Kitoto Akisa
Member
- Apr 23, 2009
- 53
- 5
Ndugu wana jamvi naomba hoja zenu katika hili mimi linanitatiza sana. Ni mara nyingi sana kila ninaposikiliza habari au matangazo mbalimbali katika redio zetu au Luninga ninapatwa na mshangao jinsi hao presenters wanavyo potosha jamii. Mfano mzuri ni jana, nilikuwa naangalia habari katika Luninga ya moja hapa Bongo, mtangazaji alikuwa anaelezea ziara ya waziri mkuu wa Kenya huko South Afrika, kilichonishangaza alisema eti nanukuu' waziri mkuu wa Kenya Bwana Raila Odinga amempongeza Rais wa Afrika Kusini Bwana Thabo Mbeki kwa uchaguzi wa Amani' sasa cha kujiuliza inamaana huyu mwandishi hajui kuwa Mbeki sio Rais wa A.kusini, ila Rais ni Jacob Zuma! na ajabu katika picha za Luninga za ziara hiyo zilimuonesha Raila akiwa na Zuma. Mimi nilifikiri yule mwandishi ataomba radhi kwa hilo, lakini wapi jamaa akaendelea na habri zingine as if ameongea kitu sawa. Siku nyingine nilikuwa nasikiliza Redio moja hapa Bongo, kilikuwa ni kipindi cha maswali kwa watoto. Mtangazaji aliwataka watoto waseme jina Moja la Mnyama, ambalo linaweza toa maneno matatu ya kiswahili yenye maana. Watot walijithidi lakini walikwama, ndio mtangazaji akatoa jibu, eti mnyama huyo ni Kangaloo, na akatoa ufafanuzi kuwa maneno hayo matatu yaliyo katika jina Kangaloo ni KANGA, ANGA NA LOO ( ladab alimaanisha "ROHO"), mimi nikakubaliana na maneno mawili ya kwanza, lakini hili la tatu, hapana . Nikajiuliza hivi neno Loo ninamaana gani katika kiswahili? na kama alinaanisha ROHO, inamaana huyu mwandishi alikuwa hajui kuwa Kangaloo haina "H" ili kuleta maana ya ROHO?
Sasa ndio nauliza jamani hawa waandishi wetu ni kasuku ambao wanakaririshwa cha kusema, au wanauelewa? hivi hakuna wahariri wa vipindi kabla havijaenda hewani? Jamani tusipokuwa makini watangazaji wa jinsi hii watapotosha umma hasa watoto wetu! Nawasilisha
Sasa ndio nauliza jamani hawa waandishi wetu ni kasuku ambao wanakaririshwa cha kusema, au wanauelewa? hivi hakuna wahariri wa vipindi kabla havijaenda hewani? Jamani tusipokuwa makini watangazaji wa jinsi hii watapotosha umma hasa watoto wetu! Nawasilisha