Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,468
- 911,174
Wapiga debe wasiokuwa na sare kufukuzwa kesho Ubungo Saturday, 22 January 2011 20:07
Mariam Sagafu, MUM
HATIMAYE lile agizo lililotolewa hivi karibuni na Waziri wa Uchukuzi, Omari Nundu la kuwataka wapiga debe wote wasiokuwa na sare za kuwatambulisha mabasi yao wanayofanyia kazi waondoke katika kituo Kikuu cha Mabasi cha Ubungo (UBT) jijini Dar es Salaam litaanza rasmi kesho kituoni hapo.
Wakizungumza jana na Mwananchi kwa nyakati tofauti kituoni hapo, baadhi ya wapiga debe hao walisema matangazo yalitolewa juzi na jana eneo hilo kupitia vipaza sauti kituo hapo, yaliyosema kuwa siku ya Jumatatu watafukuzwa kama hawataondoka kwa hiyari yao.
Tutafurahi sana kama zoezi hili likifanyiwa kazi kwani wapiga debe wasiokuwa na sare wengi wao ni wezi na kesi nyingi zimeshajitokeza na kusababisha ugumu wa kazi yao, alisema Hassan Issa ambaye ni mpiga debe katika kituo hicho.
Kwa upande wake, Christopher ambaye alijulikana kwa jina moja alikuwa amevaa sare ya basi la Mohamedi Trans alisema wanaumia sana na mambo yanayofanywa na wapiga debe holela kwani yeye ana mke na watoto watatu na anaishi kwa kutegemea kazi hiyo.
Mapema wiki iliyopita, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu aliwataka wapiga debe hao wafuate agizo la Waziri kabla serikali haijaanza kuchukua hatua.
Napenda kuwapa taarifa wapiga debe hao wafuate agizo la waziri kabla ya serikali haijachukua hatua, alisema Kenyela.
Hatua hiyo itakayochukuliwa na uongozi wa kituo inaweza ikaleta usalama zaidi kituoni hapo kwani abiria wengi wamekuwa hawana imani na wapiga debe hata wale waliosajiliwa na mabasi na kuleta ugumu wa kazi yao.
Mariam Sagafu, MUM
HATIMAYE lile agizo lililotolewa hivi karibuni na Waziri wa Uchukuzi, Omari Nundu la kuwataka wapiga debe wote wasiokuwa na sare za kuwatambulisha mabasi yao wanayofanyia kazi waondoke katika kituo Kikuu cha Mabasi cha Ubungo (UBT) jijini Dar es Salaam litaanza rasmi kesho kituoni hapo.
Wakizungumza jana na Mwananchi kwa nyakati tofauti kituoni hapo, baadhi ya wapiga debe hao walisema matangazo yalitolewa juzi na jana eneo hilo kupitia vipaza sauti kituo hapo, yaliyosema kuwa siku ya Jumatatu watafukuzwa kama hawataondoka kwa hiyari yao.
Tutafurahi sana kama zoezi hili likifanyiwa kazi kwani wapiga debe wasiokuwa na sare wengi wao ni wezi na kesi nyingi zimeshajitokeza na kusababisha ugumu wa kazi yao, alisema Hassan Issa ambaye ni mpiga debe katika kituo hicho.
Kwa upande wake, Christopher ambaye alijulikana kwa jina moja alikuwa amevaa sare ya basi la Mohamedi Trans alisema wanaumia sana na mambo yanayofanywa na wapiga debe holela kwani yeye ana mke na watoto watatu na anaishi kwa kutegemea kazi hiyo.
Mapema wiki iliyopita, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu aliwataka wapiga debe hao wafuate agizo la Waziri kabla serikali haijaanza kuchukua hatua.
Napenda kuwapa taarifa wapiga debe hao wafuate agizo la waziri kabla ya serikali haijachukua hatua, alisema Kenyela.
Hatua hiyo itakayochukuliwa na uongozi wa kituo inaweza ikaleta usalama zaidi kituoni hapo kwani abiria wengi wamekuwa hawana imani na wapiga debe hata wale waliosajiliwa na mabasi na kuleta ugumu wa kazi yao.