Wasanii wa siku hizi hawapo jukwaani

Wasanii wa siku hizi hawapo jukwaani

Izo amsha amsha wamwachie nickson gorge....wasanii wakipanda waimbe tuu
 
Hapo umeongea kweli,matamasha karibia yote upande wa sound wanachemka,yaani mziki nyenze ,MIC nazo zina katika katika.
Wanashindwa kutafuta watu Makini katika Sekta hizo Kwa kuogopa kutoa hela ndo yanayotokea kama Hayo
 
Ifike mahali na sie mashabiki tusiwe wajinga,tukiambiwa mikono juu hakuna kupandisha mikono,wakisema cjui everybody say yeah,tunanyamaza kimya,DJ akikata kipande cha mziki ili mashabiki waitikie,tunaitikia kimoyo moyo bila kutoa sauti,..mbona wataimba tu pumbavu zao,,pesa tulipe halaf tukaimbishwe mwanzo mwisho
Ndio maana hawapapendi zenji maana walwe wadudu kushughulishwa na wao mbalimbali
 
Dahh.. Ukisikizaga nyimbo zao kwenye audio sauti nzuri mnoooo, ila wakiwaga kwenye hayo matamasha jukwaani sauti kama radi.
Ukiondoa banana zoro bushoke ki ba barnaba jide chidi benz na waimbaji wa dans na taarabu wote waliobaki wanatumia auto tune kuboresha sauti zao
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] nilikua kwenye wasafi festival juzi juzi, katikati ya wimbo Diamond anaongea kwenye microphone anawaambia security kuna mtu anapigana pale I was like what the hell!
Huyo jamaa niliskia kuna show moja alionesha makalio sijui ilifanyika wapi
 
Hacheni hizo kama uelewi tulia angali Watu wanavyo toana stress na kupeana mazoezi japo mnaongea true.

Hizi ni business za Watu fanyeni yetu mtupe kilicho bora lasivyo ni kujamba ndani ya Maji nakusikiliza mlio.
 
Yani hao ma-DJ sijui wamekariri wapi kukata kata muziki kila sekunde. Pia tuna safari ndefu sana (thousand light years) kwenye sound engineering.
Nakubaliana na wewe kitu kinacholeta ugumu ni hawa mosound engineer..aisee ukiangalia show za mbele show imetulia kama coke studio Africa vile kumbe ni live show jukwaani good sound,perfect stage yaani hawa viumbe wametuacha mbali kwa kweli
 
Ni kweli boss hata leo nimeangalia shoo ya Konde youtube ile aliyopiga bure mbagala muda wote ndo hivyo sema yeah yeah,nikisema john sema maguli magufuli mara mikono juu sema konde boy konde boy sa yeah yeah khaaaa nikasema kwakuwa ni shoo ya bure sawa lakini ilikua kupoteza muda
Huyu alikuwa kwenye ukabila zaidi kwani anadai kashauriwa akamtoe mbunge wa CUF umakondeni na Mbagala wamejaa Konde, hivyo ilikuwa maandalizi ya ubunge.
 
Mimi nilidhani wenye tatizo hilo ni wasanii wa kibongo peke yao. Leo nilikuwa naangalia show moja ya Wizkid nikaona swaga ni zile zile.
Kwa na Nigeria?. Lakini U.S.A hivi kama show za R. Kelly,Joh Thomas ilikuwa wakipanda jukwaani ni kuimba mwanzo,mwisho
 
Dahh.. Ukisikizaga nyimbo zao kwenye audio sauti nzuri mnoooo, ila wakiwaga kwenye hayo matamasha jukwaani sauti kama radi.
Kabisa mkuu. Ukisikiliza audio utapenda. Sijui wana-fail wapi jukwaani?.
 
Angalia live show za Snoopy dogdog you tube . ni noma.
 
Kuna haja ya kuanza kudai hela zetu..tukiona hatuelewi somo..
 
Siku hizi mziki vijana kama hawafaidi kabisa. Tofauti na zamani miaka ya 2000's tunaenda disco,mnaburudika mwanzo,mwisho. Mnacheza kweli unarudi home umeburudika vya kutosha. Naangalia fiesta Yaani msanii yuko jukwaani inatakiwa aimbe. Lakini ajabu unapigwa wimbo wake kidogo,msanii utasikia anawaambia watu, wote mikono juu,mara mikono hivi kama mkasi,twende twende twende. Ruka ruka ruka. Sema yeyaaaa,sema wawawwaaaa,sema Wii. Piga miruz ya kutosha,tuko vizuri. Haya weka mikono hivi,twende,tuko vizuri. Mikono juu wooteeee. Mpaka anatoka jukwaani mtindo ni huo tu. Anakuja msanii mwingine mambo ni hayo hayo mtindo ni huo huo. Sasa nauliza mashabiki wanaufurahia uimbaji wa msanii au kufurahia kucheza mziki saa ngapi?. Mpaka shabiki anaondoka eneo alitoa kiingilio mikono ndio iliyochoka kwa kuipaisha juu,kama anavyotakiwa afanye na msanii. Wasanii wetu wana-FAIL wapi? Kwa nini asipande jukwaani akagonga nyimbo zake sawa sawa,mwanzo mwisho,watu waondoke pale wamesuuzika kabisa moyoni kwa burudani ya jukwaani ya kutosha?. Naona bora uende disco sasa


Si Fiesta wala Wasafi, haya matasha yote ni ya kisenge tu kwanza hakuna wasanii wa ukweli ni wauza sura tu.
 
Back
Top Bottom