Ripoti ya CAG kwa mwaka ulioishia Juni 30, 2014 yabaini ufisadi wa zaidi ya bilioni 600

mansakankanmusa

JF-Expert Member
Sep 30, 2010
4,163
787
Wakati nchi ikiwa na deni kubwa na Maisha Magumu, Wakuu wa vitengo wanaiba kwa kwenda mbele.

Siku si nyingi Waziri wa Fedha, Mh Waziri Mkuu na wadau wengine walilifuatilia sakata wizi na Mishahara hewa. Sasa! Marehemu wetu, Wastaafu wetu waonekana kupokea mishahara.

Misamaha ya Kodi Bilioni 22.33, Wastaafu Hewa Nje ya Nchi Milion 5.43, Wakwepa kodi bilioni 800, Waliocha kazi Wanakula 141.4 Milion HEWA. -===== BILION 9 NA Milion 48.16

CAG wa zamani ndugu LUDOVICK UTUOH alikuwa hana neno. Yeye anaandika ripoti yake kisha hatoi INDIVIDUAL REPORTS za kila idara ya serikali na kuweka wazi ONLINE kama ambavyo huyu CAG mpya anavyofanya. Basically UTUOH alikuwa anatoa ripoti ambazo ziko DILUTED to the public lakini zile zingine alikuwa hataki wananchi wazisome wala kujua nani anaiba nini na nani anafuja pesa. Matokeo yake wizi ulikuwa unaendelea with IMPUNITY.

CAG mpya Professa MUSSA J ASSAD amekuwaja na moto wa ajabu na anatumia visingizio kuwa anatekeleza agizo la bosi wake Professa Kikwete kuwa serikali yake ni TRANSPARENT/WAZI na wanaanchi wanayo haki ya kusoma na kujua KODI zao zinavyotumika na jinsi serikali inavyotumia pesa.

Lakini JK kutaka misifa kuonyesha kuwa anakwenda na wakati na anatekeleza mpango mzima wa OPEN GOVT INITIATIVE/PARTNERSHIP (OGP) utapelekea watu kukosa kazi na kuleta vurugu nchi hii na inawezekana serikali ikaanguka kwa sababu si kawaida ya watanzania kuona serikali ikaweka wazi ripoti za matumizi ya kodi (JAPO SHERIA INAMTAKA CAG AWEKE HIZI RIPOTI WAZI) lakini pia inasemekana kuwa huyu CAG mpya alikuwa na tabia za UNOKO toka alipokuwa anasomesha chuo kikuu cha Dar es salaam.

Sasa cha kujiuliza, Je hizi ripoti za ukaguzi za kila shirika na kila wilaya zitawekwa wazi kama ambavyo serikali WAZI na SIKIVU inavyotaka? Na je tujiandae kuona akina nani wanafikishwa mbele ya vyombo vya sheria kwa ufujaji wa pesa za walalahoi? Je inawezekana haya mambo kuwa wazi ni geresha ya CCM kutaka serikali yao kuonekana wako TRANSPARENT na ACCOUNTABLE kuelekea kwenye uchaguzi?

Au JK kaamuatuuu kuwa LIWALO NA LIWE lakini serikali yake anataka ikumbukwe kama THE MOST TRANSPARENT & ACCOUNTABLE GOVT TANZANIA ever had?

Mwisho zaidi swali ni HOW DO YOU SOLVE A PROBLEM OF CAG MNOKO kama huyu mpya?

Dodoma. Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad amewasilisha ripoti tano za ukaguzi wa fedha kwa mwaka ulioishia Juni 30, 2014 akibainisha ufisadi wa zaidi ya Sh600 bilioni katika maeneo mbalimbali na matumizi ya fedha ambayo hayana maelezo ya kutosha.

Ukaguzi huo ulifanywa katika Serikali Kuu, Serikali za Mitaa, mashirika ya umma, miradi ya maendeleo na ufanisi wa maeneo mbalimbali.

Ripoti hizo zinaonyesha jinsi watumishi hewa wa umma wanavyoendelea kulipwa mishahara, wakiwamo wa balozi za Tanzania waliostaafu, misamaha ya kodi na ukiukwaji wa ununuzi na matumizi yasiyoeleweka ya fedha katika Wizara ya Ujenzi na Kitengo cha Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu.

Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), Amina Mwidau na Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), Rajab Mbaruk Mohamed walizichambua ripoti hizo na kueleza jinsi watumishi wa Serikali wanavyotafuna mabilioni ya fedha.

Akizungumzia ripoti hiyo katika mkutano wa pamoja na CAG, Mwidau alisema imeonyesha jinsi Sh285 bilioni za Kitengo cha Maafa zilivyotafunwa licha ya kuwa zilitengwa kwa ajili ya kufanya shughuli maalumu.

Kuhusu Wizara ya Ujenzi, alisema ililidanganya Bunge baada ya kueleza kuwa Sh262 bilioni zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa barabara, kitu ambacho kimebainika kuwa siyo kweli.

“Ukaguzi unaonyesha kuwa fedha hizo zimetumika katika mambo mengine kabisa, yaani zimetumika tofauti na hakuna maelezo ya kuridhisha,” alisema Mwidau huku akifafanua kuwa wizara hiyo inadaiwa na makandarasi Sh800 bilioni.

Misamaha ya kodi


Profesa Assad alisema ofisi yake ilibaini kasoro katika mfumo wa ufuatiliaji wa misamaha ya kodi na kusababisha ukiukaji wa matumizi iliyotolewa kwa mafuta yanayotumika migodini.

Alisema mafuta yenye kodi ya Sh22.33 bilioni yaliyotakiwa kutumiwa na kampuni zilizosamehewa kodi, Geita Gold Mine na Resolute TZ Ltd, yalipelekwa kwa makandarasi wasiostahili msamaha na kusababisha hasara ya Sh22.33 bilioni,” alisema.

Alisema pia misamaha ya kodi kwa malengo tofauti na yaliyokusudiwa, ilitolewa na kusababisha upotevu wa Sh392.7 milioni katika Kampuni ya Kiliwarrior Expeditions Ltd ya Arusha iliyokuwa imesamehewa kodi Sh465.2 ili kuingiza magari 28.

Hata hivyo, alisema Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), imefanikiwa kati ya hizo kukusanya Sh72.5 milioni.

Pia, alisema misamaha ya Sh53.4 milioni ilitolewa kwa Kampuni ya Kilemakyaro Mountain Lodge Limited kwa ajili ya mradi wa ujenzi na upanuzi hoteli katika Kijiji cha Changarawe wilayani Karatu, lakini kampuni iliagiza magari matatu kwa kutumia msamaha na mengine matano ‘kuchepushwa’.

“Hata hivyo, ukaguzi ulithibitisha ununuzi wa gari moja tu ya Hyundai Santa. Magari mengine matano aina ya BMW na Toyota Land Cruiser Prado hayakufahamika yalipo,” alisema. CAG aliishauri Serikali izibe mianya ya upotevu wa kodi kupitia misamaha ya kodi aliyobaini katika ukaguzi wa mwaka huu, ikiwa ni pamoja na kuimarisha usimamizi na ufuatiliaji wa misamaha ya kodi iliyotolewa.

Mashine za EFD


Alisema katika ukaguzi wa malipo na matumizi ya mashine za kielektroniki (EFD), ofisi yake ilibaini kuwa kampuni binafsi hazitumii mashine hizo za kutolea stakabadhi.

Alisema hali hiyo imesababisha malipo ya Sh4.4 bilioni kutokuwa na stakabadhi za kielektroniki kwa taasisi za Serikali Kuu na Sh4.6 bilioni kwa sampuli 22 ya mamlaka za serikali za mitaa.

“Katika suala hili, TRA ilitoza faini Sh440.8 milioni kwa wafanyabiashara ambao walishindwa kutumia mashine za EFD ambapo jumla ya Sh72 milioni zililipwa sawa na asilimia 16 na hivyo kufanya bakaa ya Sh369 milioni ambayo haikulipwa,” alisema.

Alisema pia ukaguzi ulibaini upungufu katika usimamizi wa matumizi ya fedha za Serikali kama vile, malipo yasiyokuwa na nyaraka. Upungufu mwingine ni hati za malipo ambazo hazikuwasilishwa kwa ukaguzi, fedha zilizotumika nje ya bajeti, matumizi yasiyokuwa na manufaa na malipo ambayo hayakuidhinishwa na maofisa masuuli.

Alishauri taasisi za Serikali zisiendelee kanunua vifaa na huduma kwa wafanyabiashara wasiotumia mashine za EFD kutoa stakabadhi ya kukiri kupokea fedha.

“Hii iende sambamba na kuhakikisha kuwa maofisa masuuli wanaimarisha mfumo wa udhibiti wa ndani ikiwa pamoja na kuimarisha ukaguzi kabla ya malipo,” alisema.

Mishahara hewa

Alisema fedha zilizolipwa kwa watumishi hewa wa Serikali Kuu ni Sh141.4 milioni, “Hali hii inaendelea licha ya kuwa Serikali imewekeza kwenye mfumo wa Lawson kama njia mojawapo ya kudhibiti hali hiyo,” alisema. Hata hivyo, alisema suala hilo linazidi kupungua ikilinganishwa na mwaka jana. Lakini alisema Sh1.01 bilioni katika halmashauri 36 zililipwa kama mishahara kwa watumishi waliotoroka kazini, waliofariki, waliostaafu na kufukuzwa kazi.

Alisema kutokana na watumishi hewa, Sh845 milioni za halmashauri zililipwa kama makato ya taasisi mbalimbali kama vile mifuko ya pensheni, taasisi za fedha, Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) na TRA kwa ajili ya wafanyakazi hao hewa.

Katika balozi


CAG pia ameeleza jinsi Serikali ilivyolipa Sh543.7 milioni kutokana na kuwalipa watumishi wa balozi za Tanzania waliostaafu, waliokuwa wakifanya kazi bila kuwa na mikataba kutokana na changamoto za malipo ya kurejeshwa nyumbani.

Watumishi hao ni wa balozi za Tanzania Kinshasa (DRC), Maputo (Msumbiji), Ottawa (Canada) na Washington DC (Marekani).

Ripoti hiyo inaonyesha tarehe ambazo watumishi hao walistaafu, lakini Serikali iliendelea kuwalipa huku wakiwa katika maeneo yao ya kazi, zikijumuisha kodi za majengo huku baadhi ya watumishi hao wakifanya kazi licha ya kuwa mikataba yao kumalizika.

Ufisadi Tanesco


Ripoti hiyo pia ilibaini kuwapo kwa ununuzi wa Sh3.2 bilioni uliofanywa na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), bila kuzingatia kiasi kilichotengwa kwenye bajeti ya Sh400 milioni.

“Katika zabuni nyingine, Tanesco iliingia mkataba wa Sh340 milioni ambayo ni zaidi ya bajeti iliyotengwa ya Sh154 milioni. Ukaguzi haukuweza kupata ushahidi wa kuwapo kwa marejeo ya bajeti kwa kiasi kilichotumika nje ya makisio,” alisema

Vyama vya siasa


Kuhusu ukaguzi wa vyama vya siasa, CAG alisema hadi kufikia Juni, 2013 vyama 21 wakati vinakaguliwa, ni 12 tu ndivyo vilivyowasilisha taarifa za hesabu.Alisema kati ya vyama 12, tisa havikuwasilisha taarifa za hesabu ambavyo ni UPDP, Tadea, UDP, Demokrasia Makini, Chausta, DP, Jahazi Asilia, AFP na CCK.

Alisema katika ukaguzi huo, ilibainika kuwa vyama sita vya siasa vilipata hati ya shaka ambavyo ni CCM, Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi, TLP na Chauma na vya vingine vilipata hati mbaya ambavyo ni NRD, UMD, ADC, APPT, NLD na SAU.

Alishauri Msajili wa Vyama vya Siasa akishirikiana na Mhasibu Mkuu wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA), waandae mwongozo wa aina ya muundo wa taarifa za fedha utakaotumiwa na vyama vyote vya siasa.

Bajeti

Kuhusu bajeti, alisema tathmini waliyofanya kuhusu utekelezaji wa miradi ya maendeleo, programu na shughuli nyingine za maendeleo katika baadhi ya halmashauri, imeonyesha kuwa hadi kufikia Juni 30, mwaka jana, halmashauri hizo zilikuwa na bakaa ya jumla ya Sh29.2 bilioni sawa na asilimia 28 ya jumla fedha zilizotolewa.

Alisema kubakia kwa kiasi kikubwa cha fedha bila kutumika katika utekelezaji wa miradi kunatokana na ucheleweshaji wa kutuma fedha katika halmashauri.

Deni la Serikali

Alisema hadi kufikia Juni 30, mwaka jana, deni la mifuko ya hifadhi ya jamii lilikuwa limefikia Sh1,699 milioni na Sh975.1 milioni zilipaswa kuwa zimereshwa, lakini hadi wakati wa kuandika ripoti hiyo zilikuwa bado hazijalipwa.

Alishauri mifuko na Serikali kuzingatia na kufuata mwongozo wa uwekezaji wa fedha za mifuko ambao pamoja na mambo mengine, unatoa ukomo wa aina za mali ambazo mifuko inaweza kuwekeza.

Chanzo: Mwananchi
This is how your cash was ‘eaten’ in 2013/14
cag_assad.jpg

Dar es Salaam. A handful of influential people are stealing taxpayers’ money and depriving millions of Tanzanians of quality social services.

Controller and Auditor General Mussa Assad revealed the scam yesterday as he presented his Audit Report for the 2013/14 financial year in Parliament
. Billions of poor taxpayers’ money went to ghost workers and to retired employees who had been working in diplomatic missions and who continue to live in the countries they were posted to. Some of it was stolen through tenders that were awarded without following the right procedures and through the misuse of tax incentives by some multinational firms.

The review was based on an analysis of a sample of 176 institutions that report directly to the Central Government. Some 163 of those institutions are under the Local Government Authorities. There were also 775 development projects. And Tanzania lost Sh22.33 billion due to misuse of tax exemptions, according to Prof Assad, who succeeded Mr Ludovick Utouh in December last year.


This was the case when Geita Gold Mine and Resolute Tanzania decided to import oil using exempted documents but ended up giving the petroleum products to their contractors, who did not qualify for the incentive.

In the same vein,
the country lost Sh392 million when the Arusha-based Kiliwarrior Expeditions Limited received an exemption to import vehicles that ended up not being used for the purpose they were intended. “Another Sh53.4 million was lost due to misuse of tax exemptions by Karatu-based Kilemakyaro Mountain Lodges,” said Prof Assad. “I advise the government to fill these loopholes by making routine follow-ups on how tax exemptions are being utilised.”

Prof Assad is a Certified Professional Accountant who, prior to his appointment as CAG, taught at the University of Dar es Salaam’s Business School. He gave nine of the 176 audited Central Government institutions and some 13 of the 163 LGAs a Qualified (dirty) Opinion, signalling that he had reservations about the way they conducted their financial transactions. In auditing, a qualified opinion is offered when an independent auditor gets the impression that the audited financial statements do not reflect a fair view of the transactions. An Unqualified Opinion is essentially a Clean Bill of Health and means that the audited institution has presented its financial statements fairly.

Accompanied by the chairperson of the Public Accounts Committee, Ms Amina Mwidawa (CUF-Special Seats), Local Authorities’ Accounts Committee Chairman Rajab Mbarouk and Chairperson for the Parliamentary Budget Committee Kidawa Saleh (Special Seats, CCM), Prof Assad said the audited LGAs and Central Government institutions made transactions totalling Sh4.4 billion and Sh4.6 billion respectively with companies that did not issue receipts generated through Electronic Fiscal Devices (EFDs). This denied the government an opportunity to collect the right amount of tax. Prof Assad said:
“My audit has also established that former government employees, including those who have died, those who resigned and those who have retired, are still receiving salaries through their accounts. Health insurance, Pay As You Earn and social security contributions are still being deducted from these salaries.”

Tanzania lost some Sh1.01 billion in salaries to ghost workers while another Sh845 million was paid to pension funds, health insurance schemes, financial institutions and to Tanzania Revenue Authority (TRA) from these people’s salaries.

A total of Sh543.797 million was paid to Tanzania’s embassies and high commissions in Kinshasa in the Democratic Republic of Congo, Maputo in Mozambique, Ottawa in Canada and in Washington DC in the United States. “I advise that instead of paying Foreign Service Allowance to retirees, the ministry of Foreign Affairs and International Cooperation should consider the same amount to facilitate transportation of personal effects,” he said.

A total of Sh1.889 trillion was not disbursed for development activities to Central Government institutions as expected in the 2013/2014 budget while another Sh312.04 billion, meant for development expenditure at LGA level, was not disbursed that year.

Some more billions of taxpayers’ money were lost through tenders without following the proper bidding process. Some LGAs and Central Government Authorities paid more than the amounts that were prescribed on the contracts while some procurements were conducted outside the agreed plan for the financial year.

As for some audited public institutions, the National Housing Corporation issued Sh1.75 billion in tenders using a non-competitive bidding procedure and this led to only one company being picked to do the job. The Ngorongoro Conservation Authority issued a Sh2.3 billion tender on restrictive procedur–meaning that only a selected few bidders were allowed–and this without proper reasons.

This is how your money is being stolen - National
 
Hii kitu haiwezi kuisha na hakuna mtu mwenye nia ya dhati kumaliza hili! Waliofanya uzembe ktk report za nyuma wamechukuliwa atua gani? Kama hakuna kwa nn wasiendelee na ukiangalia watu ni wale wale kila mwaka.
 
Kipi kigeni kinachokufanya udamke asubuhi kuandika hii post? Kwanibhuo wizi wa mishahara umeanza leo? Mbona ni toka enzi za Ludovick uttoh? Riport zake zilionyesha hilo zaidi ya mara mbili, wastaafu kuendelea kupokea mishahara ni issue ya almost muongo mzima wizi katika halmashauri zetu kila mwaka ripory zinasema hivyo hivyo ubadhirifu uliopo katika manunuzi ya umma toka enzi za mkapa na kila mwaka ripot zinaonyesha hilo hadi ikulu mnikulu mkuu amefanya sana hiyo mambo, na habari zinasema hivyo kila riport ikitoka na hakuna anayechukuliwa hatua na trust me hata hili hakuna atakayechukuliwa hatua stahiki na mwakani C.A.G atafanya ukaguzi tena na yataonekana hayo hayo na vichwa vya habari vitasomeka kama vilivyosomeka mwaka huu na hakuna litakalofanyika sababu hii ni serikali ya "BUSSINESS AS USUAL" na maisha yaendelee..
 
Serikali ikubali kuingia hasara kwa kusajili upya wafanyakazi. Ili wajue nani yu hai, nani kafa, nani anaishi wapi
 
CAG wa zamani ndugu LUDOVICK UTUOH alikuwa hana neno. Yeye anaandika ripoti yake kisha hatoi INDIVIDUAL REPORTS za kila idara ya serikali na kuweka wazi ONLINE kama ambavyo huyu CAG mpya anavyofanya. Basically UTUOH alikuwa anatoa ripoti ambazo ziko DILUTED to the public lakini zile zingine alikuwa hataki wananchi wazisome wala kujua nani anaiba nini na nani anafuja pesa. Matokeo yake wizi ulikuwa unaendelea with IMPUNITY.

CAG mpya Professa MUSSA J ASSAD amekuwaja na moto wa ajabu na anatumia visingizio kuwa anatekeleza agizo la bosi wake Professa Kikwete kuwa serikali yake ni TRANSPARENT/WAZI na wanaanchi wanayo haki ya kusoma na kujua KODI zao zinavyotumika na jinsi serikali inavyotumia pesa.

Lakini JK kutaka misifa kuonyesha kuwa anakwenda na wakati na anatekeleza mpango mzima wa OPEN GOVT INITIATIVE/PARTNERSHIP (OGP) utapelekea watu kukosa kazi na kuleta vurugu nchi hii na inawezekana serikali ikaanguka kwa sababu si kawaida ya watanzania kuona serikali ikaweka wazi ripoti za matumizi ya kodi (JAPO SHERIA INAMTAKA CAG AWEKE HIZI RIPOTI WAZI) lakini pia inasemekana kuwa huyu CAG mpya alikuwa na tabia za UNOKO toka alipokuwa anasomesha chuo kikuu cha Dar es salaam.

Sasa cha kujiuliza, Je hizi ripoti za ukaguzi za kila shirika na kila wilaya zitawekwa wazi kama ambavyo serikali WAZI na SIKIVU inavyotaka? Na je tujiandae kuona akina nani wanafikishwa mbele ya vyombo vya sheria kwa ufujaji wa pesa za walalahoi? Je inawezekana haya mambo kuwa wazi ni geresha ya CCM kutaka serikali yao kuonekana wako TRANSPARENT na ACCOUNTABLE kuelekea kwenye uchaguzi?

Au JK kaamuatuuu kuwa LIWALO NA LIWE lakini serikali yake anataka ikumbukwe kama THE MOST TRANSPARENT & ACCOUNTABLE GOVT TANZANIA ever had?

Mwisho zaidi swali ni HOW DO YOU SOLVE A PROBLEM OF CAG MNOKO kama huyu mpya?
 
MAGUFULI kudanganya bunge na nchi kuhusu bilion 262-kwa mujibu wa CAG, WOTE TUNAJUA CAG sio mwanasiasa bali ni mtaalam kwa hiyo kauli yake unauzito wa kipekee
Je mwajua:Magufuri kabla ya kupandisha nauli pale kigamboni hakufanya hata upembuzi yakinifu kuwa vile vivuko na zaidi ya daraja kwa watu wakigamboni. Watu huvuka pale kwenda na kurudi zaidi ya hata mara tano kulingana na shughuli ya mtu. yeye huyu magufuri akalinganisha kivuko cha huko sengerema ambacho msafiri huvuka hata mara moja kwa mwaka ndio iwe kama Kigamboni.

Magufuri huyu nashangaa Ripoti ya CAG imeshingwa kusema chochote kuhusu tabia yake ya kujipendekeza kwa rais na kufikia kununua meli ya DAr - Bagamoyo! wamejenga pale magogoni Feri ghati ya hiyo meli kwa mamilioni ya pesa lakini ile ghati imeshindwa kutumia na sasa wanatumia ile ya Bakhresa. Huku pia kukiwa na tuhuma za kununua meli feki ambayo hutumia masaa 3 badala ya dkk 45 tu! Huyu jamaa kituko!



Huyu ASSAD watu walimmbeza ila kwa tunaomfaham tulifurahia sana uteuzi wake yaaan kama ni Gorrila war huyu ni KAGAME na sio GODOFRED kiongozi mpuuzi aliyetaka kuleta mapinduzi Burundi

kama ni bungeni huyu ni Mnyika, kama ni mziki huyu ni ali-kiba, kama ni soka huyu nemanja MATIC, kama ni spika basi huyu ni SITTA wa miaka ile alipokuwa na akili timamu, kama ni soka la bongo huyu ni Okwi na si TAMBWE AMISSI, kama ni ukuu wa majeshi jamaa ni Abdel Fattah al-Sisi. ANGELIKUWA mwanamkee Miss NINGEMFANANISHA na WEMA sepetu mrembo asiyechuja na sio SITTI MTEVU.

Hivi kulidanganya bunge ingekuwa huko china au KOREA kaskazini.
 
Kwa hiyo wewe hutaki uwazi??Tatizo siyo ufisadi tatizo la nchi hii ni jinsi mafisadi wanavyoshughulikiwa.Makomandoo wa UFISADI Idd Simba,Andrew Chenge pesa zimeingia mfukoni mwao hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa
 
Hayo yote ni ukweli mtupu..watumishi hewa bado wapo na wanalipwa ..marehemu na waastaafu kibao bado wanalipwa mishahara na stahiki mbalimbali...Hongera CAG kwa kutufumbua macho .
 
Dodoma. Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad amewasilisha ripoti tano za ukaguzi wa fedha kwa mwaka ulioishia Juni 30, 2014 akibainisha ufisadi wa zaidi ya Sh600 bilioni katika maeneo mbalimbali na matumizi ya fedha ambayo hayana maelezo ya kutosha.

Ukaguzi huo ulifanywa katika Serikali Kuu, Serikali za Mitaa, mashirika ya umma, miradi ya maendeleo na ufanisi wa maeneo mbalimbali.

Ripoti hizo zinaonyesha jinsi watumishi hewa wa umma wanavyoendelea kulipwa mishahara, wakiwamo wa balozi za Tanzania waliostaafu, misamaha ya kodi na ukiukwaji wa ununuzi na matumizi yasiyoeleweka ya fedha katika Wizara ya Ujenzi na Kitengo cha Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu.

Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), Amina Mwidau na Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), Rajab Mbaruk Mohamed walizichambua ripoti hizo na kueleza jinsi watumishi wa Serikali wanavyotafuna mabilioni ya fedha.

Akizungumzia ripoti hiyo katika mkutano wa pamoja na CAG, Mwidau alisema imeonyesha jinsi Sh285 bilioni za Kitengo cha Maafa zilivyotafunwa licha ya kuwa zilitengwa kwa ajili ya kufanya shughuli maalumu.

Kuhusu Wizara ya Ujenzi, alisema ililidanganya Bunge baada ya kueleza kuwa Sh262 bilioni zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa barabara, kitu ambacho kimebainika kuwa siyo kweli.

"Ukaguzi unaonyesha kuwa fedha hizo zimetumika katika mambo mengine kabisa, yaani zimetumika tofauti na hakuna maelezo ya kuridhisha," alisema Mwidau huku akifafanua kuwa wizara hiyo inadaiwa na makandarasi Sh800 bilioni.

Misamaha ya kodi


Profesa Assad alisema ofisi yake ilibaini kasoro katika mfumo wa ufuatiliaji wa misamaha ya kodi na kusababisha ukiukaji wa matumizi iliyotolewa kwa mafuta yanayotumika migodini.

Alisema mafuta yenye kodi ya Sh22.33 bilioni yaliyotakiwa kutumiwa na kampuni zilizosamehewa kodi, Geita Gold Mine na Resolute TZ Ltd, yalipelekwa kwa makandarasi wasiostahili msamaha na kusababisha hasara ya Sh22.33 bilioni," alisema.

Alisema pia misamaha ya kodi kwa malengo tofauti na yaliyokusudiwa, ilitolewa na kusababisha upotevu wa Sh392.7 milioni katika Kampuni ya Kiliwarrior Expeditions Ltd ya Arusha iliyokuwa imesamehewa kodi Sh465.2 ili kuingiza magari 28.

Hata hivyo, alisema Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), imefanikiwa kati ya hizo kukusanya Sh72.5 milioni.

Pia, alisema misamaha ya Sh53.4 milioni ilitolewa kwa Kampuni ya Kilemakyaro Mountain Lodge Limited kwa ajili ya mradi wa ujenzi na upanuzi hoteli katika Kijiji cha Changarawe wilayani Karatu, lakini kampuni iliagiza magari matatu kwa kutumia msamaha na mengine matano ‘kuchepushwa'.

"Hata hivyo, ukaguzi ulithibitisha ununuzi wa gari moja tu ya Hyundai Santa. Magari mengine matano aina ya BMW na Toyota Land Cruiser Prado hayakufahamika yalipo," alisema. CAG aliishauri Serikali izibe mianya ya upotevu wa kodi kupitia misamaha ya kodi aliyobaini katika ukaguzi wa mwaka huu, ikiwa ni pamoja na kuimarisha usimamizi na ufuatiliaji wa misamaha ya kodi iliyotolewa.

Mashine za EFD


Alisema katika ukaguzi wa malipo na matumizi ya mashine za kielektroniki (EFD), ofisi yake ilibaini kuwa kampuni binafsi hazitumii mashine hizo za kutolea stakabadhi.

Alisema hali hiyo imesababisha malipo ya Sh4.4 bilioni kutokuwa na stakabadhi za kielektroniki kwa taasisi za Serikali Kuu na Sh4.6 bilioni kwa sampuli 22 ya mamlaka za serikali za mitaa.

"Katika suala hili, TRA ilitoza faini Sh440.8 milioni kwa wafanyabiashara ambao walishindwa kutumia mashine za EFD ambapo jumla ya Sh72 milioni zililipwa sawa na asilimia 16 na hivyo kufanya bakaa ya Sh369 milioni ambayo haikulipwa," alisema.

Alisema pia ukaguzi ulibaini upungufu katika usimamizi wa matumizi ya fedha za Serikali kama vile, malipo yasiyokuwa na nyaraka. Upungufu mwingine ni hati za malipo ambazo hazikuwasilishwa kwa ukaguzi, fedha zilizotumika nje ya bajeti, matumizi yasiyokuwa na manufaa na malipo ambayo hayakuidhinishwa na maofisa masuuli.

Alishauri taasisi za Serikali zisiendelee kanunua vifaa na huduma kwa wafanyabiashara wasiotumia mashine za EFD kutoa stakabadhi ya kukiri kupokea fedha.

"Hii iende sambamba na kuhakikisha kuwa maofisa masuuli wanaimarisha mfumo wa udhibiti wa ndani ikiwa pamoja na kuimarisha ukaguzi kabla ya malipo," alisema.

Mishahara hewa

Alisema fedha zilizolipwa kwa watumishi hewa wa Serikali Kuu ni Sh141.4 milioni, "Hali hii inaendelea licha ya kuwa Serikali imewekeza kwenye mfumo wa Lawson kama njia mojawapo ya kudhibiti hali hiyo," alisema. Hata hivyo, alisema suala hilo linazidi kupungua ikilinganishwa na mwaka jana. Lakini alisema Sh1.01 bilioni katika halmashauri 36 zililipwa kama mishahara kwa watumishi waliotoroka kazini, waliofariki, waliostaafu na kufukuzwa kazi.

Alisema kutokana na watumishi hewa, Sh845 milioni za halmashauri zililipwa kama makato ya taasisi mbalimbali kama vile mifuko ya pensheni, taasisi za fedha, Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) na TRA kwa ajili ya wafanyakazi hao hewa.

Katika balozi


CAG pia ameeleza jinsi Serikali ilivyolipa Sh543.7 milioni kutokana na kuwalipa watumishi wa balozi za Tanzania waliostaafu, waliokuwa wakifanya kazi bila kuwa na mikataba kutokana na changamoto za malipo ya kurejeshwa nyumbani.

Watumishi hao ni wa balozi za Tanzania Kinshasa (DRC), Maputo (Msumbiji), Ottawa (Canada) na Washington DC (Marekani).

Ripoti hiyo inaonyesha tarehe ambazo watumishi hao walistaafu, lakini Serikali iliendelea kuwalipa huku wakiwa katika maeneo yao ya kazi, zikijumuisha kodi za majengo huku baadhi ya watumishi hao wakifanya kazi licha ya kuwa mikataba yao kumalizika.

Ufisadi Tanesco


Ripoti hiyo pia ilibaini kuwapo kwa ununuzi wa Sh3.2 bilioni uliofanywa na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), bila kuzingatia kiasi kilichotengwa kwenye bajeti ya Sh400 milioni.

"Katika zabuni nyingine, Tanesco iliingia mkataba wa Sh340 milioni ambayo ni zaidi ya bajeti iliyotengwa ya Sh154 milioni. Ukaguzi haukuweza kupata ushahidi wa kuwapo kwa marejeo ya bajeti kwa kiasi kilichotumika nje ya makisio," alisema

Vyama vya siasa


Kuhusu ukaguzi wa vyama vya siasa, CAG alisema hadi kufikia Juni, 2013 vyama 21 wakati vinakaguliwa, ni 12 tu ndivyo vilivyowasilisha taarifa za hesabu.Alisema kati ya vyama 12, tisa havikuwasilisha taarifa za hesabu ambavyo ni UPDP, Tadea, UDP, Demokrasia Makini, Chausta, DP, Jahazi Asilia, AFP na CCK.

Alisema katika ukaguzi huo, ilibainika kuwa vyama sita vya siasa vilipata hati ya shaka ambavyo ni CCM, Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi, TLP na Chauma na vya vingine vilipata hati mbaya ambavyo ni NRD, UMD, ADC, APPT, NLD na SAU.

Alishauri Msajili wa Vyama vya Siasa akishirikiana na Mhasibu Mkuu wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA), waandae mwongozo wa aina ya muundo wa taarifa za fedha utakaotumiwa na vyama vyote vya siasa.

Bajeti

Kuhusu bajeti, alisema tathmini waliyofanya kuhusu utekelezaji wa miradi ya maendeleo, programu na shughuli nyingine za maendeleo katika baadhi ya halmashauri, imeonyesha kuwa hadi kufikia Juni 30, mwaka jana, halmashauri hizo zilikuwa na bakaa ya jumla ya Sh29.2 bilioni sawa na asilimia 28 ya jumla fedha zilizotolewa.

Alisema kubakia kwa kiasi kikubwa cha fedha bila kutumika katika utekelezaji wa miradi kunatokana na ucheleweshaji wa kutuma fedha katika halmashauri.

Deni la Serikali

Alisema hadi kufikia Juni 30, mwaka jana, deni la mifuko ya hifadhi ya jamii lilikuwa limefikia Sh1,699 milioni na Sh975.1 milioni zilipaswa kuwa zimereshwa, lakini hadi wakati wa kuandika ripoti hiyo zilikuwa bado hazijalipwa.

Alishauri mifuko na Serikali kuzingatia na kufuata mwongozo wa uwekezaji wa fedha za mifuko ambao pamoja na mambo mengine, unatoa ukomo wa aina za mali ambazo mifuko inaweza kuwekeza.

Chanzo. Mwananchi.
 
Back
Top Bottom