Muhongo kwa sababau tu tangu kuingia kwake ofisini ameziba mianya ya uchotwaji mkubwa wa pesa za watanzania kupitia sekta ya madini, na sasa mabepari wameungana na wabunge wenye husda kupambana dhidi ya kweli na haki anayosimamia Muhongo.
Kumpoteza Muhongo kwa sababu tu yeye na Katibu mkuu wake Eliakim Maswi, hawana mawasiliano mazuri na Mwenyekiti wa PAC Zitto Kabwe (Hii inatokana na kitendo chao kudhibiti udalali wa Rasilimali).
tInanisikitisha Sana watu wanapokuja na taarifa ambazo zinaandikwa kishabiki na kuwalinda watu. Nasikitika Sana mtu anapofanya personal attack badala ya kufanya mambo kwa kuegemea facts. Kwanza kwa taarifa hii maana yake wamelitukana bunge la jamhuri ya Muungano Wa Tanzania. Unapowatukana PAC maana yake umetukana bunge.
Shaibu SufianiJUMUIYA YA WANAZUONI VIJANA TANZANIA.
MAONI NA MTAZAMO WA JUMUIYA YA WANAZUONI VIJANA TANZANIA KUHUSIANA NA MAADHIMIO YA BUNGE KUHUSU RIPOTI YA CAG YA NOV 26-28.2014
Tunaanzisha sasa hati ya maombi maalum kwa Raais (Petition Form) itakayosainiwa na mamilioni ya watanzania wanaoitakia mema nchi yetu kumuomba Rias apuuze maazimio haya ya mabepari, wahujumu uchumi na wasaka tonge walioungana na wasaka Urais.
Mungu ibariki Tanzania
Mungu wabariki wazalendo na watetezi wa kweli wa Rasilimali.
Imesomwa na
Kaimu Mratibu Umoja wa wanazuoni vijana Tanzania
View attachment 210855 View attachment 210856
wanachuo uchwara wakoje mkuu
nadhani hata kuchaguliwa kusomea kozi za mafuta ni favour walipewa na huyo wanayemtetea,watoe majina yao na kozi wanazosoma ili tuangalie kama walikidhi vigezo vya kupewa hizo scholarship.wanawakilisha wasomi wangapi?wana uhusiano gani na maesrow?
hao misukuke issue ya katiba pendekezi hawakuona mapungufu wanaona mapungufu kwenye hii issue inayomgusa mtu au watu wawili kuliko katiba inayowagusa watanzania wote kwa miongo kadhaa ijayo? Hii elimu ta siku hii balaa sana.
hao ni kweli wanazuoni walioamua kuongea neno ili kuokoa taifa lao lililo kwenye mkwamo unaosababishwa na watu wenye uchu wa rasilimali za nchi hii kama yule mpenda dogodogo
logically kama cag angekuwa ndio final kamati isingeundwa, kama serikali inatoa pesa ya kuendesha bunge na waliridhia kuundwa hiyo kamati na ikawasilisha maana yake serikali inakubali uwepo wa kamati na uwezo wa wahusika!!!!
Ndio maana inaonekana kioja cha mwaka kukubali mchakato halafu majibu yanayotokana na mchakato ulioukubali uanze kukutatanisha!!!
Vyuo vikuu vya kata shida sana.
Sishangai, hawa ndiyo 'wasomi' wa kibongobongo wanaotumia kwato na matumbo kufikiri. Wanafikiri, kuona na hata kuelewa tofauti na binadamu wote! Ni wasomi wa kisisiemusisiemu eti!
Ubongo wa umenunuliwa kwa rupia, vichwani kujazwa tope na kwa fahari wanatetea baba zao.
Walaaniwe sasa had I vizazi 100 vijavyo!