Vyama vinne vya upinzani vilivyoanzisha ushirikiano, vinafanya utaratibu wa kumuomba radhi Rais Jakaya Mrisho Kikwete kutokana na kitendo chao cha kumuweka katika orodha ya mafisadi iliyotolewa katika viwanja vya Mwembe Yanga mapema mwezi uliopita.
Habari ambazo Rai imezipata kutoka kwa baadhi ya viongozi wa upinzani, zinaeleza kwamba kimsingi vyama hivyo vimegundua kwamba yalikuwa ni makosa ya kimkakati kumtaja Rais katika tuhuma hizo kwa sababu tuhuma walizotoa juu yake ni nyepesi.
Rai imeelezwa kwamba iwapo mambo yatakwenda vizuri, wataifanya kazi hiyo siku ya Jumamosi kwa kumuomba radhi rasmi Kikwete ikiwa ni pamoja na watu wengine wawili. Rai haikufanikiwa kupata jina la mtu wa tatu lakini mtu wa pili ameelezwa kuwa ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Patrick Rutabanzibwa.
Katika tuhuma zilizosomwa na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Wilbroad Slaa, wapinzani walisema kuwa pamoja na mambo mengine, Agosti mwaka 1994, Kikwete aliingia katika mkataba na kampuni ya madini ya Kahama Mining Corporation Ltd.
Tuhuma hizo zilieleza kwamba ingawa mkataba ulionyesha kuwa ulikuwa unahusu eneo la Butobela Wilaya ya Geita Mkoani Mwanza, Agosti mwaka 1996 Kahama Mining Corporation walivamia eneo la Bulyanhulu, na kuwaondosha kwa nguvu watu waliokuwa wakiishi na kuchimba dhahabu katika eneo hilo. Baadaye Sutton Resources iliiuza Kahama Mining Corporation na Bulyanhulu kwa Kampuni ya Dhahabu ya Barrick Gold Corporation ya Toronto, Canada.
Mmoja kati ya viongozi wa kambi ya upinzani, ameiambia Rai kwamba baada ya kuangalia athari za tuhuma dhidi ya rais, wamegundua kwamba hilo lilikuwa kosa la kimkakati.
Strategically hilo lilikuwa kosa kumtaja Rais. Pia tuhuma dhidi yake zilikuwa nyepesi sana. Tunamtoa rais na wengine wawili, lakini tunaongeza wapya. Oktoba 27 tutamtoa na kumuomba radhi, alisema kiongozi huyo ambaye hata hivyo hakutaka jina lake litajwe.
Soorce Rai
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
VIONGOZI WA USHIRIKIANO WA VYAMA VYA UPINZANI KUZUNGUMZA NA WANANCHI KUHUSU UFISADI
Kuanika jinsi mabilioni mengine yalivyochotwa benki kuu
Kutaja viongozi wa serikali walivyohusika na kampuni hewa ilivyotumika
Kugawa mkataba wa Richmond kwa umma
Viongozi wa Ushirikiano wa Vyama Vya Upinzani vya CHADEMA, CUF, NCCR Mageuzi na TLP siku ya jumapili tarehe 28 Oktoba, 2007 watazungumza na wananchi katika mkutano wa ndani kutoa taarifa kwa umma kuhusu ufisadi.
Mazungumzo hayo ya ndani ambayo wananchi mbalimbali wanaalikwa kushiriki yatafanyika katika Ukumbi wa Urafiki uliopo Manispaa ya Kinondoni Jimbo la Ubungo Mkoani Dar e salaam kuanzia saa 4 mpaka saa 5 na nusu asubuhi.
Katika mazungumzo hayo viongozi wa Vyama vya Upinzani wataanika jinsi mabilioni mengine zaidi yalivyochotwa katika benki kuu ya Tanzania na kutaja viongozi wa serikali walivyohusika na kampuni hewa ilivyotumika.
Itakumbukwa kwamba tarehe 15 Septemba, 2007 katika mkutano wa hadhara uwanja wa Mwembeyanga uongozi wa ushirikiano wa vyama vya upinzani ulitaja orodha ya mafisadi nchini yenye kueleza ufisadi, wizi na/au ubadhirifu au matumizi mabaya ya rasilimali za taifa.
Pamoja na viongozi wengine pia, Dr Wilbroad Slaa, Mbunge wa Karatu(CHADEMA) atazungumza katika mkutano huo. Dr Slaa ndiye aliyeibua hoja ya kutaka kuundwa kwa kamati teule ya kuchunguza tuhuma za ufisadi katika benki kuu na kupelekea kutangazwa kwa orodha ya mafisadi. Dr Slaa amerejea hivi karibuni kutoka Marekani ziarani nchini Marekani na Mkutano wa Bunge la Kusini mwa Afrika SADC nchini Malawi.
Katika mkutano huu hatutataja orodha nyingine ya mafisadi. Tutajenga katika orodha ya awali ya mafisadi. Katika mkutano huu kitakachotajwa ni ufisadi mwingine uliopelekea mabilioni mengine kuchotwa katika benki kuu. Pia katika Mkutano huo tutagawa mkataba wenye utata wa Richmond kama tulivyofanya kwa mkataba wa Madini wa Buzwagi ili umma
Imetolewa na 26/10/2007:
John Mnyika
Mjumbe wa Kamati ya Maandalizi na
Mkurugenzi wa Vijana Taifa(CHADEMA)
0754694553