Wapangaji AICC wapanga hujuma usiku

Waziri2025

Senior Member
Sep 2, 2019
148
379
Wapangaji zaidi ya 30 wa nyumba Za kuishi zilizoko kijenge jijini Arusha zinazomilikiwa na kituo cha mikutano cha kimataifa Arusha,(AICC) wamekituhumu kituo hicho kuwapangisha kwenye nyumba mbovu zilizooza na zimekuwa zikivuja kama mwembe wakati wa mvua.

Katika kikao chao cha Siri kilichofanyika majira ya usiku katika msitu uliopo Kando na nyumba hizo za kijenge, waandishi wa habari hawakuruhusiwa kufika na wale waliofika walitimuliwa.

Wapangaji hao wakiongozwa na Kiongozi wao, Elisia Gama (Binti CCM) walionesha kuwa na nia ovu ya kutaka kukihujumu kituo hicho kikimbiwe na wapangaji na hivyo kukosa mapato ya kujiendesha.

Kikao hicho kilianza majira ya Saa 12 jioni Kwa hoja mbalimbali, ikiwa Madai yao makubwa ni kulalamikia uongozi wa kituo cha AICC kutokukarabati nyumba Zake kiasi kwamba baadhi ya nyumba zinavuja kama mwembe wakati wa mvua, kupandishiwa kodi pamoja na kuombwa rushwa na baadhi ya watendaji wake Pindi wanapompangisha Mteja Mpya.

"Mimi mwenyewe lililipa sh, Laki nne kando na kodi ili kupata nyumba hapa AICC huu ni mradi unaofanywa na watendaji na wamwgeuza dili ya kujipatia fedha haramu" alisikika Esilia alisema.

Baadhi ya wapangaji walisikika katika kikao hicho wakidai ni bora kuhamasisha watu wasusie kupanga ili zibaki magofu hatuwezi kuishi nyumba mbovu, tunaandika barua za malalamiko lakini hakuna chochote.

Mkurugenzi wa AICC, Elishilia Kaaya alisema hakuna mpangaji aliyefika ofisini kulalamika ila alisema wapangaji hao wengi wao ni wadaiwa sugu na wanatumia kigezo hicho kukwepa kodi ya pango.

Kaaya alimtaka mpangaji anayeona hastahili kuishi katika nyumba hizo aondoke.
 
Kwani nyumba za kupanga ni hizo tu? Haya hatakama nyumba ni mbovu kwani wewe mpangaji huwezi irekebisha.
 
Pamoja na Malalamiko mengi kwa wapangaji wa aicc kulalamikia kile walichodai ubovu wa nyumba za kituo hicho siri imevuja kwamba wengi wao wanadaiwa mamilioni ya fedha akiwemo kiongozi wa wapangaji hao Elisia Gama (Binti CCM )anayedaiwa kodi ya upangaji milioni 10 ambayo hajalipa katika kipindi cha miaka mitatu mfururizo.

Mkurugenzi wa aicc,Elishilia Kaaya amesema wapangaji waliokaa kikao.usiku kupanga nia ovu dhidi yake na kituo hicho wengi wao ni wadaiwa sugu na amewataka kulipa madeni yao haraka kabla ya kuwachukulia hatua ikiwemo kuwatimua katika nyumba hizo.

"Hao wote wanaolalamikaa wengi wao ni wadaiwa sugu nimeagiza wote wenye madeni makubwa wachukuliwe hatua na watolewe kwenye nyumba na vitu vyao vishikiliwe hadi wamalize kulipa madeni yao" alisema kaaya.

Awali wapangaji zaidi ya 30 wa nyumba Za kuishi zilizoko kijenge jijini Arusha zinazomilikiwa na kituo cha mikutano cha kimataifa Arusha,(AICC) wamekituhumu kituo hicho kuwapangisha kwenye nyumba mbovu zilizooza na zimekuwa zikivuja kama mwembe wakati wa mvua.

.......
 
Pamoja na Malalamiko mengi kwa wapangaji wa aicc kulalamikia kile walichodai ubovu wa nyumba za kituo hicho siri imevuja kwamba wengi wao wanadaiwa mamilioni ya fedha akiwemo kiongozi wa wapangaji hao Elisia Gama (Binti CCM )anayedaiwa kodi ya upangaji milioni 10 ambayo hajalipa katika kipindi cha miaka mitatu mfururizo.

Mkurugenzi wa aicc,Elishilia Kaaya amesema wapangaji waliokaa kikao.usiku kupanga nia ovu dhidi yake na kituo hicho wengi wao ni wadaiwa sugu na amewataka kulipa madeni yao haraka kabla ya kuwachukulia hatua ikiwemo kuwatimua katika nyumba hizo.

"Hao wote wanaolalamikaa wengi wao ni wadaiwa sugu nimeagiza wote wenye madeni makubwa wachukuliwe hatua na watolewe kwenye nyumba na vitu vyao vishikiliwe hadi wamalize kulipa madeni yao" alisema kaaya.

Awali wapangaji zaidi ya 30 wa nyumba Za kuishi zilizoko kijenge jijini Arusha zinazomilikiwa na kituo cha mikutano cha kimataifa Arusha,(AICC) wamekituhumu kituo hicho kuwapangisha kwenye nyumba mbovu zilizooza na zimekuwa zikivuja kama mwembe wakati wa mvua.

.......
Huyo biccm hata kama anadaiwa hawezi kufikisha deni la zaidi ya 2m....aicc deni la miezi 3 tu huwa wanafukuza mpangaji,labda huyu dada ndgu wa meko
 
Hao wapangaji wajiongeze, wahamie mahali pengine pazuri nyumba zipo nyingi sana wasichokijua ni kwamba siku watakayohama siku hio hio wapangaji wengine wapya wataingia mikataba hio hio ambayo wanaikataa.
 
Back
Top Bottom