John Haramba
JF-Expert Member
- Feb 4, 2022
- 365
- 1,373
Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP), Simon Sirro, mapema leo amefanya ukaguzi wa ghafla kwenye Kituo vya Polisi cha Stakishari, Tabata na Kawe jijini Dar es Salaam.
IGP Sirro amebaini changamoto ya uhalifu wa uporaji kwa kutumia pikipiki pamoja na makosa ya uvunjaji.
“Nimekuwa nikipata malalamiko kutoka kwa baadhi ya wananchi kuhusu kituo cha Stakishari, Tabata Reli na Kituo cha Kawa, nikaamua kufanya ukaguzi wa dharura, nimebaini kuna matukio ya vijana kutumia pikipiki kupora, hawa vijana ambao jina la mtaani wanaitwa Vishandu.
“Vishandu wameongezeka, mtu kashika mkoba wake, dereva bodaboda anatokea kwa nyuma anakwapua, nimeelekeza oparesheni za nguvu zipafanyike ili kuhakikisha matukio kama haya yanapungua
“Pia kuna matukio mengine madogomadogo ikiwemo uvunjaji wa usiku, nimeelekeza oparesheni za nguvu kufanyika kuhakikisha matukio haya yanapungua kwa kiasi kikubwa, vikundi vya ulinzi shirikishi vitasaidia matukio kama hayo.
“Sisi askari pekee hatutoshi, ni lazima tushirikiane tuone uharifu unapungua lakini kimsingi tuko vizuri sana, matukio yanaendelea kupungua, wananchi watupe ushirikiano,” anasema Sirro.
IGP Sirro amebaini changamoto ya uhalifu wa uporaji kwa kutumia pikipiki pamoja na makosa ya uvunjaji.
“Nimekuwa nikipata malalamiko kutoka kwa baadhi ya wananchi kuhusu kituo cha Stakishari, Tabata Reli na Kituo cha Kawa, nikaamua kufanya ukaguzi wa dharura, nimebaini kuna matukio ya vijana kutumia pikipiki kupora, hawa vijana ambao jina la mtaani wanaitwa Vishandu.
“Vishandu wameongezeka, mtu kashika mkoba wake, dereva bodaboda anatokea kwa nyuma anakwapua, nimeelekeza oparesheni za nguvu zipafanyike ili kuhakikisha matukio kama haya yanapungua
“Pia kuna matukio mengine madogomadogo ikiwemo uvunjaji wa usiku, nimeelekeza oparesheni za nguvu kufanyika kuhakikisha matukio haya yanapungua kwa kiasi kikubwa, vikundi vya ulinzi shirikishi vitasaidia matukio kama hayo.
“Sisi askari pekee hatutoshi, ni lazima tushirikiane tuone uharifu unapungua lakini kimsingi tuko vizuri sana, matukio yanaendelea kupungua, wananchi watupe ushirikiano,” anasema Sirro.