Harusi za kisabato zimekuwa za kero kubwa, wanasema hawataki kuweka vinywaji vyenye alcohol kisa imani yao, hawajui kama hayo mambo yanzuiwa kanisani tu, mkitoka kanisani huku kwingine ukumbini ni kwa Kaisali lazima watuachie ya Kaisali na ya Mungu tunakuwa tushayamaliza kanisani, kinachoudhi zaidi wanachukua michango yetu halafu wanatuchagulia cha kutumia, ile michango siyo hela yao, nakuwa nimetoam mimi na wala hoja ya kusema wananua wao si sahihi.
Kama wanasimama kwenye imani yao basi wasichangishe pesa zetu bali watumie zao na sisi tutakuja kunywa soda na juice kama wanavyotaka na siyo mchango wangu wa pesa waupangie cha kuninunulia.
Uache ujinga, kwani ulichangia wasabato au marafiki zako???? Kama ulichangia wasabato mchango wako ulitoa kwa mchungaji, mzee wa kanisa au shemasi???? Usihusishe imani ya watu na ulafi wako. Pia kama unaona mahusiano na watu wenye kiasi huhitaji, fungamana na walafi wenzako.
Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums