Swet-R
JF-Expert Member
- Jul 20, 2018
- 5,623
- 8,141
Siku hizi mziki vijana kama hawafaidi kabisa. Tofauti na zamani miaka ya 2000's tunaenda disco, mnaburudika mwanzo, mwisho. Mnacheza kweli unarudi home umeburudika vya kutosha. Naangalia fiesta Yaani msanii yuko jukwaani inatakiwa aimbe.
Lakini ajabu unapigwa wimbo wake kidogo, msanii utasikia anawaambia watu, wote mikono juu, mara mikono hivi kama mkasi, twende twende twende. Ruka ruka ruka. Sema yeyaaaa, sema wawawwaaaa, sema Wii. Piga miruzi ya kutosha, tuko vizuri. Haya weka mikono hivi, twende, tuko vizuri. Mikono juu wooteeee. Mpaka anatoka jukwaani mtindo ni huo tu.
Anakuja msanii mwingine mambo ni hayo hayo mtindo ni huo huo. Sasa nauliza mashabiki wanaufurahia uimbaji wa msanii au kufurahia kucheza mziki saa ngapi? Mpaka shabiki anaondoka eneo alitoa kiingilio mikono ndio iliyochoka kwa kuipaisha juu, kama anavyotakiwa afanye na msanii. Wasanii wetu wana-FAIL wapi? Kwa nini asipande jukwaani akagonga nyimbo zake sawa sawa, mwanzo mwisho, watu waondoke pale wamesuuzika kabisa moyoni kwa burudani ya jukwaani ya kutosha?
Naona bora uende disco sasa
Lakini ajabu unapigwa wimbo wake kidogo, msanii utasikia anawaambia watu, wote mikono juu, mara mikono hivi kama mkasi, twende twende twende. Ruka ruka ruka. Sema yeyaaaa, sema wawawwaaaa, sema Wii. Piga miruzi ya kutosha, tuko vizuri. Haya weka mikono hivi, twende, tuko vizuri. Mikono juu wooteeee. Mpaka anatoka jukwaani mtindo ni huo tu.
Anakuja msanii mwingine mambo ni hayo hayo mtindo ni huo huo. Sasa nauliza mashabiki wanaufurahia uimbaji wa msanii au kufurahia kucheza mziki saa ngapi? Mpaka shabiki anaondoka eneo alitoa kiingilio mikono ndio iliyochoka kwa kuipaisha juu, kama anavyotakiwa afanye na msanii. Wasanii wetu wana-FAIL wapi? Kwa nini asipande jukwaani akagonga nyimbo zake sawa sawa, mwanzo mwisho, watu waondoke pale wamesuuzika kabisa moyoni kwa burudani ya jukwaani ya kutosha?
Naona bora uende disco sasa