Je, umeme wako (units za luku) unaisha sana? Zingatia yafuatayo

kelphin

JF-Expert Member
Dec 24, 2019
9,120
14,492
Moja ya mambo ambayo yamekua changamoto kwa wadau wengi ni malalamiko juu ya umeme kuisha haraka pasipokujua nini sababu.

Leo kelphin ntakupa au ntakukumbusha jambo moja au zaidi ya kuzingatia. Ikiwa kuna mdau yupo anafahamu zaidi anaweza kuongezea pia.

Vifaa vyote vinavyotumia umeme hupimwa kwa watts. Watts nyingi maana yake kitatumia umeme mwingi kuzidi chenye watts chache.

Hatuongelei ukubwa wa muonekano wa kifaa tunaongelea watts zake..

Hivyo kinaweza kua kidogo kwa umbo ila kikawa kinatumia umeme mwingi kuzidi kile kikubwa kwa umbo.

Watu wengi husema”yaani sina fridge ila umeme wangu unaisha sana”
Wanasahau ya kua fridge za kisasa nyingi sasahivi vinamfumo wa kisasa wakufanya zitumie umeme mchache

Hivyo ununuapo vifaa vyako basi yakupasa sana uzingatie watts zake
Japo kua baadhi ya makampuni huandika uwongo juu ya vifaa vyao
Hivyo unashauriwa kununua vifaa kutoka kwenye makampuni yakuaminika zaidi

LAKINI pia watu wengi hupuuzia earthing ya nyumba zao
Na pengine sio mala moja kupita kwenye nyumba nyingi na kukuta earth wire imekatwa na watoto wala usizingatie.

Ila earth wire inapokatwa hushindwa kukusaidia kulinda vifaa vyako wakati wa mvua na radi bali ku balance utembeaji wa umeme wako pindi waya zako zinapopoteza ubora wake
Hivyo fuatilia earthing system yako
Hakikisha kile chuma kilichofukiwa aridhini kipo na hakijaliwa na kutu.

Kuna muda panya hutafuna waya kisha earth wire inagusana na live wire
Kitu kitakachopelekea earth kubeba umeme na kupeleka aridhini
(Hapa umeme hukimbia pasipo mfano).

Je, utajuaje kama earth yako inatumia umeme wako? Hapa panaitaji utaalamu kidogo. Itakubidi upime voltage kati ya live na earth na hakikisha unapata 220ACV kama upimavyo live na neutral.

Ukiona hupati hivyo Pima neutral na earth ukiona inasoma 220ACV basi jua earth yako inadaka umeme
Shughulikia hilo haraka iwezekanavyo.

Pia tumia njia hi: Zima kila kitu (usichomeke hata charge ya simu)…kisha angalia kama units zako zinapungua, kama ndio basi yawezekana umeme wako unavuja …hivyo ita fundi aangalie mfumo wako wa earth.

Lakini pia kumekua na changamoto kidogo juu ya utumiaji wa umeme juu ya mtu mmoja kwa mwingine kwenye nyumba za kupanga.

Jambo hili yaweza kua vigumu kidogo kulitolea majibu ya mojakwa moja kwakua huwezi jua matumizi ya mtu ndani kwake na suruhisho la jambo hili ni kila mtu kutumia mita yake.

Thus ukipita baadhi ya nyumba watu huvuta mita zao pekee(separation meter)

Ikumbukwe kua kazi ya meter ya Tanesco ni kupima matumizi yako ya umeme kulinganishwa na vifaa vyako
Hivyo vilevile unavyoongeza kuwasha vifaa vyako na kuvitumia kwa muda mrefu ndivyo unavyoongeza ulaji wako wa units zako.

Hivyo unashauriwa kuzima kabisa vifaa vyako pindi uonapo huvutumii(usiweke standby bali vizime kabisa)
Kwakua standby hupunguz tu ulaji na sio kukata 100%.

Lakini pia nkuongezee hili
Meter yako inauwezo wa kupima utumiaji wako wa umeme ..najua yaweza kua hujanielewa hapa.

Kadri unapowasha vitu vyako maana yake basi ndivyo unaruhusu mkondo wa umeme kutembea kwa wingi
Na meta inatambua, hivyo unaweza kuangalia mtililiko wa umeme kwa kuingiza code tu kulingana na meter yako.

Kama meter yako ni EDMI yaani inaanzia 430.. bonyeza 96 then ok
Itasoma current yako. Namba hizo zinakua kubwa kadri ya uwashavyo vifaa vyako na kua ndogo kadri ya uzimavyo vifaa vyako.

Hivyo basi ikiwa utazima kila kitu na kubonyeza 96 then oky na meter yako isiandike 000 basi yawezekana kuna shida kwenye wiring yako.

Nb code hizi hutofautiana kulingana na AINA ya meter yako.

Kwa wale wanaotumia meter za Inhemita yaani zenye 37… tutabonyeza 005 kisha ok

Karibu.
 
Moja ya mambo ambayo yamekua changamoto kwa wadau wengi ni malalamiko juu ya umeme kuisha haraka pasipokujua nini sababu….
Leo kelphin ntakupa au ntakukumbusha jambo moja au zaidi ya kuzingatia….
Ikiwa kuna mdau yupo anafahamu zaidi anaweza kuongezea pia…

Vifaa vyote vinavyotumia umeme hupimwa kwa watts !
Watts nyingi maana yake kitatumia umeme mwingi kuzidi chenye watts chache!
Hatuongelei ukubwa wa muonekano wa kifaa tunaongelea watts zake..

Hivyo kinaweza kua kidogo kwa umbo ila kikawa kinatumia umeme mwingi kuzidi kile kikubwa kwa umbo

Watu wengi husema”yaani sina fridge ila umeme wangu unaisha sana”
Wanasahau ya kua fridge za kisasa nyingi sasahivi vinamfumo wa kisasa wakufanya zitumie umeme mchache

Hivyo ununuapo vifaa vyako basi yakupasa sana uzingatie watts zake
Japo kua baadhi ya makampuni huandika uwongo juu ya vifaa vyao
Hivyo unashauriwa kununua vifaa kutoka kwenye makampuni yakuaminika zaidi

LAKINI pia watu wengi hupuuzia earthing ya nyumba zao
Na pengine sio mala moja kupita kwenye nyumba nyingi na kukuta earth wire imekatwa na watoto wala usizingatie
Ila earth wire inapokatwa hushindwa kukusaidia kulinda vifaa vyako wakati wa mvua na radi
Bali ku balance utembeaji wa umeme wako pindi waya zako zinapopoteza ubora wake
Hivyo fuatilia earthing system yako
Hakikisha kile chuma kilichofukiwa aridhini kipo na hakijaliwa na kutu!

Kuna muda panya hutafuna waya kisha earth wire inagusana na live wire
Kitu kitakachopelekea earth kubeba umeme na kupeleka aridhini
(Hapa umeme hukimbia pasipo mfano)

Je utajuaje kama earth yako inatumia umeme wako?
Hapa panaitaji utaalamu kidogo….
Itakubidi upime voltage kati ya live na earth na hakikisha unapata 220ACV kama upimavyo live na neutral..,
Ukiona hupati hivyo
Pima neutral na earth ukiona inasoma 220ACV basi jua earth yako inadaka umeme
Shughulikia hilo haraka iwezekanavyo..,

Pia tumia njia hi
Zima kila kitu (usichomeke hata charge ya simu)…kisha angalia kama units zako zinapungua
Kama ndio basi yawezekana umeme wako unavuja …hivyo ita fundi aangalie mfumo wako wa earth


Lakini pia kumekua na changamoto kidogo juu ya utumiaji wa umeme juu ya mtu mmoja kwa mwingine kwenye nyumba za kupanga

Jambo hili yaweza kua vigumu kidogo kulitolea majibu ya mojakwa moja kwakua huwezi jua matumizi ya mtu ndani kwake
Na suruhisho la jambo hili ni kila mtu kutumia mita yake!

Thus ukipita baadhi ya nyumba watu huvuta mita zao pekee(separation meter)

Ikumbukwe kua kazi ya meter ya Tanesco ni kupima matumizi yako ya umeme kulinganishwa na vifaa vyako
Hivyo vilevile unavyoongeza kuwasha vifaa vyako na kuvitumia kwa muda mrefu ndivyo unavyoongeza ulaji wako wa units zako…
Hivyo unashauriwa kuzima kabisa vifaa vyako pindi uonapo huvutumii(usiweke standby bali vizime kabisa)
Kwakua standby hupunguz tu ulaji na sio kukata 100%

Lakini pia nkuongezee hili
Meter yako inauwezo wa kupima utumiaji wako wa umeme ..najua yaweza kua hujanielewa hapa

Kadri unapowasha vitu vyako maana yake basi ndivyo unaruhusu mkondo wa umeme kutembea kwa wingi
Na meta inatambua
Hivyo unaweza kuangalia mtililiko wa umeme kwa kuingiza code tu kulingana na meter yako,
Kama meter yako ni EDMI yaani inaanzia 430.. bonyeza 96 then ok
Itasoma current yako
Namba hizo zinakua kubwa kadri ya uwashavyo vifaa vyako na kua ndogo kadri ya uzimavyo vifaa vyako

Hivyo basi ikiwa utazima kila kitu na kubonyeza 96 then oky na meter yako isiandike 000 basi yawezekana kuna shida kwenye wiring yako!!

Nb code hizi hutofautiana kulingana na AINA ya meter yako..

Kwa wale wanaotumia meter za Inhemita yaani zenye 37… tutabonyeza 005 kisha ok



Karibu.
🤝🤝🤝 jf kweli shule


Siku moja home umeme ulikua unaisha balaaa
Tukaita fundi alikuja akaangalia
Kumbe panya walitafuna waya ukagusanisha umeme na kile chuma
Kufukua kike chuma tukakuta chamoto kinoma

Akatengeneza na kubadili chuma pia
Tangu hapo ni safi

Asante mkuu
 
jf kweli shule


Siku moja home umeme ulikua unaisha balaaa
Tukaita fundi alikuja akaangalia
Kumbe panya walitafuna waya ukagusanisha umeme na kile chuma
Kufukua kike chuma tukakuta chamoto kinoma

Akatengeneza na kubadili chuma pia
Tangu hapo ni safi

Asante mkuu

Pole sana…

Karibu
 
Wanasema fridje ukiwasha na kuzima mara kwa mara linakula umeme sasa njia Bora ipi kuwasha Moja kwa moja au
Ndio ukiwasha na kuzima itatumia umeme mwingi kwakua inakua inaanza na upya kuzungusha na kupush gasi
Kuliko ikiwa on inajizima
Ubarid ukipungua inajiwasha kuliko kuanza upya kila wakati
 
Mtaalam naomba ufafanuzi wa Haya maneno

Current na voltage

Nimeona code za kuangalia kwenye remote yangu lkn sijaelewa ninacho angalia
 
Pia tumia njia hi
Zima kila kitu (usichomeke hata charge ya simu)…kisha angalia kama units zako zinapungua
Kama ndio basi yawezekana umeme wako unavuja …hivyo ita fundi aangalie mfumo wako wa earth
Mie pia ni fundi Umeme,njia hii hua naitumiaga mwanzo kabisa nikiwa mbali na mhusika wa jengo,afanye ivyo tena mi namwambia akishazima akae zaidi ya masaa 2 ama 3 zikiwa zikibaki kama mwanzo basi kidogo umeme upo vizuri hakuna mahali panavuja,hapo panabakia tu jambo moja la kupima vitu vingine kama kwenye termination za maungio......
 
Mtaala nisaidie hili juzi Kati TV ilikua imezimwa na socket pia lkn ilipiga radi tv ikaungua” hii InaweZekana ama vijana wamenipa sounds
kwenye tv nashauri uweke tv guard ama stablizer hii ni bora zaidi katika kuilinda tv yako,ukishindwa kupata staibilizer anza na tv guard kuweka madukani ni kati ya elfu 10 hadi elfu 20
 
Mie pia ni fundi Umeme,njia hii hua naitumiaga mwanzo kabisa nikiwa mbali na mhusika wa jengo,afanye ivyo tena mi namwambia akishazima akae zaidi ya masaa 2 ama 3 zikiwa zikibaki kama mwanzo basi kidogo umeme upo vizuri hakuna mahali panavuja,hapo panabakia tu jambo moja la kupima vitu vingine kama kwenye termination za maungio......
Sahihi
 
Back
Top Bottom