Wasifu(CV) wa Tundu Lissu

Wasifu(CV) wa Tundu Lissu

Wakawaida sana huyu jamaa!

Sent using Jamii Forums mobile app
Nigependa nikusikie ukiwaambia Lumumba mkiwa chamber.Halafu usikie watakavyokubana na kukukwambia ukathibitishe kuwasaidia mkabili. Kwa taarifa yako wanyama wengi wakimkuta simba kalala huwa wanadhani ni woga wao tuu sio mnyama wa kutisha.
 
Mbona CV nyepesi sana hii. Labda kwa wewe usiyepata Shahada ya Uzamili!
Mkuu ongeza madude hapo. Amesimamia kesi ngapi na kashinda ngapi!
Nyepesi mno, ya kawaida sana aise...kuna watu wanauza mahindi ya kuchoma kwa CV ka hiii
Aweke CV kama hii...hapo tuta BOW..
 

Attachments

Na mbwembwe zote Lissu hana PhD? Au press conference anazo fanya ni za kukusanya data na kufanya analysis ya dissertation ya hiyo PhD - sisi tunadhani ni siasa kumbe yupo darasani. Maana mimi siamini kama wafuasi wake wanavyosema ni msomi na ana masters tu? Tanzania ndio maana IQ wamesema wanazidiwa na Uganda na Kenya. Masters ni kitu kidogo - tena ukute ni ya kufundishwa darasani! Siyo by research! Elimu hiyo haitoshi ajiendeleze.

..kinachomuinua Lissu akawazidi hata wenye PhD ni wito na ujasiri alionao ktk kutetea haki na utawala wa sheria.

..Lissu hahitaji kuongeza shahada nyingine. Jamii yake inamhitaji kama mtetezi wa haki za wanyonge wa nchi hii.
 
..kinachomuinua Lissu akawazidi hata wenye PhD ni wito na ujasiri alionao ktk kutetea haki na utawala wa sheria.

..Lissu hahitaji kuongeza shahada nyingine. Jamii yake inamhitaji kama mtetezi wa haki za wanyonge wa nchi hii.
Mtetezi wa tumbo lake tu. Mbona Lema hakumtoa kwa wakati? Mbona hatetei Ruzuku ya CDM itumike vizuri angalau hata kujenga Ofisi ya Makao Makuu ya CDM?
 
Hii ndio CV (curriculum vitae) ya kamanda Tundu Lissu

Full Name: Tundu Antiphas Mughwai Lissu

Member Type: Elected Member

Constituent: Singida Mashariki

Political Party: Chama cha Demokrasia na Maendeleo

Office Location: Box 21746, Dar Es Salaam

Office Phone: +255 22 2780859/+255 754 447323/+255 786 572 571

Office E-mail: tlissu@parliament.go.tz

Date of Birth: 20 January 1968

EDUCATION

Mahambe Primary School:
CPEE (1976 - 1982) - Primary School

Galanos Secondary School:
ACSEE (1987 - 1989) - Secondary School

Ilboru Secondary School:
CSEE (1983 - 1986) - Secondary School.

University of Dar Es Salaam:
LLB (1991 - 1994) Bachelor's Degree

University of Warwick, UK:
LLM (1995 - 1996) - Masters Degree

EMPLOYMENT HISTORY
Member of The Parliament of Tanzania:Singida West Constituency (2010 - 2015)

Lawyers' Environmental Action Team (LEAT)😀irector of Researcher (2003 - 2008)

The World Resources Institute (WRI), USA:Researcher (1999 - 2002)

Lawyers' Environmental Action Team (LEAT) Researcher (1998 - 1999)

D'Souza Chambers:Advocate (1994 - 1997)

Bondeni Secondary School:Teacher (1990 - 1991)

POLITICAL EXPERIENCE
CHADEMA😀irector of Law (2004 - To Date)

NCCR-Mageuzi:Member of Parliament Candidate (1995)

MR TUNDU LISSU.jpg

Mwanasheria Mbunge wa Chama Cha Chadema Mr Tundu Lissu je ni nani?

1. Je Wajua Tundu Lissu Aliwatoa Gerezani BURE
Wananchi 466 Wa Tarime Waliofungwa Kwa
Kupinga Mwekezaji Asiwanyanganye Ardhi Yao?

2. Je Wajua Tundu Lissu Alishawai Kupigwa
Marufuku Asikanyange Nyamongo Kwasababu Ya
Harakati Zake Za Kuwatetea Wananchi Dhidi Ya
Wawekezaji?

3. Je Wajua Tundu Lissu Alipambana Na Kaka
Yake Alute Lissu Mahakamani Kwenye Kesi Ya
Kupinga Ubunge Wa Lema, Alute Akiitetea CCM Na
TL CHADEMA?

4. Je Wajua Tundu Lissu Akiwa JKT Itende
Alidhaniwa Kuwa "Usalama Wa Taifa" Kutokana Na
Tabia Yake Ya KUHOJI Bila Woga?

5. Je Wajua Tundu Lissu Alipambana Na Serikali
Ya Mkapa ISIUZE Rufiji Delta Kwa Mwekezaji Nolan,
Hadi Bank Ya EIB Ikagoma Kutoa Mkopo Kwa
Nolan?

6. Je Wajua Mwaka 2004 Freeman Mbowe
Alimuomba Tundu Lissu Ajiunge CHADEMA Baada
Ya Kumtetea Chacha Wangwe Kwenye Kesi 10 Za
Jinai?

7. Je Wajua Tundu Lissu Alianza Kushtakiwa Kwa
"Uchochezi" Mwaka 2001 Na Mpaka Leo Hajawai
Kukutwa Na Hatia?

8. Je Wajua Kwenye Kampeni 2010 Kikwete Aliwai
Kusema Ni Heri Dr.Slaa Awe Rais Kuliko Tundu
Lissu Awe Mbunge?

9. Je Wajua 70% Ya Kesi Anazozisimamia Tundu
Lissu Halipwi Chochote Na Watu Anaowatetea,
Yeye Hufurahi Akiona Mtu Haonewi Wala
Kunyanyaswa?

10. Je Wajua Tundu Lissu Hutumia Mshahara Wake
Wa Mbunge Kusafiri Maeneo Mbalimbali Nchini
Kuwatetea Walalahoi BURE Mahakamani?
*TUENDELEE KUMUOMBEA JEMEDARI HUYU*
 
Je wajua ????
Lissu alizaliwa tarehe 20 Januari 1968 na alisoma shule ya msingi Mahambe, Singida. Katika miaka yake yote saba shuleni hapo, Lissu hakukubali hata mara moja kuamka alfajiri saa 11 kuwahi namba na daima aligomea kulima mashamba ya walimu, kuwachotea maji na kazi za namna hiyo kwani kwake aliona haziko sahihi. Hii ilipelekea awe anatandikwa bakora mara kwa mara. Shuleni hapo, bakora na mwili wa Lissu vilikuwa ni kama uji na mgonjwa. Hata hivyo, kilichomsaidia ni akili yake. He was a very, very brilliant pupil.

Lissu alifaulu mtihani wa darasa la saba na kwenda shule ya sekondari ya Ilboru, Arusha. Shuleni hapo, yeye ndie aliyekuwa mwanafunzi mdogo kuliko wote. Licha ya udogo wake, alikuwa mwiba mkali kwa prefects na walimu. Akiwa kidatu cha tatu wenzake walimtaka awe prefect lakini alikataa kwani alizoea kuwaita "manyoka" kwa tabia yao ya kupenda kupeleka taarifa za wanafunzi kwa walimu.

Lissu alifaulu vizuri na kuingia kidato cha tano shule ya sekondari ya Galanosi, Tanga. Akiwa Galanosi, akapewa Uenyekiti wa Kamati ya Taaluma. Hata hivyo, akakorofishana vibaya mno na mwalimu wa taaluma na kuvuliwa cheo hicho.

Akiwa kidato cha sita mwaka 1988, kulikuwa na disko la graduation. Kidato cha sita wakaruhusiwa kwenda kucheza na Korogwe girls lakini kidato cha nne wakakataliwa na wakaambiwa wataletewa taarabu shuleni hapo. Lissu aliona huo ni uonevu na daima shuleni hapo alichukia mno mwanafunzi mwenzake kuonewa hata kama ni wa madarasa ya chini. Hivyo, akaandika Waraka "TAARAB FOR WHOSE INTEREST". Lissu hakuandika jina lake kwenye Waraka huo. Akaubandika kwenye ubao wa matangazo usiku. Walimu walipouona walichukia sana na wakachunguza na kuhisi mwanafunzi pekee aliyepinda shuleni hapo mwenye ubavu wa kuandika vitu kama vile ni Lissu tu hivyo wakamkamata. Walimu wakamwita Lissu mchochezi na hivyo akapewa suspension. Hata hivyo, baadae akarudishwa shuleni na kisha akafanya mtihani wa kidato cha sita.

Mwaka 1989 akaenda Mafinga JKT kisha Itende JKT kwa mwaka mmoja. Wakati huo, vuguvugu la vyama vingi lilikua limepamba moto nchini huku CCM ikiwa haitaki kabisa kuskia mambo ya vyama vingi. Katiba ya CCM ilikuwa inautambua Mkoa wa Majeshi hivyo ilituma viongozi wake kutembelea kambi zote na kuulezea msimamo wa CCM kutotaka kuskia takataka inayoitwa vyama vingi.

RPC Omary Mahita (Rukwa) na Kanali wa Andrew Shija wakitokea Mkoa huo wa Majeshi wakapangiwa kwenda Itende JKT kuwaelezea servicemen msimamo wa chama. Walipofika wakaitisha mkutano mkubwa na ukumbi ukawa umefurika. Katika mkutano huo, Mahita na Shija wakaeleza kwamba "Sisi haya mambo ya vyama vingi hayatuhusu. Haya ni mambo ya wazungu huko Ulaya mashariki hivyo tusiyashabikie".

Kitu ambacho viongozi hao hawakukijua ni kwamba miongoni mwa servicemen hao alikuwepo kijana mmoja very brilliant mwenye uelewa mkubwa wa mambo mengi yanayoendelea duniani asiye na simile kuongea kilichomo akilini mwake.

Lissu alikuwa ameskiliza hotuba ya Baba wa Taifa alipoongea na Baraza Kuu la Umoja wa vijana wa CCM Mwanza wiki chache kabla ya mkutano huo wa akina RPC Mahita. Mwalimu alikuwa amesema -"Wanaodhani mageuzi hayatuhusu bali yanazihusu nchi za Ulaya mashariki pekee ni wajinga kwani Tanzania sio kisiwa".

Muda wa maswali ulipofika huku wengi wakiamini hakuna atakaekuwa na ubavu wa kuuliza swali, Lissu bila kuogopa na kwa ujasili wa hali ya juu ambao haukuwahi kuonekana hapo Itende JKT, akanyoosha mkono. Servicemen wenzake waliokuwa wakijua misimamo yake isiyoyumba walijitahidi kumshusha mkono bila mafanikio. Huku akitumia lugha kali bila kumun'gunya maneno kama kawaida yake, Lissu aliwauliza viongozi hao -"Je, mjinga ni Baba wa Taifa aliyesema mageuzi ya vyama vingi yanatuhusu au ni nyie mnaosema hayatuhusu?"

RPC Mahita, kwa wajihi, ni mweupe sana lakini swali hilo lilimbadilisha na kuwa mwekunduuuu. Ghafla bin vuu maafande wakamkimbilia Lissu kutaka kumkwida kwa "kosa" la kutukana meza kuu. Bahati nzuri, Kanali Shija akawa na busara na akawazuia na kuwaambia "Huyo kijana Lissu yupo sahihi kwani hicho ndicho alichosema Baba wa Taifa." Huo ndio ukawa mwisho wa mkutano.

Baada ya songombingo na tafrani hiyo ya kipekee siku hiyo , maafande wote wa Itende JKT wakaanza kumuogopa sana Lissu wakiamini yeye ni mtu wa Usalama wa Taifa na akawa hapangiwi tena kazi bali akawa anakula shushi hadi kumaliza muda wake!

Kutokana na kufaulu vizuri kidato cha sita, Lissu alijiunga na kitivo cha sheria mwaka 1991 UDSM. Huko aliendelea na harakati zake za kupigania haki za wanafunzi na akajiunga na NCCR MAGEUZI. Miaka hiyo, chama hicho kilichokuwa chini ya mmoja ya viongozi waliowahi pendwa mno nchini, Mh. Augustin Mrema, ndicho kilikuwa chama kikuu cha upinzani nchini.

Baadae mwaka 1995, Lissu akaenda kusomea shahada ya uzamili chuo cha Warwick UK. Alipofika huko akaomba ruhusa aje kugombea ubunge Singida mashariki. Hata hivyo, kutokana na maandalizi duni, kura hazikutosha hivyo akarejea masomoni.

Lissu alipomaliza masomo yake 1997 alirejea na kufanya kazi ya sheria Arusha. Baadae akaoa na kuhamia Dar Es Salaam. Akawa mmoja wa wanasheria wa chama cha wanasheria wa mazingira (LEAT) pamoja na Dr. Rugemeleza Nshalla na Alex Shauri. Lissu akaanza kujipambanua kama mtanzania anaepigania haki za wanyonge na maliasili za nchi yake bila woga wowote.

Ujasiri wake mkubwa wa kwanza kupigania maliasili za taifa lake ulikuwa mwishoni mwa miaka ya 90. Serikali ya awamu ya tatu ilikuwa imempa raia wa Ireland aitwae Reginald Nolan hekta 20, 000 kuchimba mabwawa ya kambakoche kwenye delta ya Rufiji katika maeneo ya watu yenye vijiji nane waliokuwa wakiishi na wakilima humo. Lissu aliwahurumia sana wananchi hao wanyonge. Hivyo, aliratibu kampeni iliyoendeshwa na LEAT kimataifa kuupinga mradi huo kwa kutumia njia mbalimbali ikiwemo mitandao ya kimataifa. Hii ilikuwa ni kazi ngumu mno na yenye vitisho vingi. Ilikuwa si ajabu asubuhi kukuta chini ya mlango wa ofisi ya LEAT Mavuno house barua ya vitisho. Lissu hakujali wala kuogopa.

Kutokana na juhudi kubwa ya Lissu, hatimaye "European Investment bank", iliyokuwa tayari kutoa mkopo kwa Nolan ambao ungedhaminiwa na serikali ya awamu ya tatu, ikakubaliana na hoja kuntu za Lissu na kugoma kutoa fedha hizo. Hivyo, mradi huo ukasambaratika. Huu ulikuwa ushindi mkubwa kwa Lissu na alipongezwa mno na wanavijiji hao wanyonge waliomuona kama Mungu.

Lissu akapata umaarufu na kualikwa kwenye kipindi cha "Hamza Kasongo hour" Octoba 1998 na mzalendo mmoja akawa amempa nyaraka za Baraza la Mawaziri ambazo zilisema mradi huo ni wa hovyo na ulipitishwa kinyemela!

Mwezi Septemba 2000 alikwenda USA kama mtafiti kwa miaka mitatu kwenye kampuni ya World Resource Institute huku akirudi mara kwa mara nchini kuendelea na kazi za LEAT.

Mwaka 2001 yeye na wenzake wa LEAT walifanya Press conference maelezo na kudai wana ushahidi wa video kuhusu mauaji ya Bulyankulu. Yeye akarudi US lakini wenzake wakakamatwa. Akaskia imeelezwa ametoroka na atafutwa na Interpol. Akarudi na akakamatwa. Akasachiwa nyumbani kwake na kupelekwa Central. Akafanya ujanja na kuingia na simu na usiku kucha akawa anawasiliana na magazeti ya US na Canada. Hiyo ikamsaidia kuondokana na msala huo.

Je Lissu aliingiaje CHADEMA?

Lissu alijiunga CHADEMA kimazabe mwaka 2004. Mwaka 2003, Lissu alikwenda Tarime kwenye masuala ya madini. Akakutana na Mh. Chacha Wangwe akiwa Diwani wa Tarime akiwa na kesi kumi za jinai. Mh. Wangwe akamwambia Lissu kuwa wanataka kumfunga. Lissu akamwambia aondoe hofu hawataweza.

Mh. Mbowe akampigia simu Mh. Lissu kumuomba amtetee Mh. Wangwe kwenye hizo kesi zilizokuwa zikifunguliwa kila uchao. Lissu akakubali na akafanya kazi yake kwa weledi wa hali ya juu. Mh. Lissu akasaidia pia kushinda kesi za wananchi wanyonge 366 katika kipindi cha miezi minne tu. Hawa ni wananchi waliokuwa wakiishi pembezoni mwa migodi kabla ya kuswekwa ndani kwa kosa la kuvamia migodi hiyo. Lissu aliwatetea bure wananchi hawa mafukara na baada ya ushindi wa kesi hizo akatamka-"Uwekezaji umegeuka kuwa unyama Tanzania". Lissu akaonekana ni mtu asiye na uzalendo na taifa lake kwa kuwasema vibaya wawekezaji ambao serikali ilikuwaikidai walikuwa wakiliingizia taifa mapato makubwa. Hata hivyo, kwa wananchi hao wanyonge, Lissu alionekana ni Mfalme.

Baadae Mh. Mbowe akampigia Lissu na kumuomba asaidie kutafuta wanasheria wengine waingie CHADEMA kama yeye. Lissu akamshangaza Mh. Mbowe kwani bila kupepesa macho wala kutikisa maskio, Lissu akasema yeye ni mwanachama wa NCCR MAGEUZI! Mh. Mbowe alistaajabu sana kwani aliamini Lissu ni mwanachama wa CHADEMA. Hivyo, Lissu akamwambia Mh. Mbowe "kama unataka nijiunge nanyi basi najiunga" ndivyo Lissu alivyojiunga CHADEMA.

Lissu aliendelea na jitihada zake kuwasaidia wananchi waliokuwa wakinyanyasika migodini huku akiacha wateja wenye fedha nyingi Dar Es Salaam. Kwa Lissu, hakuna kitu kinamuuma moyoni mwake kama akiona mnyonge ana haki lakini anaonewa. Lissu kamwe hawezi kukaa kimya kuona hali hiyo ikiendelea.

Jitihada hizi zikamfanya Lissu azidi kukorofishana na serikali mara kwa mara. Serikali ikamwita ni mchochezi anaechochea wananchi kuwachukia wawekezaji wa Barrick ambao serikali ilikuwa ikidai ni wawekezaji wazuri waliokuwa wakiliingizia taifa pato kubwa.

Lissu amekuwa mstari wa mbele kwenye harakati za kutetea sekta ya madini nchini. Kwa miongo zaidi ya miwili amekuwa akipambana na wawekezaji wazungu waliokuwa wakikingiwa kifua na serikali ya awamu ya tatu na ya nne na kuonekana yeye si mzalendo. Alikuwa ni mmoja wa waliopinga hadharani na kwenye maandiko yake, sheria ya madini ya mwaka 1998 na ya 2010 kwa hoja kwamba zinawatajirisha wawekezaji wazungu na kutuachia watanzania mashimo tu na umaskini mkubwa wakati Mungu aliibariki nchi hii kwa kuipa madini mengi. Hoja hizi zilikuwa zikikejeriwa na wabunge wa CCM ambao walikuwa wakiipitisha miswada hii kutokana na wingi wao bungeni. Aidha, Lissu alipinga vikali kupitishwa na bunge sheria zote za madini kwa hati ya dharura mwaka 2015 na 2017.

Licha ya jitihada hizi kubwa za kuwapigania wananchi wanyonge na maskini huku wengi akiwatetea mahakamani bure na kupambana vikali na wawekezaji wa makampuni ya madini ambayo yeye miaka yote amekuwa akiyaita ni ya wezi wanaotuibia madini yetu na kunyanyasa wananchi migodini, Lissu anaonekana kwenye macho ya baadhi ya watu kwamba si mzalendo bali ni "kibaraka anaetumiwa na wazungu asieitakia mema nchi yetu".

Najua wajua MTU wangu!!
 
So your hero alipindaga tangu tumboni mwa mama yake..na unataka watoto wako wawe vile.!
Kweli mapenzi majani,huota popote.
 
Hii ndio CV (curriculum vitae) ya kamanda Tundu Lissu

Full Name: Tundu Antiphas Mughwai Lissu

Member Type: Elected Member

Constituent: Singida Mashariki

Political Party: Chama cha Demokrasia na Maendeleo

Office Location: Box 21746, Dar Es Salaam

Office Phone: +255 22 2780859/+255 754 447323/+255 786 572 571

Office E-mail: tlissu@parliament.go.tz

Date of Birth: 20 January 1968

EDUCATION

Mahambe Primary School:
CPEE (1976 - 1982) - Primary School

Galanos Secondary School:
ACSEE (1987 - 1989) - Secondary School

Ilboru Secondary School:
CSEE (1983 - 1986) - Secondary School.

University of Dar Es Salaam:
LLB (1991 - 1994) Bachelor's Degree

University of Warwick, UK:
LLM (1995 - 1996) - Masters Degree

EMPLOYMENT HISTORY
Member of The Parliament of Tanzania:Singida West Constituency (2010 - 2015)

Lawyers' Environmental Action Team (LEAT)😀irector of Researcher (2003 - 2008)

The World Resources Institute (WRI), USA:Researcher (1999 - 2002)

Lawyers' Environmental Action Team (LEAT) Researcher (1998 - 1999)

D'Souza Chambers:Advocate (1994 - 1997)

Bondeni Secondary School:Teacher (1990 - 1991)

POLITICAL EXPERIENCE
CHADEMA😀irector of Law (2004 - To Date)

NCCR-Mageuzi:Member of Parliament Candidate (1995)

Hivi tundu lissu ni mfuasi wa dini au hana dini. Binafsi nafata MTU sawa na dini yake na kwa utanzania wetu kijiti hiki tuna utawatibu tuliojiwekea wa kupokezana kijiti.

Na kwa sasa ni zamu ya Mprotestant au Muislam au Baniani au Materialist,

Na hadi sasa niseme tu wakatoliki muda muafaka wa kupumzika ni sasa.

And U do fail Us at all since Indepence.
 
Back
Top Bottom