duh, mambo ya kusema tabia kimakabila yalishapitwa na wakati, lakin kuna makabila hata ujitahidi vipi hayapambanuki na tabia fulani, mimi kidogo tu niuvae mkenge nikiwa kijana mbichi, isingekuwa roho ngumu sijui leo ningekuwa wapi. rafiki yangu wa karibu yalimkuta si madogo, aliugua sana miezi kadhaa yuko ICU, mama wa watu kaona hii ngoma haieleweki, siku moja kenda kumwona wodini kamwabia "sasa baba nanihii naona wewe sasa hivi haueleweki, mimi nataka niangalie ustaarabu mwingine, tunafanyaje"? jamaa bila hiyana kamwambia we nenda tu nyumbani kauze kila unachoweza hata nyumba we uza fanya unachotaka, mama wa watu kama utani katoka kaenda kuuza kila kitu katambaa, mungu siyo yusufu jamaa akapona akarudi mtaani akanyoosha tena mambo yake, yule mke kumbe alishamaliza kila kitu na mwanamume aliyempata alimpiga mateke.....aaargh, wacha niishie hapo haina maana kuendelea!