Watahiniwa wa CPA njia panda

Watahiniwa wa CPA njia panda

MTAZAMO

Platinum Member
Joined
Feb 8, 2011
Posts
19,990
Reaction score
34,838
Wakuu,

Inasemekana hadi leo bodi ya Wahasibu na ukaguzi wa mahesabu (NBAA) wameshindwa kutangaza matokeo ya CPA Exams.

Sababu kuu sijafahamu lakini kwa kumbukumbu zangu toka Prof ASSAD ateuliwe kuwa CAG nafasi yake kama NBAA Board Chairman haijajazwa.

Kama board muda wake umeisha na hakuna Chairman wa kuteua nyingine maana yake hakuna wa ku approve matokeo. Kama sababu ni hii bora itafutwe njia ya haraka kuwasaidia wanafunzi kujua matokeo na kujipanga kwa mitihani ya mwezi May 2018.

Kwavile JF ni kisima cha habari pengine tukajua exactly kinachochelewesha matokeo. Kuna wadau wamepewa deadlines vibaruani kuclear CPA toeni matokeo wajue ni mbivu ama mbichi.
 
Si ateuliwe kichwa Neema Kiure Msusa tusonge ....
 
Sasa kama wewe msukule ni tutor wa CPA hao wanafunzi watakuwaje?.....CPA holder wengi ni watupu kichwani wanachojua nikukariri tu hawana impact yoyote kwa Taifa
Mbna una chuki kubwaa... kutoka kwenye sakafu ya moyo wako?
Nakuomba tushirikishe ulichofanywa na bodi ya uhasibu... tunaweza kukupa msaada wa mawazo..

Karibu utiririke mkuu
 
Mbna una chuki kubwaa... kutoka kwenye sakafu ya moyo wako?
Nakuomba tushirikishe ulichofanywa na bodi ya uhasibu... tunaweza kukupa msaada wa mawazo..

Karibu utiririke mkuu
Hahaha ...
 
Wakuu,

Inasemekana hadi leo bodi ya Wahasibu na ukaguzi wa mahesabu (NBAA) wameshindwa kutangaza matokeo ya CPA Exams.

Sababu kuu sijafahamu lakini kwa kumbukumbu zangu toka Prof ASSAD ateuliwe kuwa CAG nafasi yake kama NBAA Board Chairman haijajazwa.

Kama board muda wake umeisha na hakuna Chairman wa kuteua nyingine maana yake hakuna wa ku approve matokeo. Kama sababu ni hii bora itafutwe njia ya haraka kuwasaidia wanafunzi kujua matokeo na kujipanga kwa mitihani ya mwezi May 2018.

Kwavile JF ni kisima cha habari pengine tukajua exactly kinachochelewesha matokeo. Kuna wadau wamepewa deadlines vibaruani kuclear CPA toeni matokeo wajue ni mbivu ama mbichi.
Taaluma za makondakta wa daladala hizo hazina pressure, ingekuwa ni madaktari na matabibu sawa!!
 
Si ateuliwe kichwa Neema Kiure Msusa tusonge ....

Hawezi kukubali huo Uteuzi kwa kuwa itamgharimu Kama ilivyomgharimu Prof Assad

Neema ni Partner wa Ernest & young

Neema anafanya Kazi ya consultancy na Treasury kwenye kutengeneza sera na uandaaji wa mahesabu ya jumla ya Serikal

Neema ni Mjumbe wa Bodi ya Wahasibu Duniani kanda ya Africa

Kwa kuteuliwa kwenye hiyo nafasi kutokana na conflict of interest atapoteza fursa nyingi japo kibongo bongo ukiteuliwa ukamchomolea Yule Mzee anakupora tenda zote kwa kumdharau
 
Sio NBAA tu, uchelewashaji wa uteuzi wa wenyeviti za board katika awamu hii imekuwa ni tabia sugu, nadhani utawala huu hauko mindful na mambo ya corporate governance na professionalism.

Taasisi nyingi sana hazina wenyeviti wa board, mpaka majuzi hapa, taasisi ya SELF MICROFINANCE ilishindwa kabisa kuendesha shughuri zake za msingi sababu tu mwenyekiti hajateuliwa.

Sasa hii ya NBAA, hapo ni mkwamo usio na lazima umesababishwa kwenye mfumo mzima wa usimamizi wa fedha nchini.

But who cares?
 
Back
Top Bottom