Warioba: Huu ndio ukweli kuhusu Mwananchi Gold

ninaomba tutengenishe nia nzuri na uvunjaji wa sheria au kuwaendea kinyume wananchi wa tanzania
1. huyu mzee analipwa pensheni ya viongozi mpaka mwisho wa maisha yake, hivyo kwa upande bado ni muajiriwa wetu, pili hiyo pensheni inmwezesha kuishi vizuri tu , hivyo aache hizo tamaa.
2 alikuwa ni mwana sheria mkuu wa serikali hivyo anajua, jinsi mashirika ya umma nk yanavyo anzishwa na utafutwaji wa hao stategic investors.na pia waziri kuu hivyo lwenye cabinet wamejadili mambo mengi tu ya uwekezaji nk , na faida zake na hasara ya different strategy
3 anajua sheria ya uanzishwaji wa bot na majukumu yake, katika kulinda na kutetea maslahi ya taifa.na jinsi serikali invyo pata mitaji katika miradi yake
4. anaelewa past experience ya bot katika kununua dhahabu na hasara walizo pata.
5 anajua uwepo wa stamico na kuwepo kwa ndc katika jukumu la kuendeleza viwanda na madini.
sasa leo hii kilicho msababisha ashindwe kuyaanisha haya yote, na kuweka maslahi ya taifa mbele, mpaka kutaka kuiweka bot katika biashara ya kusafisha dhahabu ni nini?
kwani stamico-ndc wakifanya hiyo biashara taifa hali faidiki?
kwani stamico hawana hao wataalamu wa madini mpaka wao mwananchi trust wakapeleka watu wao?
ambao hata walivyokuwa selected mimi na wewe hatujui?sijiui watoto wao au ndugu wa karibu etc etc
August,
Naona umelisoma tamshi la Warioba kwa miwani ya mbao. Ni wapi inaonyesha amekuwa na tamaa? Ni wapi ameonyesha ameshalipwa mshahara kwa kusaidia kuanzisha kampuni hiyo? Soma tena. Usijazie tu kwa dhana zako.
 
Inaelekea zengwe hili lilisukwa tangu lilipoanzishwa kwa sababu kama ni ushauri wa kisheria serikali ingeweza kuupata kwa mwanasheria Mkuu wa Serikali. Na Warioba na wenzake waliombwa kusaidia kuanzisha kampuni kisheria, ilikuwa, ilipotokea nafasi ya kuanzisha kampuni ndogondogo kwa ajili ya kuwa na hisa kwenye kampuni mama, wao tena wajitose huko na kushina nafasi mbili-washauri wa kisheria na wamiliki wa kampuni.
Inaelekea kuna mambo mengi yamejificha ambayo hayaelezwi kinagaubaga
JF Pamoja na maelezo mazuri yaliyowekwa na Mhe. Warioba nadhani kuna maswali kadhaa bado yanahitaji kujibiwa. Je haya makampuni yote yaliyotajwa ni ya kina nani, nani hasa Share holders wake. Nadhani bado kuna jambo zito limejificha hapo. Tungependa Mhe. Warioba atusaidie kupata ufumbuzi wa hili. Katika maelezo yake yote inaelekea mradi wote ni wa Serikali na uko kwa msukumo wa Serikali, jambo ambalo records tulizonazo zinaonyesha tofauti. Mhe. Warioba pasua jipu. Dr. Slaa
 
Mimi nionavyo ni kuwa mkanganyiko wote huu ni kwa sababu walioko serikalini hawana maslahi binafsi kwenye mradi huo kwa sasa. Mzee Warioba anakiri kuwa walifuatwa kama mawakili katika kuanzisha kampuni hii, anakubali pia kuwa kuna asilimia 45 ambazo zinamilikiwa na wawekezaji wa ndani kwa kutumia Mwananchi Trust. La kujiuliza hao wawekezaji wa ndani ni akina nani? Angetaja orodha ya hao wamiliki ndio unaweza kuona kwa nini inapigwa vita. Kwangu mimi inawezekana kabisa hawa ndio wanopigwa vita kwa sababu mbalimbali za kisiasa ama za kimaslahi binafsi. Pia sikuona mahali aliposema kama yeye pia ni mwanahisa kwenye hiyo Mwanachi Trust. Angesema wazi ili kuweka kumbukumbu sawa.
Wana JF nadhani tunachanganya mambo. Ni vema tukapata ufafanuzi Wanahisa wa Mwananchi Trust ni nani hasa. Je ni Serikali 100% Kama sivyo Serikali inahusika vipi na Trust hii. Ninasema hivi kwa vile nyaraka za Brela nilizo nazo hazionyeshi hivyo. Ikumbukwe kuwa Mwananchi Gold Company ni moja ya Maeneo yaliyohojiwa na Deloitte na Touche, na hatimaye pia na CAG. Hivyo haiwezi kujibiwa kirahisi hivi. Tujibu maswali mazito kwa uzito unaostahili hasa inapohusu maswala yanayohusiana au moja kwa moja au indirectly na Ufisadi.
 
Mh. Dr Slaa,
Mkuu hili shirika ni la serikali kwa nini nyie wabunge mnasubiri hadi Warioba awasaidie kuwafahamisha wabia wa hili shirika!..Kwanza itakuwa kinyume cha sheria na hapa kila mtu atamwona yeye mchawi...
Kwa nini Bunge lisiitishe kikao maalum kwa ajili ya shirika hili ambalo kutokana na madai ya Warioba ni shirika la serikali akiwahusisha BoT, NDC naaa!.. Hii ni hint moja kubwa sana msitake kupoteza muda kujaribu kufikiri kile ambacho hakiwezekani isipokuwa mbele ya sheria..
Na msije tumia makosa ya Richmond, kama kutakuwepo na uchunguzi, hiyo Kamati itatakiwa tu kuwakilisha report yake kama ni ushahidi mbele ya kamati ya maamuzi, hivyo report inawakilishwa ktk kikao cha kamati sio bungeni ambako itakutana tena na maswala ya kura za wabunge wakati hawafahamu undani wa report nzima..

Hii nikiwa na maana baada ya uchunguzi kamati inaundwa kupokea report hiyo na kuwaita wahusika moja kwa moja na kuanza process nzima ya kutafuta ukweli.. Kama mlivyoona hata mokopo ya Benki na mashrika ya magari Marekani, yalitanguliwa na kamati ambayo iliyasikiliza matatizo yote ya mashirika haya wakaita wahusika wote kujitetea/pinga kisha ndipo Bunge likatoa maamuzi yake baada ya ukweli kuwa wazi toka pande zote.. Kosa tunalotumia sisi Tanzania ni report hii kwenda Bungeni kutafuta kura za wabunge wakati hakuna UWAZI ktk report nzima toka pande zote mbili..
 
Mh. Dr Slaa,
Mkuu hili shirika ni la serikali kwa nini nyie wabunge mnasubiri hadi Warioba awasaidie kuwafahamisha wabia wa hili shirika?..
Kwa nini Bunge lisiitishe kikao maalum kwa aljili ya shirika hili ambalo kutokana na madai ya warioba ni shirika la serikali.. Hii ni hint moja kubwa sana msitake kupoteza muda kujaribu kufikiri kile ambacho hakiwezekani isipokuwa mbele ya sheria..
Na msije tumia kmakosa ya Richmond, kama kutakuwepo na uchunguzi, hiyo Kamati itatakiwa tu kuwakilisha report yake kama ni ushahidi tosha wa kuunda kamati ya maamuzi, hivyo report inawakilishwa ktk kikao cha kamati sio bungeni ambako itakutana tena na maswala ya kura..
Hii nikiwa na maana baada ya uchunguzi kamati inaundwa kupokea report hiyo na kuwaita wahusika moja kwa moja na kuanza process nzima ya kutafuta ukweli.. Kama mlivyoona hata mokopo ya Benki na mashrika ya magari Marekani, yalitanguliwa na kamati ambayo iliyasikiliza matatizo yote ya mashirika haya wakaita wahusika wote kujitetea kisha ndipo Bunge likatoa maamuzi yake baada ya ukweli kuwa wazi toka pande zote.. Kosa tunalotumia sisi tanzania ni report hii kwenda Bungeni kutafuta kura za wabunge wakati hakuna UWAZI ktk report nzima toka pande zote mbili..


Dr Slaa ameshakwambia kuwa hili si shirika la serikali pamoja na kuwa serikali ilikuwa na hisa chache kupitia BOT.

Nyaraka za Mwananchi Dr Slaa ameshawahi kuziomba rejea hoja yake kuhusu BOT

Dr Slaa ameshakwambia kuwa nyaraka anazo tayari, anachotaka ni Dr Slaa kama insider wa hiyo kampuni naye amwage ukweli kamili anaujua na si kufanya propaganda.

Asha
 
JF Pamoja na maelezo mazuri yaliyowekwa na Mhe. Warioba nadhani kuna maswali kadhaa bado yanahitaji kujibiwa. Je haya makampuni yote yaliyotajwa ni ya kina nani, nani hasa Share holders wake. Nadhani bado kuna jambo zito limejificha hapo. Tungependa Mhe. Warioba atusaidie kupata ufumbuzi wa hili. Katika maelezo yake yote inaelekea mradi wote ni wa Serikali na uko kwa msukumo wa Serikali, jambo ambalo records tulizonazo zinaonyesha tofauti. Mhe. Warioba pasua jipu. Dr. Slaa

Dr, hayo ni maswali mazuri yanayohitaji ufafanuzi zaidi toka Jaji Warioba.
 
Asha Abdala,
Dr Slaa kasema hivi:- Je ni Serikali 100% Kama sivyo Serikali inahusika vipi na Trust hii...
Hapa akiwa na maana hata yeye hafahamu undani wa shirika hili..sioni mahala amesema siii la serikali.
Hakuna propaganda ikiwa hujaulizwa mbele ya sheria. Huyu ni mwanasheria wa shirika iweje amwage vitu tuu kwa sababu Dr. Slaa kasema.. Utaratibu upo na rahisi kabisa mnashindwa kitu gani kusimamaisha sheria!
Kwa kuanzia tu mnaweza ku raise issue ya BoT (chombo cha Taifa) kujitoa kwake mkataka maelezo na sababu, kisha hapo zitafummka habari kibao zikipandiana kama ngazi..mtafika tu kwa Warioba na Mwananchi Gold yenyewe ubia wake umetokana vipi..
 
Asha Abdala,
Dr Slaa kasema hivi:- Je ni Serikali 100% Kama sivyo Serikali inahusika vipi na Trust hii...
Hapa akiwa na maana hata yeye hafahamu undani wa shirika hili..sioni mahala amesema siii la serikali.
Hakuna propaganda ikiwa hujaulizwa mbele ya sheria. Huyu ni mwanasheria wa shirika iweje amwage vitu tuu kwa sababu Dr. Slaa kasema.. Utaratibu upo na rahisi kabisa mnashindwa kitu gani kusimamaisha sheria!



Dr Slaa alishaweka wazi msimamo wake toka mwaka 2007, msome hapa chini
Mwandishi Wetu


MBUNGE wa Karatu, Dk. Wilbroad Slaa (Chadema) ametamba kuwa ana ushahidi na vielelezo kuthibitisha madai aliyokuwa ayawasilishe bungeni kuhusu ufisadi wa mabilioni ya shilingi unaodaiwa kufanyika ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT). Ametishia pia kutaja hadharani majina ya watu wanaotuhumiwa kuhusika na ufisadi huo ifikapo Septemba 15.

Dk Slaa, ambaye wiki iliyopita aliondoa hoja kuhusu madai hayo aliyokuwa aiwasilishe katika kikao kijacho cha Bunge akidai kwamba ilikuwa inapigwa danadana kupangiwa tarehe ya kusikilizwa ili kuiwezesha Serikali kujipanga upya, aliwaambia waandishi wa habari Dar es Salaam jana kwamba vielelezo alivyonavyo si vya kughushi na amevipata kutoka ndani ya taasisi za umma, ikiwamo BoT yenyewe.

Hata hivyo wakati akizungumzia madai hayo, Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge), Dk Batilda Burian alisema kitendo cha Dk Slaa kuondoa hoja yake hakikutokana na mbinu zo zote za Serikali, bali hoja yake ilikuwa ya kishabiki yenye lengo la kuonyesha mbele ya jamii kwamba wapinzani wanaonewa bungeni.

Alisema baadhi ya vielelezo vilivyopelekwa na mbunge huyo kwa Spika vilithibitika kuwa havitoshelezi hivyo alichokuwa anamtaka Spika ni kuwasilisha ushahidi zaidi na siyo kuondoa hoja. Alisema yawezekana mbunge huyo alitambua kwamba hana ushahidi wa kutosha ndiyo maana akaiondoa hoja yake.

Hata hivyo alisema Dk Slaa bado ana nafasi ya kuwasilisha hoja hiyo katika kikao kijacho cha Bunge. Madai ya Dk Slaa yanahusu tuhuma kwamba BoT ililipa deni la kampuni ya Meremeta linalodaiwa kufikia Sh bilioni 155 kinyume cha utaratibu, ililipa fedha kwa kampuni binafsi ya Mwananchi Gold na Sh bilioni 38 kwa kampuni hewa.

Alisema vielelezo alivyo navyo kuhusiana na tuhuma hizo ni vya kweli na akamshangaa Spika wa Bunge, Samuel Sitta kudai baadhi ya vielelezo vyake ni vya uongo wakati si mtaalamu wa maandishi ya kughushi. Wakati akizungumza katika kipindi kimoja cha televisheni wiki iliyopita, Sitta alisema kwamba atapeleka Polisi suala la kughushiwa kwa baadhi ya nyaraka alizowasilishiwa na Dk Slaa.

Dk Slaa aliwaambia waandishi wa habari jana kwamba alipoomba kuwasilisha hoja yake aliamini ushahidi wake kwa vile umetoka ndani ya taasisi muhimu. “Kuna Watanzania ndani ya taasisi hizi ambao wanashuhudia baadhi ya watu wanavyojineemesha kwa ufisadi, wamechoka na hawa ndiyo wanaotusaidia.”

Alitumia mkutano wa jana kuwaonyesha waandishi namna ambavyo alikuwa anaandika barua kwa Wakala wa Usajili wa Kampuni (Brela) kuomba nyaraka mbalimbali na akapewa. Akichambua tuhuma hizo kuhusu madai kwamba kampuni ya Tangold iliandikishwa kijanja kuwa ni mali ya Serikali, Dk Slaa alisema kampuni hiyo ni ya kigeni ambayo iliandikishwa kwa mara ya kwanza Mauritius mwaka juzi na baadaye ikasajiliwa nchini Februari mwaka jana. Dk Slaa alisema licha ya Serikali kudai kuwa kampuni hiyo ni ya serikali lakini hakuna hati zilizoko Brela zinazoonyesha kuwa wakurugenzi wake wanafanya kazi kwa niaba ya serikali. Pia anahoji kama ilianzishwa kwa biashara na kama imelipa kodi.

“Kampuni hii wiki nane tu baada ya kupata usajili ilipewa mkopo wa Sh bilioni 30.8 na BoT wakati hata wakurugenzi wake hawafahamiki,” alisema Dk Slaa. Kuhusu tuhuma za BoT kulipa fedha kwa kampuni binafsi ya Mwananchi Gold Co. Ltd, Dk Slaa alisema kuna utata juu ya kuandikishwa kwa kampuni hiyo, jinsi ilivyolipwa na BoT dola milioni 5.5 na jinsi BoT ilivyolipa deni la Kampuni ya Meremeta wakati mmiliki wake hajulikani.

Alisema BoT ambaye ni msimamizi wa taasisi zote za fedha na uchumi wa nchi, mwenendo wake haupaswi kutiliwa shaka. Alisema kuna malipo mengi yamefanywa na benki hiyo ambayo yanatia wasiwasi na akadai kuwa kwa sasa ana ushahidi kuonyesha namna fedha hizo zilivyohamishwa na wajanja.

HabariLeo; Thursday,August 23, 2007
 
Asha Abdala,
Dr Slaa kasema hivi:- Je ni Serikali 100% Kama sivyo Serikali inahusika vipi na Trust hii...
Hapa akiwa na maana hata yeye hafahamu undani wa shirika hili..sioni mahala amesema siii la serikali.
Hakuna propaganda ikiwa hujaulizwa mbele ya sheria. Huyu ni mwanasheria wa shirika iweje amwage vitu tuu kwa sababu Dr. Slaa kasema.. Utaratibu upo na rahisi kabisa mnashindwa kitu gani kusimamaisha sheria!
Kwa kuanzia tu mnaweza ku raise issue ya BoT (chombo cha Taifa) kujitoa kwake mkataka maelezo na sababu, kisha hapo zitafummka habari kibao zikipandiana kama ngazi..mtafika tu kwa Warioba na Mwananchi Gold yenyewe ubia wake umetokana vipi..

Rejea pia haya:

Gavana Balali aliruhusu na/au kuidhinisha na/au kunyamazia mkopo usio na riba wa Dola za Marekani 5,512,398.55 kwa kampuni ya Mwananchi Gold Co. Ltd. kati ya mwaka 2004 na tarehe 30 Juni 2006. Kati ya fedha hizo, deni la dola 2,807,920 limedhaminiwa kwa dhahabu ghafi ambayo ingenunuliwa kutokana na fedha za mkopo zilizotolewa na Benki Kuu yenyewe! Kwa maana rahisi ni kwamba kampuni ya Mwananchi Gold haijatoa dhamana yoyote inayoeleweka kwa mabilioni ya shilingi ilizokopeshwa na Benki Kuu chini ya Gavana Balali. Kwa taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu, hadi kufikia mwezi Desemba 2006 Mwananchi Gold Co. Ltd. ilikuwa imeshindwa kulipa hata riba ya mkopo huo kwa kiasi cha dola za Marekani 62,847.91. “Katika mazingira haya”, inasema barua ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu, “hatukuweza kujiridhisha kwamba deni la dola la Marekani 5512398.55 inalodaiwa (Mwananchi Gold Co. Ltd.) hadi kufikia tarehe 30 Juni 2006 linaweza kulipika.” Je, ni kampuni gani hii iliyopewa mamilioni ya fedha za umma katika fedha za kigeni bila kudaiwa riba au kupewa kipindi maalumu cha kulipa mkopo huo? Kufuatana na taarifa za BRELA, Mwananchi Gold Co. Ltd. ni kampuni binafsi ambayo wanahisa wake ni Benki Kuu ya Tanzania yenye hisa 500, Shirika la Maendeleo la Taifa (hisa 500), Mwananchi Trust Co. Ltd. (hisa 1,123) na Chimera Co. Ltd. (hisa 500). Kampuni hii ilisajiliwa kama kampuni binafsi tarehe 12 Desemba 2002. Mawakili wake ni kampuni ya mawakili ya Nyalali, Warioba & Mahalu Associates ikiwashirikisha aliyekuwa Jaji Mkuu wa Tanzania wakati huo marehemu Francis L. Nyalali, Waziri Mkuu wa zamani Joseph Sinde Warioba na aliyekuwa balozi wa Tanzania nchini Italia Profesa Costa R. Mahalu. Wakurugenzi wa Mwananchi Gold ni Joseph Sinde Warioba, Gavana Daudi Balali, Col. J. Simbakalia, Vulfrida Grace Mahalu, Yusuf H. Mushi na raia wawili wa Italia, Paolo Cesari na Patrizio Magrini. Vulfrida Mahalu ni Ofisa Mkuu Mtendaji wa kampuni binafsi ya VMB Holdings (1996) Ltd. na pia ni mke wa Profesa Mahalu ambaye kwa sasa anakabiliwa na tuhuma za kuhujumu uchumi kutokana na madai ya wizi wa zaidi ya shilingi bilioni tatu za Serikali wakati akiwa balozi wa Tanzania nchini Italia! Kanali Simbakalia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Taifa na Yusuf Mushi ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni binafsi ya Business Machines Consultants (T) Ltd;

Chanzo: http://www.chadema.net/habari/2007/orodha1/ukurasa2.php
 
Asha Abdala,
Dr Slaa kasema hivi:- Je ni Serikali 100% Kama sivyo Serikali inahusika vipi na Trust hii...
Hapa akiwa na maana hata yeye hafahamu undani wa shirika hili..sioni mahala amesema siii la serikali.
Hakuna propaganda ikiwa hujaulizwa mbele ya sheria. Huyu ni mwanasheria wa shirika iweje amwage vitu tuu kwa sababu Dr. Slaa kasema.. Utaratibu upo na rahisi kabisa mnashindwa kitu gani kusimamaisha sheria!
Kwa kuanzia tu mnaweza ku raise issue ya BoT (chombo cha Taifa) kujitoa kwake mkataka maelezo na sababu, kisha hapo zitafummka habari kibao zikipandiana kama ngazi..mtafika tu kwa Warioba na Mwananchi Gold yenyewe ubia wake umetokana vipi..

Rejea pia haya:

Gavana Balali aliruhusu na/au kuidhinisha na/au kunyamazia mkopo usio na riba wa Dola za Marekani 5,512,398.55 kwa kampuni ya Mwananchi Gold Co. Ltd. kati ya mwaka 2004 na tarehe 30 Juni 2006. Kati ya fedha hizo, deni la dola 2,807,920 limedhaminiwa kwa dhahabu ghafi ambayo ingenunuliwa kutokana na fedha za mkopo zilizotolewa na Benki Kuu yenyewe! Kwa maana rahisi ni kwamba kampuni ya Mwananchi Gold haijatoa dhamana yoyote inayoeleweka kwa mabilioni ya shilingi ilizokopeshwa na Benki Kuu chini ya Gavana Balali. Kwa taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu, hadi kufikia mwezi Desemba 2006 Mwananchi Gold Co. Ltd. ilikuwa imeshindwa kulipa hata riba ya mkopo huo kwa kiasi cha dola za Marekani 62,847.91. “Katika mazingira haya”, inasema barua ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu, “hatukuweza kujiridhisha kwamba deni la dola la Marekani 5512398.55 inalodaiwa (Mwananchi Gold Co. Ltd.) hadi kufikia tarehe 30 Juni 2006 linaweza kulipika.” Je, ni kampuni gani hii iliyopewa mamilioni ya fedha za umma katika fedha za kigeni bila kudaiwa riba au kupewa kipindi maalumu cha kulipa mkopo huo? Kufuatana na taarifa za BRELA, Mwananchi Gold Co. Ltd. ni kampuni binafsi ambayo wanahisa wake ni Benki Kuu ya Tanzania yenye hisa 500, Shirika la Maendeleo la Taifa (hisa 500), Mwananchi Trust Co. Ltd. (hisa 1,123) na Chimera Co. Ltd. (hisa 500). Kampuni hii ilisajiliwa kama kampuni binafsi tarehe 12 Desemba 2002. Mawakili wake ni kampuni ya mawakili ya Nyalali, Warioba & Mahalu Associates ikiwashirikisha aliyekuwa Jaji Mkuu wa Tanzania wakati huo marehemu Francis L. Nyalali, Waziri Mkuu wa zamani Joseph Sinde Warioba na aliyekuwa balozi wa Tanzania nchini Italia Profesa Costa R. Mahalu. Wakurugenzi wa Mwananchi Gold ni Joseph Sinde Warioba, Gavana Daudi Balali, Col. J. Simbakalia, Vulfrida Grace Mahalu, Yusuf H. Mushi na raia wawili wa Italia, Paolo Cesari na Patrizio Magrini. Vulfrida Mahalu ni Ofisa Mkuu Mtendaji wa kampuni binafsi ya VMB Holdings (1996) Ltd. na pia ni mke wa Profesa Mahalu ambaye kwa sasa anakabiliwa na tuhuma za kuhujumu uchumi kutokana na madai ya wizi wa zaidi ya shilingi bilioni tatu za Serikali wakati akiwa balozi wa Tanzania nchini Italia! Kanali Simbakalia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Taifa na Yusuf Mushi ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni binafsi ya Business Machines Consultants (T) Ltd;

Chanzo: List of Shame - Orodha ya Mafisadi
 
Asha Abdala,
Dr Slaa kasema hivi:- Je ni Serikali 100% Kama sivyo Serikali inahusika vipi na Trust hii...
Hapa akiwa na maana hata yeye hafahamu undani wa shirika hili..sioni mahala amesema siii la serikali.
Hakuna propaganda ikiwa hujaulizwa mbele ya sheria. Huyu ni mwanasheria wa shirika iweje amwage vitu tuu kwa sababu Dr. Slaa kasema.. Utaratibu upo na rahisi kabisa mnashindwa kitu gani kusimamaisha sheria!
Kwa kuanzia tu mnaweza ku raise issue ya BoT (chombo cha Taifa) kujitoa kwake mkataka maelezo na sababu, kisha hapo zitafummka habari kibao zikipandiana kama ngazi..mtafika tu kwa Warioba na Mwananchi Gold yenyewe ubia wake umetokana vipi..
Wana JF kama mtarejea hoja zangu kuhusu BOT ni pamoja na Mwananchi. Nyaraka nilizotaja ni pamoja na majina na registration na ya Makampuni yote yaliyohusika. Ndiyo maana katika hatua hii, ningelipenda Mhe. Warioba kwa vile ni mhusika mkuu, atupe details zote. Let us not put the cart before the horse". Nina hakika hatimaye tutafika. Yako Mengi ambayo Serikali bado haijajibu, mathalan Deep Green Finance Co. Ltd, Deep Green Company Ltd. Ni makosa mtu kufikiria kwamba hapa kuna swala la siasa wakati tunapambana kuokoa rasilimali za Taifa. Nadhani tukubaliane mambo ya msingi yasichanganywe na siasa kwa maana ya propaganda. Kwa bahati mbaya Bunge linafanya kazi kwa Taratibu na Kanuni na ili tupate manufaa kamili ya Kanuni ni vizuri tukawanasubira ili tusimwage mchele kwa kuku mapema. Lakini kuhoji kwangu kuna toa nafasi ya kutafuta ukweli kwa njia zote zinazoweza kupatikana. Siyo Warioba tu, na hata yeyote mwingine mwenye taarifa ya makampuni haya ni vema pia akatusaidia.
 
Asha Abdala,
Dr Slaa kasema hivi:- Je ni Serikali 100% Kama sivyo Serikali inahusika vipi na Trust hii...
Hapa akiwa na maana hata yeye hafahamu undani wa shirika hili..sioni mahala amesema siii la serikali.
Hakuna propaganda ikiwa hujaulizwa mbele ya sheria. Huyu ni mwanasheria wa shirika iweje amwage vitu tuu kwa sababu Dr. Slaa kasema.. Utaratibu upo na rahisi kabisa mnashindwa kitu gani kusimamaisha sheria!
Kwa kuanzia tu mnaweza ku raise issue ya BoT (chombo cha Taifa) kujitoa kwake mkataka maelezo na sababu, kisha hapo zitafummka habari kibao zikipandiana kama ngazi..mtafika tu kwa Warioba na Mwananchi Gold yenyewe ubia wake umetokana vipi..

Dr Slaa alishatimiza wajibu wake kama mbunge kwa kuuliza hii hoja mwaka 2008 ndani ya Bunge, kama utakumbuka ndio siku matangazo ya TBC yalikatizwa hewani na Star TV hawakurusha kwa hiyo umma haukuona jinsi serikali ilivyojikanyaga. Soma hotuba hii ya Dr Slaa utaona hoja zake kuhusu suala hili: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/14721-hotuba-ya-dk-slaa-bungeni-leo.html

Bado una swali?

Asha
 
Dr Slaa alishatimiza wajibu wake kama mbunge kwa kuuliza hii hoja mwaka 2008 ndani ya Bunge, kama utakumbuka ndio siku matangazo ya TBC yalikatizwa hewani na Star TV hawakurusha kwa hiyo umma haukuona jinsi serikali ilivyojikanyaga. Soma hotuba hii ya Dr Slaa utaona hoja zake kuhusu suala hili: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/14721-hotuba-ya-dk-slaa-bungeni-leo.html

Bado una swali?

Asha


Alishatimiza wajibu!? kwani wewe msemaji wake? kama sivyo umejuaje?

Dr Slaa anachangia wewe unaingilia ingilia kwa kusema katimiza wajibu wake, unamaana hupendi na hutaki aendelee kuulizwa maswali, kujibu maswali au kuchangia hoja humu?
 
Wana JF nadhani tunachanganya mambo. Ni vema tukapata ufafanuzi Wanahisa wa Mwananchi Trust ni nani hasa. Je ni Serikali 100% Kama sivyo Serikali inahusika vipi na Trust hii. Ninasema hivi kwa vile nyaraka za Brela nilizo nazo hazionyeshi hivyo.

Hazionyeshi hivyo vipi, hiyo ya Serikali kumiliki 100%? Kwani imedaiwa kuwa serikali ilimiliki 100%?

Unless Warioba kaongopa, mimi nadhani kaelezea hizi % za umiliki zikoje. Hakukuwa na mmiliki wa 100%.

Sasa Dr. Slaa, rekodi ulizonazo wewe zinapinganaje na za Warioba, zinasemaje?

Warioba.jpg
January 13, 2009

``Sasa katika hilo kama Serikali haitaki kumiliki hisa nyingi, na haitaki mtu wa nje awe na nyingi, ilibidi watafutwe wengine kuingia ili katika kampuni hiyo na wakaamua hao wengine wawe wa hapa ndani. Ziwe ni kampuni ndogo ndogo za hapa, ziingie mle, hiyo ndiyo iliyoleta kuundwa kwa kampuni ya pili inayoitwa Mwananchi Trust, hii ilikuwa mwavuli wa kampuni ndogo ndogo za hapa.

``Baada ya kukubaliana kwa hilo, wakakubaliana kuwa mfumo wa hisa uwe Serikali ingechukua asilimia 35, na ziligawanywa Benki Kuu ichukue 20 na NDC 15, mwekezaji wa nje angechukua 20% kwa hiyo jumla inafika 55%. Zilizobaki 45 zilikuwa ndani ya Mwananchi Trust.´´
 
Mkandara,

Unanifurahisha sana kwenye mjadala huu. Kweli mtu akipenda chongo huita Kengeza.

Yaani kila nikisoma maelezo ya hii kampuni, nashindwa kuelewa ilikuwaje mzee Warioba ambaye tunamjua kama mtu clean akiishia huko?

Hilo shirika lilikuwa mrija wa kutuibia, sawa tu na mashirika hayo mengine.

Mheshimiwa Dr. Slaa aatufumbua hata zaidi.
 
Mtanzania,
Shukran kwa maswali yako ambayo ni sehemu ya kujifunza...
Ila nadhani hakuna shirika hata moja la serikali ambalo wewe na mimi tunaweza kujibu maswali haya isipokuwa yale yaliyoanzishwa toka wakati wa Nyerere..

Lakini pamoja na yote haya ningeomba unambie ni kutokana na vitu gani umefikia kusema - 'Binafsi ni mpenzi wa miradi yetu kumilikiwa na Watanzania lakini sio mradi kama huu ambao usingelileta faida yoyote kwa mlipa kodi na hata hao wachimbaji wadogo wadogo.'

Kumbuka tu hapa hatuzungumzii tena warioba isipokuwa mradi wenyewe!..nipe sababu zilizokusukuma hadi kusema hivyo - naomnba darasa!

Mkandara,

Mbona nimeeleza kwenye maandishi yangu? Katika project yoyote tunapoangalia viability of the project ni pamoja na management team.

Madini yanachimbwa kwa sehemu kubwa kanda ya ziwa, unakuja jenga kiwanda Dar? Why?

Lakini kikubwa pamoja na kutumia mabilioni ya pesa sioni mahali popote wanaongelea management team ya kampuni.

Siku hizi kwenye balancesheet ya kampuni wanaongeza na intangible assets kama wafanyakazi ambao wanaweza kubadili shirika bovu kuwa zuri. Mfano google hawana tangible assets nyingi lakini balancesheet yao ni nono kwasababu ya intangible assets ambazo kwa sehemu kubwa ni matokeo ya ujuzi wa wafanyakazi wao.

Sasa mzee Warioba pamoja na kuunguza hayo mapesa, kwenda kusomesha watu nje, kununua mitambo, kununua uwanja bado hawezi hata kusema nani alikuwa au ni CEO wa hiyo kampuni. Nani alikuwa anatoa maamuzi yote hayo muhimu?

Mkandara kama una pesa za kutupa basi unaweza kuwekeza kwenye miradi inayoongozwa na wanasiasa ambao hawajawahi hata kuanzisha kaduka ka kuuza pipi.
 
JF Pamoja na maelezo mazuri yaliyowekwa na Mhe. Warioba nadhani kuna maswali kadhaa bado yanahitaji kujibiwa. Je haya makampuni yote yaliyotajwa ni ya kina nani, nani hasa Share holders wake. Nadhani bado kuna jambo zito limejificha hapo. Tungependa Mhe. Warioba atusaidie kupata ufumbuzi wa hili. Katika maelezo yake yote inaelekea mradi wote ni wa Serikali na uko kwa msukumo wa Serikali, jambo ambalo records tulizonazo zinaonyesha tofauti. Mhe. Warioba pasua jipu. Dr. Slaa

Kwa kuwa serikali haitaki kusema ukweli kuhusu suala hili, ni wakati muafaka sasa kwa wabunge hasa Dr. Slaa na wenzako kwa kushirikiana na wabunge wengine wa CCM wenye ujasiri wa kutetea maslahi ya Taifa, kupeleka hoja binafsi Bungeni ya kuundwa kwa kamati teule ya Bunge ili ichunguze na kuleta majibu sahihi kuhusiana na Mwananchi Gold. Nina amini kwa kufanya hivi, kamati itawaita watu wote wenye taarifa na ushahidi, au mtu yeyote ambaye kamati itaona anaweza kutoa taarifa muhimu za kusaidia kupata ukweli wa jambop lenyewe.

Ni kwa njia hii tu, pumba na mchele vitatenganishwa na ukweli kufahamika, na hatimaye suala hili kufikia tamati. Ninadhani, kwa mfano, Jaji Warioba aki-appear mbele ya tume ya bunge akaulizwa maswali na kutoa yote anayoyafahamu kuhusana na hii kampuni, hapo, mzizi wa fitina utakuwa umekatwa.
 
August,
Naona umelisoma tamshi la Warioba kwa miwani ya mbao. Ni wapi inaonyesha amekuwa na tamaa? Ni wapi ameonyesha ameshalipwa mshahara kwa kusaidia kuanzisha kampuni hiyo? Soma tena. Usijazie tu kwa dhana zako.

tamaa inakuja kwenye kuwa share holder kwa minajili ya kupata dividend, hayo ya mshahara umeongeza wewe, mimi nimesema analipwa Pensheni ya viongozi mpaka Mungu atakapo mchukua, sasa sijui mwenye miwani ya mbao au makengeza ni mimi au wewe? na hapo hapo wewe ulicho ona kibaya katika contribution yangu ni hilo tu? mbona huja zungumzia mengine? au ndio spinning yenyewe, uongo uwe ukweli na ukweli huo uongo? nakuomba usiweke dhana zako, na ujaribu kuwa un-expound akili yako? unless uniambie ulipoandika hii ilikuwa hauna sound mind kwa sababu mojanyingine au ulikuwa bado na usingizi
 
Last edited:
Madini yanachimbwa kwa sehemu kubwa kanda ya ziwa, unakuja jenga kiwanda Dar? Why?

Mkuu Mtanzania, madini hayachimbwi kanda ya ziwa peke yake. Kuna madini Ruvuma na hata Tabora. Location ya kiwanda inategemea zaidi strategies walizokuwa nazo.

QUOTE]Lakini kikubwa pamoja na kutumia mabilioni ya pesa sioni mahali popote wanaongelea management team ya kampuni.[/QUOTE]

Nadhani Warioba hakuwa na kusudio la kuzungumzia management team ya kampuni. Alichokuwa akifanya ni kuongelea kusudio la kuanzisha Mwananchi Gold, manufaa ya kuwa na kampuni kama hiyo, na masikitiko yake kuhusu kusudio la kuiua kampuni hiyo. Kama kuna mtu anaetaka kujua muundo mzima (human resource) ya kampuni, nadhani anaweza kutafuta taarifa hizo (sijui zina manufaa gani). Warioba alikuwa Mwenyekiti wa Board na wala sio Mkurugenzi mtendaji wa kampuni kama inavyoelekea kufikiriwa na baadhi ya wachangiaji.

Sasa mzee Warioba pamoja na kuunguza hayo mapesa, kwenda kusomesha watu nje, kununua mitambo, kununua uwanja bado hawezi hata kusema nani alikuwa au ni CEO wa hiyo kampuni. Nani alikuwa anatoa maamuzi yote hayo muhimu?

Nadhani ilishawahi kuelezwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mwananchi Gold alitoka BoT (jina limenitoka).
 
Mkuu Mtanzania, madini hayachimbwi kanda ya ziwa peke yake. Kuna madini Ruvuma na hata Tabora. Location ya kiwanda inategemea zaidi strategies walizokuwa nazo.

QUOTE]Lakini kikubwa pamoja na kutumia mabilioni ya pesa sioni mahali popote wanaongelea management team ya kampuni.

Nadhani Warioba hakuwa na kusudio la kuzungumzia management team ya kampuni. Alichokuwa akifanya ni kuongelea kusudio la kuanzisha Mwananchi Gold, manufaa ya kuwa na kampuni kama hiyo, na masikitiko yake kuhusu kusudio la kuiua kampuni hiyo. Kama kuna mtu anaetaka kujua muundo mzima (human resource) ya kampuni, nadhani anaweza kutafuta taarifa hizo (sijui zina manufaa gani). Warioba alikuwa Mwenyekiti wa Board na wala sio Mkurugenzi mtendaji wa kampuni kama inavyoelekea kufikiriwa na baadhi ya wachangiaji.



Nadhani ilishawahi kuelezwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mwananchi Gold alitoka BoT (jina limenitoka).[/QUOTE]

Recta,

Kama mawazo ya Watanzania ndio hayo no wonder mashirika yetu yote ya umma yamekufa.

Unavyoongelea utendaji wa shirika, unaongelea CEO. Sasa mazungumzo yote haya hata hatujui CEO alikuwa nani? Mabilioni ya umma yametumika kwa maamuzi ya akina Warioba na unataka kutuambia mradi kama huo ni viable huku hata uongozi wa kampuni haujulikani?

Mtu yeyote anayejua biashara asingelijenga hicho kiwanda Dar labda kama strategy ya hilo shirika ilikuwa ni siasa zaidi ya uchumi. Ni asilimia ngapi ya dhahabu ya Tanzania inatoka Ruvuma?

Mwananchi Gold haina tofauti na IPTL, Richmond, miradi ya Mzindakaya pamoja na mingine.

Huhitaji hata kuwa mchumi au mjuzi wa sheria kujua jinsi conflict of interest ilivyotapakaa kila sehemu.

Kama mradi ni viable si waende kukopa pesa toka bank?

Nimeuliza maswali mengi ya msingi kwenye hili na hakuna aliye na majibu.

Kweli utaendesha mradi mkubwa kama huu bila management team inayoeleweka? NI UBABAISHAJI ULE ULE WA WATANZANIA, matokeo yake wageni wanakuja, wanafanikiwa, tunaonekana Watanzania wote mbumbumbu shauri ya hawa wanasiasa wetu uchwara.
 
Back
Top Bottom