Warithi wa Mwinyi, Mkapa, Kikwete na Magufuli

mitindo huru

JF-Expert Member
Apr 26, 2016
1,607
1,596
Habari wadau,
Kuna hili jambo nalifikiria

Mwalimu Nyerere aliweza kuandaa vijana wengi kuwa viongozi wa badae nchini Tanzania na hata nchi jirani na alifanikiwa kwa asilimia kubwa

aliandaa viongozi wengi ambao watakuja kuongoza nchi katika nafasi mbalimbali za uongozi katika Taifa, nafasi kama Rais n.k

alifanya kazi hii kubwa ya kuandaa vijana kuwa viongozi wa badae tangu akiwa Mwenyekiti wa TANU na hata badae ilipoanzishwa CCM.

Lengo la Mwalimu Nyerere lilikuwa kuandaa viongozi watiifu, wazalendo na wawajibikaji kwa Taifa na wananchi pia Mwalimu Nyerere aliwaandaa vijana kuwa viongozi wa badae ili waendane na falsafa na kanuni za Mwalimu Nyerere mwenyewe binafsi na pia vijana waendane na falsafa za chama kuanzia TANU hadi CCM.

Wengi wa vijana walioandaliwa na Mwalimu Nyerere walifanikiwa kufikia malengo ya Mwalim Nyerere na Chama kwa kuwa viongozi kabla hawajachafuka na mambo mbalimbali kama ufisadi, rushwa n.k

Mfano wa vijana waliondaliwa na Mwalimu Nyerere pamoja na Chama ni pamoja na Mkapa, Kikwete Sr, Sita Sr, Makamba Sr, Warioba n.k pia inasemekana aliwaandaa viongozi wa nchi jirani kama Uganda, Rwanda na Burundi.

Hoja hapa ni kwamba kwanini viongozi wengine wameshindwa kuandaa vijana wa badae mfano tulikuwa tunajua Rais anaekuja baada ya Mkapa kutokana na Nyerere.

Mfano Mzee Mwinyi ajaandaa vijana wengi kama alivyoaandaa Mwalimu Nyerere kipindi cha uongozi wake bali tunamuona Hussein Mwinyi tu ambaye ni mtoto wake.

Kuhusu mzee Mkapa sina uhakika kama alimuandaa Raisi Magufuli au imetokea kama bahati tu, wengi wa vijana aliowaandaa wameishia kuchafuka kwa ufisadi na rushwa kabla hawajafikia malengo.

Pia Mzee Kikwete nae kaishia kumuandaa mtoto wake Ridhiwan, ila vijana wengi aliowaandaa wameishia kwenye ufisadi, rushwa, jeuri n.k mfano ni Nape, Makamba Jr, Makonda, Jerry Slaa n.k

Swali ni kwanini viongozi kama Mwinyi, Mkapa, Kikwete wameshindwa kuandaa viongozi wa uhakika wa badae kama alivyofanya Mwalimu Nyerere sababu naona wengi wa vijana walioandaliwa wameishia kukengeuka na ufisadi, rushwa, kutowajibika, jeuri n.k

hoja hapa ni kwamba Tanzania hatujui hatma yetu ya uongozi wa nchi kwa badae sababu hakuna viongozi wazalendo wanaonekana kuandaliwa kuja kuongoza nchi.

Binafsi naona hili ni tatizo sababu ni rahisi kupata viongozi mamluki wa nchi jirani.

Hapa sizungumzii CCM pekee bali na vyama vyote ikiwemo UDP, ACT, Chadema, CUF, TLP je wanautaratibu gani wa kuandaa vijana wazalendo wanaoweza kuongoza Taifa hili hapo badae?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo kubwa ni Inteligence system yetu. Marais hawana haja ya kuandaliwa bali wanasiasa wanatakiwa kuachiwa uwanja huru na nafasi sawa wajinadi wawezavyo, ili mwisho wa siku system za nchi zifanye upembuzi yakinifu.

Shida yetu kubwa ni kuwa tuna inteligence system mbovu ambayo haina uwezo wa kuwafanyia vetting wagombea kujua yupi ni mamluki na yupi si mamluki.

Unforgetable
 
Talent ya kuzaliwa na Talent ya kusomea ni vitu viwili tofauti/Kuna akili na Elimu hivi navyo ni vitu viwili tofauti.
Mzee alifanya vile kwa sababu alizaliwa kuwa kiongozi,ila kwa sasa kiti hiki kimekuwa dili ndio maana huwezi andalia mtu mwingine sababu kazi ya kuajiri ni kazi ya kampuni.
 
Tatizo kubwa ni Inteligence system yetu. Marais hawana haja ya kuandaliwa bali wanasiasa wanatakiwa kuachiwa uwanja huru na nafasi sawa wajinadi wawezavyo, ili mwisho wa siku system za nchi zifanye upembuzi yakinifu.

Shida yetu kubwa ni kuwa tuna inteligence system mbovu ambayo haina uwezo wa kuwafanyia vetting wagombea kujua yupi ni mamluki na yupi si mamluki.

Unforgetable
Upo sahihi, juzi nimesikia kiongozi wa UVCCM jijini Dar amekamatwa kwamba sio raia wa Tanzania.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Talent ya kuzaliwa na Talent ya kusomea ni vitu viwili tofauti/Kuna akili na Elimu hivi navyo ni vitu viwili tofauti.
Mzee alifanya vile kwa sababu alizaliwa kuwa kiongozi,ila kwa sasa kiti hiki kimekuwa dili ndio maana huwezi andalia mtu mwingine sababu kazi ya kuajiri ni kazi ya kampuni.
Nini kifanyike ili kuandaa viongozi wa badae au tusuburi uongozi wa nchi toka kwa Hussein Mwinyi, Ridhiwan Kikwete n.k?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Saa hii kuna UVCCM na BAVICHA. Ndio mahala wanapopikwa na kupewa fursa hawa viongozi wajao

Kuhusu quality yao kiuongozi sijui
Je kanuni na taratibu za UVCCM na BAVICHA zinatuhakikishia kupata viongozi wazuri badae?
Nina mashaka sababu juzi nimesikia kuna kiongozi wa UVCCM moja ya maeneo Jijini dar sio raia wa Tanzania

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Je kanuni na taratibu za UVCCM na BAVICHA zinatuhakikishia kupata viongozi wazuri badae?
Nina mashaka sababu juzi nimesikia kuna kiongozi wa UVCCM moja ya maeneo Jijini dar sio raia wa Tanzania

Sent using Jamii Forums mobile app
Siamini katika uchama wala mifumo ya siasa. Naamini viongozi wazuri ni wale wanaoweza kuwa watumwa wa watu na hii mtu huzaliwa nayo na wala haitegemei external forces.

Kiufupi siamini katika existing systems
 
Mkuu mambo yamebadilika sana! vijana walioandaliwa kipindi cha Kikwete ilikuwa ni kubebana na kujuana. Wengi hawakuwa na uzalendo ndani yake na mbaya zaidi rushwa ilitamalaki kuanzia ngazi ya juu kabisa ya utawala. Vijana waandaliwa walipikwa kuwa wanamtandao na hatimae wakajifunza ubinafsi na uroho wa kujilimbikizia mali make watawala waliwakumbatia.

Ukiachana na hilo wapo vijana wachache sana ambao kwamtazamo wangu wangekuja kuwa vingozi wazuri tu mathalani akina Francis Mawazo, Ben Sanane, Mtatiro, Zitto, Mnyika n.k baadhi yao harakati zao zilivurugwa na au kuuawa kutokana na udharimu wa watawala wa nchi ama ndani ya vyama vyao.

Usitegemee kiongozi kama Mbowe akuache ung'ale na akupe support ili baadae uje kuwa kiongozi mkubwa katika jamii pasipo kumsujudia.
Matokeo yake vijana wamegeuka kuwa wachumia tumbo na wapiga zumari wa watawala.
 
Siamini katika uchama wala mifumo ya siasa. Naamini viongozi wazuri ni wale wanaoweza kuwa watumwa wa watu na hii mtu huzaliwa nayo na wala haitegemei external forces.

Kiufupi siamini katika existing systems
Umeandika hoja nzuri ndugu,
Ila je, tutumie mfumo gani kama nchi ili tuweze kupata viongozi wazuri katika nchi hapo badae?
Je kuna mfumo wa siri wa kupata viongozi ambao raia wa kawaida hatuufahamu?
au tusubiri kupata viongozi kutoka kwa watoto, wajukuu na ndugu wa Mwinyi, Karume, Mkapa, Shein, Kikwete, Magufuli n.k?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kikubwa hapo mkuu mitindo huru ni watawala wawape freedom of expression, damu changa zishiriki kwenye vikao na ngazi kuu za maamuzi kuanzia ndani ya vyama na serikalini.
Kiujumla watawala wabadilike wawe na mitazamo ya kizalendo zaidi ili damu changa iige na kurithi yaliyo mema.
Bunge liwe huru ili wananchi waanze kuwamulika mapema viongozi wanaochipukia.
Vyama vya siasa vipewe uhuru wa mikutano na pia viongozi wa vyama wawape nafasi vijana wenye talanta ya uongozi na wawalee vyema waje kuwa watawala wazuri.
 
Tatizo kubwa ni Inteligence system yetu. Marais hawana haja ya kuandaliwa bali wanasiasa wanatakiwa kuachiwa uwanja huru na nafasi sawa wajinadi wawezavyo, ili mwisho wa siku system za nchi zifanye upembuzi yakinifu.

Shida yetu kubwa ni kuwa tuna inteligence system mbovu ambayo haina uwezo wa kuwafanyia vetting wagombea kujua yupi ni mamluki na yupi si mamluki.

Unforgetable
Unahisi kwamba kuna uwezekano wa kupatikana kwa kiongozi mkubwa wa nchi ,kwa ngazi ya mkuu wa nchi alafu akawa mamluki?
 
Back
Top Bottom