Wapinzani hawana sifa za Kuongoza nchi. (comparison analysis)

Ukitaka kujua chadema haina watu tizama wachangiaji wake mtandaoni wengi hawana hoja za maana zaidi ya matusi ukienda bungeni ndio uozo kabisaa

umenena vema mkuu! hawana hoja zaid ya vitisho na kuahidi kutoweka kwa aman
 
tetetetetetetetetetetetete.........HAKA KAJAMAA BWANA, YAANI KUMSEMA LOWASA VIBAYA NA KUUNGWA MKONO NA BAADHI YA WAZEE WA CCM SASA KAMEANZA KULEWA SIFA,tetetetetetetetetete.......kwiikwiii. KANAJIONA KANAJUA SANA.
 
'Sio kawaida wana ccm kujisomea" Unamaanisha nn?
Mtazamo wa Paulo kwa maana ya ushindani wa kisera kupitia vyama vya siasa ni sahihi.

Huwezi kushindana kisera na watu wasiokuwa na sera kama CCM,wanaendeshwa kwa kauli mbiu ambazo kimsingi hazitekelezi.Sisi tulioko kwenye gvt system tunajua na tunaona jinsi nchi inavojiendesha.Kwa taarifa yako mpaka sasa CDM ina sera katika maeneo 15 ndio maana wananchi wanavutiwa sana na mikutano yao.Ina sera zinazojibu kero zao za mda mrefu,CDM NI SERA,CDM NI FALSAFA,CDM NI ITIKADI,CDM NI TUMAINI JIPYA NDO MAANA TUNAFUKUZA WASALITI.Chama kisichikuwa na mwelekeo hakiwezi kuwa na wasaliti,watasaliti nini na wakati hawana common agenda.
 
Siasa ama chama chochote cha siasa ni zao la falsafa. Kuwa Mwanasiasa bila kuwa na falsafa ama kuwa na Chama cha Siasa ambacho hakina msingi wa falsafa ni kasoro kubwa ambayo hufanya mwanasiasa ama Chama Cha Siasa kutofanikiwa katika lengo lake kuu. Kukosa falsafa kunasababisha Mwanasiasa ama Chama Cha Siasa kutokuwa na dira ya kuifuata na matokeo yake ni kufanya siasa inayo- base katika matukio na kukosoa mawazo na mipango ya wengine ama vyama vingine bila kuwa na WAZO kuu ambalo unalisimamia kama mwanasiasa ama Chama Cha Siasa. Kila mwanadamu kwa asili ya Uanadamu wake hujengwa na imani juu ya kitu fulani, uamini katika mlengwa fulani unaofahamika kwa jina la ITIKADI, Hivyo Chama Cha Siasa ni mkusanyiko wa kundi la watu ambao wanaamini katika ITIKADI moja, hivyo tukiitaja CCM directly tunataja UJAMAA kama ITIKADI kuu ambayo wanachama na Viongozi wa CCM wanaiamini na kuitetea kwa hoja na nguvu zote.

Utangulizi huo unamaana moja kuu katika thread hii niliyoipa jina "UKWELI MCHUNGU" kuwa CCM imejipambanua kwa itikadi yake na kuisimamia popote pale, wapinzani hawana msingi unaotokana na ITIKADI na SERA, wamejikita katika kufanya siasa za matukio na UBISHANI. Siasa isiyo endelevu kwani matukio hukoma kwa wakati fulani, hivyo kwa wananchi walio makini hawawezi kuamini katika Chama ambacho chenyewe hakina kitu ama falsafa inayoiamini. Wananchi wanahitaji viongozi wenye falsafa wanayoiamini.

Katiba ya nchi yetu iko wazi kuwa sera kuu ni Ujamaa na Kujitegemea, vyama vya siasa vilipaswa kujipambanua kisera kuona nani zaidi katika kufikia sera hiyo kuu. CCM inajimbanua vyema katika hili, kuwa na vyama vya siasa vinavyoamini nje ya itikadi hiyo ya Taifa ni kuvunja Katiba lakini msingi wake ni kutowajibika sawasawa kwani hili lilipaswa kuangaliwa kuanzia kwenye hatua ya usajili wa Vyama. Matokeo yake ni kuja kuwa Chama ambacho kitaongoza nchi nje ya mifumo yake ya kikatiba na hivyo kuzaa uongozi dhaifu, usiozingatia na hata kuvunja katiba ya nchi.

Maana ya kuwa na Vyama vya upinzani ni kutaka kuwapa wananchi alternative ya Uongozi na falsafa. sio KAZI ya upinzani kupinga kila kitu na sio kazi ya upinzani kusifia serikali, kimsingi kazi ya upinzani ni kutoa the best alternative solution to justify that opposition is the best alternative government in waiting. Lazima upinzani ujijenge kisera, kifalsafa na kiitikadi ambayo wananchi wataona kuwa ni njia ya kufikia Maendeleo na kuwajengea matumaini ya Mafanikio na Maisha Bora (kwani ndio paramount demand ya wananchi - MAISHA BORA)

Na nasema kama Upinzani ungekuwa makini basi Serikali na Chama Kilicho Madarakani nikimaanisha Chama Changu CCM kingekuwa makini zaidi, MWALIMU Nyerere aliwahi kusema maneno ambayo mpaka leo yamewekwa kwenye bango mbele ya Ukumbi wa Mikutano ya NEC (maarufu kama whitehouse) pale Makao makuu dodoma, maneno yale yanasema " Bila CCM madhubuti nchi yetu itayumba, na Upinzani wa kweli utatoka ndani ya CCM "

TANZANIA imekosa UPINZANI MAKINI, upinzani unaojitambua nini unataka na wafanye nini kufikia hicho wanachokitaka. Wachambuzi wa siasa wanapoangalia uimara wa upinzani moja ya kigezo ni kutathimini uwezo wa mawaziri (Viongozi) na watendaji wa Chama tawala na Serikalini yake ukilinganisha na mawaziri Vivuli,na viongozi wa Upinzani. Inatakiwa Shadow Cabinet ioneshe uwezo na matumaini kuliko cabinet. Upinzani uoneshe matumaini na uwezo kuliko CCM.

Wananchi wanaangalia alternative ambayo wapinzani wanakuja nayo, wanafanya comparison analysis ya viongozi hao yaani kwa mfano, kwenye baraza la mawaziri na mawaziri vivuli:
wananchi wanaangalia kambi ya upinzani bungeni kama mfano wa Uwezo wa Viongozi wa Upinzaniti, wanaangalia kati ya:

  • Lema V/s Chikawe kwenye Wizara ya mambo ya ndani, wanajiuliza hivi ni kweli LEMA anaweza kuwa best alternative ya CHIKAWE..,kweli..?
  • Selasini V/s Dr Mwinyi kwenye Wizara ya Ulinzi, wananchi wanawapima kwa uwezo wao.
  • SUGU v/s Dr Mukangara kwenye wizara ya habari, utamaduni na michezo, wananchi wanajiuliza hivi ni kweli SUGU anaweza kuwa bora mbele ya Dr Mukangara hata washawishike kukiondoa Chama kilichomsimamisha Dr Mukangara wakipe Chama kilichowaletea SUGU kama best alternative...,kweli..?
  • Msigwa v/s Lazaro Nyalandu kwenye wizara ya Maliasili.
Wenye v/s Bernard Kamilius Membe kwenye Wizara ya Mambo ya nje.,wananchi wanajiuliza hivi kweli MEMBE akisimama na WENJE..,Wenje anaweza kuonekana bora na kiongozi wa maana mbele ya MEMBE..? wananchi makini wanayaona haya na kuyapima na kisha kufanya uamuzi kupitia sanduku la KURA.

Kwa tathimini hiyo fupi, na hata kwa Uongozi wa juu wa Vyama vya upinzani., mathalani Chama kikuu cha Upinzani yaani Chadema.,ukifanya tathimini kwa Umakini juu ya Aina na Uwezo wa Viongozi wake dhidi ya wale wa Chama Makini CCM, wananchi wanaona matumaini na future bora ya nchi kupitia CCM.

Mathalani tazama mifano hii:
  • Wenyeviti; CHADEMA-MBOWE dhidi ya CCM-KIKWETE
  • Makamu M/kiti: CHADEMA-resigned ARFI dhidi ya CCM-MANGULA
  • Katibu Mkuu: CHADEMA - DR. SLAA dhidi ya CCM- KINANA
  • Naibu K/mkuu: CHADEMA - suspended ZITTO dhidi ya CCM- MWIGULU

Ukiangalia kwa Upande wa Sekretaieti ya CCM
  1. NAPE NNAUYE
  2. MAMA ASHA-ROSE MIGIRO
  3. MAMA ZAKHIA MEGHJI
  4. DR SEIF KHATIBU

Kwa upande wa CHADEMA.
  1. ANTHONY KOMU
  2. JOHN MNYIKA
  3. LEMA GODBLESS
  4. TUNDU LISSU
  5. LWAKATARE
  6. BENSONI KIGAILA
  7. JOHN MREMA

Wananchi makini wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wanawapima viongozi wao kwa kutathimini uwezo, maarifa, na uzoefu. kwa tathimini hii ni Vipi watanzania wanaweza kuwapa Upinzani nchi hii., kwa tathmini hii ni wazi CCM itaendelea kuwa Chama bora na kitakachoendelea kutawala nchi hii kwa miaka mingine hamsini na dahari.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI..

Vivaa Vijana Vivaaa.

VIJANA KARIBUNI CCM na kazi iendelee...!!!

wewe ni boya kweli,inaonekana hujui kabisa maana ya ujamaa na kujitegemea,hebu tuambie hiyo itikadi ccm ipo?halafu imeeandika kanakwamba kila chama kinapaswa kuifuata,utafuataje kitu ammbacho hakipo hata kwenu wenye hiyo itikadi?
pili hayo maisha bora kwakila mtanzania yako wapi?hapa kwakweli umenichefua kabisaa?matibabu hovyo kabisa,ni Mungu tu ndiye anayetuponya,wakubwa zako wakiugua hata mafua haoo nje ya nchi,halafu unasema maisha bora kwa kila mtanzania!nipe mfano mmoja tu mdogo unaoonesha bora kwa watanzania.mara nyingine usingee kabisa kuhusu maisha unatuchefua kabisa vijana wenzako halafu bila aibu unatoa wito tuje ccm,ili tutumike.ni wasio makini wachumia tumbo watakuja ccm kama wewe.
unavigezo gani kusema wapinzani hawana uwezo wa kuongoza?wapinzani ndiyo wanawatoa jasho maccm hata bungeni,tena chadema tu inawakosesha usingizi kuanzia mwenyekiti wenu hadi balozi mtaani,nadikitika sana kuona kijana kama wewe unakuwa blind wa akili namna hiyo,amka njoo cdm tuikomboe nchi hii brother
 
Katika mambo ambayo nafsi yangu inajutia ni pamoja na kuwahi kuwa mwanachama na kiongozi wa Chadema. Najiuliza kwa maovu yale leo watamzania wananielewaje..?

Nasikitika kuwa nilipoteza mwelekeo na sikuwahi kujifunza siasa kama ninavyojifunza ndani ya CCM.

kijana kama Kaka yangu makonda hauwezi kumpata ndani ya Chadema.

nakuombea mungu uendelee kuwapa ukweli hawa mazuzu wasiojitambia huenda wakafinguka akili zao.
Moja ya madhara ya kufanya ukahaba ni kukosa uwezo wa kufikiri na kujenga hoja zenye mashiko! mawazo yako hayalingani kabisa na mhitimu wa elimu ya chuo kikuu!
 
Kupitia sanduku la kura wananchi waliamua kuwa Lema ni zaidi ya Matilda Buruani, Wenje ni zaidi ya Masha, Msigwa ni zaidi ya Hilda, Highness ni zaidi ya Diallo, Nassari ni zaidi ya Sumari, Selasini ni zaidi ya Mramba, Mnyika ni zaidi ya Hawa Ngulume (ambaye alikuwa zaidi ya Nape) nk..
Kupitia sanduku la kura...

Unataka kutueleza nini...
 
Upinzani ni kweli haufai kushika nchi, walahauna uwezo wa kufikirika kushika nchi; kwa sababu ni magenge ya wahuni..Mbowe, slaa akina Lema ni magenge fulani ya wahuni waliopata kibali cha kuiba kwa usafi

CCM kwa upande wake, iliishajifia siku nyingi sana, ina ongoza kwa sbbu hamna upinzani na kwa sbbu haina tena moyo wa kujiuliza wala kuuma pale inapofanya dhambi

CCM sio genge la wahuni bali ni genge la wauji na majambazi


unaposema wapinzani waifuate katiba ya nchi nakushangaa sana, eti ulitaka upinzani kila mmoja aimbe ujamaa na kujitegemea??

una hakika CCM inasimamia itikadi na falsafa zake??

ni nini kimekusukuma kuandika hii post na ukaiita ''compasrison analysis"" ??


CCM mshakufa, na hamna uwezo wa kuwanyooshea vidole wapinzani- hamuishi

wapinzani wao sio wahuni tu bali wanajiua wakijua kuna hatari ya kupoteza 'chakura'-case study Zitto



ACT mpango mzima

Sasa umeshasema upinzani hauna uwezo wala mipango ya kuongoza nchi. Halafu unamalizia na "ACT mpango mzima". Sasa ACT sio wapinzani?
Watu wengine sijui walienda shule kufanya nini!!!
 
Wananchi wanapohitaji mabadiliko huwa hawangalii haiba au sura au historia, bali wao wanaweza kuweka jiwe liwaongoze kwa ajili ya mahitaji na malengo yao ya baadaye. Na ndio maana mapinduzi yanagharimu roho za watawala muda wote.
 
Huyo mungu wako unayemuandika kwa kuanza na herufi ndogo hana madhara.Ni ushirikina kwa wengine.

Kama hauna hoja ya kuchangia ni bora ukae kimya. Au unaona ikiwa haujaonekana kuchangia kibarua kitaota nyasi. Wafuasi wa Josephine mna natatizo makubwa ya kichwa. Sasa kama nitakuuliza hapa ndo umeandika ama kuchangia nini..??
 
Huu ni ukweli mchungu hata iweje, CCM imejidhihirisha kukosa mshindani sasa iko yenyewe, itafika wakati CCM Itaacha kupiga kampeni maana wanapita bila kupingwa, wapinzani wamekwisha jikatia tamaa.
 
Kinachosikitisha ni kwamba Bunge Maalumu limesheheni watu wenye mfanano wa kifikra na ''mchambuzi'' wetu kuhusu udhaifu wa upinzani nchini!

 
Kama hauna hoja ya kuchangia ni bora ukae kimya. Au unaona ikiwa haujaonekana kuchangia kibarua kitaota nyasi. Wafuasi wa Josephine mna natatizo makubwa ya kichwa. Sasa kama nitakuuliza hapa ndo umeandika ama kuchangia nini..??

mchumia tumbo dada yangu,mahaba yamekuzidi,mpe na makonda basi!
 
Ulingia na gia ya "posho haitoshi" ukaona kupata huwezi ukaamua kuondoka na Nokia Lumia. Sasa umekuja na "COMPARISON ANALYSIS" badala ya A COMPARATIVE ANALYSIS. Kazi unayo mdogo wangu Paul Makonda!!!
 
Kama hauna hoja ya kuchangia ni bora ukae kimya. Au unaona ikiwa haujaonekana kuchangia kibarua kitaota nyasi. Wafuasi wa Josephine mna natatizo makubwa ya kichwa. Sasa kama nitakuuliza hapa ndo umeandika ama kuchangia nini..??
unashutumu watu kuwa hawawezi kuandika au kufikiri?.. yatima wewe wa vwawa lini uliwahi kuandika presentation peke yako zaidi ni kuiba kaz za watu jmana...

Umalaya huu awamu hiii hadi kundule livuje wadudu...

Na utajuta sana kozi huna mbele wala nyuma kima mkubwa wewe
 
Moja ya madhara ya kufanya ukahaba ni kukosa uwezo wa kufikiri na kujenga hoja zenye mashiko! mawazo yako hayalingani kabisa na mhitimu wa elimu ya chuo kikuu!
Punguzeni matusi na person attack bwana mnaharibu hili jukwaa. Mods nanyi kuweni makini mambo kama haya yanashusha hadhi ya forum na kufanya hata wachangiaji kudharaulika., tuweni makini basi.
 
Punguzeni matusi na person attack bwana mnaharibu hili jukwaa. Mods nanyi kuweni makini mambo kama haya yanashusha hadhi ya forum na kufanya hata wachangiaji kudharaulika., tuweni makini basi.
Kaa pembeni wewe juha, kama unadhani kumtetea huyo kahaba mwenzio kutakuongezea ujiko umekosea sana!
 
Makonda mie pamaoja na kuwa mchambuzi kiasi nilikuondoa kwenye watu wa maana tangu pale ulipomtukana Lowasa bila sababu za maana mradi tu umfuruaishe 6 kibwege. Tungependa tujue nanai alikutuma umtukane Bwana yule. Yeye kwa kuwa ana busara kakuacha tu na kwa kuwa kwake wewe ni kifaranga unayetafuta sifa uchwara kupitia kwake ndio maana anakuona ZUZU (ndio ankuona ZUZU TU) na amekuacha uangaike na dunia hii. Uchambuzi hapo haupo ila ni umaskini wa fikra tu umekutuma kuandika unyonyoto huu
 
CCM ni janga la kitaifa.Ili tupate maendeleo ya kweli katika nchi,ni lazima sisiemu waondoke madarakani.Tubadilike watanzania chama hiki ni cha kundi la wachache wanaokula hata bila kunawa na wale wanaoambulia makombo "house niggers".Jiulize ni asilimia ngapi ya watanzania walipiga kura?sisiemu hamjiulizi maswali kwani madaraka yamewalevya.Hali hii mnayoiona katika nchi hii siyo amani bali ni utulivu wa muda tu,likilipuka mtakuja kuona.Someni maandishi yaliyoandikwa ukutani."Power corrupts,but when power is absolute,corrupts asolutely.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom