Elections 2010 Waraka wa Lowassa kwa vyombo vya habari

Hivi mwalimu alituachia amani na utulivu tu?
Mbona kipindi wanapotajwa kuwa wamechakachua rasimali za taifa hawazungumzii kuwa mwalimu alituachia maadili tusiyavurughe, wanakua wadogo kama femababaton +pilton!
 
Wana JF, sometimes tuwe tunatoa maoni kulingana na hali halisi sio siasa za chuki tu. hi barua kwa mtu makini inaonyesha wazi kwamba ilichongwa, na seems na wanachadema wenzetu kitu ambacho kinaharibu tu jina la chama. Ingekuwa kweli, kwa barua ya siri kama hio, hawangeweka majina, na cha kushangaza wakaweka majina ya JK, Ridhi, EL, Rostam eti na wengineo, kiserikali ilikuwa either waweke majina yote au wasiweke.

Lowasa ana alama na popote atakapokatisha ataonekana, leo aende mwanza aisionekane, na alisema hajawahi kwenda mwanza miaka zaidi ya 2!. na Pia JK ni Rais, eti aende tu Mwanza kwa ajili ya Kupanga kuchakachua kura, haiji akilini. na wachangiaji wanachangia tu bila kupima. tuongee facts tuache matusi yasiojenga ni uppuzi mtupu
 
Sipendi hawa mafisadi wanavyotumia kisingizio cha amani ili waachiwe kutawala na kutuibia? Sipendi hawa majangili wanavyoendelea kudanganya wananchi kwamba wanaenzi Amani na utulivu wakati wanadhulumu wananchi haki zao. Sipendi wananchi wanapoendelea kukubali maneno ya kuenzi Amani kutoka kwa wale wanaowanyonya?
 
TAARIFA RASMI KWA VYOMBO VYA HABARI NOVEMBA 5, 2010

Novemba 3, 2010 mgombea urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilbrod Slaa aliwatuhumu makada 30 wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuwa walifanya kikao cha kupanga mipango ya kumwibia kura mjini Mwanza. Kati ya makada aliowatuhumu ni pamoja na
mimi.

Napenda kuufahamisha umma kuwa habari hizi si za kweli kwa sababu mwezi wote wa Oktoba, nilikuwa jimboni kwangu nikifanya kampeni za kuwania kiti cha Ubunge katika Jimbo la Monduli. Sikupata kusafiri kwenda Mwanza hata siku moja, na siku aliyoitaja ya Oktoba 19, nilikuwa katika vijiji vya Mfereji na Enguiki nikifanya kampeni siku nzima.


Ukiacha tuhuma hizo, pia upo uvumi uliosambazwa kwamba nilishiriki kikao cha mikakati ya kuchakachua kura, mjini Arusha kumsaidia mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Batilda Burian aweze kushinda kiti hicho. Nasema uvumi huu ni uzushi na si wa kweli.


Kutokana na yote haya, ninakwazika kwamba inaonekana katika nchi yetu umeanza kuingia utamaduni mpya wa kufanya siasa za uongo, uvumi, uzushi na kila aina ya hila kwa nia ya kujipatia ushindi. Kwa uzoefu wa mataifa mengi yaliyotuzunguka, ndani ya Afrika na sehemu nyingine duniani, amani hupotea kutokana usambazaji wa taarifa za uongo.


Mwasisi wa Taifa hili, Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, alituachia amani na utulivu ambavyo ni tunu ya taifa hili.


Dalili zinazoonekana, kuna watu wanaelekea kuchoshwa na amani iliyopo.


Wanajiandaa kufanya vurugu, kuliingiza taifa hili katika machafuko, na sijui wanafanya hivyo kwa faida ya nani.


Wito wangu kwa Watanzania, ni kwamba tusiichoke amani. Amani tuliyonayo ndiyo imetutofautisha na mataifa mengi yaliyotuzunguka na kuifanya Tanzania kuwa nchi ya kupigiwa mfano. Tuelekeze nguvu zetu katika shughuli halali za kutuletea kipato zisizoharibu amani yetu.


Tukiiharibu amani tuliyonayo, mwisho wa siku nchi yetu itateketea na sote hatutakuwa salama. Tutakuwa tumekwisha.


Mwisho, namsihi Dk. Slaa ajipe muda wa kuzifahamu vyema siasa za nchi hii. Asidanganywe na mahudhurio ya mikutano ya hadhara akadhani ndizo kura katika masanduku ya kupigia kura. Namsihi ajifunze` zaidi jinsi ya kufanya siasa za kistaarabu bila kueneza uvumi, uongo, chuki na uzushi vyenye kutetelesha amani ya nchi yetu. Mungu ibariki Tanzania.



Edward Lowassa

Mbunge Mteule wa Monduli



Taarifa hii ya PM aliyejiuzulu kwa kashfa ya ufisadi ya Richmond imesambazwa kwa vyombo vya habari sasa hivi na: AIKA JUNIOR <aika_junior@yahoo.com>

- Kampeni za U-Rais 2015 zimeanza hizi, I smell fish kwani ilikuwa lazima amjibu Dr. Slaa kwenye hili na wakati huu? Mambo mangapi ametuhumiwa mbona hajawahi kujibu, wakuu JF tuamke hii ni kampeni tu hamna lolote hapo!

- Nia na madhumuni ya huu waraka ni kutuambia wananchi wa hili taifa kwamba mbona nimechaguliwa tena ina maana mimi ni msafi, na sasa ninaweza tena kuongea kwenye public na soon kugombea nafasi yoyote ya taifa, be careful na hawa wanasiasa!


FMEs!
 
Katika hili Lowassa kajisafisha nadhani waraka wa Dr Slaa ulikuwa wa bandia labda kama tutapata maelezo yake baada ya watuhumiwa kadhaa kukanusha na kueleza umma jinsi wasivyohusika na kikao cha siri kule mwanza.

kwa maneno mengine ni kwamba, tunahitaji maelezo ya ziada kutoka kwa Dr Slaa juu ya makanusho hayo

Dr. Slaa hakuandika waraka, ondoa ushenzi hapa. Unakimbilia kuchangia mada wakati bado hata hujajua kitu kinachojadiliwa
 
Jamani tamko la huu kiongozi wa richmound

lenyewe linachochea vujo, nani kasema chadema wanajiandaa kufanya fujo???
Hata dk. Mwenyewe hajasema kitu

wamechakachua mambo sasa wanaleta propaganda
 
- Kampeni za U-Rais 2015 zimeanza hizi, I smell fish kwani ilikuwa lazima amjibu Dr. Slaa kwenye hili na wakati huu? Mambo mangapi ametuhumiwa mbona hajawahi kujibu, wakuu JF tuamke hii ni kampeni tu hamna lolote hapo!

- Nia na madhumuni ya huu waraka ni kutuambia wananchi wa hili taifa kwamba mbona nimechaguliwa tena ina maana mimi ni msafi, na sasa ninaweza tena kuongea kwenye public na soon kugombea nafasi yoyote ya taifa, be careful na hawa wanasiasa!


FMEs!
Totally agree. Kampeni za 2015 zimeanza rasmi. Plus, kuna taarifa nimezipata [from credible/trusted sources] kuwa, nyaraka za kuhusu hiki kikao kinachodaiwa kufanyika Mwanza, ziliachiwa zileak kwa makusudi kabisa just to discredit Dr. Slaa. I mean, inasemekana kwamba CCM walikaa nchini wakamtafuta mtu ambaye alikuwa analeak mambo ya muhimu na ya siri siku za hapo nyuma [i.e., EPA, Richmond, Radar, Buzagwi, n.k] kwenda kwenye camp ya upinzani (especially kwenda kwa Dr.Slaa) na walipompata mtu huyo (chini ya usaidizi wa Usalama wa Taifa), basi wakaamua kucheza Pele. Kwanza, kikao hicho kikahairishwa. Pili, wakaandaa nyaraka feki kuwa kuna makada 30 walikuwa wakutane Mwanza October, 19 kujadili namna ya kuiba kula, at the same time, wakihakikisha kuwa hao makada 30, walikuwa wako sehemu tofauti/mbali na Mwanza siku hiyo. Mtakumbuka kuwa Gachuma alikuwa wa wanza kudai kuwa asingeweza kufikia/lala kwenye hotel iliyotajwa kwenye nyaraka hizo kwasababu ilikuwa chini ya hadhi yake. Rostam naye akafuatia akidai kuwa alikwa S. Africa. I'm pretty sure tutapata nyaraka nyingi (kama hii aliyoitoa Lowassa kwenda kwenye vyombo vya habari); zikimshtumu Dr. Slaa kama muongo, mchochoe vurugu na mtu anayetaka kuvunja/chafua amani Tanzania. Which, to my opinion, is a total lie and Bullsh*t!!
 
Hee ww Lowassa ww ndio fisadi mwekundu, umetuibia thru Richmond, sasa umetuibia Kura, umekuja A-Town kumsaidia ur kimada, haya yote ss tunakuangalia tu, sasa unaanza kusema ni uongo, uzushi, unasingizia amani itapotea, wakati umeiba fedha zetu zote thru richmond ulisema haya haya, uongo, umesingiziwa, uzushi, Sio Dr Slaa sisi tumekuona ulikuja hapa A-town kutaka kubadili matokeo, ww unatufanya sisi mazezeta, utajuta siku zikifika, ww ni mwizi, fisadi mkubwa, halafu unadhubutu kumtaja Nyerere huna hata haya, najua ulicheka & kushangilia sana Mwl alipo aga Dunia, tunajua, ww hakuna asiye kujua acha upuuzi wa kujisafisha, tunajua, tunakuona, ww ni mchafuuu hufai balaa wewe, nakuambia one word, soma nyakati peleka upupu wako huko umasaini
 
Mwizi naye atatuambia nini?
Wengine wawe wanajifunza kukaa kimya tu badala ya kubwabwaja maneno yasiyo na maana.
 
HIVI KWA NINI KILA ANAEGUSWA KUHUSU UTENDAJI WAKE ANAKIMBILIA KUSEMA """MSINIGUSE MKIFANYA HIVYO MTAHATARISHA AMANI YA NNCHI?????"""".....SWALA LA AMANI SASA LIMEKUWA KAMA NDO FICHO LA KILA ANAEKURUPUSHWA KWA UOZO WAKE....INACHEFUA SANA!!!!:A S angry:
Hebu waambie.. Eti ukiibiwa kura ukae kimya kisa, Amani! Kweli amani ya nchi ni ficho la mafisadi, uchakachuaji nk.
 
Tetesi na Radio Mbao zinasema Edward Ngoyai Lowassa atakuwa Waziri Mkuu mpya na Andrew Chenge atakuwa Spika wa Bunge.... Je tutapona hapo??

Mkuu kama ikitokea hiyo basi ujue kuwa ndio mwisho wa Tanzania. Lowassa kuwa PM na Chenge kuwa mbunge maana yake ni kuwa nothing will be going in the parliament, bunge litakuwa rubber stamp tu. Na kama Lowassa akiwa PM itakuwa yaleyale ya vituko kama vilivyopita. Even worse tutathibitisha kuwa Tanzania tu wajinga.
 
Wana JF, sometimes tuwe tunatoa maoni kulingana na hali halisi sio siasa za chuki tu. hi barua kwa mtu makini inaonyesha wazi kwamba ilichongwa, na seems na wanachadema wenzetu kitu ambacho kinaharibu tu jina la chama. Ingekuwa kweli, kwa barua ya siri kama hio, hawangeweka majina, na cha kushangaza wakaweka majina ya JK, Ridhi, EL, Rostam eti na wengineo, kiserikali ilikuwa either waweke majina yote au wasiweke.

Lowasa ana alama na popote atakapokatisha ataonekana, leo aende mwanza aisionekane, na alisema hajawahi kwenda mwanza miaka zaidi ya 2!. na Pia JK ni Rais, eti aende tu Mwanza kwa ajili ya Kupanga kuchakachua kura, haiji akilini. na wachangiaji wanachangia tu bila kupima. tuongee facts tuache matusi yasiojenga ni uppuzi mtupu

Jwagu, ili ku-balance habari nakubaliana nawe kuwa yaweza kuwa barua si ya kweli, lakini barua kama hii iliyowazi kwa umma inachafua majiana ya watu. Dr Slaa siku zote amesema kama lipo jambo linatatiza yeye yupo tayari kwenda mahakamani, na kwa mantiki hiyo wote waliotajwa na kuhisi wamechafuliwa majina njia muafaka ni kwenda mahakamani ili mahakama iwasafishe na si kutuma habari katika vyombo vya habari kama wanavyofanya. Ni mahakama pekee itakayotuambia ukweli, vinginevyo tutabaki kuamaini kuwa barua ni ya kweli.
Historia inaonyesha kuwa hata Slaa alipotaja orodha mwembe chai walisema ni mzushi na muongo, lakini walipoombwa kwenda mahakamani hata mmoja hakutokea. Mheshimiwa Bomani akatahadharisha kuwa kwenda mahakamani kungezua mambo makubwa zaidi.

Kwa EL, amani ya nchi haivunjwi kwa taarifa za barua,huvunjwa kwa uonevu ikiwa ni pamoja na kukusanya kodi za masikini wa Tanzania na kuingia mikataba yenye manufaa kwa kikundi cha watu wasiozidi 10. Genge hili la mafisadi ndilo limeitikisa nchi na wananchi kuhisi kuwa wanaonewa kwa kulipa kodi ili hali wake zao wakizalia juu ya matenga, na keki ya taifa kutafunwa na walafi wachache wakisaidiana na raia wenye asili za kigeni. Rais alisema pale diamond jubilee kuwa kujiuzulu kwako nchi imetetereka, pengine ni kwa kashfa maana tuna PM wengi waliopita na nchi haikutetereka, kwa hiyo ni wajibu wako kuelewa kuwa katika kipindi fulani cha uongozi wa nchi, uliwahi kusababisha mtetereko wa nchi. Hiyo ndiyo kuvunja amani kwa mtazamo wangu.Kabla huja sota kidole kwa Dr Slaa ulipaswa kutuomba radhi kwa kuteteresha nchi na amani halafu ndiyo usote kidole kwa wengine. Rejea hotuba ya JK Diamond.
Ni kweli mwalimu alituachia amani, nasi sote tunaitunza kwani ni wajibu wetu. Ikumbukwe kuwa hoja iliyopo mbele yetu ni kikao na kama hakikuwepo, basi wewe kama raia mwema na uliwahi kushika uongozi wa juu wa taifa unawajibika kukomesha uvumi wowote utakaovunja amani,hii ni pamoja na kumfikisha Dr Slaa mahakamani, kwa hiyo changamoto iliyo mbele yako si kumhukumu Dr Slaa mbele ya vyombo vya habari bali kuchukua hatua. Tunajua wazi kuwa ni viongozi waliokosa uadilifu walitumia vyombo vya habari kuvunja amani Rwanda, na kwahiyo wewe hupaswi kufuata njia hiyo bali njia sahihi ya mahakama.
Mhe El, mbona wakati taifa linaporwa ukiwa PM kwa mikataba feki hukugusia wosia wa mwalimu wala madhara ya uvunjifu wa amani? Katika kadhia iliyopelekea wewe kujiuzulu hata siku moja hukuwahi kumnukuu mwalimu, vipi leo imekuwaje? Kama unapenda amani kwa dhati ya moyo wako tuambie ninini EPA, Richmondul, Green.., meremeta, n.k. Vinginevyo wapi unapata moral authority ya kumkemea Dr Slaa ambaye kwa kiwango chochote kiwacho ameonyesha mapenzi na uchungu na taifa hili.?
Mwisho, suala lililopo mbele ni barua, sijui wingi wa watu katika mikutano ya Dr Slaa vinawiana vipi na hoja iliyo mbele yetu. Mrema anapenda kubebwa na hajawahi kuvunja amani kwa kubebwa na wala si issue kwa watanzania. Kama Dr Slaa anapenda crowd ili mradi havunji sheria kuna kosa gani. Mheshimiwa, jibu hoja ya barua na si personal attack. Huu ni udhaifu mkubwa wa kujieleza kama ulivyofanya pale bungeni.
Napenda kukushauri kuwa kwa siasa za Tanzania ni bora utulie monduli na kuendeleza watu wako, kama ipo ndoto ya kurejea madarakani hiyo ni yako binafsi, lakini kuendelea kuwasiliana na umma ukiwa bado na makovu ya kashafa haikusaidii. Kama unapenda amani na chama chako, basi kaa kando kwani nguvu ya umma ''people's power'' imeonekana, na ni ushahidi kuwa kashfa zilizozuka nyakati zako za uongozi zinaweza kuwa zimechangia kuwatia hasira wananchi na wakaamu kutoa adhabu kwa kupitia sanduku la kura. Pengine huu ni mwanzo ipo siku yote yaliyofichwa chini ya kapeti yatawekwa hadharani na wahusika watawajibika. Kamuzu Banda analijua hili vema huko aliko.
 
TAARIFA RASMI KWA VYOMBO VYA HABARI NOVEMBA 5, 2010

Novemba 3, 2010 mgombea urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilbrod Slaa aliwatuhumu makada 30 wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuwa walifanya kikao cha kupanga mipango ya kumwibia kura mjini Mwanza. Kati ya makada aliowatuhumu ni pamoja na
mimi.

Napenda kuufahamisha umma kuwa habari hizi si za kweli kwa sababu mwezi wote wa Oktoba, nilikuwa jimboni kwangu nikifanya kampeni za kuwania kiti cha Ubunge katika Jimbo la Monduli. Sikupata kusafiri kwenda Mwanza hata siku moja, na siku aliyoitaja ya Oktoba 19, nilikuwa katika vijiji vya Mfereji na Enguiki nikifanya kampeni siku nzima.


Ukiacha tuhuma hizo, pia upo uvumi uliosambazwa kwamba nilishiriki kikao cha mikakati ya kuchakachua kura, mjini Arusha kumsaidia mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Batilda Burian aweze kushinda kiti hicho. Nasema uvumi huu ni uzushi na si wa kweli.


Kutokana na yote haya, ninakwazika kwamba inaonekana katika nchi yetu umeanza kuingia utamaduni mpya wa kufanya siasa za uongo, uvumi, uzushi na kila aina ya hila kwa nia ya kujipatia ushindi. Kwa uzoefu wa mataifa mengi yaliyotuzunguka, ndani ya Afrika na sehemu nyingine duniani, amani hupotea kutokana usambazaji wa taarifa za uongo.


Mwasisi wa Taifa hili, Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, alituachia amani na utulivu ambavyo ni tunu ya taifa hili.


Dalili zinazoonekana, kuna watu wanaelekea kuchoshwa na amani iliyopo.


Wanajiandaa kufanya vurugu, kuliingiza taifa hili katika machafuko, na sijui wanafanya hivyo kwa faida ya nani.


Wito wangu kwa Watanzania, ni kwamba tusiichoke amani. Amani tuliyonayo ndiyo imetutofautisha na mataifa mengi yaliyotuzunguka na kuifanya Tanzania kuwa nchi ya kupigiwa mfano. Tuelekeze nguvu zetu katika shughuli halali za kutuletea kipato zisizoharibu amani yetu.


Tukiiharibu amani tuliyonayo, mwisho wa siku nchi yetu itateketea na sote hatutakuwa salama. Tutakuwa tumekwisha.


Mwisho, namsihi Dk. Slaa ajipe muda wa kuzifahamu vyema siasa za nchi hii. Asidanganywe na mahudhurio ya mikutano ya hadhara akadhani ndizo kura katika masanduku ya kupigia kura. Namsihi ajifunze` zaidi jinsi ya kufanya siasa za kistaarabu bila kueneza uvumi, uongo, chuki na uzushi vyenye kutetelesha amani ya nchi yetu
. Mungu ibariki Tanzania.



Edward Lowassa

Mbunge Mteule wa Monduli



Taarifa hii ya PM aliyejiuzulu kwa kashfa ya ufisadi ya Richmond imesambazwa kwa vyombo vya habari sasa hivi na: AIKA JUNIOR <aika_junior@yahoo.com>

Julius Nyerere alisema kuna baadhi ya watu wakisema jambo ni vizuri kwanza kuwaangalia usoni. Ukiwaangalia usoni unaweza kujua kama kweli wanachosema kinatoka moyoni au wanazuga, na pili angalia matendo yao na tatu angalia rekodi yao. Anachoongea Lowassa ni mjinga ndiye anaweza kukubali.
 
2015 .......................................let us start campaigns now................... we want EL to be now man.:rip:

Duh kazi kweli TZ.
 
kitu kizuri kuliko vyote ni kwamba, hata wale wanaowatuma kufanya mambo, wanawageuka..documment wanazowatuma kuzipeleka wanasifujisha kwa wapinzani. kwa wale waliokuwa karibu na mapolisi kipindi cha uchaguzi, wengi walienda kupigia chama cha chadema kwani hata wao wameichoka ccm. na wakati ule wa kampeni, wapinzani si walikuwa wanalindwa, wale mapolisi walinzi, mpinzani kama slaa akiongea point walikuwa wanatikisa vichwa bila wao kujiona...hahaha.
 
Watz tuchague kati ya maneno haya ya viongozi wetu wa zamani. Kama EL anaweza kujibu ivi,mbona hakujibu kuwa yeye si fisadi. Angeongeza ivi: "Watz mi pia si fisadi, tarehe xxx mwaka Xx ndo nilipata mali zangu,namiliki ngome xxx za urithi, mi similiki mji nilioujenga uko kaskazin,sina migodi,sikuhujumu taifa,mi ni msafi si fisadi kati ya wale 11 kwenye list of shame,kwa iyo dr.ni mzushi anataka tupoze amani tuliyoirithi!" My view: ivi dr.akitutajia uovu wa watawala ndo amani inatoweka? Dr.akitaja list of shame amani inatoweka? Au amani itakuwepo pale tu tukiwasujudu mafisadi na kutoweka punde tu pale dr.akihoji! Ivi maana ya amani imebadilika? Au akitajwa mwizi wa mali ya umma basi amani inatoweka,ama kweli Tz imetekwa! Ina maana Tz amani italindwa pale tu mamwinyi wanapolinda! Ama kweli hii ndo bongo!
 
Back
Top Bottom