Jokajeusi
JF-Expert Member
- Jun 1, 2018
- 6,305
- 10,582
- Thread starter
- #21
daahh
Ndio hivyo.
Kuna kumlea mtu na kumfuga.
Kumlea mtu ni kumpa mahitaji yenye ubora ya kila namna.
Kamaa ni chakula kiwe Diet ya kutosha, nguo nzuri zinazoendana na mazingira, sio nguo ya kanisani inafanana na nguo ya msibani,
Malazi mazuri.
Kumfuga mtu ni kumpa mtu mahitaji ilimradi aishi Bila kujali ubora.
Unakuta unakula Mlo mmoja miaka nenda rudi, asubuhi kavu au chai tupu, siku ukijitahidi chai na maandazi mawili. Siku ya sikukuu ndio chai ya maziwa na chapati.
Nguo unavaa moja miak nenda rudi, kama ngozi ya wanyama, yaani siku ukibadili ni kama nyoka amevua gamba lake Kila mtu anajua.
Unalala kitanda kibaya kichafu kama mbuzi.
Mbuzi na Ng'ombe ndio wanafugwaa, hata uwape majani yale yale miaka nenda rudi hawana shida, hata walale chini au zizi la miiba hawaoni shida. Huko ni kufugwa.
Sasa unakuta mtu anajifanya amekulea kumbe amekufuga kama mbuzi kasoro kamba shingoni. Masikini bhanaa!
Hata ni sisi wanaume, usijefanye unataka heshima kwa kujigamba kuwa unamlea mkeo kwa kumpa mahitaji yake wakati kiuhalisia humlei bali unamfuga kama mbwa kasoro mnyororo tuu shingoni