Wasabato wa Adventista na wasababto wana matengenezo ni wasabato wapi wenye kweli ya Mungu?

Wasabato wa Adventista na wasababto wana matengenezo ni wasabato wapi wenye kweli ya Mungu?

Nikifa MkeWangu Asiolewe

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2024
Posts
11,250
Reaction score
24,086
Uhakika ni kwamba kande lipo tiyari kwa ajiri ya maandalizi ya sabato hapo kesho.

Mkiwa katika shamrashamra za kuipokea Sabato Takatifu naombeni mtuweke wazi leo hii.

Kwa miaka kazaa katika kujifunza kwangu maswali ya imani (Dini)

Nimekutana na madhehebu mengi mnayofanana kama Mashahidi wa yehova wasabato Waadventista na wasabato wana matengenezo.

Kwa ufupi sana mafundisho yenu yanakaribiana kama sio kulingana kabisa.


Sasa nashindwa kuwa elewa ukitaka na waadventista wanakuambia hili ndio kanisa la Mungu lenye ujumbe wa malaika watatu.

Ni kanisa pekee liliachwa na yesu kuhubiri kweli ya Mungu.

Ukikutana na wasabato wanamatengenezo wanapinga vikali mno.

Kwanza wanasema kanisa hili(waadventista) wamekengeuka wameiacha kweli ya Mungu.

Huko sasa hivi wana hubiri wanawake kama wachungaji(hii nitailetea uzi wake mtupe uhalali wa wanawake kuhubiri)

Wanasema limevamiwa na mamluki wachungaji wanawekewa mikono hata kama hajaoa!

Wanasema kanisa limegeuka kuwa la kibiashara hata siku za sabato utaona kuna machagizo kadhaa wa kadhaa.

Wana matengenezo wanasema kanisa la waadventista ndilo kanisa lililotapikwa kwa mujibu wa Ufunuo wa Yohana 3:16
[16]Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.

Hivyo wanasimama na maandiko hayo kupinga vikali maana kanisa halina tena uhalali.

wanasema leo hii mziki wa kisabato hauna tofauti na nyimbo za kitamaifa yaani ukiwauliza kimataifa wao wanakuambia ni kama tu nyimbo za akini Chino Kid,Zuchu, na wakina Bob Marley (wao kimataifa hutafasiri hivyo)

Madai yao ni mengi sana husema kwa sasa kanisa la waadventista wanacheza na kukatika hata siku za sabato madhabahuni.

Wao wanadai zile Nembo zinazo tupimiwa na waadventista wasabato ni za kishetani!

Maana hakuna mahali popote pale kwenye bibilia zime amriwa zitumike.

Wao kila wanaposali(Ombi) hupiga magoti au kusujudu.


Nimekaa nalo siku mingi najiuliza tumfuate nani sasa kati yenu ninyi wawili au watatu ikiwa sisi wa wakatoliki kutwa kucha kwenye mikutano yenu mnatutukania Papa wetu na kumuita mnyama.

Naomba mtupe muongozo. Ahsanteni

Huku tukukiimba wimbo No 87 .
 
Leo ndio nimejua wasabato wapo wawili. Je wanafanana katika kulishambulia kanisa katoliki kuliko shetani?
 
Bnafs nlishakataa kuwa chn ya kanisa au dhehebu fulan staki kbs mi nasali kanisa lolote tu, maana yote yameanzshwa na wanadamu tena mengne yameanzshwa kwa mapgano na migogoro ndpo wakajtenga na kuanzsha dhehebu ili kuwakomoa wenzao.
 
Back
Top Bottom