.......hata kwenye hiyo namba {1} bado Warioba ana maswali mengi ya kujibu:
Kama tutakuwa makini tutampata mbaya wetu kupitia kauli hii ya Warioba. Hata kama Serikali ikikaa kimya Warioba anapaswa kufikishwa Kisutu ili tumjue mdudu anayeimaliza Tanzania.
- kwanini tangu awali hakumshauri mteja wake (Serikali) achapishe nia yake ya kutumia kodi ya wananchi kupitia Government Gazzete?
- kwanini alikaa kimya ilhali akijua Serikali, ambayo tayari ilishakana Azimio la Arusha kupitia lile la siri la Zanzibar, inajiingiza kwenye biashara pasipo ridhaa ya wananchi?
- Kwanini hakuwa muungwana kuweka bayana upatikanaji wa hisa za kampuni hiyo ili wananchi na vyama vingine vya siasa wapate hisa (kama anadai "CCM Trust Company" ni mali ya SSM?
-
- Hakuna anayemchukia Warioba, ila ukweli kama wanavyosema viongozi wengi anajichukia mwenyewe, kwa sababu kwa nini ujifanye kimbele mbele na kupigia makelele ufisadi wakati wewe mwenyewe sio msafi? Sasa this is the best showdown ever, maana ninaamini within serikali ya sasa kuna mafisadi wanaotaka kumkata ngebe ngebe na yeye anadai anayajua yao na atajibu, saafi sana sasa waanikane ili wananchi tujue ukweli na tuweze kuwachambua vizuri nani ni nani wa kutinga Kisutu.
Duh, Mbona siwaelewi?
Jamani ......wowote.
Pili ushiriki wake na Kampuni yake ameusema bayana. Kama unavyojua, Memorandum and Articles of Association za Kampuni yoyote huandaliwa na wana sheria. Kampuni yake ilipewa kazi ya kufanya hivyo, pamoja na ushauri mwingine wa kisheria endapo utahitajika wakati wowote kabla na baada ya kuanzishwa kwa Kampuni hiyo (hii ameisema vizuri katika taarifa hapo juu Sijaona mahali anaposema alikuwa mwendeshaji wa Kapuni hiyo (labda kama kuna mtu anaweza kunisaidia hilo).
......hiyo.
Warioba's firm could have been contracted by the Attorney General to provide legal advice to the Mwananchi Company. I think the key issue ni ku-determine ni nani katika serikali aliyeiajiri hiyo legal firm ya Warioba. There are many precedents where the AG Chambers has hired private lawyers and/or legal firms to represent the Government even in court cases [including in conducting prosecution cases]. This is a very common practice especially in the Commonwealth countries!
In my opinion Nd. Warioba is justified to be concerned when rumours and innuendos are circulated around [including in the press] that he is about to be prosecuted. Whoever is in charge of this case in the Government should be more professional rather than spreading half truths and innuendos which just tarnish peoples names.
Warioba ana kila right ya kuwa concerned..nakumbuka miaka mitatu iliyopita kabla hata Kikwete hajakamata Kiti cha Ikulu aliwahi kuzungumzia Ufisadi nchini na watu walikuja mbogo wakimhusisha yeye na kampuni hii..Sasa ukweli umedhihirika na kipande hiki kimeniacha hoi..Uamuzi wa kuanzishwa kwa Kampuni ya Mwananchi Gold ulitokana na nia njema ya serikali. Alisema mradi uliokuwa ukiendeshwa na kampuni hiyo, ungeisaidia Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kuhifadhi dhahabu hapa nchini na ungeisaidia serikali kujua kiasi cha dhahabu kinachopatikana hapa nchini kuliko ilivyo hivi sasa ambapo dhahabu inachimbwa na kusafirishwa nje ya nchi kwa ajili ya kusafishwa, jambo linalosababisha taifa kushindwa kujua kiasi kinachochimbwa na mchimbaji.
"Watanzania wengi wanaitizama kampuni hiyo kama ni ya kifisadi, wakati ukweli ni kwamba uamuzi wa kuanzishwa kwake ulikuwa wa serikali ambayo ilikuwa ikitekeleza sera yake ya kuwasaidia wachimbaji wadogo wadogo ili waweze kusafisha dhahabu zao hapa nchini na kuziuza kwa bei halali.
"Ninasikitika kumekuwa na maneno mengi ya kupotosha kuhusu uanzishwaji wa kampuni hii na uamuzi wa serikali kulikalia kimya suala hili pasipo kueleza ukweli kuhusu kampuni hii, umenisikitisha zaidi," alisema Jaji Warioba.
Akizungumza kuhusu alivyoshiriki katika kuanzisha kampuni hiyo, alisema Kampuni ya uwakili ya Nyalali, Warioba & Mahalu, Law Associates, ambayo yeye ni mmoja wa mawakili wanaoimiliki, iliombwa na serikali kutoa huduma ya kisheria kusaidia kuundwa kwa kampuni hiyo.
Alisema, kampuni yake ilifanya kazi hiyo kama ilivyoombwa na serikali na kuiwezesha kununua kiwanja cha ekari 30, kilichopo eneo la Vingunguti, jijini Dar es Salaam ambako kulifungwa mashine za kusafishia madini na ilizinduliwa rasmi na Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, Desemba mosi mwaka 2005.
Jaji Warioba alisema, kampuni hiyo ilianza kufanya kazi kwa kununua dhahabu kutoka kwa wachimbaji wadogo wa wilayani Geita, lakini baadaye alishangazwa na uamuzi wa serikali wa kukataa kuendeleza mradi huo uliokuwa na tija kwa taifa.
Serikali iliamuru BoT na Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) na Kampuni ya MA-CE ya Italia kuunda kampuni hiyo. Baada ya uamuzi huo, serikali ilikuja kwenye ofisi yetu ya uwakili ya Nyalali, Warioba & Mahalu Law Associates ili tuisaidie kuipatia huduma ya kisheria kabla na baada ya kuundwa kwa kampuni hiyo...
Wanabodi,
Nafikiri watu hamlichukulii swala hili kwa makini lakini ukisomna maelezo ya Warioba, bila shaka mzee huyu yuko CLEAN.
Kifupi nia ya serikali kuanzisha Mwananchi hata mimi ningekubali tena ningemsifia sana Mkapa..lakini changa hili ni sawa kabisa na issue ya WMD ambayo senate waliingizwa mkenge..Kinachonipa shida kubwa ni Mkapa huo mwaka 2005 ambao ufisadi wote ulitembea within the last three month kabla Mkapa hajaondoka Ikulu.
Hivi kweli Mkapa alikuwa na nia njema na nchi yetu! hivi kweli kuna mtu anaweza kumsifia Mkapa pindi anapoweza maazimio mazuri kama haya kisha anakuja yavunja yeye mwenyewe!
Ebu rudieni maelezo haya kisha mnambie tungekuwa wapi leo hii...
Warioba ana kila right ya kuwa concerned..nakumbuka miaka mitatu iliyopita kabla hata Kikwete hajakamata Kiti cha Ikulu aliwahi kuzungumzia Ufisadi nchini na watu walikuja mbogo wakimhusisha yeye na kampuni hii..Sasa ukweli umedhihirika na kipande hiki kimeniacha hoi..
Mkubwa hoja yake ni YEYE mwenyewe sio Mwananchi Gold.. tofauti na mfano wa Richmond au rada. Warioba anataka kujisafisha yeye mwenyewe kutokana na macho ya watu.. Ameonyesha wazi kwamba yeye ni wakili tu akiyeajiriwa kama wakili kiasi kwamba Mwananchi inaweza kum dump hata kesho..Kwa hiyo wasiwasi yenu ipelekeni Mwananchi Gold na sio kulihusisha jina lake na shirika hilo!.. nani wa kuwauliza kuhusiana na Mwananchi kawataja majina yao wazi hivyo tusimfanye yeye bangusilo!..U have a question nenda kawaiulize hao....kulikoni!Kama yupo safi preemptive strike ya nini
Kama unavyofahamu kazi ya mawakili ni sawa na mwanamke malaya, unapompaka mtu mavi jina lake wateja hukimbia..
Kampuni ya Umoja inamilikiwa na familia ya Warioba, kampuni ya VMB inamilikiwa na familiaya Mahalu, kampuni ya YM inamilikiwa Yussuf Mushi, kampuni ya CCM Trust wenye hisa ni Warioba na Yussuf Mushi na si wadhamini wa CCM. Kazi kwenu
Zakumi,
Mkubwa hoja yake ni YEYE mwenyewe sio Mwananchi Gold.. tofauti na mfano wa Richmond au rada. Warioba anataka kujisafisha yeye mwenyewe kutokana na macho ya watu.
Ameonyesha wazi kwamba yeye ni wakili tu akiyeajiriwa kama wakili kiasi kwamba Mwananchi inaweza kum dump hata kesho..Kwa hiyo wasiwasi yenu ipelekeni Mwananchi Gold na sio kulihusisha jina lake na shirika hilo!.. nani wa kuwauliza kuhusiana na Mwananchi kawataja majina yao wazi hivyo tusimfanye yeye bangusilo!..U have a question nenda kawaiulize hao....kulikoni!
Besides sote tumesikia habari za yeye kuvutwa Kisutu na kuna watu wamekwisha ongea naye akasema anasubiri kwa hamu lini ataitwa..na siku alotakiwa kuvutwa serikali yenyewe ndiyo iliahirisha..
Kama unavyofahamu kazi ya mawakili ni sawa na mwanamke malaya, unapompaka mtu mavi jina lake wateja hukimbia..wengi wanaogopa uchunguzi huo usije fungua hata mafaili yao hivyo kuna uwezekano mkubwa kwamba mbali na Warioba kuharibiwa jina, shirika NWM law firm inakosa wateja acha mbali swala la Mwananchi Gold..
Unamaanisha nini hapo juu brother kaka?
Unamaanisha nini hapo juu brother kaka?
Mheshimiwa, Enron ilifilisiwa kwa mtindo wa buy back. Ila Warioba na kundi lake wamecheza mchezo wa pay us. we pay you high you give me some.
Waliishauri serikali vibaya, wakijua wazi deal ni nini? kampuni yao ya uwakili ilifunguliwa kwa deal wakijua nini wanakifanya.
Anachokifanya warioba anaona maji ya shingo. mambo tanzania huwa yalikuwa yanafanyika wazi hivyo haonewi mtu ila wanyonge ndio tunaonewa kwani wazito ndio hao.
tanzania ni nchi ya ajabu sana, wastaafu, jaji na waziri mkuu wanakubali deal la kuliza nchi???? come on now.
Hawa ni wezi kama bado wewe ni mteja wao ulikuwa unajua nini unafuata sio huduma bali mchongo , sasa beba malipo.
reading between the lines: Kupigia kelele ufisadi ni kujifanya kimbele mbele, ndivyo wanavyosema viongozi wengi
sitaki kuamini kama mkuu FMES alitaka kumaanisha hivi
- JF kwa vichwa bwana, yaani kila ukidhani umemaliza kuhesabu vichwa, then comes kichwa zaidi, saafi sana mkuu hapa tupo pamoja!
Unajua wanasema bwana Yesu alikuwa na wanafunzi 12, waliomuona akifanya vitu vyake kila siku, lakini walipoambiwa kuandika chini kila mmoja alikuja na habari yake!
Mkuu Kinepi nepi ahsante sana kwa kufikisha huu ujumbe kama ulivyoandikwa na Warioba mwenyewe bila kupunguza wala kuongeza anything!