Ni afadhali kuongozwa na fisadi mmoja aliyetubu na kubadilika, ambaye atawatetea Watanzania kwa kuongozwa na kundi la watu wasafi, kulilko mtu mwenye hila mmoja aliyewekwa chambo ili aongozwe na rundo la mafisadi nyangumi walioko ccm. Mbona hamsemi mafisadi wa meremeta, kagoda, barabara, escrow, epa, n.k walioko ccm mmewafaya nini?
Tumia akili yako vizuri.
Ni afadhili kukaa na donge moja la maji chumbani kuliko kuishi kwenye shimo la choo.
Tunamchagua Lowasa chini ya UKaWA, kwa Tanzania mpya!.[/QUOTE
Embu jitahidi kufikiria hivi kwamba huyo fisadi mmoja aliyeingia UKAWA ataenda kuwafundisha wengine kuwa mafisadi na watazichota hizo pesa za Watanzania haswa.
Nadhani kila mtu anajua kasi ya mtu mwenye njaa katika kula. Tena mtu huyo hachagui kipi cha kula yaani atakula kila kilicho mbele yake.
Tukijidai kwamba hatuyaoni haya na kumptisha Lowassa kama raisi basi madhara yake mbele tusije kuyalalamikia pia.