Wanawake tupeane siri

Wanawake tupeane siri

ragin

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2015
Posts
7,391
Reaction score
9,378
Wenzetu wakitendwa kauli mbiu "watafte pesa" mapenzi yatajileta.

Wanawake je tufanyaje?

Iko hivi

My childhood friend Zuwena (jins sio halisi) kwao wako vizuri uchumi kati Baba yao alitangulia mbele ya haki wakabaki na mama,,. Huyu Zuwena aliolewa na kubahatika mtoto 1

Aliemuoa aliaply masomo ya elimu ya juu ili kujiendeleza akiwa kazini, kwa bahati nzuri chuo alichoaply ndio karibu na ndiko wazazi wa Zuena wanakoishi,.

Mzazi wa Zuena alipopata taarifa kuwa mkwe atakuja kusoma kwa upendo wakashauriana na Zuwena wakitoka huko mkoa kwa kipindi hicho cha masomo watapanga au wakae wakae nyumbani mpaka atakapo Mali za masomo?

Zuwena aliona ni bora wafikie nyumbani kwao huku Mume wake akimaliza masomo watarudi mkoa walikotoka na ukizingatia kipindi hiko cha JIWE hata kama upo kazini husomeshwi utajisomesha kwa pesa zako so vitenda vya hela ndogondogo huwezi hata kuwa navyo ni bora wafikie kwao.

Masomo yameisha miaka 4 ya tabu, shida na masumbukohadi mama mtu kujitolea kulipia ada mkwe ili amalize semester n.k mbaya zaidi mwanaume kwao hawasapoti wala hawataki kusikia shida mama wazuwena alipoona hivo akaamua abebe huo mzigo ili amalize tu waondoke yote haya ni zuwena ndo alikuwa anamlilia mama yake amsaidie mumewe kwenye matatizo yao.

Mume wa Zuwena amesharudi kazini mwaka wa 3 sasa hajaichukua familia yake na aliaga anatangulia kuweka mazingira vizuri ndo mke na mtoto waje.

Kila Zuwena akichachamaa aende mumewe anasema hana nauli, maisha bado magumu ooh kijijini wazazi wake wanamuomba hela sijui ndugu yao amepata ajali hela zimemtoka hadi hawezi kujiendeleza n.k kwakuwa aliondoka na mizigo baadhi ya Zuwena na mtoto na pale nyumbani walibaki na nguo za kushindia tu wakijua after one month atakuwa keshaenda kwa mumewe.

Zuwena ikafika mahali akaomba arudishiwe vitu vyake ili apate walau hata nguo zakubadili ila mumewe akawa anamwambia atakuja wiki ijayo tanguliza nguo nyingine na vyombo baadhi mpe mfanyakazi mwenzangu atakuja huko bila kinyongo akampa huku akijua next week ye Zuwena atakuwa kwa mumewe kumbe ndo hivo mpaka leo 3 years now.

Swali Zuwena afanyeje? Ikiwa wanaume wana kauli mbiu "TAFTA HELA".
 
Si Zuwena apande zake gari akajijulie nini kinaendelea akishaujua ukweli anashika 18 zake anaanza upya na kumsahau uyo pimbi mazima, miaka 3 si ni kama washatengana.
 
Si zuwena apande zake gari akajijulie nini kinaendelea akishaujua ukweli anashika 18 zake anaanza upya na kumsahau uyo pimbi mazima, miaka 3 si ni kama washatengana
Maisha ya kupanga ni tofauti na umiliki wa nyumba leo utakuwa kwa mzee John kesho kwa mzee Masawe Kodi ikikushinda.
 
Huyo fala alipata mwanamke mwingine akiwa Chuo kwa kuwa alikuwa na hela ya kuchezea wakati mkwewe akilipia ada, malazi na kumtunzia familia.

Baada ya kuona huo mtelemko, haoni tena sababu ya kutunza familia wakati mama mkwe yupo. Zuwena anatakiwa bila taarifa kwa msaada wa mama yake, afungashe mizigo aende kwa mumewe watajua huko huko.
 
Labda mimi ndio sijaelewa. Yani Mume alikuwa anajisomesha au alikuwa anasomeshwa na wakwe?.

Halafu mke anashindwaje kurudi kwake kwa kukosa nauli tu wakati mama yake alikuwa hadi na uwezo wa kulipia ada ya mkwe wake?

Labda kuna tatizo lingine ambalo mtoa mada hujatuhabarisha, maana huyo mume alienda kusoma huku akiwa ni mfanyakazi na mshahara anao, anakosaje nauli kwa miaka mitatu?.
 
Kwaivo we mwenyewe unasemaje.
Aende mwenyewe apewe nauli

Lakini huoni km ni kujiendekeza na kubeba majukumu ya mwanaume huku unajua fika pesa anayo.
 
Huyo fala alipata mwanamke mwingine akiwa Chuo kwa kuwa alikuwa na hela ya kuchezea wakati mkwewe akilipia ada, malazi na kumtunzia familia.

Baada ya kuona huo mtelemko, haoni tena sababu ya kutunza familia wakati mama mkwe yupo. Zuwena anatakiwa bila taarifa kwa msaada wa mama yake, afungashe mizigo aende kwa mumewe watajua huko huko.
Sawasawa
 
Labda mimi ndio sijaelewa. Yani Mume alikuwa anajisomesha au alikuwa anasomeshwa na wakwe?.

Halafu mke anashindwaje kurudi kwake kwa kukosa nauli tu wakati mama yake alikuwa hadi na uwezo wa kulipia ada ya mkwe wake?

Labda kuna tatizo lingine ambalo mtoa mada hujatuhabarisha, maana huyo mume alienda kusoma huku akiwa ni mfanyakazi na mshahara anao, anakosaje nauli kwa miaka mitatu?.
Anajisomesha ila mikopo ya kujisomesha ilipozidi mkwe akamsaidia amalize semester

Hapo kwenye kutuma nauli huku mfanyakazi visingizio ndo km hivo nilivyo viainisha hapo juu.
 
Sasa mnapeanaje siri hadharani?

Fanyeni kikao chenu chemba.
 
Mliosoma huu uzi wekeni mchanganuo kwa ufupi tuelewe mie macho mabovu siku hizi nashindwa kusoma hizi novels
 
Sijui watu huwa wanaroga.....hivi mme unawezaje kumuambia mke "usije" na hapo ni kwenu (familia) unakuta mke nae anatulia tu kaambiwa asiende!!! Hii ni kawaida kweli?

Kama sio ushirikina basi kuna mtu anajifanya kichwa ngumu, kuna jirani yeye mume alikua mbali tangu akiwa preg miezi 5 hawajaonana na mme hadi kajifungua mtoto kafikisha miezi sita, mme hajawahi kuja sehemu yenyewe dar- arusha mke akitaka kwenda anamwambia usije ntakuita....

Baada ya kuchochewa na wachochezi kuwa aache ujinga kaamua kwenda.
Kufika mme alishahamia nyumba nyingine, anakaa na mwanamke mwingine.... akaishia kukatiwa tiketi kesho yake arudi akikotoka yeye na wanae!!!!
 
Comment yangu ilikuwa ya kwanza sahivi siioni kabisaa
 
Sijui watu huwa wanaroga.....hivi mme unawezaje kumuambia mke "usije" na hapo ni kwenu (familia) unakuta mke nae anatulia tu kaambiwa asiende!!! Hii ni kawaida kweli????

Kama sio ushirikina basi kuna mtu anajifanya kichwa ngumu, kuna jirani yeye mume alikua mbali tangu akiwa preg miezi 5 hawajaonana na mme hadi kajifungua mtoto kafikisha miezi sita, mme hajawahi kuja sehemu yenyewe dar- arusha mke akitaka kwenda anamwambia usije ntakuita....

Baada ya kuchochewa na wachochezi kuwa aache ujinga kaamua kwenda.
Kufika mme alishahamia nyumba nyingine, anakaa na mwanamke mwingine.... akaishia kukatiwa tiketi kesho yake arudi akikotoka yeye na wanae!!!!

Hii thread ni ya wanawake lakini naombeni nichangie kidogo, maana mmeamua kuliweka barazani.

Mahusiano yoyote ya mbali ukiambiwa 'usije', 'nitakuambia uje lini' au 'nitakuja mimi' hapo ujue kuna mtu kaichukua nafasi yako.
 
Hoi thread ni ya wanawake lakini naombeni nichangie kidogo, maana mmeamua kuliweka barazani.

Mahusiano yoyote ya mbali ukiambiwa 'usije', 'nitakuambia uje lini' au 'nitakuja mimi' hapo ujue kuna mtu kaichukua nafasi yako.
Ni kweli kabisa.....
Na amekuweka wazi, sema tu ndio vile kujifanya huelewi
 
Mwambie zuwena aache ufala.. Kesho akope nauli hata kwa jirani apande gari kimyakimya mpaka kwa mumewe na kama atakuta amehama walipokuwa wanakaa aende moja kwa moja kazni kwa mume wake..

Kuna wanaume wanajitafutia mikosi bure kwenye maisha yao.
Unamtelekeza mtoto na mkeo kisa papuchi mpya.. Shennnzzyyyyy kabisa
 
Yani hela ya kulipa ada ipo ila ya nauli hamna, hiki kisa Cha kubuni ni kizuri ila hakina uhalisia.
 
Back
Top Bottom