Daudi Mchambuzi
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 62,190
- 128,243
Jaji warioba anampa darasa huyu mropokaji.
Warioba hana ukweli wowote ni MTU anaependa popularity
huyu binadamu anayeitwa Wassira kwa nini anajipa shavu sana siku hizi?
Haya nakwenda GOMBE kumfuata bosi wako!!
Angalau hakudanganya kama alivyofanya Wassira
Vijana mbona mnaweweseka sana mkisikia jina la Wassira? kulikoni amewabana?
kuna wengine mnasema hafai, kama hafai si mumuache tu ili ashindwe vizuri.
Mathalani mtu hakubaliki, mbaya wa sura, anawakera, wazungu watawacheka mkimchagua, sasa mtu wa namna hiyo kwanini mnamjadili kila siku?
Ukiona nyuki wametanda msituni tena sehemu moja ujue kuna maua yanayofaa kwa asali.
mnapozidi kumshambulia Stephen Wassira mnawafanya wasiomjua kumjua zaidi, waliokuwa wanambeza kumheshimu zaidi, kwa ufupi mnapigia kampeni kwa gharama nafuu.
Kuna mgombea wa kimarekani yaliwahi kumkuta hayahaya ya kutukanwa na kubezwa, kuzomewa na kuitwa majina ya madubwasha na madudu, siasa ni upepo, kilichokuja kuwageuka wapinzani wake ni simulizi mpaka leo, yaani "mbaya huyo" aliwatimulia vumbi hawakuamini.
Hii naiona very soon kupitia huyu Stephen.
Muda haudanganyi, na ukweli haujifichi, endeleeni kupambana lakini kumbukeni Politics is a game of chance,opportunity and wording.
Warioba atabaki kuwa MWAMBA wa Taifa hili! Kwa kusema ukweli pasi na unafiki, amekuwa mtume mwema na mwaminifu. Wezi, wahafadhina, walafi, viwavi, wavivu na wapuuzi watamuona J S Warioba kama shubiri na mwiba juu ya ulafi wao! Asante Warioba. Taifa bado linakuhitaji iwe ndani ama nje ya ccm.
Nilikuwa najiuliza kwanini Makamba na Wassira ni watu wa karibu? Sasa nimepata jibu, hawa wote wako tayari kukupakazia lolote ailimuradi ana survive ktk siasa maslahi....JK akamtosa Makqmba kwa shinikizo la wenye CCM ila huyu amemganda kama ruba.....lakini ni suala la wasaa tu naye ataondoka naye ktk siasa za nchi hii, nashangaa Bulaya leo kuitwa msagaji eti kwa sababu anatishia ustawi wa Wasssira pale Bunda! Makamba , Wasira, Makinda waliwatumia Kombani na Mkulo huku Aziz Aboud aki finance operesheni tokomeza Ngasongwa 2007...2008...2010. Nikikumbuka hawa watu walivyomfanyia visa Alhaj Ngasongwa siamini mpaka leo kama kweli hii ndio Tanzania! Dhambi kubwa ni influence yake ktk kumminya Aboud Morogoro 2000 na 2005 pale alipowabeba wazawa Mazola na Dkt Mzeru.....ktk ubunge, Polyster na vitu kama hivyo. Wasira alimuhofia sana Ngasongwa huku akimuita anajifanya Msomi sana huyu jamaa. Wassira ni janga ambalo limeachwa litamalaki kwa miaka 10 ya JK. Kuna mtu alihoji kwanini Jakaya anayumbishwa na watu wawili wa Mara? kila mmoja ana mapungufu yake but Wassira is the worst thing happened to Jakaya na hana pa kujitenga naye.
mwamba wa wanywa gongo .ukiona mtu hanenepi huku anamaisha poa jua anaroho mbaya sana
Ni kipi kinachoonyesha uzee na utoto kwenye huo waraka?huo waraka akiandika Warioba nitaona uzee umemfika kiwango cha juu sasa na ni utoto.
Warioba anazeeka vibaya aisee
Bado ukweli uko palepale, Wassira alionewa, na uonevu siku zote una kikomo, kama Warioba alikuwa anapendwa sana na Wana-Bunda kulikoni akaangukia pua mwaka 1995?
Kama Warioba ni msafi kulikoni atumie gari la Waziri Mkuu na Pesa za serikali kwenye kampeni?
Nadhani hata wewe ukweli unauona alichokisema Wassira.
Kwanini Safari ya Warioba ilikomea njiani na Wssira mpaka leo anaendelea?
Katika hayo nani anakubalika na wana-Bunda?
Kwanini Warioba hajawahi kugombea tena Bunda? na kwanini mpaka leo hajarudi bunda hata kupalilia nyumba yake iliyojaa nyasi kijijini kwao Nyamuswa?
Kwanini hapendi kuwasaidia ndugu zake hata kwa Matibabu tu, Kaka yake Ndg. Chai Warioba mpaka leo anaumwa na ni fukara kupindukia kwanini asimsaidie? na hao ndio waliomnyima kura, Warioba alikosa kula mpaka za ndugu zake.
Warioba nilitarajia utaweka waraka mzito lakini nimeshangazwa kuona maandishi tu tena ya kujitetea, Wassira is always a hero to you.
Hakuna haja ya kurushiana maneno, nyie ni watu wa eneo moja, ukweli unajulikana, kukubali kushindwa ni Heshima pia.
Kwakweli nakiri kukosea kumjadili mtu huyu hapa, naishia hapa na kwa dhati naungana jamii iliyo m delete huyu mtu. Ushauri, ajistaafie na kurudi kuwa mwananchi anayesubiri hukumu yetu kwa dhambi zake.
Jaji warioba anampa darasa huyu mropokaji.
hahahaaaaaaaaaa! Njaaaas mbaya sana....kama utetezi ni huu basi atafute kambi itakayomlealea.
Pun...vu zako!