Wanawake wana lawama za ajabu sana

Wanawake wana lawama za ajabu sana

msemakweli2

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2013
Posts
1,627
Reaction score
1,886
Nyumbani kuna gari mbili hataki kuendesha, asubuhi anataka nimpeleke ofisini jioni nimpitie, mimi natoka saa tisa na nusu yeye anatoka saa moja usiku.

Nakaa nje wee kama mlinzi akitoka tunaondoka kufika home ni saa tatu saa nne. Weekend pia anataka nimpeleke mimi weekend siendi kazini, mpaka kumchukua weekend anataka nikamchukue.

Leo nimechelewa kidogo kumchukua hata kunisalimia hajanisalimia amerudi amevuta mdomo anachat mpaka muda huu tu sebuleni. Hivi hapo kosa likowapi? Kama sio habari za kipuuzi kabisa sema nimenyamaza tu.
 
Hili lihaya hili...
Wanapenda sifa hao.
Kuna mmoja tuna sali nae sku moja alikuwa anahubiri akasema mpaka namaliza chuo alikuwa na mil 10 aisee nlicheka sn sn...wakati mpaka sasa hana hata bodaboda na anafanya kazi.
 
nyumbani kuna gari mbili hataki kuendesha,asubuh anataka nimpeleke ofisini jioni nimpitie,mimi natoka saa tisa na nusu yeye anatoka saa moja usiku,nakaa nje wee kama mlinzi akitoka tunaondoka kufika home ni saa tatu saa nne,weekend pia anataka nimpeleke mimi weekend siendi kazini,mpaka kumchukua weekend anataka nikamchukue,leo nimechelewa kidogo kumchukua hata kunisalimia hajanisalimia amerud amevuta mdomo anachat mpk muda huu tu sebuleni,hivi hapo kosa likowap??kama sio habari za kipuuzi kabisa sema nimenyamaza tu,
Mtafutie dereva mkuu
 
AFFECTION bro, huna kitu kina itwa AFFECTION, aiseee wanawake huo ndio ugonjwa wao.... Na sio kila mwanaume ana uwezo wa affection...... Aiseee utachapiwa huyo in a serious note! Ngoja akutane na mwenye hii affection utaona changes.
 
Dalili za mvua mawingu, nataka kusema kitu hapa lakini sitaki nisababishe ugomvi kwenye ndoa ya mleta uzi.
 
Kiongozi.

Hebu funguka zaidi.

Je Huyo MWANAMKE anaweza kuendesha?

Maana kuna mawili,

Kuna yule ambae anaweza kuendesha na hataki, labda ni mvivu.

Na kuna yule ambae hawezi kuendesha.

Kwahiyo kabla hatujaanza kutupia lawama, inabidi tufahamu kwanza kama anafanya hivyo kwa makusudi au ni Mtu ambae hataki kujifunza
 
Ifike mahali tuache kuchukulia kuwa ni big deal mtu anaposema ana miliki gari ama nyumba.

So what if they really own it?

Let as look at the point they are trying to put forward, offer advice or walk away if we can't.

Tusiwashambulie wenzetu over what they have. Let's take it as a challenge itupe moyo na sisi tutafute vya kwetu.

Pia ifike mahali tukubali kwamba binaadamu hatufanani just like the fingers on our hands. Sio ki tabia si uwezo.

Mfano, naweza kuwa sina hata baskeli... lakini nilikimbilia kujenga. Naweza kuwa sina gari baskeli wala kibanda but faraja yangu ipo katika familia yangu. Watoto wangu wanakula wakitakacho na wanalala pazuri...

Zote hizi ni baraka na ni aina tofauti za furaha kwa wamiliki. Tusiwe na chuki kwa wenzetu ambao tunahisi wametuzidi kitu in one way or the other.

Lets be kind to each other, Positive vibes whenever we can.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom