Red Scorpion
JF-Expert Member
- Feb 1, 2012
- 5,736
- 4,254
Afisa misitu kaenda kwenye shamba la miti la jamaa kukagua. Jamaa akamwambia usiingie saa hizi. Afisa akatoa kitambulisho cha kazi, "We ni nani wa kunizuia? Kwa hiki kitambulisho hakuna wa kunizuia nisifanye shughuli zangu!" Jamaa kamfungulia geti. Baada ya muda jamaa anamuona afisa misitu akifukuzwa na nyuki huku akipiga kelele, "Mama nakufa! Nisaidie! Nyuki wananiuma!!" Jamaa akamwambia "WAONYESHE KITAMBULISHO"