Wapi nitapata machine ya kufyatua tofali ya mikono au ya kutumia mota?

Dr.adams faida

JF-Expert Member
Mar 11, 2013
1,829
3,159
Habari za Jumapili hii ndugu zangu. Kiafya mimi niko vyema kabisa, wacha niende moja kwa moja kwenye mada.

Nimekuwa nikifanya uchunguzi juu ya biashara ya ufyatuaji tofali nikaona soko kubwa lipo mijini kwa maana wajenzi wengi ndipo walipo. Nimekaa nikafikiri na kugundua kuwa wajasiriamali walio wengi wanaouza tofali wengi wao hawafungui matawi madogo madogo pembeni ya miji ambapo watu wengi hukimbilia kujenga maeneo hayo.

Sasa basi linapokuja swala la ujenzi watu hawa wanapata taabu kwenye swala la tofali kwani wengi wao huwabidi waende mijini kununua tofali ambapo kuna machine za umeme za kufyatua tofali.

Gharama za usafirishaji huwa ziko juu na pengine mteja hufikisha tofali zikiwa baadhi zimeharibika kwa kupasuka kutokana na ubovu wa miundo mbinu ikiwemo barabara kuwa mbovu.

Mteja katumia gharama kununua tofali let say kanunua tofali kwa bei ya 850/=@ tofali, mpaka kuzifikisha site na amechukua tofali 1000 ambayo thamani ya 850000/=. Mteja huyohuyo anafikisha tofali hata 20 zimevunjika ambayo ni sawa hasara ya shilingi 17000/=.

Nimekaa nikafikiri niteke soko kwa watu waliopembeni na miji wanaofanya ujenzi nianzishe mradi wa kufyatua tofali kwa kumfata mteja palepale site nitafute vijana 10 wapate utaalamu wakuzitumia mashine,pia ninunue machine kama 6 hivi niingie mitaani kuzisaka pesa nitajitahidi nahakikisha natoa bidhaa zilizo bora zaidi.

Biashara hii nimependa niifanyie Kahama kwa maana ni mji unaokua kwa kasi ya ajabu. Makazi yangu yapo Dar es Salaam ila nitafanya niwezalo ili niweze kusimamia mradi wangu.

Mwisho nataka nipate uzoefu kwa walionitangulia kwenye hii project ikiwemo changamoto zake.

Pia wapi nitapata mashine yenye ubora kwa bei nzuri?
 
Kahama kwenyewe wamejaa wauza tofali labda ukategeshee nje kidogo lakini sehem ambayo utaona watu wanakimbilia kujenga kwa kuwa Kahama inajaa evenly kama maji kwenye sahani.
 
Habari za Jumapili hii ndugu zangu. Kiafya mimi niko vyema kabisa, wacha niende moja kwa moja kwenye mada.

Nimekuwa nikifanya uchunguzi juu ya biashara ya ufyatuaji tofali nikaona soko kubwa lipo mijini kwa maana wajenzi wengi ndipo walipo. Nimekaa nikafikiri na kugundua kuwa wajasiriamali walio wengi wanaouza tofali wengi wao hawafungui matawi madogo madogo pembeni ya miji ambapo watu wengi hukimbilia kujenga maeneo hayo.

Sasa basi linapokuja swala la ujenzi watu hawa wanapata taabu kwenye swala la tofali kwani wengi wao huwabidi waende mijini kununua tofali ambapo kuna machine za umeme za kufyatua tofali.

Gharama za usafirishaji huwa ziko juu na pengine mteja hufikisha tofali zikiwa baadhi zimeharibika kwa kupasuka kutokana na ubovu wa miundo mbinu ikiwemo barabara kuwa mbovu.

Mteja katumia gharama kununua tofali let say kanunua tofali kwa bei ya 850/=@ tofali, mpaka kuzifikisha site na amechukua tofali 1000 ambayo thamani ya 850000/=. Mteja huyohuyo anafikisha tofali hata 20 zimevunjika ambayo ni sawa hasara ya shilingi 17000/=.

Nimekaa nikafikiri niteke soko kwa watu waliopembeni na miji wanaofanya ujenzi nianzishe mradi wa kufyatua tofali kwa kumfata mteja palepale site nitafute vijana 10 wapate utaalamu wakuzitumia mashine,pia ninunue machine kama 6 hivi niingie mitaani kuzisaka pesa nitajitahidi nahakikisha natoa bidhaa zilizo bora zaidi.

Biashara hii nimependa niifanyie Kahama kwa maana ni mji unaokua kwa kasi ya ajabu. Makazi yangu yapo Dar es Salaam ila nitafanya niwezalo ili niweze kusimamia mradi wangu.

Mwisho nataka nipate uzoefu kwa walionitangulia kwenye hii project ikiwemo changamoto zake.

Pia wapi nitapata mashine yenye ubora kwa bei nzuri?
Mkuu katika mji wa kibaha ukitengeneza tofali imarà ni mji unaojengeka utauza hata tofali 2000 kwa siku
Ukiwa serious nitafte nitakusaidia kuona location nzuri ila ni lazima uwe na tipper ya kuwabebea wateja
 
Mkuu nitafute 0762612213 tukuuzie mashine za tofali tunazo za mkono na zile za umeme

Na utapewa guarantee tupo dsm
 
Ya mkono laki tatu au laki tano zipo aina mbili

Na umeme zipo 2.1m ya tofali moja na ile ya tofali mbili 2.5m
mkuu ningependa pia nijue je machine hizi za mikono zinachangamoto zipi ikiwemo katika swala zima la kuharibika kwa baadhi ya vifaa,vitu gani vya kukuzingatia wakati wa matumizi?
 
Mkuu katika mji wa kibaha ukitengeneza tofali imarà ni mji unaojengeka utauza hata tofali 2000 kwa siku
Ukiwa serious nitafte nitakusaidia kuona location nzuri ila ni lazima uwe na tipper ya kuwabebea wateja
kibaha mkuu naona pia hii biashara imeshamiri nimewahi kufanya survey mpaka mlandizi njia ielekeayo lupunga mpaka mzenga naona jamaa wamejaa wenye mashine za umeme.
 
kibaha mkuu naona pia hii biashara imeshamiri nimewahi kufanya survey mpaka mlandizi njia ielekeayo lupunga mpaka mzenga naona jamaa wamejaa wenye mashine za umeme.
Ni kweli lakini uimara wa tofali ndio tatizo na mda mwingine tofali zinakosekana mpaka utoe older week ukiwekeza ki ukweli utapata faida kubwa
 
Back
Top Bottom