Waraka: Kanisa Katoliki laandaa waumini uchaguzi 2010

Status
Not open for further replies.
To Kingunge Ngombale Mwiru,

You are not Deng Xiao Ping, Zhao Zyang, Mikhail Gorbachev, or any revolutionary socialist or communist. You are like Pol Pot or Myanmar Milltary Junta.

I will urge you Kingunge to shut up and stop talking rubbish!

If CCM has failed to teach ethics and civility, then why cry wheen someone else takes charge of Mfupa Uliokushinda?

You were the lead person in Party Propaganda, which has transition from Maendeleo to Unyakuaji!
 
Nwawasifu wote walioona kuwa mzee kingunge amefulia kisiasa kwa sasa!! anajua kuwa viongozi au wanaccm tulionao sasa ndio mabomu kwa nchi hii, sasa inakuwaje mtu mzima mwenye akili ulikaribia hata kufa unatamka ndani ya bunge upupu?kwani ukiambiwa chagua kiongozi bora umetajiwa umchague nani?simple logic, asitake kutishia watu eti tutakuwa kama lebanon, labda akiendelea kuwepo atataka kujustify hilo so atafanya awezalo "kutulebanoniza". watz sasa hatutishiki tunataka kiongozi bora si bora kiongozi, atoke ccm, cuf, chadema, tu awe bora! thx
 
Mmmmmhhhhhh. Hivi ni yule Kingunge mpagani?
Sasa wakatoliki wapi na wapi na yeye?
Wao wametoa waraka kwa followers wao na yeye atoe wa kwake kwa ajili ya pagans kama yeye. asilalame bure.
Ikiwa taarifa ya Raia Mwema kuwa Mwongozo wa Katoliki umetungwa na vigogo wa serikali na taasisi za umma akiwemo Jaji Mkuu Bw. Agustino Ramadhan, Kingunge ana hoja ya msingi.... Watashindaje hao wakatoliki wenye dhamana katika uongozi wa dola kutoa siri za serikali kwa viongozi wa katoliki!! ...wakibisha nani haogopi kutengwa. Kama mchezo utakuwa vivyo hivyo kwa madhehebu na dini nyingine kweli nchi itakuwa salama kweli? hasa ukifikilia kuwa katoliki wana upendeleo wa kuleta mapadre kutoka mataifa yote duniani bila mushkheri, lakini waislamu walipothubutu kuleta masheikh na taasisi za misaada walitoposhwa kama swala kwa visingizio mbalimbali.
 
Kingunge, sioni ktk huu mwongozo chochote ambacho kiongozi mwenye nia njema na WaTz atakipinga. Kwa jumla, kama Askofu Kilaini alivyosema "Asiyetaka kupigana na Ufisadi tusimchague"

Wewe Kingunge kama unataka kuteuliwa tena Mbunge na Rais ajaye achana na ufisadi. Tunajua una Mradi wa kukusanya fedha za Parking Jijini Dar, mradi ambao ulipewa bila kuzingatia Masharti ya Zabuni kuhusu miradi ya Umma. Hata kule Ubungo Bus Stop achana nako. Ama sivyo tutapinga uteuzi wako.
 
hasa ukifikilia kuwa katoliki wana upendeleo wa kuleta mapadre kutoka mataifa yote duniani bila mushkheri, lakini waislamu walipothubutu kuleta masheikh na taasisi za misaada walitoposhwa kama swala kwa visingizio mbalimbali.

hatupo kushindana wewe dogo,ongelea hoja hapa,
 
Mwaka 2007 alipinga vikali List ya Shame ya CHADEMA. akaja na kupinga kuwa CCM haina Mafisadi leo wote wamefikishwa mahakamani na hakuna jipya hivyo hakuna haja, then yeye hana Dini kinamuuma nini Sasa

Thinking and memory worsens with age.....Kwishaa!
 
To Kingunge Ngombale Mwiru,

You are not Deng Xiao Ping, Zhao Zyang, Mikhail Gorbachev, or any revolutionary socialist or communist. You are like Pol Pot or Myanmar Milltary Junta.

I will urge you Kingunge to shut up and stop talking rubbish!

If CCM has failed to teach ethics and civility, then why cry wheen someone else takes charge of Mfupa Uliokushinda?

You were the lead person in Party Propaganda, which has transition from Maendeleo to Unyakuaji!

This is the HEAVY WEIGHT PUNCH....... YOU HAVE SAID IT ALL!!! I HOPE HE [MZE KIBOGOYO] GETS THIS MESSAGES AS IT IS, NO SUGAR ADDED!!!!

RESPECT!
 
To Kingunge Ngombale Mwiru,

You are not Deng Xiao Ping, Zhao Zyang, Mikhail Gorbachev, or any revolutionary socialist or communist. You are like Pol Pot or Myanmar Milltary Junta.

I will urge you Kingunge to shut up and stop talking rubbish!

If CCM has failed to teach ethics and civility, then why cry wheen someone else takes charge of Mfupa Uliokushinda?

You were the lead person in Party Propaganda, which has transition from Maendeleo to Unyakuaji!

Mkuu Rev, you nailed it, just to make it more bold!
 
Mimi naomba kuuliza swali kwa Askofu Kilaini na WanaJF mahakama ya kadhi na OIC zinahusiana vipi na Ufisadi naombeni jibu tafadhali.

Pili ndani waraka unasema katiba iheshimiwe naomba kama kuna mdau anayo katiba atuwekee tuanze kichambua maana kama waraka ulivyosema kuwa katiba imetungwa na wananchi na pia katiba isielekee upande mmoja iangalie pande zote mbili vinginevyo ilo ikae kimya. Tunaomba katiba wakubwa.

Mwisho upande fulani naungana na Kingunge kwamba msijijidai kutupaka mafuta huu ni unafiki wa kanisa katoliki unajulikana dunia nzima wanataka kutuwekea serikali ambayo inafata maelekezo yao ili iprotect interest za kanisa. Mara nyingi hiyo strategy huishia katika machafuko. Kama mlikuwa mnaupinga ufisadi mbona mlikurupuka alipochaguliwa JK na kumsifu kuwa ni chaguo la mungu??? five years later mnaleta muongozo wa kuchagua viongozi huu si unafiki. Mlikuwa wapi nyuma na hata huo muongozo mlioutoa mwaka 2005 mbona ulitoka kimya kimya sembuse huu au kwavile mnajua jamii inachukia ufisadi ndio mnajidai kuleta unafiki sasa hivi???

Naomba mwongozo waheshimiwa.


Sioni suala la unafiki linaingiaje hapa. Kama unafiki basi KINGUNGE KAMBALE MWITU ndio mnafiki namba moja. Usilitusi kanisa kwa kulipakazia sifa ya kishetani ya unafiki. This is blasphemy. Lakini nadhani tatizo la baadhi yetu ni kwamba hatutaki kusoma. Hebu soma huo waraka kwanza ndipo urudi kuchangia humu JF. Hata hivyo, nafurahi kuona kuwa wengi wanaonekana wameelewa nia njema ya Wakatoliki kwa nchi yetu.
 
Ikiwa taarifa ya Raia Mwema kuwa Mwongozo wa Katoliki umetungwa na vigogo wa serikali na taasisi za umma akiwemo Jaji Mkuu Bw. Agustino Ramadhan, Kingunge ana hoja ya msingi.... Watashindaje hao wakatoliki wenye dhamana katika uongozi wa dola kutoa siri za serikali kwa viongozi wa katoliki!! ...wakibisha nani haogopi kutengwa. Kama mchezo utakuwa vivyo hivyo kwa madhehebu na dini nyingine kweli nchi itakuwa salama kweli? hasa ukifikilia kuwa katoliki wana upendeleo wa kuleta mapadre kutoka mataifa yote duniani bila mushkheri, lakini waislamu walipothubutu kuleta masheikh na taasisi za misaada walitoposhwa kama swala kwa visingizio mbalimbali.

Papa aliyepita alikuwa mpoland, aliyefuata na aliyeko sasa ni mjerumani. Bulawayo Zimbabwe waepelekewa skofu mhindi na si mzimbabwe. Padre wa kanisa Katoliki anafanya kazi popote duniani kwa sababu ana kiapo cha utii kwa sakofu wake au mamlaka ya kanisa.

TUmeshakujibu hilo tuendelee na mada ili Kingunge wa vingunge aendelee kupata vidonge vyake.

Hivi nani anajua email ya Kingunge?
 
Ama kweli Tanzania ukitaka ubaya wako uanikwe basi wewe liseme vibaya kanisa katoliki.

Bila shaka kanisa hili linajiona linaweza kuongoza nchi kwa remote control. Kani kimbelembele kila pahala.

Issue ya KADHI wao wanatoa tamko
Issue ya OIC wao wanatoa tamko
uchaguzi 2010, wao wanatoa tamko(warka)
Kufuta misamaha a kodi kwa taasisi za dini na NGO ( wao tamko)

hakika wakatoliki tumewachoka toeni matamko yenu kanisani kwa waumini wenu na msichanganye dini na siasa.

BRAVO KINGUNGE. mengi watasema lakini ukweli unauma
something tells me this person has a chip on his/her shoulder........halafu ni mdini.....my advice to you barubaru....jadili hoja...
 
Hakuna nguvu yoyote inayoweza kutuzuia kuchagua viongozi waadilifu katika uchaguzi wa mwakani. Hatutaki viongozi wanaoongozwa na nguvu za giza! Katika kufikia azma hiyo tunaamini kazi iliyoanzishwa na Kanisa Katoliki ni kazi takatifu na Mungu mwenyewe ataisimamia. Yeye ndiye anayejua mioyo ya sisi waja wake. Tutachagua viongozi waadilifu bila kujali dini wanazozifuata wala kabila. Na hiyo ndiyo dhana kuu ya waraka huu wa Wakatoliki. Wote wanaopingana na hili washindwe na walegee!
 
Last edited:
kingunge mnafiki fisadi mkubwa ...anaweza kusimama mbele za watu kuongea lolote ,mnafiki mkubwa huyu na fortune hunter ..,alikuwa mshauri wa siasa wa mkapa ...alipoona mkapa anastaafu akajitosa mara moja kwa kikwete ili aendelee kula.....wenzake wote wameshastaafu ....sijui kikwete naye akistaafu atajipendekeza kwa nani...

kingunge amepoteza uhalali wa kuongea kwa ajili ya wanyonge....

..eeeh mwalimu nyerere fufuka uone uone ....wasaidizi wako wanafiki kama kingunge ..wamejuka mafisadi!!!...kawawa amekaa kimya ....nadhani naye kuna wanaopandia mgongini mwake kufanya ufisadi...japo yeye anaweza kuwa msafi!!!

kama kawawa ni msafi tunaomba umuite kingunge umuulize ...."mdogo wangu kingunge bado wewe ni mkomunisti wa imani kali!!!???"
 
Hizi ni taasisi za biashara na fedha na shughuli nyingine zinazotoa huduma katika jumuiya. Biashara zinazotoa mahitaji ya vitu/bidhaa na kubadilishana na bidhaa hizi. Taasisi za fedha zinatunza thamani ya fedha, kwa kuweka kiwango cha kubadilisha fedha.

- Katika biashara, motisha haipaswi kuwa katika faida tu. Biashara inawafikishia watu bidhaa, hivyo isiendeshwe kiunyonyaji.
- Ni vipi tunaweza kuwasaidia watu kutetea maslahi yao na kuzuia wasinyonywe.
- Moyo wa ushirika umepungua mno na matokeo yake watu wameathiriwa na biashara zilizokosa uwaminifu. Tunawezaje kusaidiana.
- Mfumo wetu wa benki unafikisha huduma kwa watu wachache tu, na hasa kwa watu wa mijini na kwa wale wenye kiwango kizuri cha kipato. Lazima tusaidiane, hasa wale ambao hawana kipato cha kutosha, kuunda SACCOS na vikundi vya kusaidiana. Kanisa lazima lifanye bidii kuhamasisha hayo.
- Wachache walio katika mamlaka au katika nafasi za juu za utawala wana marupurupu mengi mno. Tusukume kupunguziwa hayo ili wawe na maisha ya kawaida.
- Tuwe makini na uporaji wa ardhi unaofanywa na makapuni makubwa na watu binafsi, matajiri. Tukumbuke ardhi ni ya thamani na ni hitaji la lazima kwa kila mmoja.
- Rushwa katika biashara, huduma duni, bidhaa duni vinaleta sifa mbaya, na hii ni tabia iliyo dhambi. Miongoni mwa watu hali hii inawajengea hasira na kukosa uaminifu na vile vile watu hujitetea kwa nguvu na kujengea watu fikra ya kulipiza kisasi.
- Udanganyifu katika biashara ni kushusha sifa mmiliki kwa wateja.
- Serikali iwe makini katika kuweka mikataba na wawekezaji wa umma na watu binafsi. Imekwishabainika kuwa katika mikataba hiyo maslahi ya wananchi hayalindwi kikamilifu badala yake wawekezaji hupewa unafuu mkubwa kwa kisingizio kuwa ni kivutio kwao.
- Makapuni ya ndani ni lazima yatiwe moyo na kuungwa mkono ili yaweze kuboresha utendaji wao uwe wenye tija.
]



Nadhani watu wasihukumu kitabu kwa kasha lake...huu waraka sio mbaya ...la muhimu ni mtu binafsi kuchuja yale yanayohusu uchungaji achana nayo....ANGALIA YALE YA MUHIMU KWA TAIFA....NADHANI HAYA NI MAONI YAO..Wanasiasa na wananchi wachukue yale yawawaao...

ANGALIA KWA MAKINI MOJA CONTENTS KWENYE KITABU CHA KANISA..HAPO JUU.....NA UNIAMBIE KAMA NI USHAURI MBAYA AU LA!!
 
Sioni suala la unafiki linaingiaje hapa. Kama unafiki basi KINGUNGE KAMBALE MWITU ndio mnafiki namba moja. Usilitusi kanisa kwa kulipakazia sifa ya kishetani ya unafiki. This is blasphemy. Lakini nadhani tatizo la baadhi yetu ni kwamba hatutaki kusoma. Hebu soma huo waraka kwanza ndipo urudi kuchangia humu JF. Hata hivyo, nafurahi kuona kuwa wengi wanaonekana wameelewa nia njema ya Wakatoliki kwa nchi yetu.

Naona umetawaliwa na jazba na hasira but may be si kutokana na uchungu wa dini mie sina haja y kuusoma waraka wote but ninasoma vitu muhimu tu. Waraka kama huu ulienezwa Mexico, Argentina kwa mifano michache matokeo yake nchi zile zimechafuka. (Ref kitabu kinaitwa The roots of evil by Ervin Staub). Nchi hizi zimechafuka vibaya sana kwa mauaji ya halaiki na ubadhirifu na corruption ya hali ya juu kabisa.

Naomba nijibiwe je waraka ulifanya kazi????
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom