Waraka kwa Dr. Slaa

Waraka kwa Dr. Slaa

Unazungumzia UKAWa ipi kama ya Lipumba na slaa ilijifia yenyewe baada kuchukua ndondo kutoka CCM. Makaidi wananchi wamemshusha jukwaani masasi Mbele ya Babu Duni, Mbatia mcheza shoo tu anainfluency yeyote. Waasisi wa ukawa hata jukwaa LA kampeni hawapandi sasa hivi si wameshauza rights.

Kama huna majibu ya maswali yangu, surrender umeshindwa huna hoja. Kwanza Nani alikuwambia ukawa ni Lipumba na Slaa? Nyerere na Karume walipokufa Tanzania ilikufa?

Subiri 25 October ndipo ujue UKAWA ni mziki mnene!.

Hakuna haja ya kupaniki. aSubiri tarehe 25
 
Namheshimu sana Dr. Slaa, lakini napata shinda kuelewa kwa nini anajiapiza kusema ukweli wakati baadhi ya maneno anayoyasema si kweli. Kwa mfano, Slaa anajua wazi namna serikali zote zinavyofanya kazi. Katika hotuba yake ya jana ametaja mara kadhaa "Baraza la Mawaziri" katika maamuzi ya Richmond. Ni wazi kabisa kwamba kwa suala kubwa kama hili, Waziri Mkuu peke yake hawezi kufanya maamuzi peke yake. Kama Lowassa amehusika, basi yeye atakuwa amesimamia utekelezaji wa maamuzi ya wengi (ya Baraza la Mawaziri). Huu ndio ukweli ambao haugawanyiki!. Swali langu hapa kwa Dr. Slaa, je ni kwa nini bado anafikiri ni Lowassa pekee ndiye fisadi? Je ni nani mwenyekiti wa BLM? ana hakika ni Waziri Mkuu?. Watanzania tuwe waungwana, na tujiweke katika viatu vya Lowassa. Ni ukweli kabisa kwamba mtu huyu amewajibika sana kwa makosa ya watu wengi. Amekubali kuwajibika na kutukanwa kwa ajili ya watu wengi (Kwa niaba ya BLM zima). Huo peke yake ni uungwana tosha. Hatuwezi kuendelea kumzushia na kumbebesha mizigo peke yake kama vile yeye aligeuka kuwa mwamuzi wa mwisho katika mambo yote mazito ya nchi hii. Mimi ni Mkristo kama Dr. Slaa na sitakubali kubeba dhambi za aina hiyo. Aidha, wapo watu katika nchi hii ambao walikaa mezani na Lowassa katika BLM kupitisha maamuzi ya kuupitisha na kidhinisha mradi wa Richmond. Wasifanye dhambi kwa kukaa kimya na kumwacha mwenzao akitukanwa. Wajitokeze waseme wazi kwamba yalikuwa ni maamuzi ya wengi, na mwenzao kawabebea misalaba yao. Siwezi kumhukumu Lowassa kwa sababu hiyo kwani siku zote maamuzi yanayofanywa na BLM ni maamuzi ya wote na mtu mmoja hawezi kuyapinga. Tumeshamwadhibu (kwa kujiuzulu uwaziri mkuu wake) imetosna. Hatuwezi kuendelea kumbebesha mizigo ya maamuzi ya serikali yetu wakati huo.
 
Huyu fisadi hakutubu, what he did is to transfer allegations.


What did you want him to say if that was his fact? I would expect your chair and his crew would come out immediately to clear the atmosphere. Silence means consensus. Now everybody knows he is guilty.

Ulitaka Lowasa afanye nini? Amesemwa kikwete ndiye mwizi, naye kakubaliana na hata kaogopa kukanusha, ukijumlisha na kwa nini serikali yake haikumshitaki kama Gwajima alipomtukana Pengo au Jerry Muro alipopokeleshwa milini kumi?

Ni nani binadamu mwenye kichwa asielewe tu ukweli ambao sasa uko dhahiri?

Dr. Slaa mwenyewe alisema "Wameongea naye, ametoa vielelezo, wamemwelewa. Na wengine watakaokuja tutawahoji, tukiwaelewa tutawapokea, tutawaambia wananchi" Wewe hili bango lako unalibeba kutoka wapi?

Kama mlitaka kujua nani firaumi halisi mngepeleka kesi zao mahakamani muone mziki wa chooni usivyochezeka. Sasa kaondoka na kuamua kuungana na wazalendo, mnamskama. Mbona walitajwa kwenye orodha ya mafisadi kuanzia na kikwete hamuwasemi?

Mafisadi wa EPA, Meremeta, kagoda, Escrow, Richmond, Kiwra, barabara, gas, rea. n.k mmewafanya nini na mnao huko ccm? Kwanza shetani atawahukumu kabla hamjaungua moto wa Mungu.

Jifunze kuwa na haiba ya ukweli na aibu kama binadamu.
 
Dr Slaa hakuwadharau usitake kupindisha na kumfanya Lowassa ndo watetezi wa wanyonge. Lowassa alisema atakuja na wabunge 50 na ndiyo nguvu yake kubwa kwani ataipasua CCM
Sasa anapoonyesha kuwa nguvu yake ni waendesha bodaboda tena asilimia kubwa wamehongwa kuja hapo ni dhahiri huyu Lowassa ni msanii.
So hebu ondoa your false indignation na usitake kupindisha kilichosemwa!

Weka ushahidi wa boda boda kuhongwa na Lowasa na utakuwa umetusaidia. Vinginevyo hizo ngonjera zisizo na mashiko hatuna haja nazo! Yeye babu Slaa alipopokelewa alipofanywa kapi na ccm na kupewa nafasi chadema anaona ilikuwa sahihi, lakini kupokelewa kwa Lowasa imekuwa nongwa! Babu kachoka, babu ameishiwa, babu anatia huruma! Babu pumzika! Magamba wamekuingiza chaka! Fedheha ni yako peke yako! Kura zote zina thamani sawa! Hakuna tofauti ya kura ya boda boda na ile ya mbunge/mzito!
Yeye Slaa mwenyewe hana uzito wowote ameondoka na kura mbili tu! ya kwake na ya mke wake!
Babu nenda utakako umeshapitwa na wakati!!!
 
Namheshimu sana Dr. Slaa, lakini napata shinda kuelewa kwa nini anajiapiza kusema ukweli wakati baadhi ya maneno anayoyasema si kweli. Kwa mfano, Slaa anajua wazi namna serikali zote zinavyofanya kazi. Katika hotuba yake ya jana ametaja mara kadhaa "Baraza la Mawaziri" katika maamuzi ya Richmond. Ni wazi kabisa kwamba kwa suala kubwa kama hili, Waziri Mkuu peke yake hawezi kufanya maamuzi peke yake. Kama Lowassa amehusika, basi yeye atakuwa amesimamia utekelezaji wa maamuzi ya wengi (ya Baraza la Mawaziri). Huu ndio ukweli ambao haugawanyiki!. Swali langu hapa kwa Dr. Slaa, je ni kwa nini bado anafikiri ni Lowassa pekee ndiye fisadi? Je ni nani mwenyekiti wa BLM? ana hakika ni Waziri Mkuu?. Watanzania tuwe waungwana, na tujiweke katika viatu vya Lowassa. Ni ukweli kabisa kwamba mtu huyu amewajibika sana kwa makosa ya watu wengi. Amekubali kuwajibika na kutukanwa kwa ajili ya watu wengi (Kwa niaba ya BLM zima). Huo peke yake ni uungwana tosha. Hatuwezi kuendelea kumzushia na kumbebesha mizigo peke yake kama vile yeye aligeuka kuwa mwamuzi wa mwisho katika mambo yote mazito ya nchi hii. Mimi ni Mkristo kama Dr. Slaa na sitakubali kubeba dhambi za aina hiyo. Aidha, wapo watu katika nchi hii ambao walikaa mezani na Lowassa katika BLM kupitisha maamuzi ya kuupitisha na kidhinisha mradi wa Richmond. Wasifanye dhambi kwa kukaa kimya na kumwacha mwenzao akitukanwa. Wajitokeze waseme wazi kwamba yalikuwa ni maamuzi ya wengi, na mwenzao kawabebea misalaba yao. Siwezi kumhukumu Lowassa kwa sababu hiyo kwani siku zote maamuzi yanayofanywa na BLM ni maamuzi ya wote na mtu mmoja hawezi kuyapinga. Tumeshamwadhibu (kwa kujiuzulu uwaziri mkuu wake) imetosna. Hatuwezi kuendelea kumbebesha mizigo ya maamuzi ya serikali yetu wakati huo.

La kushangaza, pamoja na kumtaja Lowasa peke yake katika Richmond na kuaha kuthubutu kumgusia kikwete ambaye Lowasa kamtaja kuwa ndiye mwenye hiyo biashara, na ambaye si yeye wala serikali yake imekanusha taarifa zile zilizotolewa rasmi tena hadharani, bado hawaongelei maufisadi mengi mengine ambayo yameendelea kuwepo kama EPA, Meremeta, Kagoda, Kiwira, gas, rada, ndge ya raisi, rea, escrow n.k n.k. Je haya yote ni ya Lowasa?

Kama ni ya Lowasa kwa nini hajawahi kupelekwa mahakamani kwa ufirauni huu ili haki kwa taifa itendeke?

Kama si ya Lowasa kwa nini wahusika wake wako ccm na wanaendelea kufumbiwa macho hata mafili ya uchunguzi hawajafunguliwa? Au wanasubiriwa siku wakitangaza kuahma ccm ndiyo waana kusakamwa kijuha?

Tatu kushndwa kuwapeleka kwenye mahakama ili haki itendeke, na kuendelea kulalamika kwa wannachi haitoshi kuonyesh serikali dhaifu isiyofaa kusimamia taifa na wananchi wake hata dakika moja zaidi?


Bila shaka Mungu atabaki upande wa wanyonge, na tutashinda.

Ccm wana fedha, ccm wana kila silaha za uovu, lakini wananchi wanyonge wana Mungu na kila silaha za nuru!.

Na ijulikane leo kwamba Mungu aliyebaba wa maskini wanyonge wa tanzania, ni Mungu Mkuu mwenye Kuogofya na kwamba yko juu sana kuliko shetani wa ccm na ulaghai wake.

Leo Mungu Anakwenda kujionyesha ili dunia ijue kamba yeye anaishi Milele na hakiyake yakaa milele na wala hahongeki wala hahadaiki!.
 
tatizo ni Mshumbusi.....ufirst lady
Umri wa dr. na huyu fake first lady ni baba na mwana. Dr. alihonga u first lady akampata halafu unarudi jioni unaanza longolongo ooh tumeona tumwachie ooh! Ndo maana alitupiwa begi lenye mihogo akale na kulala kwenye gari.
Na wewe Lissu haya mambo mazito ungeyasitiri kidogo sasa kumdhalilisha Dr, tena kupitia VOA siyo fresh.
 
Sikufurahia jinsi Dr. Alivyoruhusu jazba imuongoze katika kutoa tuhuma dhidi ya CHADEMA. Alitakiwa kutofautisha kauli rasmi za Chama na zile za mitaani (pamoja na JF). Kwa mfano, sijawahi kusikia uongozi wa CHADEMA ukisema umepania kuiondoa CCM madarakani hata kwa kumtumia shetani. Nimesoma kauli hiyo kwenye michango ya manazi hapa JF.

Aidha, kuleta habari ya viongozi wa makanisa kununuliwa (kwa kauli za mtu kama Gwajima) huku akijua jinsi suala la udini linavyotumika vibaya nchini yeye binafsi akiwa mwathirika mkuu ni ukosefu mkubwa wa busara ambao sikuutegemea kwa mtu wa aina yake.

Pia sikumtarajia azungumzie tena kwa kejeli habari za watu kusombwa na malori mkutano wa UKAWA, za babu seya na za masheikh wa uamsho. Those were too low for him - kama kutoa mipasho ya kimtaani vile.

Kwa kifupi, alionekana kama mtu aliyekuwa kwenye misheni ya "kuwapasha na kuwasuta kabisa wabaya wake" badala ya kulisaidia taifa kwa ujumbe uliokamilika kwa busara (objective) kuhusu mustakabali wa taifa katika uchaguzi huu. Na kwa kufanya hivyo ameruhusu kutumiwa vizuri sana na mashetani wa upande wa pili! Na sitaki kuamini kuwa amefanya hivyo akiwa kipofu (naïve).

Mimi niliyekuwa namheshimu sana kama mtu binafsi aliyesimama katika misingi ya uadilifu hata kama kabaki pekee, sasa naamini Dr. hana (na hakuwa na sifa) za uongozi wa kisiasa. Na hapa, unafiki mbali, hakuna chama kinachoweza kuchukuana na Dr. katika harakati za kisiasa. Atafaa zaidi kwenye ulimwengu wa akina Mtikila. Siamini kama kanunuliwa kama wengi wanavyofikiri hapa. Kweli kabisa Dr. hana bei ya pesa; lakini anaingilika kirahisi kupitia jazba aliyo nayo. Hiyo ndiyo tofauti yake na akina Mtikila.
 
Unajidanganya na Magufuli, hivi kuna mtu ndani ya CCM aliyesafi? Hivi kwanini Watanzania wamekuwa na masikio ya kufa? Magufuli ni fisadi kama wanaCCM wenzake, na ufisadi ukiwa CCM ni ule wa utake usitake sababu mfumo wa CCM umekuwa hivyo miaka nenda rudi. Ni wazi kuwa Lowassa naye akiwa ndani ya CCM alikuwa ni fisadi by default LAKINI ukiwa ndani ya ukawa unakutana na mfumo mwingine ambao unakufanya unakuwa mwanamabadiliko by default.

Magufuli hawezi kufanya maajabu ndani ya li-mfumo lililooza kwa miaka zaidi ya hamsini, hawezi hata angefanyeje, JK yamemshinda na aliishia kuwaambia wezi warudishe pesa (na mpaka leo hatujui ni akina nani na walirudisha kiasi gani) wakati wezi wa kuku wanafungwa jela.

Sitampigia kura Lowassa sababu ya usafi wake bali nitampigia kura sababu yupo kwenye mfumo ambao unakiu ya kuleta mabadiliko. CCM wamekuahidi miaka yote hiyo lakini bado watu ni maskini -najua hata wewe unayesoma huu uzi ni maskini na sababu ya umaskini wako ni moja nayo ni CCM, naona ajabu sana kusikia mtu anaamini kuwa Magufuli na CCM yake wataleta mapinduzi ya maendeleo.
Wewe hivi maneno haya uliaandika kabla au baada ya kusikiliza hotuba ya Dt Slaa? ??
Ni lazima ujitambue mzee, maana utumbo wote mnaofanya pamoja na viongozi makamanda umeanikwa hadharani kweupeee. Jenga hoja njoo majukwaani kujibu hoja. Usikae kitapeli tapeli tu na kuishi kisanii sanii. Mafisadi wakubwa nyinyi. Na bado ngoja sasa Prof Lipumba naye atakapokuja kutapika yake muone. Tafuteni watu wa kuwaongoza lakini sio watanzania hawa wa leo
 
Wewe hivi maneno haya uliaandika kabla au baada ya kusikiliza hotuba ya Dt Slaa? ??
Ni lazima ujitambue mzee, maana utumbo wote mnaofanya pamoja na viongozi makamanda umeanikwa hadharani kweupeee. Jenga hoja njoo majukwaani kujibu hoja. Usikae kitapeli tapeli tu na kuishi kisanii sanii. Mafisadi wakubwa nyinyi. Na bado ngoja sasa Prof Lipumba naye atakapokuja kutapika yake muone. Tafuteni watu wa kuwaongoza lakini sio watanzania hawa wa leo

Nani alifadhili press conference ya Slaa? View attachment 283114
 
Sikufurahia jinsi Dr. Alivyoruhusu jazba imuongoze katika kutoa tuhuma dhidi ya CHADEMA. Alitakiwa kutofautisha kauli rasmi za Chama na zile za mitaani (pamoja na JF). Kwa mfano, sijawahi kusikia uongozi wa CHADEMA ukisema umepania kuiondoa CCM madarakani hata kwa kumtumia shetani. Nimesoma kauli hiyo kwenye michango ya manazi hapa JF.

Aidha, kuleta habari ya viongozi wa makanisa kununuliwa (kwa kauli za mtu kama Gwajima) huku akijua jinsi suala la udini linavyotumika vibaya nchini yeye binafsi akiwa mwathirika mkuu ni ukosefu mkubwa wa busara ambao sikuutegemea kwa mtu wa aina yake.

Pia sikumtarajia azungumzie tena kwa kejeli habari za watu kusombwa na malori mkutano wa UKAWA, za babu seya na za masheikh wa uamsho. Those were too low for him - kama kutoa mipasho ya kimtaani vile.

Kwa kifupi, alionekana kama mtu aliyekuwa kwenye misheni ya "kuwapasha na kuwasuta kabisa wabaya wake" badala ya kulisaidia taifa kwa ujumbe uliokamilika kwa busara (objective) kuhusu mustakabali wa taifa katika uchaguzi huu. Na kwa kufanya hivyo ameruhusu kutumiwa vizuri sana na mashetani wa upande wa pili! Na sitaki kuamini kuwa amefanya hivyo akiwa kipofu (naïve).

Mimi niliyekuwa namheshimu sana kama mtu binafsi aliyesimama katika misingi ya uadilifu hata kama kabaki pekee, sasa naamini Dr. hana (na hakuwa na sifa) za uongozi wa kisiasa. Na hapa, unafiki mbali, hakuna chama kinachoweza kuchukuana na Dr. katika harakati za kisiasa. Atafaa zaidi kwenye ulimwengu wa akina Mtikila. Siamini kama kanunuliwa kama wengi wanavyofikiri hapa. Kweli kabisa Dr. hana bei ya pesa; lakini anaingilika kirahisi kupitia jazba aliyo nayo. Hiyo ndiyo tofauti yake na akina Mtikila.
Mwacheni mzee wa watu aseme ukweli ili awe huru. Nafsi yake inamsuta na mimi ni mfuasi wake toka nitoke. Yeye ndie alinishawishi na ndie yeye ameshauri tujitafakari wote tena. Na tumesha jitafakari tayari. Hadanganywi mtu hapa.
Tulikuwa tunapumbazwa na hatuoni utadhani vipofu., wanajofanya ufisadi ooh sijui mfumo, yaani utapeli mtupu. Na kama alivyosema Dr Slaa uongozi wa kitapeli kama huu hauwezi kuingia ikulu kamwe. Namimi nasema ni bora tusiingie kwa manufaa mapana ya mama Tanzania. Hatudanhanyikiiiii tena naomba makamanda mrudi tena baada ya miaka ishirini labda mtakuwa mmenyooka
 
dr. Kwanza ninaomba nichukua nafasi hii kwa namna ya pekee nikushukuru kwa namna mlivyoshirikiana na viongzi wenzako kuinua upinzani na kutufikisha hapa tulipo. Umepigana vita vya hatari bega kwa bega na wana mabadiliko hata kutoa mwelekeo wa njia tunayoiendea sasa. Kila wakati yanapotajwa mabadiliko tanzania, jinalako litatajwa.

Ninapenda nikushukuru kwa kuzungumza na watanzania ambao wengi wao ni wapenzi na wafuasi wako wakubwa mimi nikiwa miongoni mwao.

Nimekusikiliza vizuri na kukuelewa kwa kiwango kikubwa. Hata hivyo nina masuala kadhaa ambayo ninaomba utusaidie kutupa maelezo kwa mtazamo wako ili tuendelee kuwa pamoja katika gurudumu la utetezi wa wanyonge uliotuthibitishia utaendelea kuwapigania bila kujali una chama ama hauna.

Kabla ya yote, ninaomba nionyeshe masikitiko yangu kwa uamuzi wako wa kuresign instantly baada ya kutofautiana na viongozi wenzako kwa sababu ninahakika tofauti zenu zilikuwa na ziko chini ya uwezo na hekima zenu za pamoja. Ninachokifahamu mimi, maamuzi yoyote yanayofanywa wakati wa hasira kali ama furaha kubwa sana, huwa hayazingatii maswala mengi ya muhimu na yenye tija kwa upana unaostahili.

Ninaomba nichukue nafasi hii kuomba ufafanuzi kwa masuala yafutayo.

1. Wakati mnapanga ujio wa lowasa, ulitaka kujua kama ni asset kama atakuja na wenzake makini viongozi wazuri na kama ni liability ikiwa atakuja na vijana wa barabarani.

Mheshimiwa, huoni kama ingelikuwa ni vizuri zaidi kumpokea bila ulazima wa kuja na idadi fulani ya watu wenye sifa kadhaa, kama vile ambavyo chadema mmekikuza kwa kumpokea mtu mmoja mmoja bila sharti la kuja na watu wengine kwa wakati huo? Kwa nini yeye lowasa mlimwekea sharti hilo ambalo kwa watu wengine halipo?

Hoja yangu nyingine, hao unaowatambua kama vijana wa mitaani, ndio watanzania ambao walistahili kuwa sehemu za kazi lakini wamewekwa barabarani kwa utawala mbovu wa ccm. Huoni kama wana haki ya kuheshimiwa na kutambuliwa uwezo wao katika suala zima la maendeleo ikiwa kutakuwa na serikali mbadala inayowajali na kwamba wana umuhimu katika kupiga kura na kuiondoa ccm madarakani ili ije serikali sahihi?

Suala la kuhitaji watendaji wazuri kutoka ccm waje na lowasa ili aqualify for membership, linanipa tabu. Dr. Wewe ni msomi mzuri na umekuwa kiongozi wa chadema kwa miaka mingi. Kama kulikuwa na knowledge gape, sikutegemea mtategemea ijazwe na watu wa lowasa kutoka ccm mahali ambako tayari umepafananisha na choo. Kwa hali yoyote, hata kama wengelikuja, hawawezi kuwa ready made kufit kwenye utaratibu na kanuni za chadema. Sasa kama ndivyo, hamkuona kabisa umuhimu wa kutengeneza watu wenu wawe kama mnavyotaka wawe kwa maslahi ya chama na taifa bila kujali wanakuja ktuoka wapi ama ni wenyeji wa mlemle chadema?

2. Umeongelea suala la demokrasia kwamba kama maamuzi ya wengi yanakuwa kinyume cha mawazo yako, unatakiwa uachie ngazi.. Ni kweli hili dr? Siyo kwamba ni kukosa uvumilivu wa kuwachukulia wengine? Kama katika vikao watu wakitofautiana kwa ajli ya demokrasia yule ambaye mawazo yake hajapitishwa anapaswa kuondoka, ni kwlei dunia ingelikuwa na amani au maendeleo? Watu wangapi wangelikuwa wanaondoka kwenye familia zao, maofisini na kila mahali kwa saa? Nilichokitegemea kwako dr. Ilikuwa ni uvumilivu wa kisiasa wa kuweza kuwachukulia wengine kwa kuamini kwamba, hata kama siku hiyo walikukatalia, siku nyingine au katika hatuanyingine wangehitaji hekima na maarifa yako.

Ninajua mchakato wa mabadiliko hauishii kwenye uchaguzi. Uchaguzi ni hatua za mwanzo sana lakini baada ya hapa kunahatua ya ujenzi wa taifa jipya ambapo ilikuwa ni nafasi yako nzuri kuongoza mabadiliko kwa kuhakikisha wanyonge uanaowatetea sasa wanakombolewa ki halisia.

Nili kutegemea kwamba wewe kama katibu mkuu wa chadema, ulitakiwa kuwa mstari wa mbele kuhakikisha chadema inapata wanachama wapya wengi bila kubagua na kuwakarabati ili makandokando wanayokuwa nayo kule wanakotoka, hayapati nafasi katika chadema. Kama ulivyosema kubeba kinyesi toka chooni na kukiweka chumbani ama sebuleni, kweli ni tatizo lakini kinyesi hicho kinaweza kuwa purified na kufaa kwa matumizi mengine ya binadamu. Kilichotakiwa ni uwezo na maarifa ya kuhakikisha kinakuwa bidhaa nyingine, inayofaa kwa matumizi badaala ya kukiacha kiendelee kuwa kero. Na hizi haiba za watu si kutoka ccm tu bali hata wasio na vyama vya siasa wanapojiunga, wanahitaji kutengenezwa.


3. Umezungumzia ufasadi wa lowasa, wakati huo huo ukihitaji aje na wenzake kutoka huko chooni. Kwenye list of shame, uliorodhesha majina ya mafisadi 11 lowasa akiwemo. Ni kwei mchakato wa richmond lowasa amekiri kuhusika lakini hakueleza in details nini kilikuwa nini. Hata hivyo amewataja viongozi wa juu yake. Nilitegemea katika suala kama hili, ni vizuri dr. Ukalisaidia taifa, kwa kuzungumzia mchakato mzima, naman ccm ilivyofanya ufisadi na kuwalinda mafisadi ambao si lowasa peke yake bali genge zima la ccm akiwemo mkuu wao kama laivyotajwa na lowasa.

Wewe mtetezi wa wanyonge, tulitegemea upaze sauti ya juu ukemee ccm na serikali yake, kushindwa kuwapeleka mahakamani watuhumiwa wote wa ufisadi ambao si lowasa wala richmond peke yake. Kitendo cha kuwasifia sita na mwakyembe kuongelea ufisadi bila kuonyesha kuguswa na kile alichokisema mwakyembe kwamba amekificha kwa kuogopa usalama wan chi, huoni kama umekuwa biased sana?

Tuanomba utamke report ya mwakyembe yote bila kuacha aliyoyoaficha iwekwe hadharani, na wahusika wa wizi ule wachunguzwe na watakaobainika kuwa na hatia za kimahakama wapelekwe mahakamani. Lakini pia ili uonyeshe fairness, usiache kuzungumzia ufisadi wa meremeta, kiwira, kagoda, escrow, miradi ya barabara, bomba la gas, mradi wa rea, nk. Nk. Kitendo cha kuishia richmond tu na kuyaacha haya mengine yanayotisha zaidi yaliyoendelezwa na mafisadi ya ccm, inaweza kutafsiriwa kama chuki binafsi dhidi ya lowasa. Makosa yote ya ufisadi yzungumziwe na yapewe uzito unaostahli bila upendeleo.

4. Dr. Kitendo cha kuwashambulia chadema kwa kumpokea lowasa, fisadi mmoja aliyeamua kubadilika na kufuata sera za chadema, huku ukiwalinda ccm ni kupigia kampeni ccm kwa kuwafichia makosa yao ambayo hasa ndiyo chimbuko la wewe kujibainisha kama mpigania haki za wanyonge (watu wa barabarani). Ninaomba upate muda mwingine, uzungumzie nini kilikufanya ujiunge na vyama vya upinzani, na nini sababu ya kuwa na wimbi kubwa la watu wanyonge tanzania ambao unahitaji kuendelea kuwapigania dhidi ya nani adui yao na ametoka wapi.

5. La mwisho katika orodha lakini la kwanza kwa umuhimu, ninaungana na wewe kukemea maneno ya waropokaji kwamba wataitoa ccm hata kwa mkataba na shetani kwa sababu ni maneno yanayovuta laana katika nchi. Haiti walitamka maneno kama yale wakati wanapigania uhuru na shetani amekaa kwao akiwatesa vizaz na vizazi. Hatumhitaji shetani katika ukombozi wa taifa hili. Ninafuta kauli hizi na ninaungama dhambi hii mbaya kwa niaba ya watanzania wote na vizazi vyetu, mungu atusamehee, asituhesabie uovu huu, katika jina la yesu kristo. Natamka atakayeendeleza kufufua maneno yanayompa shetani utukufu, kwa kiburi, afanye hivyo kwa gharama yake binafsi na si gharama ya watanzania.

Tulianza na mungu, tunaendelea mungu na tutamalizia na mungu ambayek sisi na vizazi vyetu tutamtumikia daima.

Vinginevyo sisi tunasonga mbele na ukombozi kama jeshi lenye nguvu na umoja. Tutapigana vita kwa kuheshimiana, kupendana na kushikamana. Wakati wote tutakapo tofautiana kim itazamo kwa kuwa ni binadamu, tutamaliza tofauti zetu kwa majadiliano bila kusalitiana na kuumizana. Atakayeonyesha kuchoka, hatutamtupa, tutamganga huku tukisonga mbele. Atakaye amua kurudi nyuma kwa sababu yoyote, tutalinda uhuru wake lakini tutaepuka madhara yake kwetu. Tumeshaamua kuiondoa ccm na kuweka utawala utakaojali watanzania badala yakusita sita huku ccm ikipanga kutumalizia.

Ninategemea utaendelea kuwa upande wa ukombozi wakati wote tunapopigana vita na wakati tutakapokuwa tukianza kujenga tanzanai mpya chini ya katiba mpya ya wananchi na mifumo mipya kwa maslahi ya tanzania ya sasa ni vizazi vijavyo.
hatudanganyiki tenaaaa! Njooni na gia nyingine
 
Mods wa jf mmenunuliwa kuna threads huwazitaki hasa zinawahusu ccm na maovu yao, ila za ukawa wanaziacha hata kama ni mbaya
 
Unajidanganya na Magufuli, hivi kuna mtu ndani ya CCM aliyesafi? Hivi kwanini Watanzania wamekuwa na masikio ya kufa? Magufuli ni fisadi kama wanaCCM wenzake, na ufisadi ukiwa CCM ni ule wa utake usitake sababu mfumo wa CCM umekuwa hivyo miaka nenda rudi. Ni wazi kuwa Lowassa naye akiwa ndani ya CCM alikuwa ni fisadi by default LAKINI ukiwa ndani ya ukawa unakutana na mfumo mwingine ambao unakufanya unakuwa mwanamabadiliko by default.

Magufuli hawezi kufanya maajabu ndani ya li-mfumo lililooza kwa miaka zaidi ya hamsini, hawezi hata angefanyeje, JK yamemshinda na aliishia kuwaambia wezi warudishe pesa (na mpaka leo hatujui ni akina nani na walirudisha kiasi gani) wakati wezi wa kuku wanafungwa jela.

Sitampigia kura Lowassa sababu ya usafi wake bali nitampigia kura sababu yupo kwenye mfumo ambao unakiu ya kuleta mabadiliko. CCM wamekuahidi miaka yote hiyo lakini bado watu ni maskini -najua hata wewe unayesoma huu uzi ni maskini na sababu ya umaskini wako ni moja nayo ni CCM, naona ajabu sana kusikia mtu anaamini kuwa Magufuli na CCM yake wataleta mapinduzi ya maendeleo.[/QUOTE


huu umasikini wa mali na fikra tuliopewa na ccm ni shida usishangae watu bado wanategemea mabadiliko ccm hiyo ni sawa na kusubiria meli airport. choo kitatoaje cake badala ya mavi. tusitumike kishabiki labda kama wewe ni teja lakini kwa akili ya kawaida.
 
Huyo fisadi katubu lini na nini? Hebu zinduka! Alafu ilani yenu ya Chadema na Ukawa iko wapi? Mmekubaliana nini na huyo fisadi wenu? Hujui lolote unashabikia tu!
What a hollow statement and a sad state of mind!

akili za kuambiwa changanya na zako hivi chama kinawezaje kugombea urais bila ilani . we unamsikiliza tuu magufuli na kuchukulia serious si ufanye hata kautafiti kadogo kweli ccm imewafanya mabogas ukiambiwa ilani hawana unaamini tuu. shughulisha basi akili kidogo
 
Watanzania wengi tumeshaamua kuwa tutamchagua lowassa kuwa rais na amiri jeshi mkuu wa jmt.
 
Dr Slaa alikwishasikika akisema kuwa akiwa rais atamfikisha Magufuli mahakamani kwa kuuza nyumba za serikali kifisadi . Kisha amesema Lowasa naye ni mchafu hafai kuwa rais.

Lakini hajawaambia watanzania wampigie kura nani! Ni bahati mbaya kwamba waandshi wa habari walisahau kumuuliza hili swali: Sasa kura tumpe nani? Magufuli au Lowassa?

Wewe ndiyo umesahau, waandishi waliuliza hili kisha akajibu kwamba yeye hana chama, ila watz wasije wakajuta lowassa hafai, ilikuwa bra bra bra bra tuu, yaani ukiangalia kwa makini mzee kachemka maana pale ni debe wazi kwa maccm. Kapotea kwa hili hitimisho lake, kapotea sana.

Ukawa songa mbele kwa spidi ya jet. Msijisumbue kumjadili wala kumtukana Slaa, aliwahi kuwa mtu muhimu, tuheshimu hilo, na sasa amepotoka kabisa, tuachane naye.
Naomba mjadala wa jinsi gani ya kulinda ushindi, tusiwape nafasi ccm ya kuiba hata kula moja. Tuungane kuelimisha watu huko mitaani, tusiache mjadala wowote upite iwapo tuna uwezo wa kutoa elimu ukawa, ingilia mijadala hata ya wanamama, au wazee au wanababa, huu ni muda wa ukombozi, daladala zote upandazo hakikisha zinajadili siasa na siasa yenye kuelimisha kwanini tuchague ukawa yaani lowasa na timu yake na si ccm na magufuli wao. Viva ukawa viva ukwa vivaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.
 
Rafiki yangu,mzee wangu dr Slaa.Nimeyatafakari sana maneno yako.Nimeyachunguza na naendelea kuyachunguza yanayoendelea Tanzania.Mimi,kama ilivyo kwa watz wengi, napenda nchi yetu iwe na maendeleo.Maendeleo kama taifa,pia maendeleo kwa watu mmoja mmoja.Sote tunaistahili keki hii tuliyopewa na Muumba.Tumepewa sisi na vizazi vyetu.Hii ndio nia ya mpiga kura.Kuchagua viongozi watakaoleta haya maendeleo,lakini pia usawa katika kugawana hii keki.Inapotokea haridhiki,mpiga kura hutafuta watu wengine wa kuwaweka madarakani ambao anaona wana nia kama yake.Hiyo ndio kitu tunaita MABADILIKO.Kuna wakati hutokea jamii kukosa maadili sana,kiasi cha candidates wote wanaojitokeza kutokosa kasoro.Mara nyingi mpiga kura hutafuta penye nafuu.Hata kama pana kasoro lakini pana njia ya kuifikia ile nia yake hata kama ni baada ya muda mrefu.Hata hivyo hili linahitaji voter mwenye uelewa,anayejua anachokitaka ni kipi,anakipataje na gharama zake ni zipi.Hii ndio hatua tuliyofikia watz.Huko nyuma hatukuwa tunajitambua.Hivyo hakukuwa na mwamko wa kudai haki na maendeleo stahiki kama leo.Baadae mwamko ukaanza,watu wakatambua kuna kitu wanahitaji lakini hawajui namna ya kukipata.Hawa ndio wale waliosukuma gari ya Mrema pale Jangwani mwaka 95 bila kumpigia kura.Baadae wakaelewa namna ya kukipata,bila kujua gharama ya kukipata.Hawa ndio waliompa JK 80% mwaka 2005,lakini wakaangushwa mwaka 2010.Wakagundua kumbe kuna gharama kubwa.Sio tu kumchagua mtu unayemtaka,bali pia kupambana kumwekea mfumo salama utakaombana na kuhakikisha anatekeleza matarajio.Sasa hapo pana gharama.Gharama ambayo watz leo wako tayari kuilipa.Ndio maana wanataka kubadili mfumo.Hapo ndipo tofauti yako na watz ilipo mzee wangu Slaa.Unamzungumzia mtu mmoja Lowasa.Sisi voters tunao wawili,Lowasa na Magufuli,wanaonadi mifumo miwili tofauti.Mfumo anaoutumikia Magufuli tumeuchoka.Tunataka mfumo mpya wenye tija.Kile wanachokinadi UKAWA kinatuvutia zaidi.Ila kuna jambo linatatiza.UKAWA wameweka candidate kutoka mfumo wa zamani,bwana Lowasa.Huu ndio ugomvi wako mkubwa sana dokta.Binafsi nakubaliana nawe,sikupendezwa na hatua hiyo.Lakini katika ufinyu huu wa options uliopo,inahalalisha kubakiza mfumo wa zamani?Kwangu nasema hapana.Ni vema tukabadili.Why?Nina sababu mbili.Mosi,Upinzani bado kumejaa watu wengi waliokuwa groomed huko.Haiwezekani Lowasa kuwapelekesha,ni wao watakaompelekesha.Kama Lowasa angekuja na kundi la wabunge,wenyeviti na viongozi lukuki toka CCM kama ulivyotaka wewe mzee,basi Lowasa angekuwa "liability"(mzigo) maana hilo kundi la viongozi lingeteka nguvu ya maamuzi ndani ya UKAWA na tusingejua nini kitatokea,in fact ingekuwa gambling.Lakini Lowasa amekuja na viongozi wachache sana,ila ameleta wapiga kura.Wale mashabiki wake wanaomsapoti,hao unaowaita bodaboda,mama ntilie n.k,hao ndio kawaleta.Hao hawashiriki vikao vya kamati kuu.Wao kazi yao ni kupiga kura.Hawatachukua nafasi za kimaamuzi za akina Mnyika,wameletwa kutiishwa chini ya UKAWA.Hii ni "asset". Na sitaki kuamini eti UKAWA kuna gap la uongozi,no.UKAWA kulikuwa na gap la wapiga kura.Kwa sababu ni timu mpya,inayojenga ngome yake gradually,na hii ya Lowasa ni opportunity with moderate risk,kaleta voters,sio think tanks, na UKAWA inahitaji voters,haihitaji Kingunge wengi na mimi nashukuru hao wabunge 50 hawajaja,nasema wabaki huko huko,hawa bodaboda ndo wanahitajika,huu ndio "uwezo wa Lowasa kuiangusha CCM" aliosema Lissu.Kumbuka maneno yake:"hatujamchukua Lowasa kwa usafi wake,bali UWEZO WAKE WA KUIANGUSHA CCM".Baada ya hapo atatumikia mfumo mpya,nyuma yake wakiwepo akina Duni Haji,Mbowe,Mbatia,Lissu,Marando etc nao wakiwa under pressure ya voters wa both UKAWA,CCM,etc. Huo utakuwa mwanzo wa mabadiliko kwa kuwajibishana.La pili,mimi kama voter,bado naona ni heri kuwapa nchi UKAWA na Lowasa wao,kwa sababu hii ndio njia pekee ya kurudisha uwajibikaji wa viongozi kwa wananchi.Siku watz tukiiondoa CCM madarakani,tutaheshimiwa na wale watakaofuatia.Utakuwa mwanzo wa kurefine uongozi wa umma.Itatokea mitikisiko,ila mbele ya safari tutapata tunachokitaka.Tutaheshimiana tu.Utapata uongozi kwa sababu wenye nchi tunakutaka na sio babako anataka!Mabadiliko haya yataleta uwajibikaji wa viongozi,na pia voters wenyewe kuwajibika kwa kile wanachokichagua,hata UKAWA nao wakizingua tunapiga chini,tunaleta wengine while learning how to get the best out of our society.Ni gradual but hii ni formula nzuri kwa maendeleo na ustawi wa any democratic state.To us,this is just the beginning.Ni hayo tu mzee wangu.Nakutakia maisha mema ila ukirudi ni vema ukawajibu hawa wanaohoji gharama za ile press conference yako.
 
Mwacheni mzee wa watu aseme ukweli ili awe huru. Nafsi yake inamsuta na mimi ni mfuasi wake toka nitoke. Yeye ndie alinishawishi na ndie yeye ameshauri tujitafakari wote tena. Na tumesha jitafakari tayari. Hadanganywi mtu hapa.
Tulikuwa tunapumbazwa na hatuoni utadhani vipofu., wanajofanya ufisadi ooh sijui mfumo, yaani utapeli mtupu. Na kama alivyosema Dr Slaa uongozi wa kitapeli kama huu hauwezi kuingia ikulu kamwe. Namimi nasema ni bora tusiingie kwa manufaa mapana ya mama Tanzania. Hatudanhanyikiiiii tena naomba makamanda mrudi tena baada ya miaka ishirini labda mtakuwa mmenyooka


Ni kitu gani ambacho Dr. Slaa alikisema ambacho wewe kwako kimekuwa kipya na kibaya sana ambacho kimesababishwa na viongozi wa CHADEMA kinachokufanya uone CHADEMA ina uongozi wakitapeli? Be specific!.
 
Ni afadhali kuongozwa na fisadi mmoja aliyetubu na kubadilika, ambaye atawatetea Watanzania kwa kuongozwa na kundi la watu wasafi, kulilko mtu mwenye hila mmoja aliyewekwa chambo ili aongozwe na rundo la mafisadi nyangumi walioko ccm. Mbona hamsemi mafisadi wa meremeta, kagoda, barabara, escrow, epa, n.k walioko ccm mmewafaya nini?

Tumia akili yako vizuri.

Ni afadhili kukaa na donge moja la maji chumbani kuliko kuishi kwenye shimo la choo.

Tunamchagua Lowasa chini ya UKaWA, kwa Tanzania mpya!.[/QUOTE

Embu jitahidi kufikiria hivi kwamba huyo fisadi mmoja aliyeingia UKAWA ataenda kuwafundisha wengine kuwa mafisadi na watazichota hizo pesa za Watanzania haswa.

Nadhani kila mtu anajua kasi ya mtu mwenye njaa katika kula. Tena mtu huyo hachagui kipi cha kula yaani atakula kila kilicho mbele yake.

Tukijidai kwamba hatuyaoni haya na kumptisha Lowassa kama raisi basi madhara yake mbele tusije kuyalalamikia pia.
 
Back
Top Bottom