Mke ni kitu cha ajabu sana!

Mke ni kitu cha ajabu sana!

Me na mke wangu tulikutana bar tena kulikuwa na show ya singeli. Me nimeenda kwa stress zangu sikujua kama Kuna show bhana.

Huku na huku nikaona tako lile pale linazungusha miuno ya uzazi taratibu huku likiwa limekaa kwenye kiti kirefu. Nikajitosa kuomba kampani. Nilipigwa za uso na aliyekuwa nae mpaka aibu.

Badae nikajua kuwa wanapenda kwenda pale kila weekend. Weekend iliyofata ndio nikafanikiwa japo kupata namba.

Nilikuwa namchukulia poa na kahaba tuu, ila weekend iyo niliishia kupewa lifti na gari ake mpaka nilikopanga, na kwakuwa nilikuwa nimelewa sana alirudi mchana kunicheki naendeleaje.

Akakuta geto halitamaniki akaanza kufua, kufanya usafi na kupika. Mahusiano yakaanzia hapo.

Baada ya Kodi yangu kuisha akaniongezea kiasi Cha pesa ili nikapange walau nyuba ya maana zaidi.

Hivi Leo ni mama wa watoto wetu watatu, ameacha pombe, ameacha singeli na Huwa nahimizwa kusali jumuiya na kwenda chechi kila jumamosi na jumapili kitu ambacho kimenishinda kwakweli.

Ile bar tuliyokutana Sasa hivi imengwa hoteli nzuri tuu,basi mara chache tunaenda kulala ipi kujikumbushia tulipokutana.

Kweli mke ni kitu Cha ajabu sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom