Umeongea facts mzee na utawajua kupitia comment zao hapa.Wafuasi na wapenzi wa CHADEMA. Kwa maoni yangu binafsi kwasasa hapa nchini wafuasi na wapenzi wa CHADEMA ndio kundi la watu wenye Hasira kali zaidi.
Watu hawa wamegawanyika sehemu mbili
1: Tabaka la Uongozi wa CHADEMA. Viongozi wa hiki chama ni watu wenye Hasira kali Sana, Chuki, husuda, visasi
Ukisikiliza hotuba zao utagundua hilo. Ni watu wenye kutamka maneno makali yenye kubeba hisia nzito kutoka mioyoni mwao ambazo wanatamani watanzania wote wawe nazo. Vyama pinzani vyote vingine wanataka viunge mkono CHADEMA kwa chochote kile watacho sema kinyume na hapo basi ni mamluki wa CCM.
Ikitokea siku moja Tanzania kila mtaa unawaka moto, huku watoto wakibakwa kikatili, kuuawa na vilio kila Kona basi siku hiyo kwao itakuwa ni sherehe kubwa sana.
2: Wafuasi na chama, wapenzi na wakeleketwa. Hawa nao ni watu wenye Hasira kali sana, ni watu wenye maneno makali yenye lengo la kuudhi hata pasipo sababu kabisa.
Mfano Mzuri ni hapa jukwaani ole wako ukianzisha mada isiyo sifu CHADEMA tena bahati mbaya iwe na hoja ngumu kujibika zenye ukweli kuhusu chama chao, hapo ndipo hasira huwaka zaidi. Utakutana na kauli za ajabu Kama:
Mataga
Uza ubongo mana unakaa nao kwa hasara.
Lissu amewasika kunako
Huna akili
Pumba n.k
Wakiambiwa na viongozi wao kuhusu kuandamana kudai haki basi hapo hulipuka kwa shangwe kubwa sana wengine hudiliki kusema damu imwagike!
Muda huo wanakuwa wamesahau kuwa.
Yawezekana mumewe au mke ni wa chama kingine tofauti na yeye.
Mwanaye, mjomba, shangazi, boss wake ofisini, jirani yake, mpangaji mwenzake, mfanya biashara mwenzake, rafiki wa familia yake n.k ni watu wa vyama tofauti na yeye. Hajui kwamba akianza kumwaga hiyo damu itaanzia nyumbani kwake kumwagika.
Kwa kifupi hao ndio CHADEMA a.k.a watanzania wanao ishi kwa hofu kubwa sana kwa mujibu wa maneno yao ya mitandaoni.
Kwa mtu asiye ijua Tanzania au anaye ishi nje ya Tanzania akifuatilia kundi hili la CHADEMA wa mitandaoni anaweza kudhani nchi inawake moto.
Ukitaka kundi hili liwe na furaha sana na uitwe mwenye akili kubwa basi unatakiwa useme:
CHADEMA ndio chama bora Cha siasa kuliko vyote barani Afrika.
Lissu ndio mwanasheria bora zaidi kuliko wote Tanzania.
Lissu ndio binadamu pekee mwenye akili nyingi kuwazidi watanzania wote.
Yote tisa kumi, tukana serikali kwa kadiri uwezavyo hapo utakuwa umewakonga nyoyo zao haswaa.