Watanzania
JF-Expert Member
- Jul 7, 2009
- 727
- 42
TAARIFA RASMI KWA VYOMBO VYA HABARI NOVEMBA 5, 2010
Napenda kuufahamisha umma kuwa habari hizi si za kweli kwa sababu mwezi wote wa Oktoba, nilikuwa jimboni kwangu nikifanya kampeni za kuwania kiti cha Ubunge katika Jimbo la Monduli. Sikupata kusafiri kwenda Mwanza hata siku moja, na siku aliyoitaja ya Oktoba 19, nilikuwa katika vijiji vya Mfereji na Enguiki nikifanya kampeni siku nzima.
Edward Lowassa
Siku moja ina masaa 24. Kampeni zinaisha saa 12 jioni. Barua inasema kikao cha kuchakachua kiliendeshwa hadi usiku. Kwa nini tumwamini Lowasa na siyo barua iliyosainiwa na Kabwe. Kwani kinachoshindikana ni nini kwa Lowasa kusafiri baada ya kampeni na kwenda Mwanza na kurudi Monduli. Dr. Slaa amefanya mikutano mingapi sehemu tofauti kwa siku kwa kutumia helkopita?. Taarifa ya Lowasa haikubaliki.