TAARIFA RASMI KWA VYOMBO VYA HABARI NOVEMBA 5, 2010
Novemba 3, 2010 mgombea urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilbrod Slaa aliwatuhumu makada 30 wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuwa walifanya kikao cha kupanga mipango ya kumwibia kura mjini Mwanza. Kati ya makada aliowatuhumu ni pamoja na
mimi.
Napenda kuufahamisha umma kuwa habari hizi si za kweli kwa sababu mwezi wote wa Oktoba, nilikuwa jimboni kwangu nikifanya kampeni za kuwania kiti cha Ubunge katika Jimbo la Monduli. Sikupata kusafiri kwenda Mwanza hata siku moja, na siku aliyoitaja ya Oktoba 19, nilikuwa katika vijiji vya Mfereji na Enguiki nikifanya kampeni siku nzima.
Ukiacha tuhuma hizo, pia upo uvumi uliosambazwa kwamba nilishiriki kikao cha mikakati ya kuchakachua kura, mjini Arusha kumsaidia mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Batilda Burian aweze kushinda kiti hicho. Nasema uvumi huu ni uzushi na si wa kweli.
Kutokana na yote haya, ninakwazika kwamba inaonekana katika nchi yetu umeanza kuingia utamaduni mpya wa kufanya siasa za uongo, uvumi, uzushi na kila aina ya hila kwa nia ya kujipatia ushindi. Kwa uzoefu wa mataifa mengi yaliyotuzunguka, ndani ya Afrika na sehemu nyingine duniani, amani hupotea kutokana usambazaji wa taarifa za uongo.
Mwasisi wa Taifa hili, Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, alituachia amani na utulivu ambavyo ni tunu ya taifa hili.
Dalili zinazoonekana, kuna watu wanaelekea kuchoshwa na amani iliyopo.
Wanajiandaa kufanya vurugu, kuliingiza taifa hili katika machafuko, na sijui wanafanya hivyo kwa faida ya nani.
Wito wangu kwa Watanzania, ni kwamba tusiichoke amani. Amani tuliyonayo ndiyo imetutofautisha na mataifa mengi yaliyotuzunguka na kuifanya Tanzania kuwa nchi ya kupigiwa mfano. Tuelekeze nguvu zetu katika shughuli halali za kutuletea kipato zisizoharibu amani yetu.
Tukiiharibu amani tuliyonayo, mwisho wa siku nchi yetu itateketea na sote hatutakuwa salama. Tutakuwa tumekwisha.
Mwisho, namsihi Dk. Slaa ajipe muda wa kuzifahamu vyema siasa za nchi hii. Asidanganywe na mahudhurio ya mikutano ya hadhara akadhani ndizo kura katika masanduku ya kupigia kura. Namsihi ajifunze` zaidi jinsi ya kufanya siasa za kistaarabu bila kueneza uvumi, uongo, chuki na uzushi vyenye kutetelesha amani ya nchi yetu. Mungu ibariki Tanzania.
Edward Lowassa
Mbunge Mteule wa Monduli
Taarifa hii ya PM aliyejiuzulu kwa kashfa ya ufisadi ya Richmond imesambazwa kwa vyombo vya habari sasa hivi na: AIKA JUNIOR <aika_junior@yahoo.com>
Katika hili Lowassa kajisafisha nadhani waraka wa Dr Slaa ulikuwa wa bandia labda kama tutapata maelezo yake baada ya watuhumiwa kadhaa kukanusha na kueleza umma jinsi wasivyohusika na kikao cha siri kule mwanza.
kwa maneno mengine ni kwamba, tunahitaji maelezo ya ziada kutoka kwa Dr Slaa juu ya makanusho hayo
Totally agree. Kampeni za 2015 zimeanza rasmi. Plus, kuna taarifa nimezipata [from credible/trusted sources] kuwa, nyaraka za kuhusu hiki kikao kinachodaiwa kufanyika Mwanza, ziliachiwa zileak kwa makusudi kabisa just to discredit Dr. Slaa. I mean, inasemekana kwamba CCM walikaa nchini wakamtafuta mtu ambaye alikuwa analeak mambo ya muhimu na ya siri siku za hapo nyuma [i.e., EPA, Richmond, Radar, Buzagwi, n.k] kwenda kwenye camp ya upinzani (especially kwenda kwa Dr.Slaa) na walipompata mtu huyo (chini ya usaidizi wa Usalama wa Taifa), basi wakaamua kucheza Pele. Kwanza, kikao hicho kikahairishwa. Pili, wakaandaa nyaraka feki kuwa kuna makada 30 walikuwa wakutane Mwanza October, 19 kujadili namna ya kuiba kula, at the same time, wakihakikisha kuwa hao makada 30, walikuwa wako sehemu tofauti/mbali na Mwanza siku hiyo. Mtakumbuka kuwa Gachuma alikuwa wa wanza kudai kuwa asingeweza kufikia/lala kwenye hotel iliyotajwa kwenye nyaraka hizo kwasababu ilikuwa chini ya hadhi yake. Rostam naye akafuatia akidai kuwa alikwa S. Africa. I'm pretty sure tutapata nyaraka nyingi (kama hii aliyoitoa Lowassa kwenda kwenye vyombo vya habari); zikimshtumu Dr. Slaa kama muongo, mchochoe vurugu na mtu anayetaka kuvunja/chafua amani Tanzania. Which, to my opinion, is a total lie and Bullsh*t!!- Kampeni za U-Rais 2015 zimeanza hizi, I smell fish kwani ilikuwa lazima amjibu Dr. Slaa kwenye hili na wakati huu? Mambo mangapi ametuhumiwa mbona hajawahi kujibu, wakuu JF tuamke hii ni kampeni tu hamna lolote hapo!
- Nia na madhumuni ya huu waraka ni kutuambia wananchi wa hili taifa kwamba mbona nimechaguliwa tena ina maana mimi ni msafi, na sasa ninaweza tena kuongea kwenye public na soon kugombea nafasi yoyote ya taifa, be careful na hawa wanasiasa!
FMEs!
Hebu waambie.. Eti ukiibiwa kura ukae kimya kisa, Amani! Kweli amani ya nchi ni ficho la mafisadi, uchakachuaji nk.HIVI KWA NINI KILA ANAEGUSWA KUHUSU UTENDAJI WAKE ANAKIMBILIA KUSEMA """MSINIGUSE MKIFANYA HIVYO MTAHATARISHA AMANI YA NNCHI?????"""".....SWALA LA AMANI SASA LIMEKUWA KAMA NDO FICHO LA KILA ANAEKURUPUSHWA KWA UOZO WAKE....INACHEFUA SANA!!!!:A S angry:
Tetesi na Radio Mbao zinasema Edward Ngoyai Lowassa atakuwa Waziri Mkuu mpya na Andrew Chenge atakuwa Spika wa Bunge.... Je tutapona hapo??
Wana JF, sometimes tuwe tunatoa maoni kulingana na hali halisi sio siasa za chuki tu. hi barua kwa mtu makini inaonyesha wazi kwamba ilichongwa, na seems na wanachadema wenzetu kitu ambacho kinaharibu tu jina la chama. Ingekuwa kweli, kwa barua ya siri kama hio, hawangeweka majina, na cha kushangaza wakaweka majina ya JK, Ridhi, EL, Rostam eti na wengineo, kiserikali ilikuwa either waweke majina yote au wasiweke.
Lowasa ana alama na popote atakapokatisha ataonekana, leo aende mwanza aisionekane, na alisema hajawahi kwenda mwanza miaka zaidi ya 2!. na Pia JK ni Rais, eti aende tu Mwanza kwa ajili ya Kupanga kuchakachua kura, haiji akilini. na wachangiaji wanachangia tu bila kupima. tuongee facts tuache matusi yasiojenga ni uppuzi mtupu
TAARIFA RASMI KWA VYOMBO VYA HABARI NOVEMBA 5, 2010
Novemba 3, 2010 mgombea urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilbrod Slaa aliwatuhumu makada 30 wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuwa walifanya kikao cha kupanga mipango ya kumwibia kura mjini Mwanza. Kati ya makada aliowatuhumu ni pamoja na
mimi.
Napenda kuufahamisha umma kuwa habari hizi si za kweli kwa sababu mwezi wote wa Oktoba, nilikuwa jimboni kwangu nikifanya kampeni za kuwania kiti cha Ubunge katika Jimbo la Monduli. Sikupata kusafiri kwenda Mwanza hata siku moja, na siku aliyoitaja ya Oktoba 19, nilikuwa katika vijiji vya Mfereji na Enguiki nikifanya kampeni siku nzima.
Ukiacha tuhuma hizo, pia upo uvumi uliosambazwa kwamba nilishiriki kikao cha mikakati ya kuchakachua kura, mjini Arusha kumsaidia mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Batilda Burian aweze kushinda kiti hicho. Nasema uvumi huu ni uzushi na si wa kweli.
Kutokana na yote haya, ninakwazika kwamba inaonekana katika nchi yetu umeanza kuingia utamaduni mpya wa kufanya siasa za uongo, uvumi, uzushi na kila aina ya hila kwa nia ya kujipatia ushindi. Kwa uzoefu wa mataifa mengi yaliyotuzunguka, ndani ya Afrika na sehemu nyingine duniani, amani hupotea kutokana usambazaji wa taarifa za uongo.
Mwasisi wa Taifa hili, Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, alituachia amani na utulivu ambavyo ni tunu ya taifa hili.
Dalili zinazoonekana, kuna watu wanaelekea kuchoshwa na amani iliyopo.
Wanajiandaa kufanya vurugu, kuliingiza taifa hili katika machafuko, na sijui wanafanya hivyo kwa faida ya nani.
Wito wangu kwa Watanzania, ni kwamba tusiichoke amani. Amani tuliyonayo ndiyo imetutofautisha na mataifa mengi yaliyotuzunguka na kuifanya Tanzania kuwa nchi ya kupigiwa mfano. Tuelekeze nguvu zetu katika shughuli halali za kutuletea kipato zisizoharibu amani yetu.
Tukiiharibu amani tuliyonayo, mwisho wa siku nchi yetu itateketea na sote hatutakuwa salama. Tutakuwa tumekwisha.
Mwisho, namsihi Dk. Slaa ajipe muda wa kuzifahamu vyema siasa za nchi hii. Asidanganywe na mahudhurio ya mikutano ya hadhara akadhani ndizo kura katika masanduku ya kupigia kura. Namsihi ajifunze` zaidi jinsi ya kufanya siasa za kistaarabu bila kueneza uvumi, uongo, chuki na uzushi vyenye kutetelesha amani ya nchi yetu. Mungu ibariki Tanzania.
Edward Lowassa
Mbunge Mteule wa Monduli
Taarifa hii ya PM aliyejiuzulu kwa kashfa ya ufisadi ya Richmond imesambazwa kwa vyombo vya habari sasa hivi na: AIKA JUNIOR <aika_junior@yahoo.com>