Waraka kwa Dr. Slaa

Waraka kwa Dr. Slaa

Katika biblia kuna Mtu Mmoja aliitwa sauli, ambae ndio Mtume Paulo

Alikuwa muuaji na akiwatesa sana Wakristo, siku moja akakutana na Mungu akamwambia mbona unawatesa watu wangu, akambadili jina palepale akamwambia Tangu leo wewe ni Paulo, Uutangaze Ukristo

Tangu siku iyo huyu jamaa akabadilishwa ndio alitangaza ukristo haijawai tokea. Katika biblia ana vitabu Zaidi vitano kaandika. wagalatia, waefeso, wafilipi, watesalonike, wakolosai. nk nk

Muuaji aliekuja kuwa shujaa wa Ukristo.

Nakifananisha kisa hiki na story za kumuita Edward Lowasa fisadi, Sawa, yawezekana ni kweli, kama Paulo alivokuwa Muuaji, lakini Mungu amemuita Lowasa, asiwe tena Sauli Mtesaji na Muuaji bali (Paulo Mueneza ukristo).

Mungu hutumia wadhambi maana hajawai zaliwa malaika.

Lowasa, umetumwa na Mungu kutupeleka kaanani, TUTAFIKA.

Musa hakuiona kaanani lakn waisrael walirudi Nyumbani na walifika. Lowasa ameletwa kuturudisha Nyumbani. Tutafika.
Na haturud Misri.

Mkuu Dumelang; umesema sahihi. Maumivu yetu tunayougulia sisi na watoto wetu tuliyopewa na ccm tunayajua sisi. Tunasonga mbele hadi ukombozi umepatikana.

Ccm adui yetu na mtesi wetu anajitahidi kutuchonganisha, kutugawa na kutukatisha tamaa kwa kushadadia hotuba ya Dr. slaa wakidhani watanzanai ni majuha hawatatumia akili kuchambua punje na mchanga.

Hata hivyo imekula kwao na aibu inabaki kuwa yao milele. Wapiganaji wamepata mori wa ajabu na sasa wanakwenda kwa speed ya mwanga, kuizika ccm.

Uharamia wa ccm haujatuvunja mioyo bali umetuongezea nguvu. Tumetambua kweli ccm ni mumiani aliyekusudia kuliua taifa na kufuta kizazi chetu katika uso wa dunia. Sasa kazi ni moja tu. Kuikomboa Tanzania kutoka kwa mafisadi wakoloni wa ndani ccm.

Watanzania wamepania kuwaonyesha ccm kwamba wao si mapumbavu au wa barabarani kama wanavyowaita.


Kwa mara nyingine dunia inakwenda kushuhudia Tanzania yenye neema Ikiongozwa na Lowasa chini ya UKAWa.
 
1441115723611.jpg
 
Tabby

nimesikia na kusoma kuwa uamuzi was kumkubali EL CDM ulifikiwa baada ya tafakuri ya muda so mfupi. hats hivo, muda huo ukipimwa unakidhi mahitaji ya wakati? au kwa ule mfano was kinyesi toka choono hadichumbani, je, na wenyewe ulikuwa wa kukurupuka? ikiwa maamuzi haya yalifanywa bila tafakuri ya maana huenda kukawa na athari huko mbele ya safari na hienda maamuzi yalifanywa kwa malengo ya muda mfupi. sasa, he, malengo ya muda mfupi no kinyesi chenye harufu Kali? he, harufu ile haiwezidhibitiwa au kutumika kwa manufaa ya muda mrefu?
nionavo mimi, hakuna kisichowezekana chini ya jua. angependa, Dr. angeweza kuonyesha uvumilivu Fulani kiasi sisi tunaompeda kumwelewa hisia zake kwani wapo wengi waliokuwa na msimamo kama wake. naamini, Tabia hubadilika. ni suala la muda tu.
naona kama vile Dr. hakuupa uvumilivi muda wa kutosha.
sasa Dr. kajitoa lkn harakati za ukombozi zitaendelea na huenda zikafanikiwa kwa mapenzi ya Mungu. ingependeza zaidi ikiwa baada ya kijitoa, hatashiriki ktk kuhujumu harakati hizo. mchango wake bado tunauhitaji hats akiwa nje ya chama.
NAMWOMBA MUNGU AMJALIE AFYA NJEMA AENDELEE KUWA NASI KWA NJIA MOJA AU NYINGINE. MCHANGO WAKE TUNAUHITAJI
 
Last edited by a moderator:
Umenena mkuu ni kweli kulikuwa na walakini kwenye hotoba ya Dr
 
Huyo fisadi katubu lini na nini? Hebu zinduka! Alafu ilani yenu ya Chadema na Ukawa iko wapi? Mmekubaliana nini na huyo fisadi wenu? Hujui lolote unashabikia tu!
What a hollow statement and a sad state of mind!


Kama hata hujui ilani ya CHaDEMA na UKaWA kama ipo, hufai hata kuchangia hapa.
 
Ni afadhali kuongozwa na fisadi mmoja aliyetubu na kubadilika, ambaye atawatetea Watanzania kwa kuongozwa na kundi la watu wasafi, kulilko mtu mwenye hila mmoja aliyewekwa chambo ili aongozwe na rundo la mafisadi nyangumi walioko ccm. Mbona hamsemi mafisadi wa meremeta, kagoda, barabara, escrow, epa, n.k walioko ccm mmewafaya nini?

Tumia akili yako vizuri.

Ni afadhili kukaa na donge moja la maji chumbani kuliko kuishi kwenye shimo la choo.

Tunamchagua Lowasa chini ya UKaWA, kwa Tanzania mpya!.

Nyuma ya lowassa wapo akina nani, wanaomchangia na.kumpa hela za kuendelea kununua watu na media coverage. Watu safi akina lossy, mnyika watazidiwa nguvu tu na lowassa na watu wake hao waliojificha nyuma ya pazia na yatakua yale yale ya choo kunuka kama alivyosema slaa
 
Dr Slaa hakuwadharau usitake kupindisha na kumfanya Lowassa ndo watetezi wa wanyonge. Lowassa alisema atakuja na wabunge 50 na ndiyo nguvu yake kubwa kwani ataipasua CCM
Sasa anapoonyesha kuwa nguvu yake ni waendesha bodaboda tena asilimia kubwa wamehongwa kuja hapo ni dhahiri huyu Lowassa ni msanii.
So hebu ondoa your false indignation na usitake kupindisha kilichosemwa!

Alisema wapi hii kauli?
Naomba kukumbushwa
 
Hituba hii ilitakiwa somwe tarehe 28/07/3015 tungeweza kuona nia yake njema. Kwa sasa amechelewa sana. Hatuwezi kufikia malengo bila kuanza safari. Cha msingi ni kuwa na dhamira njema, hii itaondoa makandokando kwa kiasi fulani. Nasisitiza safari lazima iendelee. Ni bora kuanza sasa kuliko tuanze miaka 10 au zaid ijayo.
 
Hatuwezi kulilia Tanzania MPYA, SAFI na iliyokombolewa ikiwa tutaruhusu FISADI papa kukaa kwenye jumba letu la state house.

Hivyo basi, kama tunahitaji mema kwa nchi yetu, chaguo la pekee ni Magufuli tu.

Lowasa ni mtu wa mungu
 
Tabby

No.3 na 4, kila mkutano au maelezo yana.maudhui yake na unamna ya kuwasilisha yaeleweke.kwa walengwa wake. Dr slaa hakupaswa kuongelea mabaya ya CCM kwenye mkutano ule.alikuja kutujuza kwa nn kaacha siasa za upinzani na uthibitisho wa zile tuhuma za aliyemsababisha aache hizo.siasa fullstop.
Wewe ungependa aseme hayo hiyo ni nafsi yako wengine wengi.wamemuelewa
 
Last edited by a moderator:
No.3 na 4, kila mkutano au maelezo yana.maudhui yake na unamna ya kuwasilisha yaeleweke.kwa walengwa wake. Dr slaa hakupaswa kuongelea mabaya ya CCM kwenye mkutano ule.alikuja kutujuza kwa nn kaacha siasa za upinzani na uthibitisho wa zile tuhuma za aliyemsababisha aache hizo.siasa fullstop.
Wewe ungependa aseme hayo hiyo ni nafsi yako wengine wengi.wamemuelewa

Unahitaji kupanua uelewa wako. Hakuna msemaji duniani kote wa ukwei anayeweza kuchukua ka piece kadogo ka imformation kwenye agenda akaficha ukwei wote halafu wenye akili timamu kama yeye walazimishe watu kuitikia eti kaeleweka.

Lazima uwe na matatizo makubwa kwenye kichwa na dhamira yako. Period!.
 
Nyuma ya lowassa wapo akina nani, wanaomchangia na.kumpa hela za kuendelea kununua watu na media coverage. Watu safi akina lossy, mnyika watazidiwa nguvu tu na lowassa na watu wake hao waliojificha nyuma ya pazia na yatakua yale yale ya choo kunuka kama alivyosema slaa

Ni mt asiye na ufahamu wa kutosha pekee ndiye anayeweza kuhoji Lowasa anapata wapi fedha za kampeni.

Mtu ambaye kichwa chake kinawalakini asiyeweza kuelewa kwamba Lowasa ni mgombea wa Institution ambayo ina funds kwa ajli ya kampeni ya mgombea wao. Halafu asihoji mtu binafsi anayekula mihogo na kuuz amkaa anapata wapi fedha za kuishi Serena hotel, kwenda SA kwa mapumziko na kulipia press conference ya vyombo vyote vya habari nchini kwa masaa matatu.


Ninaanza kupata picha ni kwanini Dr. Slaa amewaita ccm ni choo cha mavi.

Tumia akili yako vizuri, jipange na uache kutuonyesha namna umechanganyikiwa.

Tarehe 25 October, tutaheshimiana tu!.
 
Dr Slaa hakuwadharau usitake kupindisha na kumfanya Lowassa ndo watetezi wa wanyonge. Lowassa alisema atakuja na wabunge 50 na ndiyo nguvu yake kubwa kwani ataipasua CCM
Sasa anapoonyesha kuwa nguvu yake ni waendesha bodaboda tena asilimia kubwa wamehongwa kuja hapo ni dhahiri huyu Lowassa ni msanii.
So hebu ondoa your false indignation na usitake kupindisha kilichosemwa!

Lembeli na Bulaya wanatosha. CCM ingekuwa na wabunge 50 mahiri hii nchi isingekuwa na matatizo tuliyonayo sasa. Afadhali hawakuja wangekuwa mzigo tu. Kura za hao bodaboda na vijana wa mtaani ni asset tosha kuliko hao mafisadi wa CCM. Ushahidi wako kwamba asilimia kubwa ya bodaboda wamehongwa uko wapi? Wacha kujenga hoja kwa kutumia maneno ya mtaani na propaganda za Lumumba. Tuletee facts. Dr Slaa amejishushia heshima sana kwa kuwadharau bodaboda wote tumelisikia hilo. Yaleyale majivuno yake ya kuita watu sisimizi.
 
Huyo fisadi katubu lini na nini? Hebu zinduka! Alafu ilani yenu ya Chadema na Ukawa iko wapi? Mmekubaliana nini na huyo fisadi wenu? Hujui lolote unashabikia tu!
What a hollow statement and a sad state of mind!

Ilani ili iqualify kuwa ya ukawa inatakiwa Iwe na title iliyoandikwa ukawa au ikubaliwe na iakisi michango ya vyama vya ukawa
 
Ni afadhali kuongozwa na fisadi mmoja aliyetubu na kubadilika, ambaye atawatetea Watanzania kwa kuongozwa na kundi la watu wasafi, kulilko mtu mwenye hila mmoja aliyewekwa chambo ili aongozwe na rundo la mafisadi nyangumi walioko ccm. Mbona hamsemi mafisadi wa meremeta, kagoda, barabara, escrow, epa, n.k walioko ccm mmewafaya nini?

Tumia akili yako vizuri.

Ni afadhili kukaa na donge moja la maji chumbani kuliko kuishi kwenye shimo la choo.

Tunamchagua Lowasa chini ya UKaWA, kwa Tanzania mpya!.

Lowassa ametubu lini? Amebadilika kivipi?
 
Nyuma ya lowassa wapo akina nani, wanaomchangia na.kumpa hela za kuendelea kununua watu na media coverage. Watu safi akina lossy, mnyika watazidiwa nguvu tu na lowassa na watu wake hao waliojificha nyuma ya pazia na yatakua yale yale ya choo kunuka kama alivyosema slaa

Umemsikiliza dr kwa makini anadai kampeni za cdm,zinafadhiliwa na rostam wa ccm,na wiki iliypita nilimsikia bashe akiomba kura jimboni ila akadai magufuri ni mdogo kwa nafasi ya urais,na kwa majibu ya tundu lisu kuna mambo mengi yanatatiza kwenye siasa za Tanzania mkuu
 
Mahakama ya mafisadi je ni kwa ajiri ya lowasa tu ? Kama wapo wengine mbona hawasemwi kama lowasa?.
 
Itabid tuseme msemo mmoja wa marekani **whether he will bring development or not we will choose obama to show the world that America is for everyone.,na sis tunasema,whether he will bring development or not we will choose LOWASA from UKAWA to show the world that Tanzania is for every one, not ccm only. Tuma ujumbe huu kwa wadau wasiopungua hamsini ili kuleta mabadiliko ya kweli. Lowasa oyee,,
 
Hatuwezi kulilia Tanzania MPYA, SAFI na iliyokombolewa ikiwa tutaruhusu FISADI papa kukaa kwenye jumba letu la state house.

Hivyo basi, kama tunahitaji mema kwa nchi yetu, chaguo la pekee ni Magufuli tu.

Hamy-D

Nasikia eti hao tunaowaruhusu ndiyo wenye Epa, Kagoda, Twiga, Escrow, Madawa ya kule vya na kazalika. Hapo unasemaje?
 
Back
Top Bottom