Wapinzani Kamuombeni Msaada Kikwete

Wapinzani Kamuombeni Msaada Kikwete

Kama nilivyowahi kuandika uzi huu, Shukran Rais Kikwete Kwa Kuwapa Darsa la Siasa Upinzani..., sasa nnawakumbusha tena upinzani kuwa warudi kwa Kikwete akawape darsa vipi wakabiliane na hali ya kisiasa inavyokwenda kwa sasa nchini. Na vipi wao kama upinzani wakabiliane nayo.

Kikwete ni muelewa na kwa kuwa sasa ni "mzee" mstaafu tena mwenye busara sana, ni wakati muafaka upinzani umuone ili wakwamuke walipokwama.

Kikwete ni kipenzi cha wote na nnauhakika upinzani mna mengi ya kujifunza kwake, msichoke nendeni mkachote.


Hapa Tundu Lisu akiwa wa kwanza kukimbilia Kahawa Ikulu, huku Baregu akikodolea macho, hiki ndicho wanachokikosa akina Tundu Lisu!

CDM5.jpg
 
Nahisi nae (Faiza) katumia njia ile ile ya JK alioitumia pale chuo juzi kati pale, alifikisha ujumbe kinamna na bi mkubwa nae ka copy style hiyo hiyo; mi nimemwelewa sana huyu mama

Ikiwa ukisoma huelewi basi hata picha huoni?

CDM7.jpg



Nendeni tu mkamuombe hikma zake na kudeka kama mlivyokuwa mkideka alipokuwa Ikulu.
 
Kama nilivyowahi kuandika uzi huu, Shukran Rais Kikwete Kwa Kuwapa Darsa la Siasa Upinzani..., sasa nnawakumbusha tena upinzani kuwa warudi kwa Kikwete akawape darsa vipi wakabiliane na hali ya kisiasa inavyokwenda kwa sasa nchini. Na vipi wao kama upinzani wakabiliane nayo.

Kikwete ni muelewa na kwa kuwa sasa ni "mzee" mstaafu tena mwenye busara sana, ni wakati muafaka upinzani umuone ili wakwamuke walipokwama.

Kikwete ni kipenzi cha wote na nnauhakika upinzani mna mengi ya kujifunza kwake, msichoke nendeni mkachote.
Kwa uwelewa wako unazani macomrade waikina mdee,mbowe,lisu na wengne hawalijui hilo la jinsi ya kwenda na mwenendo wa kisiasa hapa nchin au kuna nafasi umehaidiwa teyari?
 
sasa si aibu tulivyomnanga wakati ule
Muelewa yule mzee,mi naimani naye anaweza saidia...maake dah! Ukijiajiri kelo,tra,polisi,traffic,sijui mammlaka gani zote zinakuja kutaka vibali,bei ya vibal na kodi sasa...unafunga ofisu unarudi nyumbani..ukiuliza ajira una ambiwa vumilia au jiajiri!! Kazi ipo
 
Ukweli utabakia ukweli,baada ya tafakari pana sasa naamini Mwl Nyerere Baba wa Taifa ni mwanasiasa mwenye maono makubwa.Wakati uleee alisema Rais tunayemtaka lazima awe na ufahamu wa siasa ya dunia (Mambo ya Nje)Lazima awe ni mtu anaye heshimu KATIBA.

Kwanini nashangaa sasa wakati wake alikuwa akipendelea wagombea waliopitia wizara ya mambo ya nje au mabalozi sikujua ni kwanini nilimlaumu sana tena sana.

Rais wetu katokea wizara ya Ujenzi,siasa za dunia hakuwahi kuzifanyia kazi kipindi chote cha uhai wake wa kisiasa.Leo unashangaa anamkaribisha mfalme wa Morocco wakati anajua wazi sababu za sisi kumtenga bado zipo.Leo tumekosa misaada ya MCC,hoja dhaifu zinadai Tanzania haina haja na misaada tutajitegemea wenyewe ????.Suala la mgogoro wa Zanzibar kama mkuu wa nchi alitakiwa kulishughulikia kwa taadhari kubwa huku diplomasia ya hali ya juu ikichukua mkondo wake,sote tunajua alipokwenda Zanzibar alisema nini.

Chini ya utawala wa awamu ya nne demokrasia ilichukua nafasi yake,kipindi chake hali imekuwa si hali.Hatukuwahi hata siku moja kukosa chanjo na madawa muhimu hospital za serekali leo hali si hali.Elimu ya juu wanafunzi wengi walipata mkopo leo .......

Nitakuwa mtu wa mwanzo kabisa ikiwa fursa ya kwenda kumpongeza Dr Jakaya Mrisho Kikwete itajitokeza.Mungu mbariki Kikwete Mungu mjalie afya njema.
 
Naona miamala kutoka Lumumba imeanza kusoma, maana mlikuwa mmepotea tokea walivyositisha buku 7.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom