Wanne kati ya sita waliojaribu kumteka Tarimo wahukumiwa kwenda jela miaka saba

Wanne kati ya sita waliojaribu kumteka Tarimo wahukumiwa kwenda jela miaka saba

Nyakijooga

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2018
Posts
427
Reaction score
666
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kivukoni, Kinondoni, imewahukumu vijana wanne kifungo cha miaka saba jela kila mmoja baada ya kupatikana na hatia ya kujaribu kumteka mfanyabiashara Deogratus Tarimo, huku washtakiwa wawili wakiachiliwa huru kutokana na ushahidi kutokuthibitisha ushiriki wao.

Waliyoachiwa huru ni Nelson Msela (24), dereva teksi, na Anitha Temba (27), baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha mashtaka dhidi yao.

Waliohukumiwa ni Fredrick Nsato (21), askari mkazi wa Kibamba, Isaack Mwaifuani (29), bondia kutoka Kimara, Benki Mwakalebela (40), wakala wa mabasi Stendi ya Magufuli, na Bato Tweve (32), bondia mkazi wa Kimara Bonyokwa.

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Mkazi Mkuu Ramadhani Rugemalira amesema ushahidi wa upande wa Jamhuri umeweza kuthibitisha bila kuacha shaka kwamba washtakiwa hao wanne walihusika katika jaribio la utekaji, ingawa hawakufanikiwa kumteka mwathirika.

“Washtakiwa wote wanne mnahukumiwa kifungo cha miaka saba jela kwa kosa la kujaribu kumteka mfanyabiashara Deogratus Tarimo, kwa kuwa ushahidi umeonyesha walikuwa kwenye harakati ambazo hazikufanikiwa,” amesema Hakimu Rugemalira.

Kabla ya hukumu, upande wa mashtaka uliiomba Mahakama itoe adhabu kali kama fundisho kwa jamii, huku washtakiwa wakiomba kupunguziwa adhabu wakidai walidanganywa na Nsato kwamba walikuwa wakisaidia kumkamata mtuhumiwa.

Tukio hilo lilitokea Novemba 11, 2024 eneo la Kiluvya Madukani, Wilaya ya Kinondoni, ambapo inadaiwa washtakiwa walipanga kumteka Tarimo wakitumia mtego uliopangwa na Anitha Temba, aliyemshawishi mfanyabiashara huyo wakutane kwenye hoteli kwa mazungumzo ya biashara.

Baada ya Tarimo kufika kwenye eneo aliloelekezwa, alisubiri kwenye baa kama alivyoambiwa, ndipo washtakiwa walipofika kwa gari aina ya Toyota Raum lenye namba T 237 EGE na kujaribu kumteka, kabla ya mpango huo kushindikana.


FB_IMG_1760975852199.jpg

Chanzo: Nipashe Digital
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kivukoni, Kinondoni, imewahukumu vijana wanne kifungo cha miaka saba jela kila mmoja baada ya kupatikana na hatia ya kujaribu kumteka mfanyabiashara Deogratus Tarimo, huku washtakiwa wawili wakiachiliwa huru kutokana na ushahidi kutokuthibitisha ushiriki wao.
View attachment 3491212
Chanzo: Nipashe Digital
Danganya toto kutuliza upepo mbaya!
 
Watu hupita na upepo, wenzao Wengine Wana kinga kubwa hivyo hutowasikia popote pale.
 
Hakuna kitu hapa hii danganya toto, kwa hili wimbi kubwa la utekaji na serikali kuhusishwa baadhi ya matukio mengi wa resume tukio la hawa jamaa kama njia moja wapo ya kujisafisha.
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kivukoni, Kinondoni imewahukumu vijana wanne akiwemo askari mmoja Fredrick Nsato (21) na mabondia wawili kifungo cha miaka saba jela baada ya kupatikana na hatia ya kujaribu kumteka mfanyabiashara Deogratus Tarimo, ambapo pia mahakama hiyo imewaachia huru dereva teksi Nelson Msela (24) na Anitha Temba (27) baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha mashtaka dhidi yao kama walihusika na tukio hilo.

Vijana hao waliohukumiwa ni Nsato (21) mkazi wa Kibamba, bondia Isaack Mwaifuani (29) mkazi wa Kimara, Benk Mwakalebela (40) wakala wa mabasi katika stendi ya Magufuli na bondia Bato Twelve (32) mkazi wa Bonyokwa.

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Mkazi Mkuu Ramadhani Rugemalira alisema baada ya kupitia ushahidi wa upande wa mashtaka, vielelezo na utetezi wa washtakiwa, upande wa Jamhuri umeweza kuthibitisha bila kuacha shaka kwa washtakiwa wanne kati ya sita.

“Washtakiwa waliotiwa hatiani ni Fredrick Nsato, Benki Daniel, Bato Twelve, Isaack Mwaifuani na mahakama inawaachia huru washtakiwa watano na sita, Nelson na Anitha,” alisema Hakimu Rugemalira.



Akifafanua adhabu hiyo, Hakimu Rugemalira alisema awali washtakiwa walikuwa wakishtakiwa kwa kosa la utekaji lakini wamehukumiwa kwa kosa la kujaribu kuteka kwa sababu ushahidi wote unaonesha Tarimo aliachwa eneo la tukio.

“Washtakiwa wote wanne mnahukumiwa kifungo cha miaka saba jela kwa kila mmoja kwa kujaribu kumteka mfanyabiashara Deogratus Tarimo kwa sababu Jamhuri haikuthibitisha kama alitekwa, mazingira ya ushahidi yalikuwa kwenye harakati ambazo hazikufanikiwa,” alisema.



Washtakiwa waliomba wapunguzwe adhabu kwa madai kwamba mshtakiwa wa kwanza ambaye ni askari alikuwa akitekeleza maagizo, lakini ombi hilo halikukubaliwa.
Screenshot_20251020-215351.png
 
Waliohukumiwa ni Fredrick Nsato (21), askari mkazi wa Kibamba, Isaack Mwaifuani (29), bondia kutoka Kimara, Benki Mwakalebela (40), wakala wa mabasi Stendi ya Magufuli, na Bato Tweve (32), bondia mkazi wa Kimara Bonyokwa.
Hawa jamaa ndio waliojifanya wasiojulikana? Bado siamini
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kivukoni, Kinondoni, imewahukumu vijana wanne kifungo cha miaka saba jela kila mmoja baada ya kupatikana na hatia ya kujaribu kumteka mfanyabiashara Deogratus Tarimo, huku washtakiwa wawili wakiachiliwa huru kutokana na ushahidi kutokuthibitisha ushiriki wao.

Waliyoachiwa huru ni Nelson Msela (24), dereva teksi, na Anitha Temba (27), baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha mashtaka dhidi yao.

Waliohukumiwa ni Fredrick Nsato (21), askari mkazi wa Kibamba, Isaack Mwaifuani (29), bondia kutoka Kimara, Benki Mwakalebela (40), wakala wa mabasi Stendi ya Magufuli, na Bato Tweve (32), bondia mkazi wa Kimara Bonyokwa.

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Mkazi Mkuu Ramadhani Rugemalira amesema ushahidi wa upande wa Jamhuri umeweza kuthibitisha bila kuacha shaka kwamba washtakiwa hao wanne walihusika katika jaribio la utekaji, ingawa hawakufanikiwa kumteka mwathirika.

“Washtakiwa wote wanne mnahukumiwa kifungo cha miaka saba jela kwa kosa la kujaribu kumteka mfanyabiashara Deogratus Tarimo, kwa kuwa ushahidi umeonyesha walikuwa kwenye harakati ambazo hazikufanikiwa,” amesema Hakimu Rugemalira.

Kabla ya hukumu, upande wa mashtaka uliiomba Mahakama itoe adhabu kali kama fundisho kwa jamii, huku washtakiwa wakiomba kupunguziwa adhabu wakidai walidanganywa na Nsato kwamba walikuwa wakisaidia kumkamata mtuhumiwa.

Tukio hilo lilitokea Novemba 11, 2024 eneo la Kiluvya Madukani, Wilaya ya Kinondoni, ambapo inadaiwa washtakiwa walipanga kumteka Tarimo wakitumia mtego uliopangwa na Anitha Temba, aliyemshawishi mfanyabiashara huyo wakutane kwenye hoteli kwa mazungumzo ya biashara.

Baada ya Tarimo kufika kwenye eneo aliloelekezwa, alisubiri kwenye baa kama alivyoambiwa, ndipo washtakiwa walipofika kwa gari aina ya Toyota Raum lenye namba T 237 EGE na kujaribu kumteka, kabla ya mpango huo kushindikana.


View attachment 3491212
Chanzo: Nipashe Digital
Sio rahisi kuamini haya....
 
Hakuna kitu hapa hii danganya toto, kwa hili wimbi kubwa la utekaji na serikali kuhusishwa baadhi ya matukio mengi wa resume tukio la hawa jamaa kama njia moja wapo ya kujisafisha.
Kuna baadhi ya watanzania wanafiki sana,serikali ikijitahidi kila hali na mali ya kufanya jambo jema katika kuwamata wanadhihakiwa,kuna mda jifunzr ku appriciate!
 
Tukio hilo lilitokea Novemba 11, 2024 eneo la Kiluvya Madukani, Wilaya ya Kinondoni, ambapo inadaiwa washtakiwa walipanga kumteka Tarimo wakitumia mtego uliopangwa na Anitha Temba, aliyemshawishi mfanyabiashara huyo wakutane kwenye hoteli kwa mazungumzo ya biashara.
 
Tukio hilo lilitokea Novemba 11, 2024 eneo la Kiluvya Madukani, Wilaya ya Kinondoni, ambapo inadaiwa washtakiwa walipanga kumteka Tarimo wakitumia mtego uliopangwa na Anitha Temba, aliyemshawishi mfanyabiashara huyo wakutane kwenye hoteli kwa mazungumzo ya biashara.

Kwenye Sheria kuna viloop hole unaweza kuponea ukijua namna ya kujielezea.

Anitha yeye atakuwa amesema alikuwa na meeting ya biashara na katika ya meeting ndio watu wakavamia na yeye hawajui wala hawakupanga njama.
Mahakama kama haijadhibitisha njama kama ilipangwa bas Anitha hana kosa.
 
Hao ni watekaji wa kiraia ndio maana hayo yanetokea,kuna wale watekaji wa kiserikali ambao hawahojiwi na mtu
 
Back
Top Bottom