Wassira: Nitagombea urais 2015

Wassira: Nitagombea urais 2015

Basi hilo litakuwa jinamizi la hatari!. Na ili nisiote hilo lindoto, bora nisilale kabisa. WASSIRA HATAKUJA KUWA RAISI WA NCH YOYOTE DUNIANI!!!!. Take it from me. Hata akihamia chama gani, watakaomwinua lazima wapoteze!!!!!!!!!..

Usiyemtaka ndie atakaye kua mkuu
 
Wasira nae awe rais...hivi ccm mmesahau maneno ya nyerere..."kiongozi bora ni yule asiyetaka kuwa kiongozi"..kauli hii ina maana kubwa sana tofauti na hawa ccm wanavyogombea wenywe kwa wenyewe..nyerere alisema upinzani haupo nje ya ccm bali utakuwa ndani ya ccm sasa nimeanza kuona...yani wanasema kuhusu ukawa istoshe ukawa ipo ndani ya ccm wenyewe..embu wajipime vizuri sio kila mtu anatumia mgongo wa kusema kaombwa na watu wengi hicho sio kigezo cha kuwa kiongozi..tutajuaje waliokuomba ni ndugu zako na sio watanzania wote au ni wale wanaotaka ukiwa rais wapate cheo..embu jichunguzeni kwanza sio kila mtu anafaa kuwa kiongozi kwa kuombwa..halafu wasira mbona hizo sera zako ni weak sana kwa taifa hili yani sijaona kipya na wakati ulikuwa waziri wa kilimo mbona haya yote hukupendekeza zaidi ya kuwa kama waziri pazia tu..sijaona kipya mpaka sasa kwa wagombea wote zaidi ya purukushani na uchu wa madaraka..na wengine ndani ya ccm wanampiga vita lowasa maana wanajua akiwa rais watakiona cha mtema kuni walivyomchongea ajiuzulu uwaziri mkuu
.
 
Wasira hata bungeni hatarudi sasa izo ndoto za urais ni kujitafutia umaarufu tu wa mwisho mwisho

Mkuu hiyo ni njia nyepesi ya kujitoa kiaina kwenye ubunge, maana ameshapima kabisa ndani ya chama hatatoboza kwenye kura za maoni! Kale kabinti kasagaji kamembana mpaka hapumui, huku nje nako Dr. Webiru anamtoa kamasi siyo kidogo, hivyo sokwe anatafuta mlango Wa kutokea!! "SIONGOZWI NA SOKWE MIMI"
 
Ni sheeedah....
1. Katika CCM Mzee wasira ndio kiongozi anayeweza kurudisha mshikamano na umoja ndani ya chama kwa kuwa hana makundi ya kisiasa.
2. Uadilifu wake ni sifa ya kiongozi tunayehitaji kwa sasa ili aweze kusimamia maendeleo ya nchi hii lakini pia kusimamia maadili ya nchi yetu ambayo yamepotoka kwa hali ya juu sana
3. Usafi wake dhidi ya ufisadi ndio silaha tunahitaji kwa kiongozi ajaye ili awe huru na jasiro kupambana na mafisadi na wala rushwa bila aibu kwani atakuwa hadaiwi na mtu na atakuwa hahitaji kumlipa mtu fadhira zozote.
4. Ujasiri wake ndio nguzo katika kutetea na kusimamia amani ya nchi yetu, hatakuwa legelege.
5. Uwezo wake katika masuala ya kiuchumi na mipango ndio tunachohitaji katika kuelekea katika uchumi wa gesi na jinsi ya kusimamia vizuri rasilimali za taifa katika kukuza uchumi.....

Mzee wasira ni mteteZi wa Taifa
Mzee wasira ni mtetezi wa Chama
Mzee wasira ni hazina ya Taifa
Akigombea uraisi atatufaa, tumuombee afya njema na umri mrefu.
 
urais ni taasisi, sio mtu au kakundi ka watu fulanifulani! haya ndo madhara yanayotukumba pindi kakundi fulani kanapomweka kibaraka wao madarakani! viongozi wote wa kisiasa hasa nchi zetu wanafananafanana, wakichaguana ni njia ya kupeana ulaji tu!
 
duh kweli 2015 ni shiiida mpaka huyu mzee anataka uraisi
 
Na mimi nagombea urais kupitia ccm! nina nia ya dhati ya kuleta maendeleo kwa wananchi!
 
Hata kwa dawa siwezi kumpa kura yangu! Mzee kama huyu anataka uraisi ili iweje? hana mawazo mapya kwanza uwezo wa kufikiri nao hana tena!
 
Hata kwa dawa siwezi kumpa kura yangu! Mzee kama huyu anataka uraisi ili iweje? hana mawazo mapya kwanza uwezo wa kufikiri nao hana tena!

Nani anamawazo mapya Mkuu. Mi naona Mara mi huyu Mzee Nchi hoi vyeo vya kupeana.na safar za Rais nje ya nchi zitapungua
 
Ni sheeedah....
1. Katika CCM Mzee wasira ndio kiongozi anayeweza kurudisha mshikamano na umoja ndani ya chama kwa kuwa hana makundi ya kisiasa.
2. Uadilifu wake ni sifa ya kiongozi tunayehitaji kwa sasa ili aweze kusimamia maendeleo ya nchi hii lakini pia kusimamia maadili ya nchi yetu ambayo yamepotoka kwa hali ya juu sana
3. Usafi wake dhidi ya ufisadi ndio silaha tunahitaji kwa kiongozi ajaye ili awe huru na jasiro kupambana na mafisadi na wala rushwa bila aibu kwani atakuwa hadaiwi na mtu na atakuwa hahitaji kumlipa mtu fadhira zozote.
4. Ujasiri wake ndio nguzo katika kutetea na kusimamia amani ya nchi yetu, hatakuwa legelege.
5. Uwezo wake katika masuala ya kiuchumi na mipango ndio tunachohitaji katika kuelekea katika uchumi wa gesi na jinsi ya kusimamia vizuri rasilimali za taifa katika kukuza uchumi.....

Mzee wasira ni mteteZi wa Taifa
Mzee wasira ni mtetezi wa Chama
Mzee wasira ni hazina ya Taifa
Akigombea uraisi atatufaa, tumuombee afya njema na umri mrefu.

Umenena vyema kiongozi, japo wote wanamapungufu lakini huyu anastahil kuwa Rais na Mkt Wa CCM Taifa
 
Mkuu hiyo ni njia nyepesi ya kujitoa kiaina kwenye ubunge, maana ameshapima kabisa ndani ya chama hatatoboza kwenye kura za maoni! Kale kabinti kasagaji kamembana mpaka hapumui, huku nje nako Dr. Webiru anamtoa kamasi siyo kidogo, hivyo sokwe anatafuta mlango Wa kutokea!! "SIONGOZWI NA SOKWE MIMI"

Ulipotokea wewe ndio alipotokea nae rudi kapatazame
 
Basi hilo litakuwa jinamizi la hatari!. Na ili nisiote hilo lindoto, bora nisilale kabisa. WASSIRA HATAKUJA KUWA RAISI WA NCH YOYOTE DUNIANI!!!!. Take it from me. Hata akihamia chama gani, watakaomwinua lazima wapoteze!!!!!!!!!..
Maneno ya hovyo yanayotoka kwa MTU hovyo. Alilopanga Mungu Mwanadamu hana nafasi WASIRA FOR 2015
 
Wasira nae awe rais...hivi ccm mmesahau maneno ya nyerere..."kiongozi bora ni yule asiyetaka kuwa kiongozi"..kauli hii ina maana kubwa sana tofauti na hawa ccm wanavyogombea wenywe kwa wenyewe..nyerere alisema upinzani haupo nje ya ccm bali utakuwa ndani ya ccm sasa nimeanza kuona...yani wanasema kuhusu ukawa istoshe ukawa ipo ndani ya ccm wenyewe..embu wajipime vizuri sio kila mtu anatumia mgongo wa kusema kaombwa na watu wengi hicho sio kigezo cha kuwa kiongozi..tutajuaje waliokuomba ni ndugu zako na sio watanzania wote au ni wale wanaotaka ukiwa rais wapate cheo..embu jichunguzeni kwanza sio kila mtu anafaa kuwa kiongozi kwa kuombwa..halafu wasira mbona hizo sera zako ni weak sana kwa taifa hili yani sijaona kipya na wakati ulikuwa waziri wa kilimo mbona haya yote hukupendekeza zaidi ya kuwa kama waziri pazia tu..sijaona kipya mpaka sasa kwa wagombea wote zaidi ya purukushani na uchu wa madaraka..na wengine ndani ya ccm wanampiga vita lowasa maana wanajua akiwa rais watakiona cha mtema kuni walivyomchongea ajiuzulu uwaziri mkuu
.

Hata yeye alitaka kuwa kiongozi maneno ya zama zile hii no Bongo Digital mkuu
 
kila mgombea atuambie ameifanyia nchi nini mpaka sasa.maana wapo kila siku kwenye sytem.
 
Back
Top Bottom