papag
JF-Expert Member
- Jul 31, 2009
- 1,137
- 1,608
umemalizaaa mkuu,wengine wanabeat around the bushes......big upukweli jamaa kaanika mfupa hapa na nionavyo wengi katika uchangiaji wanaumauma meno tu, dalili za ukweli huo ni mkubwa, ingawa kuna wanaoolewa, lakini idadi kubwa hawaolewi.
Dhana hii inatokana na ukweli wa mapokea katika jamii zetu za kitanzania kwamba msichana mwenye umri mkubwa hafai kuolewa, na zama hizo alitakiwa kuwa mke wa pili akishapitisha umri mzuri wa ubichi. Pengine wengi wetu ni ule woga wa ukweli kuhusu usawa na haki za mwanamke ndani ya nyumba. Wanaume wasiokuwa tayari kwenda na wakati wanaona bora kwenda kuoa asiyeelimika au ambaye yuko tayari na mfumo dume wa mapokea. Lakini kazi anayokuwa nayo ni kubwa katika familia tofauti kama angemwoa msichana msomi wangetegemezana vizuri katika kujenga familia yao.
Wasichana waliohitimu vyuo vikuu wanatakiwa kujieleza kwa uwazi ubora wao kama mwanaume atawaoa na advantage tofauti na akioa msichana ambaye hana elimu na ana umri mdogo.