Ndumbayeye
JF-Expert Member
- Jan 31, 2009
- 7,333
- 3,896
kwani warioba kala shilingi ngapi? si keshasema hesabu zote ziko safi?
Mzee Warioba alichokifanya yeye ni kuandika chini kimya kimya.Halafu anamalizia kwa kuuliza aliye msafi aanze kumrushia huyu jiwe.Ile sasa anaanza kuinuka anashangaa HAONI HATA MMOJA ALOBAKI ili arushe ilo jiwe.
Hakuna kitu hapa.Go Mzee Warioba.
Nasema kamwe hatothubutu mtu kujaribu kufikiria kwenda kisutu kumshitaki.I bet now na nasubiri mwanakijiji ambae nae ka-bet tuone itakuwaje.
Jamani tusishangae serikali kuomba ushauri kutoka kwa law firm binafsi ya kina warioba.Nasakumbusha kuwa tusimuone jaji warioba kama jaji tuu msitaafu bali tukumbuke kuwa ni Waziri mkuu Mstaafu wa Tanzania hadi sasa.
Sijawahi kumpenda Warioba ila sasa mimi naanza kuwa big fan wake.Mzee hakurupuki huyu,halopoki,na kibaya yuko makini sana.sasa nyie CCM jifanye kuikana CCM Trust muone "mlima wa madocuments" hapo ndo mtajiju.
INaelekea katika kutafuta maendeleo ya haraka, serikali ilikiuka misingi mingi sana, ambayo sasa inaifanya (au kuwafanya viongozi wake) kuingia kwenye matatizo makubwa.
Nakubaliana na wengi kwamba, inawezekana kuwepo kwa utata katika uanzishwaji na uendeshaji wa Mwananchi Gold. Ila naamini kuwa kuwepo kwa mkono wa Serikali katika mchakato mzima, kulifanya walioshiriki katika uanzishwaji/uendeshaji huo, kuona kuwa kila kitu kilikuwa halali na sahihi kabisa (akiwemo Mzee Warioba). Kila baada ya chaguzi zinazosababisha kubadilika kwa Serikali, mambo mapya hufichuka. Mambo ya zamani huonekana hayafai, labda kwa kuwa yalikiuka taratibu ama hayakuwa na maslahi kwa watu au taasisi mpya zinazokuja na Serikali mpya. Yote yanawezekana.
Katika issue ya Mwananchi Gold, sijui nani atamshitaki nani. Maana Serikali, CCM, BoT na baadhi ya Kampuni zinaonekana kumiliki Mwananchi Gold. Labda wamiliki wote washitakiwe. Ila kumshitaki mmiliki mmoja, sijui kama itatosheleza mahitaji ya kisheria (naomba msaada hapo).
Itakapofika wakati ambapo Serikali ya awamu hii ikabadilika (kwa uchaguzi) baada ya kumaliza muda wake, watakaoingia nao wataanza kufukuafukua mambo yao vile vile. Nao watatueleza mengi sana.
Naona hii style ni nzuri sana na itasaidia kutupeleka kwenye rule of law na baadhi wanaopenda shortcut za maisha kuwa makini kama endapo watakubali kutumiwa dont you think so? I think we will ultimately agree kuunda system itakayolinda maslahi ya nchi na siyo inayolinda individual interest. NAIPENDA HII STYLE na naomba idumu mpaka hapo tutakapo nyooka na kukubali rule of law.