Wastaafu wa TAZARA wamemkosea nini Mungu?

Mbavu mbili

JF-Expert Member
Apr 25, 2011
1,456
872
Habari, Naandika uzi huu kwa machungu makubwa! Mara nyingi huwa sipendi kuandika andika humu,
Mzeewangu alistaafu kazi katika shirika la reli la Tazara mwaka 2005-
ni miaka 11 mpaka sasa anafuatilia mafao yake pasipo mafanikio yoyote. Wazee hawa wana hali mbaya sana mitaani kwa sasa. Ombi langu kwa wahusika, muwasaidie wazee wetu hawa waliojenga reli hiyoo miaka ya 1970's na kulitumikia Taifa kwa uzalendo na weledi wa hali ya juu.
Binafsi, ninataambua juhudi za serikali ya awamu ya tano katika kusimamia ustawi wa watumishi wake. Ninaomba wahusika waanze na hili, wawakomboe wazee wetu hawa ambao wamekata tamaa kwa hali ngumu ya maisha. Kuna wakati huwa najiuliza Wazee wetu hawa walimkosea nini Mungu?
 
Kujitia Ufahar wakununua mandege yanayosimangwa na kutenga bajeti yakuhamia dom,kulipa madeni ya nje wakati mnadaiwa ndani ni kujitaftia lana.

Kuna kipindi serikal ya chama cha mapinduzi ingejishtukia na kuwalipa hawa wazee wa watu.
 
Nchi hi haiwajali wazee hata kidogo japo wana kauli mbiu yao isemayo "Wazee Kwanza"ila hamna lolote
 
Hivyo Nani Mwenye Wajibu Wa Kuwalipa Hao Wazee, Tazara au Serikali?
 
Wako wale wazee wa EAC pale Mnazi Mmoja....wanatia huruma.Na hawa pia tuwaombee walipwe haki zao
 
Habari, Naandika uzi huu kwa machungu makubwa! Mara nyingi huwa sipendi kuandika andika humu,
Mzeewangu alistaafu kazi katika shirika la reli la Tazara mwaka 2005-
ni miaka 11 mpaka sasa anafuatilia mafao yake pasipo mafanikio yoyote. Wazee hawa wana hali mbaya sana mitaani kwa sasa. Ombi langu kwa wahusika, muwasaidie wazee wetu hawa waliojenga reli hiyoo miaka ya 1970's na kulitumikia Taifa kwa uzalendo na weledi wa hali ya juu.
Binafsi, ninataambua juhudi za serikali ya awamu ya tano katika kusimamia ustawi wa watumishi wake. Ninaomba wahusika waanze na hili, wawakomboe wazee wetu hawa ambao wamekata tamaa kwa hali ngumu ya maisha. Kuna wakati huwa najiuliza Wazee wetu hawa walimkosea nini Mungu?
N ukumbuke wale wa EA COMMUNITY..........Nchi hii ndo maana watu wanaiba,ukishastaaf ww huna thaman unless uwe rais mstaaf, makamo wa rais mstaaf na waziri mkuu mstaaf
 
Mkuu mbavu mbili anko wangu alikuwa mlimba, makambako,mngeta,chita na kisaki kafanya kaz kama injinia akastaafu lakn hadi leo hawajalipwa cjajua serikali yetu inawazaga nin
 
Serikali tunaomba mtambue mchango wa wazee katika mafanikio ya nchi hii mpaka tulipo fikia hapa
 
Wakuu mnaonaje tukiarrange tukakutana tuone jinsi ya kuwasaidia hawa wazee wetu? Na mimi nina uncle wangu alikua Tazara, toka astaafu 2000 huu mwaka wa 16 wanamzungusha tuu, Nssf hawajalipa. Yaani wanateseka mno kisaikolojia. Kama kweli ni haki yao walipwe. Au kama hamna kitu waambiwe tu ukweli.
 
ccm ni majambazi hatari Sana, watanzania tukiondoe hiki chama Kwa nguvu zote.
Ndo wamefungia mafao yote wakitulaghai eti hadi uzeeni.
Uko wapi Mungu wangu usimame na watu wako tunateswa na majahili.
 
Poleni sana Mkuu umenikumbusha wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki (Tanzania, Kenya na Uganda) wastaafu wa Kenya na Uganda wote walilipwa mafao yao na wale Watanzania wakadhulumiwa mchana kweupe na wengine wameshafariki. Hawa haki yao ndiyo imeshapotea, kama nanyi mnasubiri kwa miaka 11 sasa basi uwezekano wa Mzee wako kupata haki yake ni mdogo sana. Inasikitisha na kuumiza sana

Habari, Naandika uzi huu kwa machungu makubwa! Mara nyingi huwa sipendi kuandika andika humu,
Mzeewangu alistaafu kazi katika shirika la reli la Tazara mwaka 2005-
ni miaka 11 mpaka sasa anafuatilia mafao yake pasipo mafanikio yoyote. Wazee hawa wana hali mbaya sana mitaani kwa sasa. Ombi langu kwa wahusika, muwasaidie wazee wetu hawa waliojenga reli hiyoo miaka ya 1970's na kulitumikia Taifa kwa uzalendo na weledi wa hali ya juu.
Binafsi, ninataambua juhudi za serikali ya awamu ya tano katika kusimamia ustawi wa watumishi wake. Ninaomba wahusika waanze na hili, wawakomboe wazee wetu hawa ambao wamekata tamaa kwa hali ngumu ya maisha. Kuna wakati huwa najiuliza Wazee wetu hawa walimkosea nini Mungu?
 
Hivyo Nani Mwenye Wajibu Wa Kuwalipa Hao Wazee, Tazara au Serikali?

Kama Serikali imefikia hatua ya kulipa mishahara ya wafanyakazi wa TAZARA - yaani Management ya TAZARA pamoja na resources walizo achiwa na Wachina za ku generate fedha ya kujiendesha pamoja na kulipa mishahara ya wafanyakazi - TAZARA imeshindwa kabisa ku raise revenue za kuweza kuwalipa mishahara wafanya kazi - siku hizi mishahara inatoka Serikalini wanagharimia Shirika ambalo ambalo uzalishaji wake huko ICU - Serikali inaendelea kulea uzembe.

Sasa wafanyakazi walio staafu kwa nini Serikali aingilii kati ikawalipa mafao yao, wao walistaafu wakati Shirika likiwa linaendeshwa kiufanisi sio sehemu ya ufisadi unao endelee kwenye Shirika lenyewe hivi sasa, sasa kwa nini wawe victim wa circumstances.

Mimi naomba Serikali sikivu ya Dk.Magufuli suala hili iliangalie kwa undani zaidi, wastaafu walipwe mafao yao na kiinuwa mgongo kama Wazambia wanavyo lipwa, hakuna haja ya kuwadhalilisha Wazee - cha ajabu member wa top management ambao wakistaafu wanalipwa kila kitu, je, hizo fedha za kuwalipa viongozi wa ngazi za juu wa TAZARA wanapo staafu zinatoka wapi - kwa nini pawepo double standards kwenye Shirika moja?
 
Poleni sana Mkuu umenikumbusha wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki (Tanzania, Kenya na Uganda) wastaafu wa Kenya na Uganda wote walilipwa mafao yao na wale Watanzania wakadhulumiwa mchana kweupe na wengine wameshafariki. Hawa haki yao ndiyo imeshapotea, kama nanyi mnasubiri kwa miaka 11 sasa basi uwezekano wa Mzee wako kupata haki yake ni mdogo sana. Inasikitisha na kuumiza sana

Mkuu balaa zinazo likumba Taifa zinatikana na laana za kudhulumu wazee/kuwapuuzia mafao yao - hii ni tabia mbaya kabisa, kwa nini tushindwe Serikali za Uganda na Kenya zinazo jali wastaafu wao kwa kuwalipa on time mafao yao yote, hapa kwetu kunani?
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Hakika mwenyezimungu yupo na wenye kusubiri.Viongozi wetu wa dini acheni siasa mutufundishe dini.Tukijuwa dini hakutakuwepo na figisufigisu na hayo mambo ya wastaafu
 
Back
Top Bottom