Wataalam wa umeme hii haiwezekan

Wataalam wa umeme hii haiwezekan

JO MAIKO

Member
Joined
Sep 4, 2011
Posts
22
Reaction score
1
Wataalam wa umeme na wenye ufaham juu ya umeme kuna kitu kinaniumiza kichwa kidogo ningeomba mtegeu kitendawi hicho ndani ya kichwa changu.

Je haiwezekan nikatumia umeme kwa kuunganisha waya wa LIVE na waya wa EARTH ili utumike kama NEUTRAL??
Kama haiwezekan ni kwanin haiwezekan wakati ukigusisha waya wa live na earth kunakuwa na short??

Nawasilisha kwenu wataalam??
 
Kiukweli inawezekana 100%. Ukiwa na live ukafunga kweye bulb kwenye terminal moja na termina nyingine ukaunga earth wire taa itawaka kama kawaida. Neutral ni mrejesho wa umeme uliotumika kukamilisha mzunguko.
 
Ni kweli itawezekana, maana hata neutral iko grounded nadhani kwenye transformer. Ila lazima uelewe kuwa kazi ya neutral ni kukamilisha circuit na kazi ya earth ni kumlinda binadamu asipigwe na shoti.
Elewa kwamba utakuwa umevunja sheria na utakua umeondoa ulinzi unaoletwa na earth.
 
Kiukweli inawezekana 100%. Ukiwa na live ukafunga kweye bulb kwenye terminal moja na termina nyingine ukaunga earth wire taa itawaka kama kawaida. Neutral ni mrejesho wa umeme uliotumika kukamilisha mzunguko.

ok kama inawezekana inaweza kupiga kazi fresh mpaka kiwango gan??

Mim niliwah jaribu hiyo kitu lkn ilikuwa inajizima kwenye circuit breaker. Je hapo tatizo ni nin??
Na unaweza ukawasha tv,fen,taa na redio kwa kutumia style hiyo ya earth wire??

Mkuu hiyo kitu sijui kama itakubali mim kwangu ishanigomea.
 
inawezekana ila haijawekwa kwa matumizi hayo unayoyataka
 
Hili linawezekana ila bulb itakuwa dim. Hii kutokana na resistance kubwa kati ya earth rod ya nyumba na earthing rod ya tanesco transformer, Return current inapitia ardhini badala moja kwa moja kwenye neutral ambayo resistance yake ndogo.
 
Mkuu what are you trying to achieve?
Kitaalamu hayo ni makosa na kama una circuit breaker lazima itakukatalia kwa kuji off
Labda utusaidie mwezetu unalengo gani katika hili
 
Mkuu what are you trying to achieve?
Kitaalamu hayo ni makosa na kama una circuit breaker lazima itakukatalia kwa kuji off
Labda utusaidie mwezetu unalengo gani katika hili

Anajaribu kuiba umeme
 
Ki-kawaida huwezi kupata umeme mzuri kwani una force.ni sawa na kulazimisha binaadamu kuzaa na nyani unaweza ukabahatika lakini mtoto anaweza kuwa hatari kwenu.maana mnakuwa mmeleta chotara mwenye tabia si zake.
 
Kama umeunganisha Live na Ground(jambo ambalo siafiki) ili kulinda Electrical component na mtumiaji ni lazima kuwe na Automatic switch itakayo kata umeme pale tu current ya Ground ikiwa < than current ya live.

hNNduC7ITEIAAAAASUVORK5CYII=

Main switch kadhaa za siku hizizimejengwa na intelligence ndani ukijaribu kuunganisha Live na Neutral circuit breaker inakata kwa sababu ya kukompea Live current agensti ile ya neutral.Kwa lugha nyingineni kwamba Circuit breaker inkuwa imekuzidi akili
 
Kitaalam kazi ya earth ni kumlinda mtumiaji wa kifaa cha umeme. Iwapo panatokea hitilifu/shoti katika kifaa ,umeme unapita kwenye earth badala ya kumdhuru mtumiaji. Lengo la muanzishaji thread la kutaka kutumia earth badala neutral linatia mashaka.
 
Anajaribu kuiba umeme

Na jaribio lake litafeli (halitampa matokeo anayoyapendelea/tarajia) ambacho hajui ni kuwa meter hupima flux flow kwenye waya mmoja i.e live. Shida huongeza uwezo wa kufikiri jinsi ya kikabiliana na hali halisi.
 
Wataalam wa umeme na wenye ufaham juu ya umeme kuna kitu kinaniumiza kichwa kidogo ningeomba mtegeu kitendawi hicho ndani ya kichwa changu.

Je haiwezekan nikatumia umeme kwa kuunganisha waya wa LIVE na waya wa EARTH ili utumike kama NEUTRAL??
Kama haiwezekan ni kwanin haiwezekan wakati ukigusisha waya wa live na earth kunakuwa na short??
Nawasilisha kwenu wataalam??

Inawezekana; lakini kwanini ufanye hivyo? Kazi ya Earth wire inapoungwa na cct breaker inajulikana kuwa ni kwa ajili ya kumlinda binadamu na mali zake in case ikitokea fault. Neutral ni kwa ajili ya
completion of a circuit, inatumika kama return circuirt. Mkuu motive hapa ni kwamba unataka ku-bypass njia ya umeme! Utakamatwa!
 
ok kama inawezekana inaweza kupiga kazi fresh mpaka kiwango gan??

Mim niliwah jaribu hiyo kitu lkn ilikuwa inajizima kwenye circuit breaker. Je hapo tatizo ni nin??
Na unaweza ukawasha tv,fen,taa na redio kwa kutumia style hiyo ya earth wire??

Mkuu hiyo kitu sijui kama itakubali mim kwangu ishanigomea.

Circuit breaker imekudesigned ili kuakikisha kuna complete loop ya current flowing,sasa ulipofanya hivyo kulikuwa na incomplete loop ndio maana circuit breaker ilizima.
 
Ni kinyume na utaratibu. Kwanza tueleze lengo na madhuni yako kabla hatujatoa ufafanuzi zaidi.
 
Okay kama nimekuelewa vizuri! umejaribu kuunganisha wire wa live na earth, unajua matokeo yake ni kutengeneza short-circuit ambayo inasababisha easy flow of current towards the ground (hii inakuonyesha tabia iliyo sawa na wakati wa fault ambazo current kubwa inakuwapo) hivyo circuit breaker lazima lidetect na ku-trip kulinda system yako. Unless, terminal moja unayounga kwenye load ni live wire, na terminal nyingine ya load unaiunga kwenye earth wirre.
 
anachofikiria labda nikugundua circuit nyingine well mkuu hata kina faraday walianza hivo hivo..
 
Na jaribio lake litafeli (halitampa matokeo anayoyapendelea/tarajia) ambacho hajui ni kuwa meter hupima flux flow kwenye waya mmoja i.e live. Shida huongeza uwezo wa kufikiri jinsi ya kikabiliana na hali halisi.

Electric Circuit Theory :

Q1.what happens when you provide a parallel and discrete live wire across meter? 5 marks.
 
Back
Top Bottom