Bluray
JF-Expert Member
- Mar 25, 2008
- 3,449
- 127
Nakushauri uweke landline nyumbani au hata ile ttcl mobile na uiweke sebuleni au jikoni. Nilikuwa na tatizo hili na mke wangu, tuligombana sana mwisho nikaona isiwe tabu, nikaja na hiyo solution, nikaweka landline! akiwa nyumbani nikapiga mobile mara 1 bila kupokea, napiga landline (si unajua linavyolia) basi hata sekunde haipiti nasikia ''hallow'', akiwa ofisini natumia ya ofisini, akiwa ametoka, nimeweka ttcl mobile kwenye gari lake..... basi full covered nampata muda wowote. Hili ni tatizo la wanawake wengi, so usikasirike, tafuta solution!
Halafu baada ya shida yote hiyo, umempigia kwenye landline ya nyumbani, unamuuliza "Uko wapi" anakujibu "nipo nyumbani, si umenipigia simu ya nyumbani?" "Nilikuwa nakusalimia tu"