Elections 2010 Wasifu wa Dr. Slaa: Download, SAMBAZA!

Status
Not open for further replies.
Labda wenzangu mnifafanulie kidogo kwa mtazamo wenu.

1. Dr W Slaa anafaa kuitwa Doctor.
wapi kafanya Post Graduate, Masters?

2. najua bila kuna wengi sana humu wa CHADEMA labda wamfikishie ujumbe huu kuwa Utafiti wake katika PhD alifanya khusu nini?

3.mnazionaje hizi degree za st.st.st?

Mbavu zangu mieeeeeeeeeeeeeeeeee!!
 
EDUCATION
International Eye H. Centre Certificate in Eye Health 1993-1993

TransWorld Tutorial College, London Certificate in Management 1985-1985

St. Thomas Aquinas University Advanced Diploma in Rural Development 1980-1981

St. Urban University, Rome PhD (JCD) Law 1977-1981 [Doctor of Canon Law (Latin: Juris Canonici Doctor or JCD)]

Kipalapala Seminary Certificate in Theology 1974-1977
Kibosho Seminary School Certificate in Philosophy 1972-1973

Itaga Seminary School A-Level Education 1970-1971
Dung'unyi Seminary School O-Level Education 1966-1969

Karatu Primary School Primary Education 1962-1965
Daudi Primary School Primary Education 1961-1961
Kwermusl Primary School (Mbulu) Primary Education 1958-1960

EMPLOYMENT HISTORY
Tanzania Society for Blind Managing Director 1992-1998
Tanzania Episcopal Conference Secretary General 1985-1991
Diocese of Mbulu Development Director 1982-1985
Diocese of Mbulu Vicar General 1982-1985
Diocese of Mbulu Development Director 1977-1979
Diocese of Mbulu - Roman Catholic Church Padre 1977-1991

POLITICAL EXPERIENCE

CHADEMA Principal Secretary 2002
CHADEMA Vice Chairman 1998 2002
CHADEMA Member of Parliament (Karatu Constituency) 1995 To date
CHADEMA Member of National Executive Committee 1995 -
Chama Cha Mapinduzi - CCM Secretary Foreign Branch (Rome) 1980 1982
Youth Union -TANU Secretary 1974 1977
TANU Chairman (Kipalapala Branch) 1974 1977

Retrieved on 13/7/2006 - www.parliament.go.tz


Advanced Diploma ya Mwaka Mmoja?!!! Hapa ndipo mnaponichanganya changanya kama sio utani!!!!
 
Sio kudanganya mkubwa ndio wataalamu walioweka vyeo vya kielimu waliamua hivyo. Usidahni Theolojia ni mchezo.

Unaweza kusema kwa nini
Matabibu wa afya ya binadamu wakimaliza degree wanaitwa ma Dr?

Inawezekana upo sahihi lakini uzoefu unaonesha kwamba hata ktk elimu ya sekondari madent wanaongoza kwa kubabua A's na B's za Divinity na hapo ndipo tunapopata mashaka!!!!!! Unakuta mtu ana full F's lakini ana "A" ya Divinity!!!!! isije ikawa na kwenye matheology nako ndo kamchezo kenyewe!!!
 
Labda wenzangu mnifafanulie kidogo kwa mtazamo wenu.

1. Dr W Slaa anafaa kuitwa Doctor.
wapi kafanya Post Graduate, Masters?

2. najua bila kuna wengi sana humu wa CHADEMA labda wamfikishie ujumbe huu kuwa Utafiti wake katika PhD alifanya khusu nini?

3.mnazionaje hizi degree za st.st.st?

Mie sioni kitu hapo, yani advanced diploma to phd directly tena ya different profession, Mhhhh!!!!!!!??????. Weee Kaa chonjo!!!!!!!!

They way I know:
Mtu anaweza kufanya master's by dissertation (yaani no course work) then akifanya vizuri sana akatimiza masharti ya chuo husika plus na akawa amefanya at least one journal paper (article) kwenye accredited journal (sio any conference). Huyo mtu anaweza ku upgrade master's yake na kuwa phd directly kwa kuongezea more research ambayo pia ultimately lazima aproduce journal article katika accredited journal. Huyo mtu hatapewa master's degree tena bali atapewa phd directly. Ila aki fail phd atanyimwa vyote (yaani hapewi master's wala phd).

Ok, Dr. Slaa. Mie sioni kama anafaa kuitwa doctor, nimemtafuta kwenye google scholar sijaona kazi yake hata moja.

Kama ni Dr wa dini sawa kapewa na kanisa. lakini pia alitakiwa awe ame upgrade au alifanya master's b4 that.
So, mbele ya watu wenye PhD asijitape yeye ni doctor tutamtoa nishai.
Mie simchukii naomba tu akipata huo urais tabia za kikaskazini huko kwao aziache zisije kutuharibia nchi. Tunawajua watu wa kaskazini wanapenda sana short cuts za maisha.
 
Mie sioni kitu hapo, yani advanced diploma to phd directly tena ya different profession, Mhhhh!!!!!!!??????. Weee Kaa chonjo!!!!!!!!

They way I know:
Mtu anaweza kufanya master's by dissertation (yaani no course work) then akifanya vizuri sana akatimiza masharti ya chuo husika plus na akawa amefanya at least one journal paper (article) kwenye accredited journal (sio any conference). Huyo mtu anaweza ku upgrade master's yake na kuwa phd directly kwa kuongezea more research ambayo pia ultimately lazima aproduce journal article katika accredited journal. Huyo mtu hatapewa master's degree tena bali atapewa phd directly. Ila aki fail phd atanyimwa vyote (yaani hapewi master's wala phd).

Ok, Dr. Slaa. Mie sioni kama anafaa kuitwa doctor, nimemtafuta kwenye google scholar sijaona kazi yake hata moja.

Kama ni Dr wa dini sawa kapewa na kanisa. lakini pia alitakiwa awe ame upgrade au alifanya master's b4 that.
So, mbele ya watu wenye PhD asijitape yeye ni doctor tutamtoa nishai.
Mie simchukii naomba tu akipata huo urais tabia za kikaskazini huko kwao aziache zisije kutuharibia nchi. Tunawajua watu wa kaskazini wanapenda sana short cuts za maisha.

mkuu mbona unauwa kipindi cha lala salama hiki...
 
chekecha medula,you will know the truth and if you don't want it you are killing yourself
 
Labda wenzangu mnifafanulie kidogo kwa mtazamo wenu.

1. Dr W Slaa anafaa kuitwa Doctor.
wapi kafanya Post Graduate, Masters?

2. najua bila kuna wengi sana humu wa CHADEMA labda wamfikishie ujumbe huu kuwa Utafiti wake katika PhD alifanya khusu nini?

3.mnazionaje hizi degree za st.st.st?

Kwahiyo una-question integrity ya chuo kilichompa PhD Dr. Slaa?? Anyway, tangu lini mtu akapewa PhD bila kufanya utafiti??? Ukiona ni PhD Holder ujue utafiti alifanya, otherwise asingepewa.... Labda nikuulize, unadhani kati ya Dr Slaa na Dr. JK ni yupi msomi wa ukweli???

Hebu tupe vigezo vya kukidhi ili upewe PhD please (in your understanding)

Eagerly waiting for your response mdau
 
Mnao hangaika na elimu ya dk. Slaa mnajua ni nini kinasomwa ktk seminari nilizoziorodhesha hapa chini?

Kipalapala Seminary Certificate in Theology 1974-1977

Kibosho Seminary School Certificate in Philosophy 1972-1973

kwa kuwasaidia tu kwani naona hamuijui elimu ya seminari kuu. ukimaliza form 6 unaingia course ya mwaka 1 (certificate in philosophy). Then ukifaulu unaanza certificate in theology for 3 yrs na kwa mfumo wa seminary this is more than master degree.

Kwa hiyo kama unasoma ktk mfumo wa shule za kawaida ndo utakuta hizo masters n.k. na wapo mapadre waliosoma pia ktk mfumo wa shule za kawaida.

Kwa dk. Slaa hiyo ni system ya kiseminari kwa hiyo baada ya kusoma miaka 4 after A-level, you go straight to doctorate. Kama mtu anashaka na chuo alicho soma check kwenye mtandao ujiridhishe.


Ndugu wana JF, mimi nimesoma pia seimnari kuanzia mwanzo hadi mwisho na hivyo naweza kuchangia vizuri zaidi kwa hili kwa wale wenye mashaka.

Kuna seminari ndogo (minor seminary) – kinachofundishwa ni elimu ya sekondari na maadili na seminari kuu (major seminary: university level) – kinachofundishwa ni falsafa/teolojia na vilevile maadili.


Ili mtu ajiunge na major seminary,



Anatakaiwa amalize elimu ya sekondari (kidato cha sita) na awe amefaulu vizuri. Kuna mashirika ndani ya Kanisa Katoliki kama vile Wamisionari wa Afrika (White Fathers) au Jesuits miaka ya 1970 hadi 1990 walikuwa wanapokea tu wenye division I au II (baadaye waliweza kuruhusu division III kwa wale wanaochukua masomo ya sayanzi) ili kwenda kuanza falsafa na teolojia. Nia ni kupata watu wenye uelewa mzuri ili watakapofundishwa mambo magumu wasiharibikiwe - maana kwenye falsafa na hata teolojia wanafunzi wanafundishwa kukuza udadisi na kuhoji vitu 'critical thinking' na reasoning. Kuna baadhi ya wanafunzi wanapoteza imani kabisa baada ya masomo yao ya falsafa na ndiyo maana kinachosisitizwa katika masomo ni uelewa mzuri na 'good judgement'.
  1. Msomo ya falsafa siku hizi ni miaka 3 na mtu akimaliza anapata degree ingawa baadhi ya vyuo wanaweza kutoa certificate (kama enzi za Dr Slaa) au diploma lakini kwa kawaida ni equivalent na degree kwa kila namna: kuanzia qualifications, walimu wanaofundisha na syllabus husika. Kuna 'classmate' wangu alichaguliwa kwenda kusoma falsafa Uganda na alipomaliza alipata BA wakati wale waliosoma Tanzania darasa lilelile wao walipata diploma. Lakini hawa wa Tanzania walionekana wako 'more advanced' na walipoendelea na masamo ya juu nje hatimaye wote walipata degrees zinazofanana.
  2. Masomo ya teolojia ni miaka 3 pia - kuna vyuo kama umemaliza falsafa, unapohitimu teolojia unapata masters. Vyuo vingine wanakupa tu BA na vyuo vingine wanaangalia masomo, jinsi mtu alivyofaulu na anavyoendelea kufaulu vizuri kwa miaka aliyotumia na kufanya 'accreditation'.
  3. Binafsi nilisoma Missionary Institute London (MIL) iliyokuwa affiliated kwa universities 2: Middlesex University (London) – three years & Louvain University (Belgium) – four years. Darasa letu baadhi ya wanafunzi walikuwa wanachukua masomo chini ya Louvain University na pass mark yao ilikuwa 60%. Mimi nilikuwa nachukua masomo yaliyofuata syllabus ya Middlesex University na pass mark yetu ilikuwa 41. Ili mtu apate first class haikutosha tu apate mfano 90% - ilibidi pia akidhi vingezo vya 'award panel' kuona kama anafaa kupata first class (licha ya kuwa na mark ya juu na walikuwa wanaangalia 'progressive performance' ya mtu kuanzia mwaka wa 1).
  4. Kwa upande wa Dr Slaa, baada ya kumaliza falsafa na teolojia, ingawa kwa wakati aliosoma walikuwa wanachukua miaka 2, anakuwa sawa na mtu aliye na masters kwani haiwezekani mtu aliyesoma chuo 1972-1977 (yaani miaka 5 - falsafa & teolojia - kwa level ya university) halafu apate certificate sawa na mtu anayefanya kozi ya miezi 9. Kinachoangaliwa ni masomo na credits alizo'cover' na kufaulu. Ninavojua Dr Slaa alipata first class katika masomo yake ya teolojia na pia PhD wakati masomo yao ni magumu mno (unatakiwa u'cover' vitu vingi na kwa muda mfupi).
  5. Baadhi ya wana JF hawajui kinachofundishwa katika falsafa na teolojia na ndio maana wanadhani ni elimu ya hivihivi tu. Kinachofundishwa falsafa na teoljia ni kujenga ‘thinking & reasoning capacity' ili mwanafunzi aweze kujifunza na kuelewa vizuri na baadaye aweze kufanya kazi yake sehemu yoyote na watu wa aina yoyote wasomi na wasio wasomi. Of course, baada ya falsafa na teolojia, kuna wale wanaofanya 'specialisation' katika branch mojawapo:
i.Wanaojifunza Biblia wanasomea maandika matakatifu na wanaitwa biblical scholars – hawa wanajifunza kwanza lugha za asili kama Hebrews, Greek & Aramaic na exegesis pamoja na archaeology na mara nyingi ni wataalamu wa lugha, historia, geographia na maandiko matakatifu.

ii.Wanaochukua falsafa proper wana'specialise' katika logic & language, anthropology, epistemology, metaphysics, philosophy of sciences au political philosophy.

iii.Wengine wana'specialise' Islamology, Arabic Language & culture.

iv.Wanaochukua Code of Canon Law – wana'specialise' katika canon law and law in general.

v.Kuna wengine wanaenda ku'specialise' katika psychology, counselling, medicine, international relations & peace processes, LLB etc.

Kwa hiyo, ndani ya Kanisa Katoliki kuna wataalamu wa kila aina na karibu katika kila kitu.


Falsafa inayofundishwa katika vyuo vya Kanisa Katoliki ina masomo yafuatayo au zaidi:

a) A history of philosophy (history of over 200 philosophers & where they were born, what they studied & got their ideas from - kuanzia poets kama Homer about (850 BC) & Hesiod (750 BC) to contemporary philosophers & political thinkers - including African philosophers).

b) Systematic philosophy: philosphical anthropology, psychology, philosophical ethics, political philosophy, natural philosophy, logic & language, epistemology, metaphysics/ontology, philosophy of sciences, Marxism-Leninism etc.

c) Study methodology.

d) Research paper/dissertation.

6. Katika teolojia: kuna masomo kama moral theology (concept of right & wrong including moral dilemmas - masturbation, genetic engineering & human cloning, capital punishment, homosexuality, contraception, suicide, sexuality, pre-marital sex, abortion, euthanasia, just war & pacifism - introduction to canon law (concept of law and how it came about, how it differs from civil law) & canon law of marriage, sexual ethics, bioethics, fundamental theology, human development, world religions (Judaism, Christianity, Islam, Hinduism, Shintoism, African traditional religions, Taoism, Confucianism, Buddhism, Sikhism etc), political theology (human rights, peace building, non-violence etc), sacraments, inclulturation, natural theology, positive theology, social & cultural anthropology, initiation, reconciliation, justice & peace (social justice) Church & Ministry, counselling, economic theology & structures, environemtal theology, public speaking & preaching... study methodology, research paper/dissertation.

7. Mtu akimaliza masomo yote haya, ambayo ni kati ya miaka 7-10 kutegemea na chuo mtu alipo, anapata BA, MA or equivalent na kwa kawaida huwa ameiva kwelikweli kimaarifa. Mtu kama huyo akienda vyuo vingine, kinachoangaliwa ni masomo aliyokwisha jifunza, credits alichukua na alama alizofaulu ili kuona kama kulingana na chuo alichosoma awali anaweza kupata 'accredition' au la.

8. Baada ya masomo haya ambayo ndiyo basic ili mtu awe padre, wengine wanaweza kuendelea na masomo ya juu kwa ngazi ya ‘specialisation'. Mfano, Dr Slaa yeye alichukua Canon Law (na husomi tu canon law bali pia namna gani inafanana au kutofautiana na sheria za nchi). Kwa hiyo, Dr Slaa licha ya kuwa amebobea katika falsafa proper, anajua pia teolojia na ni mtaalamu wa sheria (canon law & na ana uelewa wa LLB kulingana na interrelationship and use of legal jargons). Ana advantage zaidi kwa maana kwamba anajua mambo mengi zaidi na kwa kitaalamu kuliko mtu anayemaliza PhD UDSM, UDOM au hata London University.

Kwa vile watu wengi hawajui, wanatilia mashaka usomi wake. Nilishauliza siku moja ni kipi kinafundishwa mfano UDSM kwa level ya PhD, ambacho Dr Slaa hakujifunza au hana au hajui? Kwa wale wasiomjua Dr Slaa: the guy is knowledgeable! Nenda fanya naye interview ndipo utakajua kuwa anajua.


PhD requirements:
The detailed requirements for award of a PhD degree vary throughout the world. In some countries (the US, Canada, Denmark, for example), most universities require coursework in addition to research for PhD degrees. In many other countries (such as the UK) there is generally no such condition. It is not uncommon, however, for individual universities or departments to specify additional requirements for students not already in possession of a master's degree or equivalent or higher.

This process differs greatly from other Doctor degrees such as the Juris Doctor JD or the Medical Doctor MD. The PhD may be earned in as little as 60 credits while the JD requires 85 credits and the MD requires about 90 credits.

In countries requiring coursework, there is usually a prescribed minimum amount of study - typically two to three years full time, or a set number of credit hours - which must take place before submission of a thesis. This requirement is usually waived for those submitting a portfolio of peer-reviewed published work. The candidate may also be required to successfully complete a certain number of additional, advanced courses relevant to his or her area of specialisation.

A candidate must submit a thesis or dissertation consisting of a suitable body of original academic research, which is in principle worthy of publication in a peer-refereed context. In many countries a candidate must defend this work before a panel of expert examiners appointed by the university; in other countries, the dissertation is examined by a panel of expert examiners who stipulate whether the dissertation is in principle passable and the issues that need to be addressed before the dissertation can be passed.

Universities in the non–English-speaking world have begun adopting similar standards to those of the Anglophone PhD degree for their research doctorates.

A PhD student or candidate is conventionally required to study on campus under close supervision. With the popularity of distance education and e-learning technologies, some universities now accept students enrolled into a distance education part-time mode.

http://en.wikipedia.org/wiki/Doctor of Philosophy
 
Kwahiyo una-question integrity ya chuo kilichompa PhD Dr. Slaa?? Anyway, tangu lini mtu akapewa PhD bila kufanya utafiti??? Ukiona ni PhD Holder ujue utafiti alifanya, otherwise asingepewa.... Labda nikuulize, unadhani kati ya Dr Slaa na Dr. JK ni yupi msomi wa ukweli???

Hebu tupe vigezo vya kukidhi ili upewe PhD please (in your understanding)

Eagerly waiting for your response mdau

Swali ni alifanya utafiti kwenye maneo gani?
 
Kipalapala Seminary Certificate in Theology 1974-1977
Kibosho Seminary School Certificate in Philosophy 1972-1973
Jamani kama hatuelewi ni bora tukae kimya. Hapa kwetu shule za kawaida utasoma miaka 6 upewe certificate tu? Hizo ni zaidi ya certificate, lazima tuzingatie na contents plus duration
 
Mwenyewe ameandika kuwa Kipalapala na Kibosha amefanya Certificates.
Ni vipi certificates zikawa sawa na Degree au Masters. hapa naomba ufafanuzi zaidi nijiridhishe.

Na vipi ile Segerea Senior Seminary wanatoa nini kule?

Nadhani zamani (enzi hizo) Kibosho, Ntungamo, Peramiho & Kipalapala walikuwa wanatoa certificates kwa vile walikuwa bado kwenye process ya 'affiliation' kwa St Urban University. Nchi nyingine kama Ghana na Nigeria na hata Ulaya wanafunzi wao walikuwa wanapata degree moja kwa moja japo syllabus ni ileile katika minor & major seminaries zote.

Ndiyo maana unakuta mtu anasoma miaka kama saba hivi halafu anapata certificate. Siku hizi wanatoa degree. Vyuo vingi vimebadilisha mfumo wa award na kuwa affiliated na vyuo fulani fulani ambavyo ni very reputable kama Louvain University au St Urban in Rome.

Chuo nilichosoma mimi (Uingereza) kilikuwa kinaitwa Missionary Institute London (MIL) na tulikuwa affilliated kwa universities 2: kuna wanafunzi waliokuwa wanachukua masomo kwa kufuata syallus ya Louvain University (Belgium) - miaka 4 na wengine Middlesex University (London) - miaka 3.

Cha msingi ni kwamba mfumo wa kumkubali mtu kufanya PhD unatofautiana kutoka nchi na nchi kulingana na utaratibu wa chuo husika. Kama wanaotilia mashaka PhD ya Dr Slaa wataleta uthibitisho kuwa kuna 'uniform requirements' na au Dr Slaa haku'qualify' kupata PhD, watakuwa wamejenga hoja nzuri kuliko kujadili kitu 'out of ignrance'. Na hii ni hatari sana maana inaonesha tu jinsi watu walivyozoea majungu na siyo hoja za msingi! Tunasubiri wanaotilia mashaka walete uthibitisho ni kwa jinsi gani PhD ya Dr Slaa siyo PhD.
 
Hivi vielimu vya Slaa me sivielewi kabisa ! bora jamaa aliyemfananisha na Dr Remmy ! sijaona kitu masters wala kinachofanana na Masters ! halafu CV ni ndogo mno maana maisha yake yote amepata experience mbulu.
 
tuache kudanganyana Dr slaa hana masters na wala huwezi kulinganisha certificate ca theology na masters , nazani hata wewe hujui tofauti ya masters na certificate, nani alikwambia certificate kuna research?
huyu hana sifa ya kuwa Dr labda kwa mambo yao ya dini.

Kwa nini uongee tu bila uthibitisho? Kuwa na mdomo siyo maana yake kuongea tu bali kujenga hoja na kuweza kuisimamia. Sasa jenga hoja na kuisimamia kwa ku'analyse' alichosoma Dr Slaa na uoneshe kuwa he's totally ignorant or incapable of addressing economic issues within or outside the country. Na siyo kusema tu kama mwenda wazimu!
 
Advanced Diploma ya Mwaka Mmoja?!!! Hapa ndipo mnaponichanganya changanya kama sio utani!!!!

My God! Hata kuhesabu hujui? Ukianza masomo Jan-Nov 1980 halafu ukianza tena Jan-Nov 1981 ni mwaka mmoja? Utaratibu wa kuanza muhula wa masomo ni tofauti kutoka nchi moja hadi nyingiine. Mfano, mke wangu alisoma Cambridge na kupata international diploma ndani ya miezi tisa wakati kuna rafiki yangu alipata diploma ya falsafa kwa miaka 3. Unaweza kueleza kwa nini?
 
unajua hivi karibuni nilikutana na wanawake eti wanasema JK ndo anfaa kutuongoza kwakuwa ni HB,

Yaani kidogo nilie
 
Mie sioni kitu hapo, yani advanced diploma to phd directly tena ya different profession, Mhhhh!!!!!!!??????. Weee Kaa chonjo!!!!!!!!

They way I know:
Mtu anaweza kufanya master's by dissertation (yaani no course work) then akifanya vizuri sana akatimiza masharti ya chuo husika plus na akawa amefanya at least one journal paper (article) kwenye accredited journal (sio any conference). Huyo mtu anaweza ku upgrade master's yake na kuwa phd directly kwa kuongezea more research ambayo pia ultimately lazima aproduce journal article katika accredited journal. Huyo mtu hatapewa master's degree tena bali atapewa phd directly. Ila aki fail phd atanyimwa vyote (yaani hapewi master's wala phd).

Ok, Dr. Slaa. Mie sioni kama anafaa kuitwa doctor, nimemtafuta kwenye google scholar sijaona kazi yake hata moja.

Kama ni Dr wa dini sawa kapewa na kanisa. lakini pia alitakiwa awe ame upgrade au alifanya master's b4 that.
So, mbele ya watu wenye PhD asijitape yeye ni doctor tutamtoa nishai.
Mie simchukii naomba tu akipata huo urais tabia za kikaskazini huko kwao aziache zisije kutuharibia nchi. Tunawajua watu wa kaskazini wanapenda sana short cuts za maisha.

Of course, huoni kitu kwa vile PhD hujui vyuo mbali mbali vinatoaje PhD zao na kwa vigezo gani. Kwa akili yako mtu akisoma miaka 5 (1972-1977) at university level huwa ni sawa na certificate?
 
Angalizo:

Ahadi ya Dr. Slaa na CHADEMA ni Elimu bure hadi kidato cha Sita na si Chuo Kikuu (Mlimani). Free hadi Mlimani ni CUF.

Kutaja "Wahindi" sounds ubaguzi. Simply say wawekezaji wabovu wasio na uwezo. wako wengi hawa: Wazungu, Waasia, na hata Waafrika.

Si kweli ahadi za 2005 za CCM hazijatekelezwa, baadhi zimetekelezwa. Ila Maisha Bora kwa kila Mtanzania haijatimia.

Mafisadi 11 hawakutajwa Mnazi Mmoja, ilikuwa Mwembe Yanga Temeke.

Hayo machache ni kuweka records sawa tu. Mengine yako poa.

Mahakama ya kadhi nayo bado kuitafutiwa ufumbuzi (CCM manifesto 2005-2010) au ilikuwa namna ya kupata kura?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom