Wastegate yalipuka ?

Wastegate yalipuka ?

mshumbue-soi

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2013
Posts
1,842
Reaction score
1,148
Wanajamvi,

Hivi sasa wastagate imelipuka na kutoa moshi mkubwa
Jambo lililostua watazamaji na police walioko nje kupokea maelekezo na kukimbia kwenye maeneo yanayozunguka

Police na magari yakifanya operation kubwa.

Watangazaji wamesema tutazame hawawezi toa maelezo ya kulikoni wanasubiria mamlaka husika itoe taarifa ya mlipuko huo mkubwa.

magari ya kuzima moto na police wanatamka pishapisha

citzen tv live from wastgate
 

Attachments

  • Photo0132.jpg
    Photo0132.jpg
    4.6 KB · Views: 1,498
Yesu alisema Amri Kuu nawaachieni... "UPENDO" uwa namkubali sana huyu Nabii aliona mbali sana. Al Shabaab, Al Qaeda, LRA, Siasa chafu na wengineo ni matunda ya kukosa upendo.
 
ina maana sasa wameamua kujilipua kabisa??
aisee kuna vitu ukijiingiza lazima uwe na akili ya ziada
 
Haijalipuka bali umesikika mlipuko na moshi mzito kutoka ndani na milio ya risasi.
 
hao waisraeli na wamarekani wanafanya nin sasa huko??
 
Hata mi nmeskia al shabaab wamejilipua, ngoja tusubiri ukweli wa mambo
 
Poleni wakenya wote,hizi ndizo gharama za ukarimu wenu,hata TZ zamani wakati wa mapambano ya uhuru kusini mwa Afrika tulionja machungu ya hata kususiwa na nchi marafiki lakini tukabaki salama na msimamo wetu sasa tunaonja mazuri ya kazi ile nanyi siku moja mtaonja matunda ya ukarimu wenu.
 
Siku tatu yaani masaa 72 bado wanapambana...Poleni :- Al-Shabab walifikaje hapo katikati ya Nairobi na Kenya in general maana wameacha mipaka na miji yote na kutinga NBR. itakuwaje Kenya ilidharau ONYO la shabab...? Nasikia CIA FBI na ISRAEL agents wameingia katika uwanja wa mapambano security forces zinashindwa nini na vijana 9 au 10 ...! Halafu tatizo ni mchana kweupe wanashindwa nini ?
 
Hiyo sio picha ya wastegate na haijalipuka bali umesikika mlipuko na moshi mzito kutoka ndani na milio ya risasi. Tuache upotoshani

Sio upotoshaji, umetokea mlipuko mkubwa na baadae moshi kufuatia. Penye moshi, pana moto!!!!! Haijulikani kama wameamua kulipua baada ya vyombo vya usalama vya Kenya kuvamia hiyo Mall au kama vyombo vya usalama ndivyo vimefanya huo ulipuaji.

Tiba
 
Hiyo sio picha ya wastegate na haijalipuka bali umesikika mlipuko na moshi mzito kutoka ndani na milio ya risasi. Tuache upotoshani
Kumbe sio picha ya tukio? Ila nimeskia pia kumelipuka, mayb mleta mada katuwekea hiyo picha kuonesha msisitizo tehteh
 
Yesu alisema Amri Kuu nawaachieni... "UPENDO" uwa namkubali sana huyu Nabii aliona mbali sana. Al Shabaab, Al Qaeda, LRA, Siasa chafu na wengineo ni matunda ya kukosa upendo.

Kweli upendo ungalikuwepo hali hii isingalikuwepo
 
Back
Top Bottom