Wanawake, this is too much (kali ya mwaka)

Wanawake, this is too much (kali ya mwaka)

KIUNGOMCHEZESHAJI

Senior Member
Joined
Oct 4, 2013
Posts
120
Reaction score
255
Wanawake/akina dada, najua ukweli unauma lakini mkubali tuu kuwa wengi wenu hamtaolewa kwa sababu mmepoteza dira ya maisha yenu. Kufuatia malalamiko ya akina kaka wengi nimeamua kufanya simple research, nitaielezea kidogo nadhani mtanielewa.

Nilifungua fake facebook account, nikaamua kuwaadd marafiki wa kike ninaowafahamu na pia nisiowafahamu ili mradi tuu sample research yangu iwe kubwa. Katika wale ninaowafahamu kwa sababu jina sio la kweli wakaniadd wasijue kama mimi ni yule yule wanayemfahamu na wengine ni wapenzi na ambao nimeshatembea nao. Nikaanza kuchat nao na kuwapa infomation tofauti kabisa na zangu kama vile mahali nilipo, kazi yangu na status yangu. Nikasajili namba ya simu kwa wrong name.

Wastani wa akina dada 8 kati ya 10 walikataa kunipa namba nilipowaomba wakisema hawawezi kumpa namba mtu asiyemfahamu. Kadiri tulivyozidi kuchat kuhusu maisha wakasema maisha magumu, na mimi nikajifanya matawi ya juu, wakaanza kuniomba vocha. Ikawa kila mmoja wao namjibu kuwa hapa mfukoni sina hela cash ila nina hela kwenye M pesa nitakutumiaje? Fasta, wote wakanipa namba zao kwa ajili ya kutumiwa M pesa. Mwisho wa siku sikuwahi kutuma hata senti moja. Hivi nawaenjoy sana na wengine tuko nao tunafanya kazi sehemu moja. Ni wastani wa watu wawili kati ya kumi ambao walikataa kata kata na hawakutaka chochote toka kwangu.

Jambo lingine, 7 kati ya kumi walianza kuniomba hela hata kabla hatujazungumza lolote kuhusu mapenzi. Nilipowachombeza kuhusu mapenzi walikubali haraka huku wakisisitiza nitume hizo hela. Sasa jamani, hivi unaweza kumuita mtu mpenzi hamfahamiani wala hata hujaona sura yake fb, lakini unalainika ili kumlainisha naye atoe wallet yake? Mara "ooh nakupenda sana naomba nitumie nauli nije kukuona". Haya basi haitoki hata senti ila nazidi kuwajifunza hawa viumbe dhaifu.
 
hata wanaume tupo wengi wenye tabia kama hizo.
Kwakifupi, uzinifu ndio unaosumbua sana jamii na dunia kwa ujumla. Na mzinzi haendani na asiekuwa mzinzi, hivyo ulichoona kwa wanawake hata wanaume lipo.
 
hata wanaume tupo wengi wenye
tabia kama hizo.
Kwakifupi, uzinifu ndio unaosumbua sana jamii na dunia kwa ujumla. Na
mzinzi haendani na asiekuwa mzinzi, hivyo ulichoona kwa wanawake hata
wanaume lipo.

Mmh! Embu acha kutudhalilisha, hizo ni tabia za kike, kama we unazo usisingizie na wengine.
 
hata wanaume tupo wengi wenye tabia kama hizo.
Kwakifupi, uzinifu ndio unaosumbua sana jamii na dunia kwa ujumla. Na mzinzi haendani na asiekuwa mzinzi, hivyo ulichoona kwa wanawake hata wanaume lipo.
kungekuwa na like 100 ningekupa kweli..
kuna mtu najribu kumuelewesha swala la like poles attract na jinsi unavyomuwazia mwenzako most times ndo nae anajikuta hivyo haelewi..
 
Ndo ujue watu wamepinda, mie aka kwa gia kama hiyo wala usingenipata. Malengo yangu yako kifuture zaidi na mwanaume wa fb au jf hawezi kuntimizia. Yani hapa ni kushikamana na mume wangu naamin tukiwa na nia moja tutafika mbali.
 
ah! Mambo ya fb huku hayatuhusu sie,wapelekee hukohuko fb ulikofanyia the so called research yako.
 
Kiukweli hii mitandao imerahisisha sana utongozaji. Ukiwa mjanja wa kuzitazama picha za hawa dada zetu zinakupa taswira nzima na uhusika wamtu kuanzia tabia had matamsh yake... Hapo huna haja yakuchokoza. Hakika nakuambia fbk imenipa mchumba hatimae mke. Nidada niliekuanae fbk kwa mda wa mwaka mmoja na miezi miwili ndipo alipokubali kuonana nae nahata siku tulipoonana hatukuongea zaid ya dakika 15.. Baada ya hapo nilianza kupata cm zake za usiku mwema nk. Naamin c wanawake wooote ktk mitandao ni wahuni huni tu, la hasha... Ila ukifanya reseach kwa hawa wanaopiga picha zakuonyesha makalio yao nk. Lazima upate wrong re-seach!
 
hii ni balaaa nilimuibia demu wangu password na username maana alikua hataki kunipa. nilitumia njia ya spynifer nikapata details zake zote za username na password. nilichokikuta fb account yake ni balaaa. anawapenzi zaidi ya wanne na kwachat zao inaonesha alishagegedwa nao. sikumwambia kitu nikapunguza mawasiliano nae kidogo kidogo mpaka nikakata kabisa. niliingia pia kwenye email zake ndio mamaaa balaaa. jamani kama hali ndio hii ni hatari
 
ungetuma hela ili uone kama penzi ungepata, hapo research yako ingekaa vyema

Unaweza kudhani umewapata kumbe na wao katika akili zao wanawaza hivyo hivyo ni kama ule wa mtu anayetoa hela bandia naye anauziwa dhahabu bandia.

pengine na wao walikua kwenye risechi yao

Inawezekana kabisa,kwamba na wao walikuwa na account fake nao wanafanya research vilevile,unauza cheni feki ukifika home unakuta hela ulizopewa ni ni hela za bandia,chezea bongo wewe!
 
Fanya na Jf humu uone tofauti ya kule fb na humu, humu watu wapo real, mi mwenyewe nilikua nafanya research nilipewaga no. ya mchungaji mbona ilikamilika siku hiyo hiyo
 
Hinzo tabia siyo kwa wanawake tu hata wanaume pia unavosema wasoyolewe una manisha hata dada yako nae asiyolewe
 
Back
Top Bottom