Nilimpenda dada mmoja ambaye nilimzidi miaka 8 wakati nimemaliza form six yeye alikuwa form 1.Nilipanga ndiye angekuwa mke wangu hasa ukizingatia nilipenda kuoa mke ambaye ni bikira kwa kuwa hata mimi nilijitahidi kujitunza na kwa kuwa nilitaka asome nilikuwa nikimuasa asifanye mambo hayo ila akazanie masomo tu nikiwa na malengo hapo baadaye akifika angalau A level ndiyo nimtamkie lengo langu juu yake.Tatizo lilikuja pale nilipokuwa mwaka wa pili chuo Kikuu niliporudi likizo baadhi ya vijana ambao alikuwa akisoma nao shule moja walinipa taarifa kwamba ameanza kumegwa kisawasawa mpaka hata na walimu wake hii ilitokea mara tu baada ya kuja kunisalimia na kunikuta na hao vijana ambao walikuwa wakinichukulia kama kaka na mwalimu wao maana nilikuwa nawafundisha tuition kabla sijaenda chuo kikuu ndipo walipoanza kunipa taarifa hizo.Pia kwa kuwa mama yangu mzazi alihisi huenda hapo baadaye nikamchumbia kumbe alikuwa na yeye akimfuatilia kimyakimya na yeye alikuwa na majibu kama ya wanafunzi wenzake hivyo yeye alikuwa akimponda kama kunipa tahadhari.Niliamua kumuitamdogo wangu ambaye walikuwa wanasoma naye shule moja ili kupata uhakika, mdogo wangu aliniambia siku hizi ni kweli amebadilika.Kwa kuwa wote tulikuwa tunaishi mtaa mmoja niliamua kuamini walichokisema, nikamuuliza mhusika lakini hakutaka kutoa ushirikiano yeye akawa anapotezea mada.Hivyo nikaamua kuachana naye.
Nilirejea Chuoni kumalizia semister ya pili ya mwaka wa pili.Mwisho wa semister nilikutana na dada mmoja ambaye tulikuwa tunasoma naye course moja ila nilikuwa namzidi mwaka mmoja nilitokea kumpenda nakuonyesha nia ya kuja kumuoa baadaye lakini sasa historia ya maisha yake haikuwa nzuri kwani alikuwa ameishatembea na wanaume wanne.Roho yangu ilishutuka sana kwani mimi nilitaka nioe mwanamke ambaye hajaguswa kwani hata mimi nilijitunza sana.Kibaya zaidi huyu dada alinieleza mtu wa nne alikuwa naye kwenye mahusiano ya miaka minne na ndiye alikuwa anatarajia kumuoa lakini alikula kona baada ya yeye kuingia chuo kikuu kwa kuhofia kuzidiwa na mke kielimu kwani huyo mchumba wake alikuwa na diploma.Huyo dada alikuwa akinisimulia huku analia jambo ambalo nilinigusa nikashindwa hata kula kona (kumkimbia) kwa kumuonea huruma.
Nilimfuata mtumishi wa dini ili anipe ushauri, aliniambia niache mambo ya kiswahili kwani nikifanya hivyo naweza kukosa mke mwema tena alinifokea sana.Hivyo nikakubaliana naye kwa shingo upande.Baada ya kumaliza mitihani yangu ya mwisho mwaka wa tatu, nikiwa katika maandalizi ya kutaka kuondoka chuoni yule dada alikuja chumbani kwangu ili aniage na kwa kuwa alikuwa ni mzoefu katika mambo ya kikubwa alinishawishi nikafanya naye tendo la ndoa bila kutumia kinga hivyo akapata ujauzito.Namshukuru Mungu hakuwa na maambukizi ya HIV hivyo wote tulikuwa salama ingawa nilijutia sana.Niliamua kumuoa ingawa lengo langu lilikuwa ni kuoa mke ambaye hajaguswa kwa kuhofia mwanangu kukosa mapenzi yangu pia kumtenda tena yule dada.
Yanayonisibu katika ndoa mpaka wakati mwingine nahisi nilikosea:
1. Siku zote mimi ndiyo nimekuwa initiator wa tendo la ndoa mpaka nahisi labda ni kwa sababu alitumia vibaya usichana wake, Kwani siku zote gari used halifanyi kazi kama jipya.
2. Kwa kuwa dhehebu langu hufundisha mambo ya ndoa vizuri na jinsi ya kumuandaa mke vizuri, kwa kuwa nimesoma sehemu mbalimbali za jinsi ya kumpa mke kitu roho inapenda nikishiriki na mke wangu yeye hupata mpaka multiple orgasm katika round moja tu.Nikitaka kwenda round ya pili yeye huwa amechoka kabisa hivyo ananiacha nasikilizia maumivu.
3. Akipata ujauzito ukafikia miezi mitano hakuna kufanya tendo la ndoa mpaka miezi mitatu baada ya kujifungua muda wote huo napata maumivu.Nijuavyo mimi mama mjamzito anaweza ku do hata mpaka mwezi mmja kabla ya kujifungua.
4. Viongozi wa dini walikuwa wanatuasa tuvumilie kwani tukioa tunaweza kufanya mambo ya kikubwa hata kila siku jambo ambalo kwangu ni ndoto.
5. Tukiwa kunako sita kwa sita anataka style moja tu ndiyo itumike yaani missionary.
6. Nimezaa nae watoto watatu mpaka sasa na kwakuwa nawajali watoto wangu hivyo nimeamua kuishi na maumivu ya kutoridhishwa katika ndoa.Najitahidi kuvishinda vishawishi kutoka kwa wakinadada mbalimbali ambao wako tayari kuchukua nafasi.
Ninavyodhani mimi kosa langu lilikuwa ni kumuoa mke aliyetumika sana ambaye haendani na mimi ambaye ndiyo kwanza nataka kufaidi mambo ya kikubwa.Kwani hata gari usedi halina mwendo kama gari mpya.
Wadau wapi pengine mnazani nimekosea, Nitakuwa makini kwa mwanangu wa kiume kuhakikisha hapati kama yaliyonikumba.