa Tanzania wao huwahukumu moja kwa moja kwa kuamini uongo wa police ambao hawapendi wageni kwa kiwango cha kutisha
 
Ubalozi wa Tanzania Nchini Afrika Kusini umethibitisha kukamatwa kwa zaidi ya raia 90 wa Tanzania na kuwekwa katika Kituo cha Lindela kufuatia msako wa Wahamiaji Haramu unaoendelea Nchini humo.

Akizungumza kwa njia ya simu na AyoTv_ Balozi wa Tanzania Nchini humo James Bwana amethibitisha kuwapo kwa Watanzania waliokamatwa kutokana na vuguvugu linaloendelea dhidi ya Raia wa Kigeni.

Soma Pia: Balozi Bwana: Video inayosambaa mitandaoni haihusiani na matukio ya vurugu dhidi ya Waafrika Kusini na raia wa kigeni, Watanzania wapo salama

"Hawa 60 wanatoka maeneo ya kwetu huko Nchini Tanzania ikiwemo Mbagala, Ilala, Tandika,Kilwa, Magomeni, Temeke, Kariakoo, Mbezi Juu, Manzese, Mwananyamala, Kiwalani, Keko, Mbezi, Kimara, Tabata, Zingiziwa na mmoja ni Tanga kwahiyo ukiangalia hapo kwa tathmini ya haraka asilimia 99 ya hawa Watu wanatoka mkoa wa Dar es salaam”—— Bwana.

Ubalozi wa Tanzania wajifunze kuhakiki kujiridhisha kwanza kwani police wa South Africa wana uhuni mwingi ni wajinga sana
 
Mgeni unapoingia Nchi ya kigeni unatakiwa kutoa taarifa kwa Balozi wa Nchi yako ili aweze kujua kuwa upo huko kwa shughuri gani
Pia akuandikishe kwenye rosta yake ili kuweza kukupatia stahiki zako kama raia wa Nchi yake
Je watanzania wote mnaoenda S.A mnafuata huo utaratinu ?
Jibu ni hapana, wengine wanazamia na kuanza kufanya shughuri zisizo rasmi na hata kujiingiza kwenya biashara haramu:
Nani wa kulaukiwa hapo?
 
Mgeni unapoingia Nchi ya kigeni unatakiwa kutoa taarifa kwa Balozi wa Nchi yako ili aweze kujua kuwa upo huko kwa shughuri gani
Pia akuandikishe kwenye rosta yake ili kuweza kukupatia stahiki zako kama raia wa Nchi yake
Je watanzania wote mnaoenda S.A mnafuata huo utaratinu ?
Jibu ni hapana, wengine wanazamia na kuanza kufanya shughuri zisizo rasmi na hata kujiingiza kwenya biashara haramu:
Nani wa kulaukiwa hapo?
Na kwa nini huo ubalozi usiwe unafuatilia taarifa za uhamiaji kuhusu watu wake?Wanasubiri wapelekewe taarifa?Wamekuwa akina "Beans"? They're there to seat back and look,huh?
 
Police wa South Africa huwapora passport na kuzichana kisha kuwabambikia kesi za uongo kuwa ni wahamiaji Haramu, Ubalozi huwa wanawahukumu juu kwa juu hawaka kusogea walipo wawasikilize wajue ukweli, Nchi zingine huwa hawataki huo ujinga wa police wa South Africa balozi zao hufanya uchunguzi na kujiridhisha kwanza ikiwemo kuangalia viza immigration kujua uingiaji wao, lakini kwa Tanzania wao huwahukumu moja kwa moja kwa kuamini uongo wa police ambao hawapendi wageni kwa kiwango cha kutisha
Ubalozi uwarudishe Home tu, kwanini wang'ang'anie huko na wenyewe hawataki. Rudini nyumbani kumenoga.
 
Na kwa nini huo ubalozi usiwe unafuatilia taarifa za uhamiaji kuhusu watu wake?Wanasubiri wapelekewe taarifa?Wamekuwa akina "Beans"? They're there to seat back and look,huh?
We unajua kuwa sio wote wanaoenda S.A wanaenda kwa njia rasmi:
Wengine wanaenda kwa njia za panya
Pia Balozi anaweza kupata taarifa ya wanaoingia kwa usafiri rasmi kwa kuletewa habari toka mamlaka ya usafirishaji.
Lakini jukumu la kwenda kujitambulisha ubalozini ni jukumu la raia mwenyewe

Kuna wengine wanaenda kwa usafiri rasmi lakini hawataki kujulikana na mamlaka kutokana kuhofia kueleza malengo ya safari zao:
Mfano aina ya wale waliokamatwa Airport ya S.A wakiwa na Mabegi ya madawa ya kulevya,
mtu kama huyo hawezi kwenda jitambulisha ubalozini kwani safari yake ni ya matendo haramu:
Kuna hawa wanaoenda S.A kwa kuzamia usafiri wowote ule kama Gali na Meli:
Wengi hawajui hata wajibu wao wa kutakiwa kutambulika na mamlaka ya ubalozi:
Wajibu ni WA wewe raia kwenda kujitambulisha Ubalozini:
 
Mgeni unapoingia Nchi ya kigeni unatakiwa kutoa taarifa kwa Balozi wa Nchi yako ili aweze kujua kuwa upo huko kwa shughuri gani
Mkuu hilo si kweli, unaenda ubalozini halafu watakusaidia nini?
Cha msingi usifanye makosa au kupata majanga nchi ya ugenini.
Nimesafiri mara nyingi nchi tofauti duniani, sikufika ubalozini hata mara moja, isipokuwa nchi moja ambayo Balozi alikuwa rafiki yangu.
 
We unajua kuwa sio wote wanaoenda S.A wanaenda kwa njia rasmi:
Wengine wanaenda kwa njia za panya
Pia Balozi anaweza kupata taarifa ya wanaoingia kwa usafiri rasmi kwa kuletewa habari toka mamlaka ya usafirishaji.
Lakini jukumu la kwenda kujitambulisha ubalozini ni jukumu la raia mwenyewe

Kuna wengine wanaenda kwa usafiri rasmi lakini hawataki kujulikana na mamlaka kutokana kuhofia kueleza malengo ya safari zao:
Mfano aina ya wale waliokamatwa Airport ya S.A wakiwa na Mabegi ya madawa ya kulevya,
mtu kama huyo hawezi kwenda jitambulisha ubalozini kwani safari yake ni ya matendo haramu:
Kuna hawa wanaoenda S.A kwa kuzamia usafiri wowote ule kama Gali na Meli:
Wengi hawajui hata wajibu wao wa kutakiwa kutambulika na mamlaka ya ubalozi:
Wajibu ni WA wewe raia kwenda kujitambulisha Ubalozini:
Maelezo yako ni marefu lakini bado haukuelewa nililenga kipi? Asante kwa maelezo "ndefu"!
 
Unaenda South Africa kuuza bangi wakati ungeweza kuuzia tu Manzese bila bughudha
 
Back
Top Bottom