Wapendwa nisaidieni kwa hili

Wapendwa nisaidieni kwa hili

Ng'wanapagi

JF-Expert Member
Joined
Sep 18, 2013
Posts
9,116
Reaction score
8,658
Ndugu zangu habari za weekend.

Tangu nianze kuota ndevu zimekuwa zinaongezeka kila mara. Mwanzoni nilikuwa natumia nyembe za Gillet lakini nikinyoa natokwa na upele unaowasha sana. Baadaye nikaanza kuhudhuria saloon lakini hali ni ileile, baadae nimeanza kutumia magic powder hapo ndo tatizo la upele na muwasho likaisha.

Tatizo kubwa linalonikumba ni kuwa kila baada ya siku tatu ndevu zinakuwa nyingi na zinawasha hadi ninyoe kwa magic ndipo tapata usingizi tofauti na hapo ndugu zangu usingizi hakuna. Kuna kipindi niliambiwa na rafiki zangu nisizinyoe na zitaniwasha mwanzoni lakini itafikia hatua zitaacha na nilitii lakini nilionekana kituko kwa watu walionizoea kwa kuitwa majina mbalimbali japo hata mimi sipendi kufunga ndevu.

Ndugu zangu kwa yoyote anaweza kunisaidia naomba anipe msaada wa vitu vya kutumia aidha kupunguza wingi wa ndevu zinazoota au muwasho pindi zinapoanza kuota kwani sawa hivi sasa nina uwezo wa kutumia hivyo bidhaa (magic powder,Eskinol,After shave) lakini naamini maisha huwa yanachenji na ukajikuta hata wembe huwezi nunua. Nisaidieni waungwana.
 
Pole sana mkuu.I hope utapata msaada,mi situmii kabisa nyembe natumia mashine najinyoa mwenyewe,niliona kila siku kukwangua ngozi na wembe inaweza kuleta matatizo mbele au vipele vikubwa.

kuna jamaa yangu zamani alikuwa anatumia dawa flani akipaka zinakuwa zinakatika zenyewe si kunyoa,sijui inaitwaje nadhani inaweza kukusaidia,ila hapo kwenye kuota ndevu fasta sijui
 
Pole sana mkuu.I hope utapata msaada,mi situmii kabisa nyembe natumia mashine najinyoa mwenyewe,niliona kila siku kukwangua ngozi na wembe inaweza kuleta matatizo mbele au vipele vikubwa.

kuna jamaa yangu zamani alikuwa anatumia dawa flani akipaka zinakuwa zinakatika zenyewe si kunyoa,sijui inaitwaje nadhani inaweza kukusaidia,ila hapo kwenye kuota ndevu fasta sijui

Asante sana bro. Ningeipata hiyo ya kupaka ingenisaidia sana lakini nashkuru kwa mawazo yako.
 
Back
Top Bottom