Maisha haya! Hii dunia ina mambo sana, hivi wapangaji wenzangu mnakabiliana vipi na mpangaji mwenzako asiyetaka kulipia maji na umeme jamani na mnatumia wote?
Huyu jirani yangu kanishinda tabia walahi, angekuwa bidhaa ningemgawa bure kabisa maana hafai msikitini wala kanisani, hafai kwa mchuzi wala kuchomelea, kha, mtu gani kila bili ana sababu mpya jamani mwaka mzima halipi maji, umeme kaweka 5000 mwaka unaisha!
Jirani yangu ana mwaka hapa alihamia akanikuta, tangu kaja hajawahi lipa maji hata siku moja, yeye kila bili ana sababu ni magomvi tu jamani mpaka nachoka kupigizana naye kelele maana tupo wawili tu ila halipi, mtaishia kugombana tu na bili halipi na kutumia anatumia tena akianza kufua nguo moja anasuuza na ndoo moja ya maji.
Yeye hana mtoto anaishi peke yake ila ana wageni wa kke kila baada ya masaa mawili anakuja mtu na huyo mgeni wake ataoga na kama ni kufua atafua, nafahamu kwa sababu yeye hana choo cha ndani anatumia cha nje hivyo naona maana kipo usawa wa dirisha langu.
Mie nina familia ya watu 5, ila mara nyingi tupo 3, kiustarabu nilimwambia umeme aweke wa 10000 na mie wa 20000 kwa sababu mie nina friji yeye hana ila vingine vyote tuko navyo sawa vinavyotumia umeme akajibu sawa.
Akanunua umeme wa 5000 akasema ataweka 5000 tena ukiisha umeme haujawekwa wala kununuliwa tena nikimwambia anajibu yeye hana matumizi ya 10000 kwa mwezi sababu hana watoto matumizi yake ni madogo sana, mie ndio nitakuwa namaliza umeme hivyo hanunui na saa ni mwaka umepita tangu aweke 5000.
Maji nayo anadai watoto wangu ndio watakuwa wanamaliza maji yeye hana matumizi ya maji hivyo halipi bili, kifupi ni mkorofi kuliko kawaida mpare huyu.
Yaani hana aibu hata kidogo anatumia na halipi na sio shida zake kha, juzi ndio kanitolea kali ya mwaka, anasema hawezi lipa bili ya maji na huku yeye hana bomba la maji ndani kama mimi, kwa nini mie niwe na maji ndani yeye hana hivyo halipi bili!
Soma:Nimechoka kufungiwa MITA ya maji na jirani yangu