Wanawake zamani VS. Wanawake Sasa

Wanawake zamani VS. Wanawake Sasa

Zemanda

JF-Expert Member
Joined
Jan 10, 2021
Posts
10,651
Reaction score
22,819
1. Zamani : Mwanamke anakutana na mwanaume kakonda hana mwili, kimoyomoyo " huyu mwanaume hana mtu anayemtunza hadi ana dhoofu afya nipambane niolewe nae nimtunze hadi apendeze"

Sasa : Mmmmhmn MUNGU aniepushe na hiki kikombe, mtu kakondeana kama mti wa dawa afu anajiamini kunitongoza, usikute ana ngoma,hebu ukoo"

2. Zamani: Mwanamke anakutana na mwanaume miaka 30 bachelor hana hata mtoto. "MUNGU kajibu maombi yangu kanipa wa kwangu wa kujehga nae familia from scratch"

Sasa : Mmmmhmn huyu atakuwa ni muhuni,ogopa mwanaume ambaye hajazaa na mtu na hana hata mtoto wa kusingiziwa. Mimi hapana kwakweli ni bora niendelee kuwa single kuliko mtu wa hivi"

3. Zamani: Mwanamke anatongozwa na mume wa mtu. " Mmmmhmn hii si sawa,nitapata laana kuvunja ndoa ya mtu,watoto watateseka wazazi wao wakitengana,na ni dhambi kwa MUNGU wacha tu nisubirie kupata wa kwangu"

Sasa: " ooooh Hallelujah,ngoja niende kwa mwamposa kutoa sadaka kwa kunieletea mwanaume wa ndoto zangu, ana mali, biashara na ananijali,mkewe na watoto wake itabidi wajikaze mimi siwezi kupishana na bahati"

4. Zamani: Mwanamke anakutana na kijana amehitimu masomo ila hana ajira na anajitafuta. " Hongera kwa kumaliza masomo,usijali, MUNGU atatufungulia njia huko mbeleni tutapata mali kwasasa tujibidiishe na maisha".

Sasa : " mmmmmmmmmn sasa mwanaume hauna hela,hauna kazi unanitaka utanihudumiaje kwa mfano, au unataka ukanifubaze nichakae ndio ufurahi? We kuweza"

5. Zamani : mwanamke akienda nyumba ya ibada. " MUNGU baba naomba unilinde na kuniweka mbali na vishawishi na uovu wa shetani,nilinde huu mwili wangu na hiii bikra yangu hadi ndoa niwe mke mwema na kuishi kwa namna ya kukupendeza"

Sasa : " eeeeh Yesu naomba uningezee tako , shepu na rangi ya mtume ili wanaume wakiniona wachanganyikiwe,nisamehe kwa kutoa mimba ya tatu niliogopa kuzaa mtoto asiteseke. Naomba unipe mume handsome,mrefu,rangi nzuri,ajue kuvaa,awe na hela nyingi,kwao wawe matajiri,awe wangu pekee yangu anipende pekee yangu.


Kwa kifupi wamebadilika sana.
 
Zamani huko chachi demu akiombwa uchumba hakatai na hamchambui huyo anayemchumbia yukoje kiumri, kiuchumi na kielimu bora tu kiroho chake kiko safi. Tofauti siku hizi demu anakuwa na wachumba wengi halafu anachagua yupi mwenye mpunga mwingi ndiyo atamuoa hata kama ni muhuni poa tu mradi ana hela za kutosha kuliwa na demu huyo
 
Kuna demu kamkandia jamaa mmoja aliyemtongoza na kudaia atafia kifuani kwake, anamuona ni mzee aliyekondeana. Kamdharau ile mbaya huyo mshua. Kumbe huyo demu ni malaya mwenye kutaka wenye hela tu
Hawataki ambaye hajatimia. Wanataka ambaye yupo tayari.
 
Zamani huko chachi demu akiombwa uchumba hakatai na hamchambui huyo anayemchumbia yukoje kiumri, kiuchumi na kielimu bora tu kiroho chake kiko safi. Tofauti siku hizi demu anakuwa na wachumba wengi halafu anachagua yupi mwenye mpunga mwingi ndiyo atamuoa hata kama ni muhuni poa tu mradi ana hela za kutosha kuliwa na demu huyo
Na ndio maana wengi wanaingia Chaka pamoja na kuchagua kote huwa wanaangukia pua sababu ys tamaa,ujuaji na standards nyingi kudadadeki.
 
1749070708893.jpg
 
Mademu wa siku hizi wao ndio huchagua wa kuwaoa kwa kutaka sifa kuwa wameolewa na kijana mtanashati mwenye hela maisha mazuri ni kula na kuvaa each and everything available. Hawataki waume wa kuletewa wasio na sifa za kusisimua kiuchumi, tofauti na zamani ukiletewa mchumba hata kama hujampenda huchomoi na ndoa ilidumu
 
Back
Top Bottom