wangoni wana nini jamani??

Hivi ni kwa nini majina yao yako hivyo, hawajui kuwa ni ya wanyama!!
 
@katavi,tumuulize bwana chimunguru hv hawajuagi kama majina ni ya wanyama au wanakitu wanataka kuki-associate nacho au,anyways myself huwa napenda kusikia majina yao kama chuoni nimesoma na mmoja anaitwa RITHA NGURUWE-B.A in CULTURE AND HERITAGE MANAGEMENT pale UDSM,Of course she was proud of be ngoni,sengwile wanajf kwa michango juu ya wa-ngoni
 
Umesahau Lumecha, Mlilayoyo, Mawa, Hanga, Matimila, Likuyufusi, Mdwema, Ngwinde, Namkongo, Msindo, Msalabamkuu, Njomlole, Mateka, Liganga... niendelee?
 
Endelea 2. Hiyo namkongo ni ile ya namtumbo? Nandembo, kilimasera, masuguru, huria, matemanga, luhuwiko, mitomoni, msamara maeneo ya otawa na pale rtd(tbc), nakawale, muhukuru, igalawasenga. Luwekei, maguhu,matiri, kigonsera kwa mama sophia pale!
 
Chimunguru!! Wakunyumba nimekukubali! na mie wa kunyumba mwenzako ila sijafikaga huko home na najipanga niende mkuu ili nijue kwetu! Nice oneee!
 
Du Chimunguru wewe mwisho we reli! hata mm nimekukubali. Nasikia hawa jamaa walikuwa wawindaji hodari sana, wakawinda hadi wanyama wote wakaisha, basi wakaamua wapeane majina wa wanyama kuwa wewe utaitwa Tembo, Mapunda, Tumbili n.k.
Kuna stori kuwa Pope John Paul alipoenda Songea (sikumbuka mwaka) akawauliza awafanyie nn? wakamjibu wanaomba afute amri ya sita kwani inawabana sana! teh teh!
 
Jambo wana jf,napenda kufahamu asili ya majina ya kingoni/Wangoni maana utasikia mara ngonyani,mapunda,sungura,tembo,nguruwe......mmmh ,wanajf naomba nyongeza ya majina ya wangoni na kuelewa why wanapenda majina ya wanyama?




Mkuu kumbe watani zangu hawa bado wanaitwa wangoni? Mi nilisikia kuwa wamerekebisha jina la kabila yao kwa kutoa hiyo herufi "n" na sasa wanaitwa Wagoni........hahahahahah watani bana mpooooooooooooo..................
 
Mkuu kumbe watani zangu hawa bado wanaitwa wangoni? Mi nilisikia kuwa wamerekebisha jina la kabila yao kwa kutoa hiyo herufi "n" na sasa wanaitwa Wagoni........hahahahahah watani bana mpooooooooooooo..................

Duh,kuumbe nii wagoni eeeeh ,makuuuubwa.
 
Mkuu kumbe watani zangu hawa bado wanaitwa wangoni? Mi nilisikia kuwa wamerekebisha jina la kabila yao kwa kutoa hiyo herufi "n" na sasa wanaitwa Wagoni........hahahahahah watani bana mpooooooooooooo..................
Te he te he eeh eti wagoni!!
 
fisi,kenge,mbwa,nyati,paka shume,nyoka,mjusi kafiri,nyangumi,papa,nondo mla watu,...........
 
:sick:Umesahau, kijiji changu, cha SINAI, pale karibuni na PERAMIHO!!!!!!!!!!!:sick:
 
Jambo wana jf,napenda kufahamu asili ya majina ya kingoni/Wangoni maana utasikia mara ngonyani,mapunda,sungura,tembo,nguruwe......mmmh ,wanajf naomba nyongeza ya majina ya wangoni na kuelewa why wanapenda majina ya wanyama?

Faru, Mbogo, Katembo
 
teheteh kaka sisi ni waSauzi bana njia yote tulikopita wapo Ngoniz kibao hapo zambia akina Tembo, Njovu, Soko wako kibao tu Zimbabwe wamejaa, ukienda Swaziland kibaooooo, sauzi huko kibao nako akinza Zenda, hahahahahaha Malawi so we conquered many a tribe. Wakati mfalme Zulu anatawala kule bondeni alikuwa katili mnooo so tukalala mbele kutafuta vibonde wetu na sie, so tutapiita kooote tukaja ishia Songea hapo. sisi tuna watani wengi sana wakiwemo wafipa, wanyamwezi, wasukuma wahehe, wapogoro, wazaramo wamatumbi, wahyao na wengine wengi tu huko kote tulipiga na kusambaratisha na wakaacha njia. Songea bana raha sana nakumbuka Ngoma yetu swafi sana inaitwa Lizombe, kuna LIGIHU(hii ilikuwa wazee wanacheza) na ligwamba. Kuna beta hahahahaha hii tamu mnoo halafu kuna ngoma flani hivi TAMU AJABU miaka ya 80 mpaka 84-85 ilikuwa maarufu sana kwa vijana pale songea mjini ikiitwa KAMBINDI!!! fika kimolo, mateka, makambi, matogoro, luhila seko, kule Box 2 aka Songea BOYS ikifika kumi na mbili jioni ni ngoma kwa kwenda mbele. Kuna ule wimbo maarufu wa SOKONI SIENDI TENA, SOKONI SIENDI TENA NILIKUMTA BINTI MMOJA EEEEH LIWAYA AMEVAA KANGA EEEH LIWAYA KANGA SIO KANGA EEENH LIWAYA BALI ......... EEEH LIWAYA, NAMBENDO SIENDI TENA NAMBENDO SIENDI TENA.. hapo kambindi aka KAMBUSU imepamba moto halafu ilikuwa inatembea dizaini km mdundiko vile aaaaah ilikuwa raha saaaaana. Basi ule mdundo wa ndoma tulikuwa tunaupa maneno eti dombi eenh sidombi tena x3 hahahaha

Umenikumbusha sana BOX TWO mkuu! Nakumbuka sana siku tuliyowatia adabu watoto wa TAMSALA (Songea Girls) enzi hizo tukaishia mahabusu. We acha tu...
 
uwiiiiiiiiiiiiiiiiii, mbavu zangu mie jamani nafa kwa kucheka, jina jingine KASUKU
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom